Bandari za Tanganyika hazijauzwa wala kukodishwa kwa waarabu wa Dubai bali zote wamepewa bure!

Bandari za Tanganyika hazijauzwa wala kukodishwa kwa waarabu wa Dubai bali zote wamepewa bure!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Nimesikitika sana kusikia malumbano ya watu mbalimbali kuhusu suala la kuuzwa dhidi ya kukodishwa kwa bandari zote za mwambao wa bahari ya Hindi upande wa Tanzania bara kwenda kwa waarabu wa Dubai (DP world).

Baada ya kupitia kwa kina, kipengele kwa kipengele, kusikiliza maoni tofauti tofauti ya watu wenye uelewa na weredi kuhusu mikataba na sheria, nimegundua wazi bila shaka yoyote kuwa, Bandari zote za mwambao wa bahari ya Hindi upande wa Tanzania bara amepewa BURE muarabu wa Dubai. Narudia kusema muarabu wa Dubai amepewa BURE. Hajauziwa wala kukodishiwa. Sababu muhimu ni hizi hapa.

1. Hakuna mahali popote kwenye mkataba panaposema ameuziwa bandari au kueleza bei ya manunuzi ama kiasi kilicholipwa ili muarabu apewe bandari. Mkataba indirectly unasema Muarabu wa Dubai amepewa milele ili apaendeleze na hatupaswi kumfanya chochote akishindwa kupaendeleza!

2. Hakuna mahali popote kwenye mkataba panapotaja ni lini au namna gani bandari yetu tutarejeshewa tena. Ukodishaji wowote wa jambo unabanwa na mambo mawili tu. Mosi mipaka ya muda (ni lazima useme ukomo wa muda wa kukodisha) na pili Urejeshaji ya kile kilichokodishwa (ni vipi mkodishaji atarudishiwa mali yake aliyoikodisha). Kwenye mkataba huu hakuna popote panaposema hayo. Pako kimya kabisa.

Note
Tafsiri nyingine ya kiujumla jumla ya BURE ni; Uuzwaji wa kitu cha thamani kwa bei ndogo sana isiyolingana na bei ya soko au uuzwaji wa tunu (kitu chenye thamani kubwa kijamii isiyoweza kubadilika na chenye kuwa na sifa ya kurithiwa na vizazi vyote vijavyo milele)

Pia kukodisha kitu kwa mtu mwingine kwa kipindi cha muda mrefu unaopitiliza muda wa matarajio ya wewe au kizazi chako cha sasa kuendelea kuwepo hai (kiutendaji) duniani maana yake ni kubadilisha umiliki kutoka kwako kwenda kwa yule unayemkodishia. Ukodishaji wowote unaozidi miaka 20 huo ni umilikishaji.
 
Hatare nisawa na Msukuma au Masai kushindwa kufuga ngombe zao kuleta Wamarekani kuanzisha maranchi Wasukuma na Masai kuajiriwa kuchunga ngombe Kwa kulipwa maziwa yahao ngombe Nyama na ngozi zao
 
Hakuna mahali popote kwenye mkataba panaposema ameuziwa bandari au kueleza bei ya manunuzi ama kiasi kilicholipwa ili muarabu apewe bandari. Mkataba indirectly
Daaah 🤔🤔🤔😪😪😪😪 Hata kishika uchumba hakuna?
 
Tz ilipata kiongozi mzuri mkawa mnamtusi humu,ukitoa mapungufu kidogo tu alikuwa anaipenda nchi yake.
Sasa mtajua hamjui.
 
Ni yeye tu sasa aamue ila ndio mkoloni wetu mpya baada ya Muingereza.
 
Huna lolote!. Hebu nakili hicho kipengele kama umeusoma kweli.
 
Ajabu kuna wajinga wanaosema wamechoka kujadili hili jambo, jambo litaloumiza vizazi vyetu, ujinga wa mtu mmoja, maumivu yake yatawahusu mpaka ambao hawajazaliwa.
Waliochoka kujadili ndo hao wanaofaidika na huu mkataba.
Mshika remote katulia tulii anaamini kuwa hili nalo litapita..

Teuzi za juzi za kina Lukuvi ni jawabu ama ujumbe kwa msela kuwa ameshastukiwa.... Tenguzi ile ya awali ilifanyika ili mwanae apate nafasi
 
Tz ilipata kiongozi mzuri mkawa mnamtusi humu,ukitoa mapungufu kidogo tu alikuwa anaipenda nchi yake.
Sasa mtajua hamjui.
Tatizo yule kiongozi alitubagua wapinzani tukaonekana sio raia wa nchii hii, ndio maana mini namchukia Sana. Ila huyu wa Sasa hata ni tatizo sana.
 
Waliochoka kujadili ndo hao wanaofaidika na huu mkataba.
Mshika remote katulia tulii anaamini kuwa hili nalo litapita..

Teuzi za juzi za kina Lukuvi ni jawabu ama ujumbe kwa msela kuwa ameshastukiwa.... Tenguzi ile ya awali ilifanyika ili mwanae apate nafasi
Hata nami nilijua hilo, yule Lukuvi amerudishwa ili kupunguza nguvu ya mashambulizi anayotupiwa msaliti aliyetuuza Uarabuni, anataka angalau aunganishe makundi aliyoyatupa mwanzo yamuunge mkono kwenye huu ujinga wake wa bandarini, lakini kimsingi Lukuvi alishatupwa pembeni.
 
Hata nami nilijua hilo, yule Lukuvi amerudishwa ili kupunguza nguvu ya mashambulizi anayotupiwa msaliti aliyetuuza Uarabuni, anataka angalau aunganishe makundi aliyoyatupa mwanzo yamuunge mkono kwenye huu ujinga wake wa bandarini, lakini kimsingi Lukuvi alishatupwa pembeni.
Huyo Lukuvi yeye hajatia serikali hasara au mmesahau??
 
Back
Top Bottom