KERO Barabara inayoelekea Hospitali ya Magunga Korogwe ina shimo ambalo linazidi kuongezeka kila leo, mamlaka shughulikieni hili

KERO Barabara inayoelekea Hospitali ya Magunga Korogwe ina shimo ambalo linazidi kuongezeka kila leo, mamlaka shughulikieni hili

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Saad30

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2020
Posts
2,737
Reaction score
5,464
Moja kwa moja kwenye mada.

Viongozi wa Mji wa Korogwe hamuoni ile barabara ya kuelekea Hospitali ya Magunga? Barabara mpya ambayo inaonganisha mtaa wa Mountain view na Kanisa la Roma imeanza kuleta shida.

Shimo ambalo limeanza kuonekana litaweza kusababisha ajali usiku na pia uharibifu wa barabara ile maana linazidi kuchimbika na kutanuka pia. Viongozi litazameni hili jambo na pia rekebisheni yale mataa maana usiku ni giza la kutosha barabarani.

Nawapa pongezi kwa utengenezaji wa barabara na kuunganisha pale mlipoishia.

Mungu ibaraki wilaya Korogwe
Mungu ibariki Tanga
Mungu ibariki Tanzania

Mungu mpe afya tele Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan.
 
Mkuu tuone picha ya hilo shimo basi
IMG_20240402_154443.jpg
 
Ukifatilia idara husika inabajeti kwajili ya mameneja eneo Hilo kutembelea kilasiku kutazama shida za mabarabara

Umenifanya nirudie kutazama YouTube magufuli alivosikitika siku morogoro daraja lilivokatika
 
Ukifatilia idara husika inabajeti kwajili ya mameneja eneo Hilo kutembelea kilasiku kutazama shida za mabarabara

Umenifanya nirudie kutazama YouTube magufuli alivosikitika siku morogoro daraja lilivokatika
Inakata sana mkuu ukifikiria
 
Back
Top Bottom