Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

St. Paka Mweusi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2010
Posts
7,956
Reaction score
5,149
Naanza kwa kuwasalimia wakuu. Hapa ntaongelea matukio mawili niliyoyashuhudia kwa macho yangu.. Pia ntaongelea matukio machache niliyoyasikia.

Mwezi mmoja uliopita mida ya saa 11 alfajiri nikiwa napita maeneo ya Mbezi mwisho jirani na stendi ya mabasi ya Magufuli nilishuhudia mwili wa mwanamke ukiwa katikati ya matairi ya nyuma ya Lori( Semi Trailer lenye mzigo) dereva wa Lori hilo akiwa amekimbia na kuacha gari ikiwa imenasa mwili wa mwanamke huyo marehemu.

Siku nne zilizopita tukiwa maeneo ya Kibamba Hospitali muda wa saa nne usiku, Kijana mmoja aliwaaga wenzake kuwa anaenda upande wa pili wa barabara atarudi baada ya muda mfupi.. Alipokuwa akivuka barabara aligongwa na gari ndogo tukishuhudia. Akapoteza maisha palepale.

Miezi miwili iliyopita kijana mmoja ambaye alikuwa katibu wa vijana wa CCM aligongwa akiwa kwenye pikipiki maeneo ya Luguruni na kupoteza maisha palepale.

Miezi kama mitatu iliyopita mama mmoja akiwa anavuka barabara maeneo ya Kibamba CCM aligongwa na Lori(Semi Trailer) na kupoteza maisha palepale.

Sasa nachojiuliza.. TUTASUBIRI MPAKA AFE NANI NDIO TUCHUKUE HATUA..?? Matukio ni mengi sana. Watu wanakufa kwa sababu ya ajali za barabarani. Wahusika wapo wapi? Tukumbuke kuwa barabara hii ni High way inayopita kwenye makazi ya watu. Huyu mwananchi anayetumia barabara hii tunamlinda vipi kama watu wanakufa kwa kugongwa kwenye Zebra Crossings?

USHAURI WANGU KWA TANROADS
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.

Vivuko hivi vitawasaidia waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, na hata waendesha bodaboda kuvuka barabara hii bila kuathiri madereva wa magari. Na nina imani kuwa tutapunguza vifo vitokanavyo na ajali ka kiasi kikubwa sana.

NAOMBA KUWAKILISHA KWA HESHIMA NA TAADHIMA.
 
Hiyo bara bara inavutia sana kuendesha spidi kalii..
Upo sahihi kabisa mkuu.. Kila unapokanyaga mafuta gari inazidi kutulia na kukubali mwendo.. Lakini huyu mwenda kwa miguu anayetumia barabara hii tunamlindaje?? Tukumbuke kuwa ajali nyingi kwenye barabara hii zinatokea kwenye Zebra Crossings.. Kwa hiyo basi tuseme tu kuwa Zebra Crossings kwenye barabara hii hazina msaada kwa waenda kwa miguu..
 
Kwanza poleni wafiwa wote, halafu barabara hiyo haina vivuko kimsingi na ndio ajali huanzia hapo
 
kuna siku saa sita temboni karibu ma mataa ingawa wkt huo hakukuwa na taa naona kuna kitu mbele nikajua ni mbwa yani nafika karibu nagundua ni binadamu, lkn alikiluwa ameshapitiwa na magari mengi ameshaharibika sana nilimkwepa kiasi kuwa kama lane inayofuata kungekuwa na gari ningepata ajali.

nilifika home nikalala hata kula tena sikuweza.
 
kuna siku saa sita temboni karibu ma mataa ingawa wkt huo hakukuwa na taa naona kuna kitu mbele nikajua ni mbwa yani nafika karibu nagundua ni binadamu, lkn alikiluwa ameshapitiwa na magari mengi ameshaharibika sana nilimkwepa kiasi kuwa kama lane inayofuata kungekuwa na gari ningepata ajali.

nilifika home nikalala hata kula tena sikuweza.
Utawezaje kula mkuu.. Hali inatisha.. Na maiti za ajali mara nyingi zinakuwa zimeharibika vibaya sana..
 
ila hii barabara ilivyo sasa hivi nashauri watumiaji wa bodaboda wawe makini sana lakini pili watu wanaopiga mitungi kama ni watumiaji wa hii njia wafikirie mara mbili yani ni bora wanywe karibu na home kuliko kunywa sinza alafu anakaa kibaha, tatu na mwisho ni wavukaji wa hii barabara na hasa hao wanaopiga vyombo wawe makini sana.
 
USHAURI WANGU KWA TANROADS..
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.. Vivuko hivi vitawasaidia waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, na hata waendesha bodaboda kuvuka barabara hii bila kuathiri madereva wa magari.. Na nina imani kuwa tutapunguza vifo vitokanavyo na ajali ka kiasi kikubwa sana..
NAOMBA KUWAKILISHA KWA HESHIMA NA TAADHIMA..
... na hicho ndicho kinachotakiwa na sio kuweka mazebra kila baada ya 25m! Imagine vituo vya mwendokasi; ilitegemewa wasafiri wangekuwa wanaingia na kutoka vituoni through tunnels lakini ujinga uliofanyika ndio kama hivyo ni foleni za magari mwanzo mwisho! Mji umejaa foleni all the way!
 
ila hii barabara ilivyo sasa hivi nashauri watumiaji wa bodaboda wawe makini sana lakini pili watu wanaopiga mitungi kama ni watumiaji wa hii njia wafikirie mara mbili yani ni bora wanywe karibu na home kuliko kunywa sinza alafu anakaa kibaha, tatu na mwisho ni wavukaji wa hii barabara na hasa hao wanaopiga vyombo wawe makini sana.
... pale stendi za Mbezi (upande mmoja ya daladala na upande wa pili ya Magufuli) pana daraja la waenda kwa miguu ila hakuna anayetaka kulitumia - sio watato, vijana, akina mama, wala wazee! Always wanalazimisha magari yasimame ili wao wawahi kwanza! Ajabu sana.
 
... pale stendi za Mbezi (upande mmoja ya daladala na upande wa pili ya Magufuli) pana daraja la waenda kwa miguu ila hakuna anayetaka kulitumia - sio watato, vijana, akina mama, wala wazee! Always wanalazimisha magari yasimame ili wao wawahi kwanza! Ajabu sana.
alafu tatizo likitokea wanalaumiwa madereva, ila sasa wahandisi nao waweke madaraja rafiki kama manzese na buguruni unavuka kwa mda mfupi, hakuna daraja linatia uvivu kama daraja la kimara hadi uvule upande wa pili ni kama umetembea km moja.
 
Hii mada inakuja kwa mara nyingine humu, tuache siasa tuongee ukweli ili marekebisho yawe ya kisayansi sio kisiasa, Ile ni freeway, pedestrians, bodaboda hawatakiwi kuwepo pale, pia tulete wataalamu watufanyie uchunguzi kama ile barabara imejengwa kwa kuangalia usalama wa watumiaji, kuwekwe pedestrians traffic lights 🚥 ambazo zitatumiwa na binadamu wanaotaka kukatiza ile freeway, kujengwe fixed speed cameras to control speed ya magari, na pia tuweke camera's za kurekodi muda ambao gari ina safiri kutoka point A to B,overspending iwe ni fine kubwa(sio spot fine)ila irekodiwe na kumbukumbu za driver, taa za barabarani pale hazifanyi kazi, tuziweke hizi ili visibility iwe nzuri, tuta zote zile futilia mbali ni usumbufu tu
 
alafu tatizo likitokea wanalaumiwa madereva, ila sasa wahandisi nao waweke madaraja rafiki kama manzese na buguruni unavuka kwa mda mfupi, hakuna daraja linatia uvivu kama daraja la kimara hadi uvule upande wa pili ni kama umetembea km moja.
... inaudhi sana! Tatizo wataalamu wetu wanadhani wanajua jamii inachohitaji kuliko jamii yenyewe! Badala yake wanajifungia maofisini na kubuni kwa niaba ya jamii.

Ukiona infrastructure imewekwa pale halafu jamii haitaki kuitumia au nguvu nyingi zinatumika (kwa mfano huo wa daraja la Kimara uliotoa) including kuzungushia uzio wa km.5 ili kulazimisha watumiaji warudi darajani kwa mfano; that's an indicator MLIKOSEA. Funny enough pamoja na makosa ya kila mara (TANROADS) hawabadiliki.
 
Mawazo ni mazuri sema hujatoa mapendekezo nn kifanyike zaidi maana umeishia Wabuni vivuko,ila mm ningependekeza pawepo na matuta,na kibao kinacho onyesha madereva wapunguze speed
elimu zaidi ya mara kwa mara itolewe lakini matuta hapana.

sasa hivi sio tu kutumia TV hata huku kwenye mitandao ya jamii watu wapate elimu.
 
Mawazo ni mazuri sema hujatoa mapendekezo nn kifanyike zaidi maana umeishia Wabuni vivuko,ila mm ningependekeza pawepo na matuta,na kibao kinacho onyesha madereva wapunguze speed
Unajua maana ya high way? Hakuna high way yenye matuta Duniani kote. Jitahidi uwe unaenda nchi za wenzetu uone mambo yakoje barabarani.
 
Naanza kwa kuwasalimia wakuu.. Hapa ntaongelea matukio mawili niliyoyashuhudia kwa macho yangu.. Pia ntaongelea matukio machache niliyoyasikia..

Mwezi mmoja uliopita mida ya saa 11 alfajiri nikiwa napita maeneo ya Mbezi mwisho jirani na stendi ya mabasi ya Magufuli nilishuhudia mwili wa mwanamke ukiwa katikati ya matairi ya nyuma ya Lori( Semi Trailer lenye mzigo) dereva wa Lori hilo akiwa amekimbia na kuacha gari ikiwa imenasa mwili wa mwanamke huyo marehemu..

Siku nne zilizopita tukiwa maeneo ya Kibamba Hospitali muda wa saa nne usiku, Kijana mmoja aliwaaga wenzake kuwa anaenda upande wa pili wa barabara atarudi baada ya muda mfupi.. Alipokuwa akivuka barabara aligongwa na gari ndogo tukishuhudia.. Akapoteza maisha palepale..

Miezi miwili iliyopita kijana mmoja ambaye alikuwa katibu wa vijana wa CCM aligongwa akiwa kwenye pikipiki maeneo ya Luguruni na kupoteza maisha palepale..

Miezi kama mitatu iliyopita mama mmoja akiwa anavuka barabara maeneo ya Kibamba CCM aligongwa na Lori(Semi Trailer) na kupoteza maisha palepale..

Sasa nachojiuliza.. TUTASUBIRI MPAKA AFE NANI NDIO TUCHUKUE HATUA..?? Matukio ni mengi sana. Watu wanakufa kwa sababu ya ajali za barabarani.. Wahusika wapo wapi..?? Tukumbuke kuwa barabara hii ni Hi way inayopita kwenye makazi ya watu. Huyu mwananchi anayetumia barabara hii tunamlinda vipi kama watu wanakufa kwa kugongwa kwenye Zebra Crossings..??

USHAURI WANGU KWA TANROADS..
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.. Vivuko hivi vitawasaidia waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, na hata waendesha bodaboda kuvuka barabara hii bila kuathiri madereva wa magari.. Na nina imani kuwa tutapunguza vifo vitokanavyo na ajali ka kiasi kikubwa sana..
NAOMBA KUWAKILISHA KWA HESHIMA NA TAADHIMA..
usiku ndio inaua sana kwa kuwa hakuna taa ni giza njia nzima aibu kweli kwa serikali hii! au kuua kwao ndio u freemason unakamilika?
 
Sikuhizi kuna na tochi matrafiki wanapiga magari ingawa Kwa muda wa jioni ni hatari zaidi hasa kwenye zebra.
Huku mitaa yetu ya mbagala tunasubiri mwendokasi iishe maana kama ajali huku Ndiyo itakuwa balaa
 
Back
Top Bottom