Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

USHAURI WANGU KWA TANROADS
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.

Pia pembezo kuwepo njia za waenda kwa miguu kama zilivyo ktk barabara za Mandela express way Ubungo mpaka bandarini pia kama ilivyo barabara za Nyerere Road kwenda Airport ya JNIA DSM hata barabara ya Morogoro kuanzia Kisutu, Fire, Magomeni hadi Ubungo zote zipo jijini Dar es Salaam na zimejengwa huku kuna njia za waendao kwa miguu kwa usalama wao na kuondoa vurugu za magari na waendao kwa miguu kuwepo.


Ni jambo la kushangaza barabara zinazojengwa sasa za 'Magufuli' kukosa njia za waendao kwa miguu pande zote mbili kama vile barabara hizo zinapita porini kusipokuwa na makaazi ya watu.


BARABARA YA ZAMANI YENYE USALAMA :
Barabara ya Nyerere Road kutoka Lumumba mpaka Airport ya Julius Nyerere ikiwa na njia za waenda kwa miguu pia service road pembezoni



Barabara ya new bagamoyo jijini Dar es Salaam iliyo na sehemu za wapita miguu pande zote za barabara

 
Kwa kweli huyu mkandarasi aliyechora hi michoro ya madaraja ya waenda kwa migu hayupo sawa mtu anatembea KM 1 kuvuka barabara yenye urefu wa mita 10 Kuna na lile la moroco pale na lingine naona linajengwa Mbagala

Wakati wangichimba kwa chini ingekuwa ni rafiki kwa watumiaji pia hata gharama ya ujenzi ingekuwa ndogo
Wangechimba chini mvua ikinyesha mpite wapi? Ungezingatia miundombinu ya maji taka hapa Dar usingeongea kupinga wajenzi na idea ile. Ukitaka ukwepe hayo tiyari unaingia gharama vilevile. Ukijenga kupitia chini maintenance inakuwa kubwa naamini hivyo
 
Naanza kwa kuwasalimia wakuu. Hapa ntaongelea matukio mawili niliyoyashuhudia kwa macho yangu.. Pia ntaongelea matukio machache niliyoyasikia.

Mwezi mmoja uliopita mida ya saa 11 alfajiri nikiwa napita maeneo ya Mbezi mwisho jirani na stendi ya mabasi ya Magufuli nilishuhudia mwili wa mwanamke ukiwa katikati ya matairi ya nyuma ya Lori( Semi Trailer lenye mzigo) dereva wa Lori hilo akiwa amekimbia na kuacha gari ikiwa imenasa mwili wa mwanamke huyo marehemu.

Siku nne zilizopita tukiwa maeneo ya Kibamba Hospitali muda wa saa nne usiku, Kijana mmoja aliwaaga wenzake kuwa anaenda upande wa pili wa barabara atarudi baada ya muda mfupi.. Alipokuwa akivuka barabara aligongwa na gari ndogo tukishuhudia. Akapoteza maisha palepale.

Miezi miwili iliyopita kijana mmoja ambaye alikuwa katibu wa vijana wa CCM aligongwa akiwa kwenye pikipiki maeneo ya Luguruni na kupoteza maisha palepale.

Miezi kama mitatu iliyopita mama mmoja akiwa anavuka barabara maeneo ya Kibamba CCM aligongwa na Lori(Semi Trailer) na kupoteza maisha palepale.

Sasa nachojiuliza.. TUTASUBIRI MPAKA AFE NANI NDIO TUCHUKUE HATUA..?? Matukio ni mengi sana. Watu wanakufa kwa sababu ya ajali za barabarani. Wahusika wapo wapi? Tukumbuke kuwa barabara hii ni Hi way inayopita kwenye makazi ya watu. Huyu mwananchi anayetumia barabara hii tunamlinda vipi kama watu wanakufa kwa kugongwa kwenye Zebra Crossings?

USHAURI WANGU KWA TANROADS
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.

Vivuko hivi vitawasaidia waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, na hata waendesha bodaboda kuvuka barabara hii bila kuathiri madereva wa magari. Na nina imani kuwa tutapunguza vifo vitokanavyo na ajali ka kiasi kikubwa sana.

NAOMBA KUWAKILISHA KWA HESHIMA NA TAADHIMA.
Hapo ndio utaonekana umuhimu wa kuwepo njia mbadala yenye Road toll, ambayo huko nyuma NSSF kupitia Dau walipeleka mapendekezo serilikali ikakataa, High way huwa kuna speed zake na ni hatari sana wakati mwingine hata anaendesha mwendo wa Pole Pole anakuwa hatarini
 
Kivuko kikubwa cha watu kipo pale Mbezi mwisho, kwanini wasipite kwenye kivuko? Sio kila kitu kulaumu serikali, watu wengine wabishi sana..

Na dunia nzima, hakuna High way yenye matuta, hiyi itakuwa kifo kwa watu na magari mengi mno, haiwezekani kabisa kabisa highway kuweka tuta, utaua watu kwa ajali kila siku, sbb gari zitaua balaa, high haiwezekani kuweka matuta na haipo kokote kule, that is most dangerous.

Watu waache kiburi na ubishi, watumie kivuko cha miguu kikubwa na kizuri kipo pale.
 
Upo sahihi kabisa mkuu.. Kila unapokanyaga mafuta gari inazidi kutulia na kukubali mwendo.. Lakini huyu mwenda kwa miguu anayetumia barabara hii tunamlindaje?? Tukumbuke kuwa ajali nyingi kwenye barabara hii zinatokea kwenye Zebra Crossings.. Kwa hiyo basi tuseme tu kuwa Zebra Crossings kwenye barabara hii hazina msaada kwa waenda kwa miguu..

Zebra cross kwenye highway ni mambo ya zamani na sio solution sahihi. Vivuko vya juu ya chini ya barabara ndio solution sahihi. Tatizo vibaka nao wanapenda hivi vivuko kama manzese darajani enzi hizo.
 
Hiyo ni highway lazima watu wawe makini. Usipokua makini hata barabara za ndani tu utagongwa na kufa
 
Hii mada inakuja kwa mara nyingine humu, tuache siasa tuongee ukweli ili marekebisho yawe ya kisayansi sio kisiasa, Ile ni freeway, pedestrians, bodaboda hawatakiwi kuwepo pale, pia tulete wataalamu watufanyie uchunguzi kama ile barabara imejengwa kwa kuangalia usalama wa watumiaji, kuwekwe pedestrians traffic lights 🚥 ambazo zitatumiwa na binadamu wanaotaka kukatiza ile freeway, kujengwe fixed speed cameras to control speed ya magari, na pia tuweke camera's za kurekodi muda ambao gari ina safiri kutoka point A to B,overspending iwe ni fine kubwa(sio spot fine)ila irekodiwe na kumbukumbu za driver, taa za barabarani pale hazifanyi kazi, tuziweke hizi ili visibility iwe nzuri, tuta zote zile futilia mbali ni usumbufu tu
Walikuja wazungu wanaojenga barabara za Qatar zitakazohudumia world cup! wakasema hiyo barabara inamiss vitu vingi muhimu.
 
... pale stendi za Mbezi (upande mmoja ya daladala na upande wa pili ya Magufuli) pana daraja la waenda kwa miguu ila hakuna anayetaka kulitumia - sio watato, vijana, akina mama, wala wazee! Always wanalazimisha magari yasimame ili wao wawahi kwanza! Ajabu sana.
Mkuu hata mimi nashanga !!! Serikali imejenga daraja kwa waenda kwa miguu lakini hao watu halitumii na wang'ang"ana kuvuka barabarani kupishana na magari.
 
Zebra cross kwenye highway ni mambo ya zamani na sio solution sahihi. Vivuko vya juu ya chini ya barabara ndio solution sahihi. Tatizo vibaka nao wanapenda hivi vivuko kama manzese darajani enzi hizo.
Vibaka sioni kuwa ni tatizo kama tutakabidhi vivuko hivyo kwa serikali ya mtaa husika.. Ni suala la kuwatumia vijana wa ulinzi shirikishi wa eneo husika wenye nidhamu wahakikishe usalama wa vivuko hivyo..
 
Mkuu hata mimi nashanga !!! Serikali imejenga daraja kwa waenda kwa miguu lakini hao watu halitumii na wang'ang"ana kuvuka barabarani kupishana na magari.
Upo sawa katika maeneo yenye vivuko.. Lakini kuna maeneo mengi yasiyo na vivuko.. Tunawasaidiaje watembea kwa miguu na madereva katika maeneo hayo..??
 
Naanza kwa kuwasalimia wakuu. Hapa ntaongelea matukio mawili niliyoyashuhudia kwa macho yangu.. Pia ntaongelea matukio machache niliyoyasikia.

Mwezi mmoja uliopita mida ya saa 11 alfajiri nikiwa napita maeneo ya Mbezi mwisho jirani na stendi ya mabasi ya Magufuli nilishuhudia mwili wa mwanamke ukiwa katikati ya matairi ya nyuma ya Lori( Semi Trailer lenye mzigo) dereva wa Lori hilo akiwa amekimbia na kuacha gari ikiwa imenasa mwili wa mwanamke huyo marehemu.

Siku nne zilizopita tukiwa maeneo ya Kibamba Hospitali muda wa saa nne usiku, Kijana mmoja aliwaaga wenzake kuwa anaenda upande wa pili wa barabara atarudi baada ya muda mfupi.. Alipokuwa akivuka barabara aligongwa na gari ndogo tukishuhudia. Akapoteza maisha palepale.

Miezi miwili iliyopita kijana mmoja ambaye alikuwa katibu wa vijana wa CCM aligongwa akiwa kwenye pikipiki maeneo ya Luguruni na kupoteza maisha palepale.

Miezi kama mitatu iliyopita mama mmoja akiwa anavuka barabara maeneo ya Kibamba CCM aligongwa na Lori(Semi Trailer) na kupoteza maisha palepale.

Sasa nachojiuliza.. TUTASUBIRI MPAKA AFE NANI NDIO TUCHUKUE HATUA..?? Matukio ni mengi sana. Watu wanakufa kwa sababu ya ajali za barabarani. Wahusika wapo wapi? Tukumbuke kuwa barabara hii ni Hi way inayopita kwenye makazi ya watu. Huyu mwananchi anayetumia barabara hii tunamlinda vipi kama watu wanakufa kwa kugongwa kwenye Zebra Crossings?

USHAURI WANGU KWA TANROADS
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.

Vivuko hivi vitawasaidia waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, na hata waendesha bodaboda kuvuka barabara hii bila kuathiri madereva wa magari. Na nina imani kuwa tutapunguza vifo vitokanavyo na ajali ka kiasi kikubwa sana.

NAOMBA KUWAKILISHA KWA HESHIMA NA TAADHIMA.
Wafe tu, wajinga ni wengi sana nchi hii
 
Wapige tu fensi kublock njia kama buguruni au pale ubungo mataa
 
... na hicho ndicho kinachotakiwa na sio kuweka mazebra kila baada ya 25m! Imagine vituo vya mwendokasi; ilitegemewa wasafiri wangekuwa wanaingia na kutoka vituoni through tunnels lakini ujinga uliofanyika ndio kama hivyo ni foleni za magari mwanzo mwisho! Mji umejaa foleni all the way!
Zebra crossing Kwa nchi yetu hatujawah kuheshimiwa..
 
Kwa kweli huyu mkandarasi aliyechora hi michoro ya madaraja ya waenda kwa migu hayupo sawa mtu anatembea KM 1 kuvuka barabara yenye urefu wa mita 10 Kuna na lile la moroco pale na lingine naona linajengwa Mbagala

Wakati wangichimba kwa chini ingekuwa ni rafiki kwa watumiaji pia hata gharama ya ujenzi ingekuwa ndogo
Miundombinu ya Dar es Salaam haifai kuchimba chini kujenga vivuko vya barabara hususani kipindi cha mvua.
 
Kuna mtu aligongwa pale mbezi mwisho junction ya Goba. truck lilimsaga na nyama nyama zimetapakaa..wakati napita alfajili saa kumi na moja .yaani siku yangu nzima ilivurugika kuona kifo kile.. hiyo barabara ni hatari Sana ..vifo ni vingi Sana hicho kipande

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom