Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

Barabara ya Kimara mpaka Kibaha itazamwe upya, vifo vya watu kutokana na kugongwa na magari vimekuwa vingi sana

ila hii barabara ilivyo sasa hivi nashauri watumiaji wa bodaboda wawe makini sana lakini pili watu wanaopiga mitungi kama ni watumiaji wa hii njia wafikirie mara mbili yani ni bora wanywe karibu na home kuliko kunywa sinza alafu anakaa kibaha, tatu na mwisho ni wavukaji wa hii barabara na hasa hao wanaopiga vyombo wawe makini sana.
Mmh, kwa mpiga vyombo, ni wachache sana wanaofikilia itakuaje, baada ya kulewa.
Umenikumbusha bibi mmoja, mlemavu wa macho haoni kabisa, kabla barabara haijajengwa, alikua anatoka mbezi kibanda cha mkaa, anakuja kulewa mbezi karibu na stendi ya Daladala, upande wa kulia ukitokea mjini.

Pale palikua panaitwa Dodoma, kabla ya bomoa bomoa ukiingia pale, unajikuta sawa uko uwanja wa fisi tu.
Tukirudi kwa yule bibi, wakati wa kuja, hufuatana na mtu, ambae humuongoza kwa kushika fimbo yake, ila akilewa sasa, hataki kuongozwa na mtu, akijaribu mtu asiye mjua kumpa msaada, humtukana huku ajitapa umeona mimi sijui njia ya nyumbani we mpu.. nini, ila baada ya barabara haonekani, itakua anakunywa karibu karibu.
 
Barabara hiyo ifungwe tu magari yatafute njia nyingine
 
Miundombinu ya Dar es Salaam haifai kuchimba chini kujenga vivuko vya barabara hususani kipindi cha mvua.
Labda sababu ya gharama lakini sio kwamba haifai. Watu wamechimba chini ya mito mikubwa na bahari ndio ishindikane Dar? Sio kweli.
 
ila hii barabara ilivyo sasa hivi nashauri watumiaji wa bodaboda wawe makini sana lakini pili watu wanaopiga mitungi kama ni watumiaji wa hii njia wafikirie mara mbili yani ni bora wanywe karibu na home kuliko kunywa sinza alafu anakaa kibaha, tatu na mwisho ni wavukaji wa hii barabara na hasa hao wanaopiga vyombo wawe makini sana.
Utaendeshaje gari ukiwa umelewa? Hata kunywa tu pombe na kuendesha siyo sahihi. Kweli kabisa haingii akilini. Na hii ndo chanzo kikubwa cha ajali zembe. Unakuta watu wamepaki magari yao Bar.
 
6 lane unawekaje zebra, si kichekesho hicho
Actually ni 8 lanes roughly 40m. Kusubiri waenda kwa miguu wavuke umbali huo ni foleni zisizo na sababu. Kuna mawili, zebra ziwe penye taa tu ili waenda kwa miguu wavuke sambamba na magari.

Zebra ambazo haziko penye taa ufumbuzi mwingine utafutwe hususan madaraja ya juu and they shouldn't be complicated daraja's like Kimara's but simple ones. India wamefanya hivyo and it is so safe. Unajua umati wa India? Dar ni kitongoji!
 
Mkuu hata mimi nashanga !!! Serikali imejenga daraja kwa waenda kwa miguu lakini hao watu halitumii na wang'ang"ana kuvuka barabarani kupishana na magari.
... wanakera sana; always daraja liko tupu ila chini ya daraja hilo hilo kuna foleni kubwa ya waenda kwa miguu na magari na watu wanagongwa hapo hapo chini ya daraja. Kuna ujinga sana nchi hii.
 
USHAURI WANGU KWA TANROADS
Wakandarasi wa TANROADS wabuni vivuko vya kupita chini ya barabara ambavyo ni nafuu kuvijenga ikilinganishwa na madaraja ya kupita juu ambayo yana gharama kubwa zaidi.
Kwa ilipofikia hiyo barabara ni bora wajenge vivuko vya juu kwa kutumia chuma kigumu kisichopata kutu, kuchimba madaraja uvunguni ni gharama zaidi
 
Walikuja wazungu wanaojenga barabara za Qatar zitakazohudumia world cup! wakasema hiyo barabara inamiss vitu vingi muhimu.
It's obvious wala haihitaji mzungu aseme. Fikiria zebra za pale Manzese, Tip Top, Mahakama ya Ndizi, Kimara Korogwe, n.k. tena both ends za vituo vya mwendokasi! Miundombinu haiko sawa.
 
Hii mada inakuja kwa mara nyingine humu, tuache siasa tuongee ukweli ili marekebisho yawe ya kisayansi sio kisiasa, Ile ni freeway, pedestrians, bodaboda hawatakiwi kuwepo pale, pia tulete wataalamu watufanyie uchunguzi kama ile barabara imejengwa kwa kuangalia usalama wa watumiaji, kuwekwe pedestrians traffic lights 🚥 ambazo zitatumiwa na binadamu wanaotaka kukatiza ile freeway, kujengwe fixed speed cameras to control speed ya magari, na pia tuweke camera's za kurekodi muda ambao gari ina safiri kutoka point A to B,overspending iwe ni fine kubwa(sio spot fine)ila irekodiwe na kumbukumbu za driver, taa za barabarani pale hazifanyi kazi, tuziweke hizi ili visibility iwe nzuri, tuta zote zile futilia mbali ni usumbufu tu

Na ndicho wanachotaka; kuweka matuta.

Nilifanya utafiti mdogo wa muda wa safari kwa daladala:

Mbezi-Maili Moja= dk 20

Maili Moja-Vigwaza=dk 40

Barabara hii ina tija na ni nzuri sana ila shida ipo kwa Wabongo wanaojiita wazoefu wa mjini kutaka kutumia hii njia kama zamani na watakavyo.

Ni kweli ajali zipo, lakini ni shida ya waenda kwa miguu. Kimsingi, mtu haruhusiwi kuvuka kabla gari haijasimama hata kama ni kwenye zebra.

Dereva anatakiwa apunguze mwendo tu pindi afikapo kwenye zebra na halazimiki kusimama iwapo hajamuona mtu anavuka.

Anayevuka ndiye mwenye jukumu la kuhakikisha kwamba kwanza ameliona gari na pia dereva amemuona na gari imesimama ndipo avuke.

.................
BARABARA NI ENEO HATARI KABISA, MWENDA KWA MIGUU HUTAKIWI KUCHEZACHEZA AU KUENENDA KIZEMBE KIZEMBE KWENYE ZEBRA AU KANDONI MWA BARABARA.
1. Acha kuvuka barabara ukiwa unaongea na simu
2. Acha kuvuka barabara ukiwa unapiga stori na mwenzako
3. Acha kuvuka barabara ukiwa na headphone masikioni
4. Kwenye kivuko cha waenda kwa miguu simama wima huku ukionesha nia ya kuvuka barabara.
5. Angalia magari barabarani kushoto, kulia na sehemu zote kukuzunguka, na sikiliza. Kwa kufanya hivi dereva atakuona na hivyo kusimama kukuruhusu uvuke.
6. Usitumie eneo la Zebra kama kijiwe cha kupigia stori, kuuza bidhaa, au kuongea na simu.
7. Usitegemee sana uwepo wa Polisi kumwadhibu dereva kwani dereva ataadhibiwa lakini wewe utakuwa umepoteza viungo vyako ukapata ulemavu wa kudumu au ukapata kifo, wakati dereva atalipa 50,000 na kuachiwa.
Zingatia Wajibu wa Mwenda kwa Miguu kwenye Kivuko cha Waenda kwa Miguu Uliowekwa na Sheria
1. Kif.65(6) kinamtaka mwenda kwa miguu atumie kivuko cha waenda kwa miguu anapotaka kuvuka barabara ikiwa kivuko hicho kipo. Lakini pili, anapovuka avuke kwa umakini (exercise due care);
2. Kifungu cha 65(7) anapotumia kivuko chenye alama na michoro basi anawajibika kuzingatia yafuatayo:
(a) Kutii maelekezo yaliyotolewa na ishara (mf.taa)
(b) Asisimame katikati ya barabara ikiwa taa zimeruhusu au askari ameruhusu gari zipite.
(c) Asiweke mguu barabarani (shall not step onto the carriage way) kuanza kuvuka bila kuzingatia umbali na spidi ya magari yanayokuja.
3. Kifungu cha 65(8) kinasema mwenda kwa miguu hatakiwi kuenenda barabarani katika namna ambayo ni hatari au inaweza kuwa chanzo cha hatari kwake yeye au kwa mtumiaji mwingine wa barabara.
KUMBUKA kwamba kifungu cha 64A kinamtaka kila mtumiaji wa barabara azingatie umakini na utimamu na wakati wote achukue tahadhari kutohatarisha au kuzuia magari au kuhatarisha watumiaji wengine wa barabara.
DAIMA TAMBUA kuwa barabara ni eneo hatari ambalo chochote kinaweza kutokea:
1. Gari inaweza kuacha njia na kukufuata ulipo hata kama upo nje kabisa ya barabara;
2. Gari inaweza kufeli breki kwenye zebra na bado ukagonjwa na ndio maana sheria inataka kabla hujaanza kuvuka uzingatie umbali na spidi ya gari inayotakiwa kusimama kukupisha
Heshimu barabara, Nenda salama barabarani
RSA Tanzania.
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote.


..................
Fungo Augustus ▶ ‎RSA TANZANIA(Road Safety Ambassadors)

JE NI WAKATI GANI NISIMAME KWENYE ZEBRA CROSSINGS AU JE NI AMRI KUSIMAMA KWENYE ZEBRA HATA KAMA HAKUNA MWENDA KWA MIGUU ANAYEVUKA? Sheria inasemaje?
Sheria ya usalama barabarani kifungu cha 65 kinahusu vivuko vya waenda kwa miguu, yaani pedestrian crossings.
Kifungu cha 65(1) kinamtaka mhandisi mkuu kusimika alama za vivuko vya waenda kwa miguu mahali panapofaa barabarani.
Kifungu cha 65(2) kinatamka kwamba mahali popote ambapo alama itakuwa imewekwa itachukuliwa kuwa imewekwa kihalali na itakuwa halali isipokuwa kama itakanushwa au kuthibitishwa vinginevyo.
Kifungu cha 65(6) kinamtaka kila anayetumia kivuko cha waenda kwa miguu kufanya hivyo kwa tahadhari kubwa na atumia kivuko hicho kuvuka barabara. Aidha kifungu cha 65(7) kinamtaka mtumiaji kivuko huyo kutokanyaga barabara ili avuke bila kuzingatia umbali na spidi ya magari yanayokuja
Kifungu cha 65(10) kinasema itakapotokea mtembea kwa miguu anatumia au anataka kutumia kivuko cha waenda kwa miguu, dereva wa gari atasimama kabla ya kivuko hicho ambacho hakiongozwi na taa za barabarani, ishara za barabarani au askari. [Hivi vivuko vinavyokuwa vimechorwa barabarani kwa mistari ya pundamilia ambapo mtu anavuka bila usimamizi wa askari au maelekezo ya taa]. Dereva ataendelea tu na safari ikiwa atajiridhisha kuwa hakuna mtembea kwa miguu anayetumia(anayevuka) au anakusudia kuvuka barabara.
KWA MINAJILI YA REJEA KIFUNGU CHENYEWE CHA 65(10) Kinasema hivi katika lugha yake asili "(10) Where a pedestrian is using or is about to use a pedestrian crossing, a driver of a vehicle shall stop before a pedestrian crossing on a carriageway which is not regulated by traffic lights, traffic signals or by a police officer."
HIVYO BASI, JIBU NI KWAMBA sio lazima dereva asimama kwenye kila zebra crossings hata kama hakuna anayevuka, dereva atapunguza mwendo na kuangalia iwapo kuna mtu anavuka au ananuia kuvuka, kama hakuna ataendelea na safari. Kwa hiyo, dereva asimama kwenye eneo kabla ya zebra crossing pale wakati wote ambapo kuna mtu au watu wanavuka au wanakusudia kuvuka.
Ni matumaini yangu tumeelewana. Mwelimishe na mwenzio.
RSAadmin1
RSA TANZANIA
USALAMA BARABARANI NI JUKUMU LETU SOTE.
ZINGATIA: Maelezo haya hayahusishi zile ZEBRA crossings ambazo kabla yake kunakuwa na mchoro chini au alama ya amri iliyoandikwa kabisaaa STOP. Hapa utatakiwa kusimama hata kama hakuna anayevuka.
 
Kivuko kikubwa cha watu kipo pale Mbezi mwisho, kwanini wasipite kwenye kivuko? Sio kila kitu kulaumu serikali, watu wengine wabishi sana..

Na dunia nzima, hakuna High way yenye matuta, hiyi itakuwa kifo kwa watu na magari mengi mno, haiwezekani kabisa kabisa highway kuweka tuta, utaua watu kwa ajali kila siku, sbb gari zitaua balaa, high haiwezekani kuweka matuta na haipo kokote kule, that is most dangerous.

Watu waache kiburi na ubishi, watumie kivuko cha miguu kikubwa na kizuri kipo pale.
Sasa mtu yupo Kibamba Kwa mangi unataka arudi mbezi mwisho au chama kuvuka , mnafikr Kwa kutumia nini , na hata pale chama like daraja sio rafiki , sababu sioni kama lina lane ya waenda Kwa miguu , ... Kama wanataka madaraja ya waenda Kwa miguu waweke kila kituo cha dalala , mwisho wa sku yataonekana kama uchafu , underground tunnel ndo suluhisho pekee , tatizo ni too late , hzo zingeenda sambamba na ujenzi ili kupunguza Gharama , na assessment ya water flow in case mvua ikanyesha ingefanyika mapema , Kwa sasa kuanza kuchimbua italeta mkanganyiko mana road tayar ishajengwa, changamoto ya vivuko vya chini ni uwepo wa vibaka , Ila ni bora na zinafanya barabara iwe ya kuvutia bila uwepo wa hayo manundu ya madaraja ya juu , highway ni high speed huwez kuepuka ,
 
... pale stendi za Mbezi (upande mmoja ya daladala na upande wa pili ya Magufuli) pana daraja la waenda kwa miguu ila hakuna anayetaka kulitumia - sio watato, vijana, akina mama, wala wazee! Always wanalazimisha magari yasimame ili wao wawahi kwanza! Ajabu sana.
na hiyo ndio shida yetu, ubishi na ujuaji mwingi matokeo yake tunakufa kwa kwa ujinga wetu wenyewe.

Sehemu maalumu za kuvukia zimejengwa lakini unakuta mijitu inag'ang'ana kuvuka kwenye mapipa/wavu upumbavu kabisa!!

hata ufanyaje kwa akili za raia wetu lazima watagongwa na kufa kila siku hadi pale kila mmoja atakapo amua kubadilika na kustaarabika.
 
Sasa mtu yupo Kibamba Kwa mangi unataka arudi mbezi mwisho au chama kuvuka , mnafikr Kwa kutumia nini , na hata pale chama like daraja sio rafiki , sababu sioni kama lina lane ya waenda Kwa miguu , ... Kama wanataka madaraja ya waenda Kwa miguu waweke kila kituo cha dalala , mwisho wa sku yataonekana kama uchafu , underground tunnel ndo suluhisho pekee , tatizo ni too late , hzo zingeenda sambamba na ujenzi ili kupunguza Gharama , na assessment ya water flow in case mvua ikanyesha ingefanyika mapema , Kwa sasa kuanza kuchimbua italeta mkanganyiko mana road tayar ishajengwa, changamoto ya vivuko vya chini ni uwepo wa vibaka , Ila ni bora na zinafanya barabara iwe ya kuvutia bila uwepo wa hayo manundu ya madaraja ya juu , highway ni high speed huwez kuepuka ,
If I were to choose between madaraja ya juu kuonekana kama uchafu Vs kuokoa maisha na kuondoa foleni I would choose the former unless there is a better and feasible option.
 
RSA Tanzania

BARABARA NI ENEO HATARI KABISA, MWENDA KWA MIGUU HUTAKIWI KUCHEZACHEZA AU KUENENDA KIZEMBE KIZEMBE KWENYE ZEBRA AU KANDONI MWA BARABARA.
1. Acha kuvuka barabara ukiwa unaongea na simu
2. Acha kuvuka barabara ukiwa unapiga stori na mwenzako
3. Acha kuvuka barabara ukiwa na headphone masikioni
4. Kwenye kivuko cha waenda kwa miguu simama wima huku ukionesha nia ya kuvuka barabara.
5. Angalia magari barabarani kushoto, kulia na sehemu zote kukuzunguka, na sikiliza. Kwa kufanya hivi dereva atakuona na hivyo kusimama kukuruhusu uvuke.
6. Usitumie eneo la Zebra kama kijiwe cha kupigia stori, kuuza bidhaa, au kuongea na simu.
7. Usitegemee sana uwepo wa Polisi kumwadhibu dereva kwani dereva ataadhibiwa lakini wewe utakuwa umepoteza viungo vyako ukapata ulemavu wa kudumu au ukapata kifo, wakati dereva atalipa 50,000 na kuachiwa.
Zingatia Wajibu wa Mwenda kwa Miguu kwenye Kivuko cha Waenda kwa Miguu Uliowekwa na Sheria
1. Kif.65(6) kinamtaka mwenda kwa miguu atumie kivuko cha waenda kwa miguu anapotaka kuvuka barabara ikiwa kivuko hicho kipo. Lakini pili, anapovuka avuke kwa umakini (exercise due care);
2. Kifungu cha 65(7) anapotumia kivuko chenye alama na michoro basi anawajibika kuzingatia yafuatayo:
(a) Kutii maelekezo yaliyotolewa na ishara (mf.taa)
(b) Asisimame katikati ya barabara ikiwa taa zimeruhusu au askari ameruhusu gari zipite.
(c) Asiweke mguu barabarani (shall not step onto the carriage way) kuanza kuvuka bila kuzingatia umbali na spidi ya magari yanayokuja.
3. Kifungu cha 65(8) kinasema mwenda kwa miguu hatakiwi kuenenda barabarani katika namna ambayo ni hatari au inaweza kuwa chanzo cha hatari kwake yeye au kwa mtumiaji mwingine wa barabara.
KUMBUKA kwamba kifungu cha 64A kinamtaka kila mtumiaji wa barabara azingatie umakini na utimamu na wakati wote achukue tahadhari kutohatarisha au kuzuia magari au kuhatarisha watumiaji wengine wa barabara.

DAIMA TAMBUA kuwa barabara ni eneo hatari ambalo chochote kinaweza kutokea:
1. Gari inaweza kuacha njia na kukufuata ulipo hata kama upo nje kabisa ya barabara;
2. Gari inaweza kufeli breki kwenye zebra na bado ukagonjwa na ndio maana sheria inataka kabla hujaanza kuvuka uzingatie umbali na spidi ya gari inayotakiwa kusimama kukupisha
Heshimu barabara, Nenda salama barabarani

RSA Tanzania.
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote.
 
Fungo Augustus ▶ ‎RSA TANZANIA(Road Safety Ambassadors)

JE NI WAKATI GANI NISIMAME KWENYE ZEBRA CROSSINGS AU JE NI AMRI KUSIMAMA KWENYE ZEBRA HATA KAMA HAKUNA MWENDA KWA MIGUU ANAYEVUKA? Sheria inasemaje?
Sheria ya usalama barabarani kifungu cha 65 kinahusu vivuko vya waenda kwa miguu, yaani pedestrian crossings.
Kifungu cha 65(1) kinamtaka mhandisi mkuu kusimika alama za vivuko vya waenda kwa miguu mahali panapofaa barabarani.
Kifungu cha 65(2) kinatamka kwamba mahali popote ambapo alama itakuwa imewekwa itachukuliwa kuwa imewekwa kihalali na itakuwa halali isipokuwa kama itakanushwa au kuthibitishwa vinginevyo.
Kifungu cha 65(6) kinamtaka kila anayetumia kivuko cha waenda kwa miguu kufanya hivyo kwa tahadhari kubwa na atumia kivuko hicho kuvuka barabara. Aidha kifungu cha 65(7) kinamtaka mtumiaji kivuko huyo kutokanyaga barabara ili avuke bila kuzingatia umbali na spidi ya magari yanayokuja
Kifungu cha 65(10) kinasema itakapotokea mtembea kwa miguu anatumia au anataka kutumia kivuko cha waenda kwa miguu, dereva wa gari atasimama kabla ya kivuko hicho ambacho hakiongozwi na taa za barabarani, ishara za barabarani au askari. [Hivi vivuko vinavyokuwa vimechorwa barabarani kwa mistari ya pundamilia ambapo mtu anavuka bila usimamizi wa askari au maelekezo ya taa]. Dereva ataendelea tu na safari ikiwa atajiridhisha kuwa hakuna mtembea kwa miguu anayetumia(anayevuka) au anakusudia kuvuka barabara.
KWA MINAJILI YA REJEA KIFUNGU CHENYEWE CHA 65(10) Kinasema hivi katika lugha yake asili "(10) Where a pedestrian is using or is about to use a pedestrian crossing, a driver of a vehicle shall stop before a pedestrian crossing on a carriageway which is not regulated by traffic lights, traffic signals or by a police officer."
HIVYO BASI, JIBU NI KWAMBA sio lazima dereva asimama kwenye kila zebra crossings hata kama hakuna anayevuka, dereva atapunguza mwendo na kuangalia iwapo kuna mtu anavuka au ananuia kuvuka, kama hakuna ataendelea na safari. Kwa hiyo, dereva asimama kwenye eneo kabla ya zebra crossing pale wakati wote ambapo kuna mtu au watu wanavuka au wanakusudia kuvuka.
Ni matumaini yangu tumeelewana. Mwelimishe na mwenzio.
RSAadmin1
RSA TANZANIA
USALAMA BARABARANI NI JUKUMU LETU SOTE.
ZINGATIA: Maelezo haya hayahusishi zile ZEBRA crossings ambazo kabla yake kunakuwa na mchoro chini au alama ya amri iliyoandikwa kabisaaa STOP. Hapa utatakiwa kusimama hata kama hakuna anayevuka.
 
Back
Top Bottom