KERO Barabara ya Mbagala hadi Kongowe ni nyembamba, ina mashimo na inasababisha foleni mara nyingi

KERO Barabara ya Mbagala hadi Kongowe ni nyembamba, ina mashimo na inasababisha foleni mara nyingi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
photo_2024-12-19_10-31-53.jpg

photo_2024-12-19_10-30-25.jpg
Nimetoka Lindi leo kabla tu ya mchana na basi letu limeenda mwendo mzuri tu! Hata Vikindu foleni haikuwepo.

Saa kumi na nusu ndo tunaikuta foleni ya Kongowe, imeanzia nyuma ya shule ya St Matthews. Hiyo foleni imechukua dk kama 45 hadi kufika makutano ya Kongowe kwenda Kigamboni.

Kwenda Kigamboni hakupitiki maana kuna daladala kama saba zimesimama hadi katikati mwa barabara, zinapakia na kushusha abiria.

Na toka Kigamboni kuna trela inashindwa kuingia barabara kuu, maana imezongwa na bajaji na gari ndogo zinazo jichomeka.
photo_2024-12-19_10-30-22.jpg

photo_2024-12-19_10-30-14.jpg
Sie haoo tukaenda barabara ya Mbagala na huko ndo tukakuta foleni ya kufa mtu! Kale kadaraja kabla ya kupanda kilima cha kuingia Mbagala kamezongwa.

Pale kwenye kadaraja magari zaidi ya 20 kila moja inajaribu kuingiza pua ili ipite.

Hapo foleni ya saa moja na nusu nzimaa na kagiza kanaanza kuingia, na ni saa moja kasoro.

Tumefika Mbagala ndo tunakuta ile barabara ya 2 lanes kwenda mjini, sasa ni half lane. Lane moja nzima ni machinga, nusu lane ni daladala zinazopakia abiria.

Hapo ni kilometa nzima na zaidi. Na foleni hapo ni nusu saa na natazama saa yangu ni saa moja na nusu, tayari ni masaa matatu toka Kongowe.

Hadi kushuka basi kuingia gari dogo Mwenge nafika saa tatu!

Nikifikiria, safari toka Lindi hadi Kongowe masaa manne na nusu, lakini toka Kongowe hadi mjini ni masaa matatu au manne.

Halafu tunasema tunainua mikoa ya kusini, Lindi na Mtwara, we are joking!

Kwa ufupi, Barabara za kutoka Mbagala - Kongowe kwakweli ipo katika hali mbaya, barabara ni finyu (njia moja) na imejaa mashimo jambo ambalo linapelekea uwepo wa foleni.

Ikizingatiwa njia hiyo ni njia kuu ambayo inaunganisha Mkoa wa Dar na Mikoa mingine ya Kusini, lakini pia ni njia inayotegemewa kupitisha malighafi na bidhaa za viwanda kutoka kwenye viwanda vilivyopo ukanda wa Pwani hususani Wilaya ya Mkuranga.
photo_2024-12-19_10-30-04.jpg

photo_2024-12-19_10-30-09.jpg
Pia soma ~ Meneja TANROADS aelezea ulipofikia mchakato wa Ujenzi wa Barabara ya Mbagala Mzinga - Kongowe - Kisemvule
 
Jibu langu rahisi tu CCM wanataka watu wajinga inakuwaje Barabara yenye viwanda vingi Tanzania Ndio njia mbovu kuliko zote?Yaani miaka mitatu mfululizo mkuranga Ndio inaongoza kukusanya Kodi lakini Barabara ni mbovu ???CCM ni watu hatariiiiiii sana
 
Hii nchi kuna upumbavu mwingi sana. Serikali inatakiwa itanue hio njia. Lakini madereva nao wakiacha upumbavu hio foleni haiwezi kuwa ya masaa matatu.
 
Saa kumi na nusu ndo tunaikuta foleni ya Kongowe, imeanzia nyuma ya shule ya St Matthews.
Hiyo foleni imechukua dk kama 45 hadi kufika makutano ya Kongowe kwenda Kigamboni.

Kwenda Kigamboni hakupitiki maana kuna daladala kama saba zimesimama hadi katikati mwa barabara, zinapakia na kushusha abiria.
Na toka Kigamboni kuna trela inashindwa kuingia barabara kuu, maana imezongwa na bajaji na gari ndogo zinazo jichomeka.
Dawa ni njia 6 au 8
 
Kwanza hiyo barabara imeua watu sana ,hapo mwezi haupiti bila lory kudondoka na kua ama bajaji au bodaboda.
kuna mteremko mkaili wenye kona hapo dereva wengi wa lori wanaziangusha sana.

Kitu cha kushangaza hiyo ni barabara anayopita Waziri Mkuu,Tamisemi na Ujenzi ,nikajua watakuwa wa kwanza kupigia debe maana inaunganisha na maeneo yao ya kimkakati (Viwanda na mazao kutoka kusini)

Nilinusurika kufa hapo baada ya kupigwa na lori kwa nyuma lilipofail break
 
Nimetoka Lindi leo kabla tu ya mchana na basi letu limeenda mwendo mzuri tu! Hata Vikindu foleni haikuwepo.

Saa kumi na nusu ndo tunaikuta foleni ya Kongowe, imeanzia nyuma ya shule ya St Matthews. Hiyo foleni imechukua dk kama 45 hadi kufika makutano ya Kongowe kwenda Kigamboni.

Kwenda Kigamboni hakupitiki maana kuna daladala kama saba zimesimama hadi katikati mwa barabara, zinapakia na kushusha abiria.

Na toka Kigamboni kuna trela inashindwa kuingia barabara kuu, maana imezongwa na bajaji na gari ndogo zinazo jichomeka.
Sie haoo tukaenda barabara ya Mbagala na huko ndo tukakuta foleni ya kufa mtu! Kale kadaraja kabla ya kupanda kilima cha kuingia Mbagala kamezongwa.

Pale kwenye kadaraja magari zaidi ya 20 kila moja inajaribu kuingiza pua ili ipite.

Hapo foleni ya saa moja na nusu nzimaa na kagiza kanaanza kuingia, na ni saa moja kasoro.

Tumefika Mbagala ndo tunakuta ile barabara ya 2 lanes kwenda mjini, sasa ni half lane. Lane moja nzima ni machinga, nusu lane ni daladala zinazopakia abiria.

Hapo ni kilometa nzima na zaidi. Na foleni hapo ni nusu saa na natazama saa yangu ni saa moja na nusu, tayari ni masaa matatu toka Kongowe.

Hadi kushuka basi kuingia gari dogo Mwenge nafika saa tatu!

Nikifikiria, safari toka Lindi hadi Kongowe masaa manne na nusu, lakini toka Kongowe hadi mjini ni masaa matatu au manne.

Halafu tunasema tunainua mikoa ya kusini, Lindi na Mtwara, we are joking!

Kwa ufupi, Barabara za kutoka Mbagala - Kongowe kwakweli ipo katika hali mbaya, barabara ni finyu (njia moja) na imejaa mashimo jambo ambalo linapelekea uwepo wa foleni.

Ikizingatiwa njia hiyo ni njia kuu ambayo inaunganisha Mkoa wa Dar na Mikoa mingine ya Kusini, lakini pia ni njia inayotegemewa kupitisha malighafi na bidhaa za viwanda kutoka kwenye viwanda vilivyopo ukanda wa Pwani hususani Wilaya ya Mkuranga.
Yaani Huko utadhani hakuna RC, hakuna DC, hakuna Mkuruugenzi, Hkauna Polisi wala Traffic.

Is such a barbaric lifestyle
 
Nimetoka Lindi leo kabla tu ya mchana na basi letu limeenda mwendo mzuri tu! Hata Vikindu foleni haikuwepo.

Saa kumi na nusu ndo tunaikuta foleni ya Kongowe, imeanzia nyuma ya shule ya St Matthews. Hiyo foleni imechukua dk kama 45 hadi kufika makutano ya Kongowe kwenda Kigamboni.

Kwenda Kigamboni hakupitiki maana kuna daladala kama saba zimesimama hadi katikati mwa barabara, zinapakia na kushusha abiria.

Na toka Kigamboni kuna trela inashindwa kuingia barabara kuu, maana imezongwa na bajaji na gari ndogo zinazo jichomeka.
Sie haoo tukaenda barabara ya Mbagala na huko ndo tukakuta foleni ya kufa mtu! Kale kadaraja kabla ya kupanda kilima cha kuingia Mbagala kamezongwa.

Pale kwenye kadaraja magari zaidi ya 20 kila moja inajaribu kuingiza pua ili ipite.

Hapo foleni ya saa moja na nusu nzimaa na kagiza kanaanza kuingia, na ni saa moja kasoro.

Tumefika Mbagala ndo tunakuta ile barabara ya 2 lanes kwenda mjini, sasa ni half lane. Lane moja nzima ni machinga, nusu lane ni daladala zinazopakia abiria.

Hapo ni kilometa nzima na zaidi. Na foleni hapo ni nusu saa na natazama saa yangu ni saa moja na nusu, tayari ni masaa matatu toka Kongowe.

Hadi kushuka basi kuingia gari dogo Mwenge nafika saa tatu!

Nikifikiria, safari toka Lindi hadi Kongowe masaa manne na nusu, lakini toka Kongowe hadi mjini ni masaa matatu au manne.

Halafu tunasema tunainua mikoa ya kusini, Lindi na Mtwara, we are joking!

Kwa ufupi, Barabara za kutoka Mbagala - Kongowe kwakweli ipo katika hali mbaya, barabara ni finyu (njia moja) na imejaa mashimo jambo ambalo linapelekea uwepo wa foleni.

Ikizingatiwa njia hiyo ni njia kuu ambayo inaunganisha Mkoa wa Dar na Mikoa mingine ya Kusini, lakini pia ni njia inayotegemewa kupitisha malighafi na bidhaa za viwanda kutoka kwenye viwanda vilivyopo ukanda wa Pwani hususani Wilaya ya Mkuranga.
Dawa ni kuhamia Masaki.
 
Kilwa road ni kichefuchefu mpaka mkuranga huko tabú tupu barabara ni finyu sana. Panatakiwa 4 ways.

Mbunge wa huko SASA ni waziri WA ujenzi labda atafanya miujiza
Huyo waziri akipita wote mnawekwa pembeni. Ndani ya hiyo miaka yote hajawahi kukaa hata kwenye taa za barabarani.

Tuondoe misafara ta mawaziri na watendaji wao kuondoa huu ujinga
 
Hii nchi kuna upumbavu mwingi sana. Serikali inatakiwa itanue hio njia. Lakini madereva nao wakiacha upumbavu hio foleni haiwezi kuwa ya masaa matatu.
Unazungumzia foleni ya masaa matatu? Utakuwa una bahati sana, sisi tumezoea likiharibika lorry moja tuu linaloelekea upande wowote foleni yake ni masaa4 na kuendelea hadi trafic waje watunusuru
 
Back
Top Bottom