Barabara ya Njia 4 Kibaha - Morogoro itakuwa na Tozo

Barabara ya Njia 4 Kibaha - Morogoro itakuwa na Tozo

Madini,gesi,utalii kwa viongozi waelevu vinatosha kabisa kuendeshea nchi ila hawa wala keki wa taifa kikubwa wanachofikiria ni kumkwamua mlalahoi ili waendeshe nchi!
Yani nikipewa madaraka nitakuwa Magufuli x 10 yake sicheki na boya. Kazi tu!

Maadui zangu ni wajinga wajinga wezi na mafisadi ndio ntawanyoosha. Hukumu ni shaba tu hamna kingine. Ukikutwa umedokoa hela na ushahidi ukapatikana jua ni shaba moja kwa moja.
 
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Godfrey Kasekenya amesema TANROADS imetangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya njia 4 kutoka Kibaha hadi Morogoro ambayo itajengwa kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construct and Finance (EPC + F).

Kasekenya alisema gharama za ujenzi wake zitatolewa na Serikali au na Sekta Binafsi (PPP) kwa utaratibu wa Jenga, Endesha, Rudisha (BOT).

Na hivyo Sekta Binafsi itajenga barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 205 kwa fedha zake na kuiendesha hadi pale itakaporejesha fedha hizo kupitia Tozo za Magari.

=====================

SERIKALI kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya njia nne kutoka Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro yenye urefu wa kilometa 205.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Godfrey Kasekenya alilieleza bunge jijini Dodoma Jumanne wakati akijibu swali la Mbunge wa Kibaha Mjini, Sylevester Koka (CCM).

Mbunge Koka alitaka kujua serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro.

“Barabara hiyo itajengwa kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construct and Finance (EPC + F),” alisema.

Alisema gharama za ujenzi wake zitatolewa na serikali au na sekta binafsi (PPP) kwa utaratibu wa jenga, endesha, rudisha (BoT).

Katika utaratibu huo, sekta binafsi itajenga barabara hii kwa fedha zake na kuiendesha hadi pale itakaporejesha fedha zake kupitia tozo za magari.

Katika swali la nyongeza, Mbunge Koka alitaka kujua barabara ya Tamko- Mapinga imekuwa ikisuasua kwa muda mrefu na wananchi wa kata za Tangani na Pangani waliopisha ujenzi wa barabara hiyo lini watalipwa fidia.

Pia aliuliza: “Barabara ya zamani ya Dar es Salaam –Morogoro katika eneo la Picha ya Ndege-Mlandizi, imekuwa msaada mkubwa kunapotokea changamoto katika barabara kuu ya ajali magari hupita katika barabara hiyo, je, serikali ipo tayari kurekebisha barabara hiyo ili kuendelea kutumika wakati barabara kuu inapokuwa na changamoto?”

Kasekenya alijibu kwamba ni kweli barabara ya Tamko-Mapinga inasuasua na baadhi ya watu hawakulipwa fidia. Alisema serikali inalifahamu hilo na inalifanyia kazi ili kuhakikisha wananchi wanalipwa na ujenzi wake unakamilika kwa wakati.

Kuhusu barabara ya zamani ya Picha ya Ndege-Mlandizi kufanyiwa maboresho, alisema analichukua hilo kama wizara atazungumza na Tanroads ili kuangalia namna gani wanaweza kuboresha ili kuendelea kuwa msaada wa kukwamua msongamano unapotokea katika barabara kuu.

Chanzo: HABARI LEO
Napinga kwa nguvu zote huu utaahira, tozo tunazokatwa zitumike kujenga hiyo barabara, kufanya hivi ni sawa na kuiuza nchi vipandevipande na kutuuza wanachi utumwani
 
Aliyejenga njia 8 Ubungo - Kibaha yeye hakuona umuhimu wa tozo au nyie ndio mnaijua sana hela?
Kwa mtanzamo wangu naona Sawa Tu kwasababu serikali hawataingiza pesa zao kwenye mradi kitakachofanyika ni kutangaza tender na atakayeshinda atatengeneza barabara na ikikamilika ataanza kutoza pesa ili hela yake irudi(shida itakuja Kwa huyu mzabuni anaweza kupiga pesa Kwa miaka mingi huku akitoza hela nyingi Kwa gari moja)..
Serikali ingekuwa ina Akili timamu wangetia hela wenyewe Tu
 
Tuko razi kulipia Toll kama tunatumia huduma tutalipa Tozo sio hizi Tozo za Mwigulu ambazo ni za zulma tu.

Napinga kwa nguvu zote huu utaahira, tozo tunazokatwa zitumike kujenga hiyo barabara, kufanya hivi ni sawa na kuiuza nchi vipandevipande na kutuuza wanachi utumwani
Hii ni kama style ya wenye nyumba kariakoo yaani unaingia mkataba na mwenye mpunga Kwa miaka 30 anabadilisha nyumba yako na kuwa ghorofa la biashara na baada ya miaka 30 mjengo unarudi kwako...
Acha tuingie Huko Tu kuliko kusubiri tozo zijenge barabara hii
 
Si mlisema kwamba jamaa ni mshamba 😂 mara ooh dikteta. Yule mzee alazwe pema peponi mazuri yake ni mengi kuliko udhaifu wa kibinadamu aliokuwa anasimangwa nao.
Limbukeni, mchunga ng'ombe,poripori.sasa tu niwambie watu wa bush huwa Ni watu wa kazi na hawana shobo na kuwapandishia watanzania gharama za maisha Kama za umeme ama kusaini software kwa 69bilioni yaani kufuatilia umeme ulipokatika nchini.


Watu wa bush huwa Wana Ile feelings ya mtu wa chini. Akifanya maamuzi anamuwaza mama mwenye beseni la ndizi kichwani na mtt mgongoni.
 
Hizi hazijengwi kwa Kodi yetu Basi tusilipe Kodi ili tuwe tunalipia hiyo road sio mbaya.
Mafuta toeni Kodi,sukari,mitumba ,sabuni,mafuta ya kula ,wanataka Vita ipiganwe. Sema huwa naamini hakuna maendeleo bila ya umwagaji wa damu ama sie blacks tuna shida zetu.
Maana hizi Singapore Malaysia China waliwataliwa na hapo miaka ya 60 tulikuwa nao sawa kiuchumi yaani gape Ni negligible mno sema Ni Kama hakuna Ila saivi tunawaomba Msaada. Jitahidi ufanye kizazi chako kiwe cheupe mbona Kama huko Argentina wali whatize waafrika wakaishia.
 
Back
Top Bottom