Barabara za mitaani ndani ya Manispaa ya Morogoro ni miaka mitatu sasa bila matengenezo: Je, TARURA Morogoro Mpo?

wajingawatu

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2013
Posts
2,046
Reaction score
2,453
Barabara za mitaani ndani ya Manispaa ya Morogoro zimeharibika hadi kero. Ndugu zetu wahusika, yaani TARURA, wanavuta mpunga tu na kuotesha vitambi bila kujali wakazi wa Manispaa hi pendwa wanateseka kwa barabara zetu kukosa matengenezo.

Ubovu wa barabara hizi ni wa muda mrefu, yapata miaka mitatu sasa, lakini hakuna lolote lililofanyika kutuondolewa adha hii tuipatayo sisi waadhirika. Au mnataka tuandamane kama ndugu zetu wa Kenya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…