Baraka hutoka kwa Baba; Laana hutoka kwa Mama, utaamua mwenyewe

Baraka hutoka kwa Baba; Laana hutoka kwa Mama, utaamua mwenyewe

Mama hana kitu kingine ambacho anaweza kutoa zaidi ya laana ?

Unawakosea sana kina mama mkuu pengine ulipo soma ndio wamekufundisha hivyo na kama umetoa kichwani kwako jitafakari..

Kwanini mama umpe hasi Baba umpe chanya kwanini usingewape wote hasi au wote chanya na kuzichambua ueleweke .. watalaumiwa walimu wako sio wewe..

Mtoto akilelewa/akimuelewa na Baba kwa kawaida Baba ni mantiki yaani mtoto anakuwa na maendeleo ya kiuchumi anafanikiwa katika kipato na utawala uongozi wowote ulee na mambo yake mengine yanakuwa na mafanikio .. ndio mafundisho sahihi..

Na mtoto akilelewa/akimuelewa Mama kwa kawaida mtoto anakuwa na tabia njema na matendo ya kuwapendeza watu kwa sababu mama ni tabia mtoto atakuwa na hadabu atafanikiwa kwenye upendo na nidhamu kiujumla.. ndio mafundisho sahihi...

Na ikitokea mtoto akalelewa/kuelewa wote wawili Baba na Mama basi anapata vyote hivyo maendeleo kiuchumi/kifedha na utawala (utekelezaji )kwa Baba kwa kuwa Baba ni kiongozi/mantiki wa familia pia atafanikiwa ki-matendo na tabia njema kwa mama kwa kuwa mama ni mjumuiko ya tabia njema mtoto atakuwa na nidhamu nzuri na upendo pia yaani mapenzi bora kwa wenzake..

Na mtoto akiwa na vyote hivyo hakuna atayeweza kumuendesha popote aendapo kinyume chake akikosa kimoja au vyote ataendeshwa popote aendapo ..

Jitahidi mtoto wako apate vyote hivyo..
 
BARAKA HUTOKA KWA BABA, LAANA HUTOKA KWA MAMA! UTAAMUA MWENYEWE!

Anaandika, Robert Heriel,
Mwanafalsafa.

Utaamua mwenyewe, utapima na kuamua maisha yako mwenyewe.

Baba ndiye mungu wa dunia, utake usitake, Mama ni msaidizi wa Baba upende usipende. Endapo hili halitatokea maisha ya mtoto huwa mashakani. Mtoto akigombana na Baba hukosa baraka, hata hivyo Baba hawezi kumlaani mtoto, Baba yu atoa baraka tuu, hana nguvu katika laana.

Mtoto akigombana na Mama hapo huchukua Laana, mama ndiye mwenye uwezo wa kutoa laana katika huu ulimwengu ikashika pasipo kizuizi. Lakini pamoja na umuhimu wa Mama hapa duniani lakini kamwe hana uwezo wa kumbariki mtoto aliyemzaa, hana mamlaka na hata akimbariki mara elfu moja mtoto hawezi kupata baraka hata moja. Labda sieleweki. Lakini mtanielewa tuu.

Unapoishi na wazazi lazima uelewe kila mzazi anamajukumu yake, anamipaka yake, ipo nafasi ya mama ambayo kamwe baba haiwezi ku-cover, lakini pia ipo nafasi ya Baba ambayo mama hata apinduke vipi kamwe hawezi kui-cover. Hata hivyo Mama anaweza beba majukumu karibu yote ya Baba na akayafanya kwa usahihi kabisa lakini jukumu la kumbariki Mtoto kamwe Mama hawezi kuli-Cover.

Kuna mtu anaweza akasema, mbona kuna watoto waliolelewa na Mama pekee, wakagombana na Baba zao, wakawatukana Baba zao, na bado wamefanikiwa kwenye maisha; Ukweli ni kuwa unaweza ukawa umefanikiwa kwenye maisha lakini maisha yako yasiwe ya baraka. Lazima ujue kutofautisha mafanikio na Maisha ya Baraka, aliyebarikiwa. Unaweza ukakuta mtu kafanikiwa lakini ni shoga, teja, anaharibu wanawake kwa kulala nao kama mnyama, amefanikiwa katika maisha lakini maisha yake hayana baraka kwa jamii.

Huwezi mkuta mtu aliyebarikiwa na Baba yake akawa na matatizo ndani ya jamii, hilo halijawahi kutokea na halitakuja kutokea kamwe.

Watoto wa zama hizi, najua mazingira ya karne hii ni magumu, huenda mama yako alitelekezwa akiwa na mimba yako, huenda Baba yako alikukataa, huenda Mama yako alifukuzwa na Baba yako, au sababu yoyote ile ambayo inakufanya usiwe karibu na Baba yako, inakufanya mchukie Baba yako, leo Taikon nakuambia kuwa, huyo ndiye Baba yako, huyo ndiye mwenye uwezo wa kukubariki ukapata baraka, huyo ndiye mungu katika nafasi ya hapa duniani, huyo Mama yako ni msaidizi wa huyo Baba yako tuu, atakupa kila kitu lakini kamwe hawezi kukupa baraka.

Lazima ujifunze kumheshimu Baba yako hata kama humjui, lazima ujifunze kumheshimu hata kama humuoni, heshima ndio ufunguo wa baraka zako katika maisha. Jamii zote duniani zilizoendelea na zilizostaarabika zinajua jambo hili, hata kama Baba atakuwa na mapungufu makubwa kiasi gani lakini huyo ndiye Baba, mungu mdogo aliyeshikilia dunia yako.

Kumkataa Baba ni sawa na wale wanaojiita Atheist, wasiomuamini Mungu, wasiotaka kutambua uwezo wa Mungu, lakini wanatambua uwepo wa Mama Dunia wanayemuona, Mama dunia anaweza kukupa yote lakini kuna mambo ya msingi kamwe hawezi kukupa. Uhai na baraka kamwe dunia haiwezi kukupatia.

Nisiandike sana, kuwachosha nafikiri nilichokuwa nataka kukisema mumekielewa, Msidanganywe na hawa wanawake ambao baadhi yao wanachuki na Baba zenu, tambueni kuwa wanawagombanisha na watu muhimu ambao ndio wenye uwezo wa kuwabariki mkabarikiwa, Wapendeni Mama zenu, lakini waheshimuni Baba zenu, nafikiri nimeeleweka.

Wababa nanyi mtambue kuwa hamna uwezo wowote wa kumlaani mtoto na laana ikashika, hakuna kitu kama hicho duniani,
Baba unachoweza kukifanya ni kutoa baraka. Wamama nanyi mtambue kuwa hamna uwezo wowote wa kubariki hata muwakumbatie watoto wenu kama dhahabu, mnachoweza ni kutoa laana ikashika. Hilo kila mmoja aliweke akilini.

Mwisho; Kwa mustakabali mwema wa watoto lazima Mama na Baba muwe kitu kimoja, muwajenge watoto katika misingi mema, mkijua kuwa bila ninyi wawili maisha ya mtoto yapo hatarini,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam.
Andiko lako ni upotoshaji mkubwa otherwise utupatie marejeo ya andiko lako sio kutunga na kutulisha matango pori
 
Andiko lako ni upotoshaji mkubwa otherwise utupatie marejeo ya andiko lako sio kutunga na kutulisha matango pori

Sio kila mtu anarejelea, marejeleo ni Kwa watu waliojifunza Kwa wengine,
Mimi sijajifunza hili Kwa yeyote, ni Jambo nililoliona Kwa macho tuu ya kawaida, hata watu wengine wanaweza kuwa wameliona sema hawakuandika.

Ninyi ndio mtarejelea, mliozoea kujifunza Kwa watu wengine,
 
Vipi ambao baba zetu ambao walifariki tukiwa wadogo lakini tukalelewa na ndugu wengine wa kiume. Inakuaje hapa taikon na wametulea vizuri na majukumu ya ubaba wameyabeba kwa 100%.
Nb mama hakuolewa tena baada ya baba kufa.

Swali :je hao walionilea mf bamdogo, shemeji nk nao hutoa baraka?
 
Baba mzazi, achana na hao wanaojipa majukumu yasiyoyao
Hakika nakubalianq na wewe mkuu. Kwani hata biblia inasema
Ibrahim alimbariki Isaka akabarikiwa na uzao wake, nae Isaka alpokaribia kufa alimuambia mwanae aliempenda Esau akamfanyie mawindo ili amuandalie chakula akipendacho ale ashibe aweze kumbariki, lakini mama aliposikia alimuambia mwanae aliempenda nae ni Yakobo alete ndama ili aandae chakula apewe baba ili ambariki kwani tayari Isaka alishakuwa kipofu. Baada ya kushiba alimbariki yakobo, na Esau aliporudi alikuta baraka imeshatolewa kwa wingi wote kwa Yakobo mdogo wake. Sijaona popote mama akibariki bali baba. Hakika bataka hutoka kwa baba na liana hutoka kwa mama.
 
Hakika nakubalianq na wewe mkuu. Kwani hata biblia inasema
Ibrahim alimbariki Isaka akabarikiwa na uzao wake, nae Isaka alpokaribia kufa alimuambia mwanae aliempenda Esau akamfanyie mawindo ili amuandalie chakula akipendacho ale ashibe aweze kumbariki, lakini mama aliposikia alimuambia mwanae aliempenda nae ni Yakobo alete ndama ili aandae chakula apewe baba ili ambariki kwani tayari Isaka alishakuwa kipofu. Baada ya kushiba alimbariki yakobo, na Esau aliporudi alikuta baraka imeshatolewa kwa wingi wote kwa Yakobo mdogo wake. Sijaona popote mama akibariki bali baba. Hakika bataka hutoka kwa baba na liana hutoka kwa mama.


Watakubishia
 
Mama hana kitu kingine ambacho anaweza kutoa zaidi ya laana ?

Unawakosea sana kina mama mkuu pengine ulipo soma ndio wamekufundisha hivyo na kama umetoa kichwani kwako jitafakari..

Kwanini mama umpe hasi Baba umpe chanya kwanini usingewape wote hasi au wote chanya na kuzichambua ueleweke .. watalaumiwa walimu wako sio wewe..

Mtoto akilelewa/akimuelewa na Baba kwa kawaida Baba ni mantiki yaani mtoto anakuwa na maendeleo ya kiuchumi anafanikiwa katika kipato na utawala uongozi wowote ulee.. ndio mafundisho sahihi.. hii Ina maana baba kama hawezi kuwa kiongozi na kusimamia majukumu yake huyo sio baba..

Na mtoto akilelewa/akimuelewa Mama kwa kawaida mtoto anakuwa na tabia njema na matendo ya kuwapendeza watu kwa sababu mama ni tabia mtoto atakuwa na hadabu atafanikiwa kwenye upendo na nidhamu kiujumla.. ndio mafundisho sahihi.. hii Ina maana mama kama hana tabia njema huyo sio mama ..

Na ikitokea mtoto akalelewa/kuelewa wote wawili Baba na Mama basi anapata vyote hivyo maendeleo kiuchumi/kifedha na utawala (utekelezaji )kwa Baba kwa kuwa Baba ni kiongozi/mantiki wa familia pia atafanikiwa ki-matendo na tabia njema kwa mama kwa kuwa mama ni mjumuiko ya tabia njema mtoto atakuwa na nidhamu nzuri na upendo pia yaani mapenzi bora kwa wenzake..

Na mtoto akiwa na vyote hivyo hakuna atayeweza kumuendesha popote aendapo kinyume chake akikosa kimoja au vyote ataendeshwa popote aendapo ..

Jitahidi mtoto wako apate vyote hivyo..
Kama nimekuelewa vizuri wewe na mzee Robert ni kwamba, mzee Robert kaeleza facts za mambo yalivyo duniai, halafu wewe ungependa hiyo hali i balance; kwa maneno mengine wewe unapenda HAKI sawa na sio facts, yaani ungependa kama ingewezekana pia hata mama awe anatoa MBEGU na baba abebe mimba which is not possible.
Maelezo ya mzee Taikon ni kwa mtazamo wa ki fact sio anavyo penda yeye IWE, mfano, hivi unadhani yeye kama mwanaume HAPENDI kulaani mtoto wake msumbufu? May be anapenda but facts zinakataa, baba hana uwezo wa kulaani mwanae isipokua ana uwezo only wa kumbariki mwanae. Hebu msome tena, nadhani huyu mzee haja kurupuka. Labda ungemuuliza, hu ni utafiti wake binafsi au mambo ya IMANI? Binafsi nakubaliana nae kwa almost 95% ya aliyasema, nimeyaona, nimeyashuhudia!
 
Hakuna kitu chepasi kukifafanua kama baraka na laana katika maisha haya ya siku hizi. Yaaani we unakuwa tu unalazimisha matatizo na laana mafanikio na baraka. Unaduka lako ikatokea ukamzidishia chenji mteja kimakosa unasema laana hii inanisumbua. Ila siku unachukua bidhaa ukapewa zingine za mkopo hapo baraka za baba zinafanya kazi. Kwenye maisha lazima kipindi kigumu kiwemo ila pia kipindi cha furaha razima kiwemo. Mfano kitu ulichocheza na akili zetu nikuwa. Hata kama utafanikiwa pasipo baraka za baba basi lazima mafanikio yako yawe na shida kwenye jamii. So kwabinadamu wa sasa uwe na mafanikio kisha jamii ikuchukulie safi tu na haya mawivu ya watu siyo rahisi

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Kama sikosei wewe ndio uliandika andiko kuwa USIWAONEE HURUMA WANAWAKE kama sikosei ni wewe mkuu.. kwa vile tupo Tanzania tu na labda huu mtandao upo mafichoni kidogo ila ingekuwa tunaishi kweli HAKI ZA BINAADAMU zingelikutafuna kitambo.. haya mkuu hongera kwa uelewa wako wa juu kabsa

Hakuna haki ya kuonewa huruma Mkuu?

Wala hakuna sheria yoyote inayomtaka mtu kumuonea huruma mtu mwingine, huruma ni hiyari ya mtu.

Wanawake wanahaki ya kupendwa,
 
Hakuna kitu chepasi kukifafanua kama baraka na laana katika maisha haya ya siku hizi. Yaaani we unakuwa tu unalazimisha matatizo na laana mafanikio na baraka. Unaduka lako ikatokea ukamzidishia chenji mteja kimakosa unasema laana hii inanisumbua. Ila siku unachukua bidhaa ukapewa zingine za mkopo hapo baraka za baba zinafanya kazi. Kwenye maisha lazima kipindi kigumu kiwemo ila pia kipindi cha furaha razima kiwemo. Mfano kitu ulichocheza na akili zetu nikuwa. Hata kama utafanikiwa pasipo baraka za baba basi lazima mafanikio yako yawe na shida kwenye jamii. So kwabinadamu wa sasa uwe na mafanikio kisha jamii ikuchukulie safi tu na haya mawivu ya watu siyo rahisi

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app

Na laana ni pale upo kipindi cha mafanikio lakini yanaleta madhara ndani yako, familia au jamii.
 
Vipi ambao baba zetu ambao walifariki tukiwa wadogo lakini tukalelewa na ndugu wengine wa kiume. Inakuaje hapa taikon na wametulea vizuri na majukumu ya ubaba wameyabeba kwa 100%.
Nb mama hakuolewa tena baada ya baba kufa.

Swali :je hao walionilea mf bamdogo, shemeji nk nao hutoa baraka?
@ROBERT HERIEL
 
Mama hana kitu kingine ambacho anaweza kutoa zaidi ya laana ?

Unawakosea sana kina mama mkuu pengine ulipo soma ndio wamekufundisha hivyo na kama umetoa kichwani kwako jitafakari..

Kwanini mama umpe hasi Baba umpe chanya kwanini usingewape wote hasi au wote chanya na kuzichambua ueleweke .. watalaumiwa walimu wako sio wewe..

Mtoto akilelewa/akimuelewa na Baba kwa kawaida Baba ni mantiki yaani mtoto anakuwa na maendeleo ya kiuchumi anafanikiwa katika kipato na utawala uongozi wowote ulee na mambo yake mengine yanakuwa na mafanikio .. ndio mafundisho sahihi.. hii Ina maana baba kama hawezi kuwa kiongozi na kusimamia majukumu yake huyo sio baba..

Na mtoto akilelewa/akimuelewa Mama kwa kawaida mtoto anakuwa na tabia njema na matendo ya kuwapendeza watu kwa sababu mama ni tabia mtoto atakuwa na hadabu atafanikiwa kwenye upendo na nidhamu kiujumla.. ndio mafundisho sahihi.. hii Ina maana mama kama hana tabia njema huyo sio mama ..

Na ikitokea mtoto akalelewa/kuelewa wote wawili Baba na Mama basi anapata vyote hivyo maendeleo kiuchumi/kifedha na utawala (utekelezaji )kwa Baba kwa kuwa Baba ni kiongozi/mantiki wa familia pia atafanikiwa ki-matendo na tabia njema kwa mama kwa kuwa mama ni mjumuiko ya tabia njema mtoto atakuwa na nidhamu nzuri na upendo pia yaani mapenzi bora kwa wenzake..

Na mtoto akiwa na vyote hivyo hakuna atayeweza kumuendesha popote aendapo kinyume chake akikosa kimoja au vyote ataendeshwa popote aendapo ..

Jitahidi mtoto wako apate vyote hivyo..

Mimi nimelezea Baraka na Laana, nikaeleza nani anauwezo wa kuamua kati ya hivyo.

Majukumu mengine ya mama ambayo ni mema sijayaeleza kama ilivyo kwa baba.

Labda kama unahisia kama ninawazingua kinamama, lakini sivyo, kama ningeongea kinyume chake ningekuwa nawazingua.
 
@ROBERT HERIEL

Yes huweza kutoa baraka, lakini baraka ni matokeo ya matendo mema uyatendayo, kutokumdharau Baba na mama yako. Iwe akiwa hai au akiwa amekufa.

Baba hawezi ruhusu watoto wamdharau mama yao hata kwa nini,
Ila wamama wanaweza kuruhusu mtoto amdharau Baba yake,
Ndio maana wa mama wengi(sio wote) husema mapungufu ya Baba kwa watoto wao, ila ni ngumu kumkuta baba akisema mapungufu ya mama kwa watoto.

ushahidi upo
 
Back
Top Bottom