Baraza Kuu la CHADEMA laridhia kufukuzwa kwa Halima Mdee na wenzake 18. Asilimia 97.6 waafikiana na maamuzi

Baraza Kuu la CHADEMA laridhia kufukuzwa kwa Halima Mdee na wenzake 18. Asilimia 97.6 waafikiana na maamuzi

Ikitokea tulia akagoma kuwafukuza itakuwaje

Tatizo mnakuwa wagumu kuelewa chadema haina shida wenyewe kuwa wabunge bali imewafuta Kwenye list ya Wanachama wake. Kama Tulia ataendelea kuwatambua aendelee lakini ajue wale sio Wanachama wa Chadema na chadema haina mbunge wa viti maalum bungeni. Waendelee kula pesa ya serikali ya vilaza wasio jitambua.
 
Faida ya kwanza ni kuonekana ni chama kinachosimamia katiba na itikadi zao ukizikiuka hata kama ni Tundu Lissu unafukuzwa!

Mzee Mdee na wenzake kuna mahala wameandaliwa ngoja uone wanakoenda
Mzee Mdee ni yupi?
 
Tokea jana katika kikao cha CHADEMA walifika wabunge 19 ambao kulikuwa na mzozo nani aliyewapa baraka wakati hakuna makubaliano.

Kitu ambacho tunaweza kushangaa kule bungeni hawata vuliwa na mwisho wa siku watapokelewa juu kwa juu wataingia ccm na watabaki kuwa bunge.

Hii topic msipuuze
 
Hakuna Cha Kushangaza hapo...Sakosi nyingi huwa Zinaendeshwa hivyo....!

Wakatafute Vyama Sasa na Sio Sakosi..!
 
Napongeza hatua ya baraza kuu la Chadema kuwafukuza uanachama hao waliyokuwa wabunge wa....Lakini nawashauri waliwofukuzwa kama wanandoto za kuendelea na siasa wakajiunge ktk vyama wanavyofikiri vitawafaa ingawa najuwa hata kuwa maarufu kama mwanzo mana wapo walotoka wenye majina makubwa lakini wamezimika.Au wachaguwe kuachana na siasa mana kuna maisha nje ya siasa wasiwe tegemezi ktk mwelekeo mmoja tu.Kila la heri.
Mimi nakushauri ujifunze kuandika kiswahili vizuri....mfano [waliwofukuzwa=waliofukuzwa]. Asante
 
Asa yale magwanda watapeleka wapi 😂😂😂
Inasikitisha! Lakini Maamuzi yaliyofanyika ni ya busara sana kwani yatakifanya chama kiwe na nidhamu ya hali ya juu sana. Kama kwerli hao covid-19 ni wanachadema kweli, bado kuna room ya kuludi chamani. Ni kuomba upya uwanachama
 
Yani kwa Ile statement ya Mbowe kwamba yeyote atakayesaliti chama hatavumiliwa nilijua kabisa Covid imekula kwao.

Anyway wameshatengeneza hela ya kutosha na Kama wamechukua mikopo dhamana ni mshahara wa ubunge hivyo serikali italipa huo mkopo.

Magufuli na Ndugai walituharibia sana bunge. Anyway wapumzike waende CCM Sasa waone Kama watapewa nafasi kule.
Mkuu hela huwa hazitoshi siku zote!!tena kama ulishawahi kuwa mbunge kwenye pesa za bure huko, ukitemeshwa hata kama umebakiza mwezi mmoja tu, lazima uumie tu, wapi utapata malipo ya milioni 12 kwa mwezi, hata ukiwa na elimu ya std seven?prof.mwenyewe hafiki huko.

Na kwa siasa za sasa hata kuhamia ccm ni ngumu, ili kupata vyeo kama wakati wa jiwe.Mama ana mapungufu yake kama kiongozi yoyote lakini ametutoa jehanamu ya siasa.MUNGU FUNDI.
 
Mimi nashauri waombe upya uanachama waendelee kubaki CDM! Wakienda huko kwenye vyama vingine watapotea kabisa katika ulimwengu wa siasa za nchi yetu.
Wabaki na kuomba uanachama upya, Watanzania na hususani Wana CDM watawaelewa wakiomba radhi kufuatia siasa za chuki visasi Mwendazake.
 
Kuna mbweha alisema atajitoa jamiiforum kama chadema watawafukuza covid-19.
britanicca yan huyu jamaa tangu Magufuli Afe na tangu Urusi avamie Ukraine amekua mjinga kwel kwel humu jukwaan ..kapoteza heshima yake kwel kwel kutokana nambo anayosimamia..Haya sasa ngoja tuone atafanyaje.

Pascal Mayalla naye sijui anasema nini kuhusu hil maana amekua akiamin jambo la covid19 lina baraka ya mwenyekit na kamati kuu...Mara kangaroo cort na mambo mengine meengi
 
Mkuu, unaweza kunieleza kufukuzwa kwa hao wanachama kuna faida gani kwa chadema?
usaliti kwa chama hautakiwi na imani kwa wanachama juu ya maumivu waliokuwanayo unapozeka sasa. Safi sana.
 
Wasaliti kama Hawa sijui hata watoto wao watajifunza nini!? Halima ulikamata kura feki ukathibitishia Dunia uchaguzi ulikuwa feki, iweje Tena uwe sehemu ya uchafu huo
 
HALIMA MDEE NA WENZAKE 18 WAFUKUZWA RASMI CHADEMA

Baraza Kuu la #CHADEMA limezitupilia mbali Rufaa za Halima Mdee na wenzake 18 wakipinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya chama hicho kwa kukubali kwenda kuapishwa na kuwa wabunge wa Viti Maalumu bila baraka za chama
======
UPDATE:

View attachment 2221145

Halima Mdee: Kilichofanyika ni Uhuni, hata Mbowe (Freeman) mwenyewe anajua

John Mrema: Baada ya uamuzi wa Baraza Kuu, Katibu Mkuu ataandika barua kumuarifu Spika kuwa suala lao limehitimishwa; tutamwachia spika afanye uamuzi kama alivyosema anasubiri Rufaa zao
=======

Matokeo ni kama ifuatavyo;

Kanda ya Victoria (Wajumbe 44)
-Wanaokubalia wavuliwe uwanachama 42
-Wasiokubali 1
-Wasiofungamana na Upande wowote 1
Jumla kura 44

Kanda ya Nyasa (Wajumbe 57)

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 57
-Wasiokubalina 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 57

Kanda ya Unguja (Wajumbe 22)

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 19
-Wasiokubali 1
-Wasifungamana na Upande wowote 1
Jumla ya Kura 22

Kanda ya Pemba 15
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 12
-Wasiokubali 1
-Wasifungamana na Upande wowote 2
Jumla ya Kura 15

Kanda ya Kusini 32

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 32
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 32

Kanda ya Pwani 47

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 45
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 2
Jumla ya Kura 47

Kanda ya Kati 44

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 44
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 44

Kanda ya Serengeti Wajumbe 41

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 41
-Wasiokubalina 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 41

Kanda ya Magharib Wajumbe 37

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 37
Wasiokubali 0
Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 37

Kanda ya Kaskazini Wajumbe 61

-Wanaokubali wavuliwe uanachama 61
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 61

MATOKEO YA JUMLA

Idadi ya wajumbe 423

Waliokubalina na maamuzi ya Kamati ya kuwafukuza Uanachama ni 413 sawa 97.6%

Wasiokubaliana na uamuzi wa Kamati kuu ni 5 sawa na 1.2%

Wasiofungamana na upande wowote ni 5 sawa na 1.2%


Pia, soma;

1). BAVICHA: Tumesikitishwa sana na walioenda kuapa, ni kitendo cha usaliti, hujuma na hakiwezi kuvumilika. Wataka hatua kali zichukuliwe

2. Uchaguzi 2020 - CHADEMA yaitaka Tume ya Uchaguzi NEC kutoa Ufafanuzi kuhusu Majina ya Wabunge wa Viti Maalum Wanaodaiwa wamepelekwa Bungeni

3). Mnyika: Ni miezi 5 sasa NEC hawajajibu barua yangu kuhusu walikopata majina ya Wabunge 19 na nani amesaini fomu zao

4). Uchaguzi 2020 - Hatimaye Wabunge wa Viti maalumu wa CHADEMA wajitokeza kuapishwa Dodoma. Viongozi wa CHADEMA wakana kupeleka majina yao

5. Uchaguzi 2020 - Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

6. Spika Ndugai: Wabunge waliofukuzwa CHADEMA wapo kwenye mikono salama

7. Halima Mdee: Walichofanya wajumbe wa Baraza Kuu CHADEMA ni UHUNI!
Safi sn waende CCM au ACT wasaliti wakubwa
 
Back
Top Bottom