Baraza la Maaskofu ni wanadamu, wanakosea kwenye mengi hata waraka wao kupinga uwekezaji wa bandari ni makosa.

Baraza la Maaskofu ni wanadamu, wanakosea kwenye mengi hata waraka wao kupinga uwekezaji wa bandari ni makosa.

Mwanadamu ndiye anaweza kukosea 😂

Kanisa Moja Takatifu la Mitume usilifananisha na Kusanyiko la Ufufuo na Uzima pale Ubungo!
Kanisa na viongozi wa kanisa ni vitu viwili tofauti, waraka umetolewa na viongozi wa kanisa ila wametumia mgongo wa kanisa.

Kanisa ni imani ya kiroho, ungekuwa ni waraka wa kiroho hapo sawa lakini kwa huu wa uwekezaji ni makosa yamefanyika.
 
Point ya mleta uzi ni kwamba Mwanadamu anaweza kukosea kwasababu wao na Majoho/Kanzu zao haziuondoi uwanadamu wao
Kwa maana hiyo hata wenye mamlaka Yani viongozi wa serikali wanaweza kukosea sababu na wao ni watu! Kama hiyo ndio logic basi wamekosea na makosa yamekua dhahiri hawana budi kijirekebisha Kwa hili linaloendelea na makosa yao wameoneshwa na hao TEC Miongoni mwa watu wengine ukiacha anahrakati na mahakama ambayo dhahiri iliomesha kushangaa baadhi ya mambo na ikajizuia kuingilia maamuzi ya hovyo ya bunge!
 
Kwa maana hiyo hata wenye mamlaka Yani viongozi wa serikali wanaweza kukosea sababu na wao ni watu! Kama hiyo ndio logic basi wamekosea na makosa yamekua dhahiri hawana budi kijirekebisha Kwa hili linaloendelea na makosa yao wameoneshwa na hao TEC Miongoni mwa watu wengine ukiacha anahrakati na mahakama ambayo dhahiri iliomesha kushangaa baadhi ya mambo na ikajizuia kuingilia maamuzi ya hovyo ya bunge!
Walishavuta rushwa ya DP World inawatesa kinyama
 
Yaani unafikiria mpaka tupige kura ya maoni! Kisa tu ni huo mkataba wenu na DP WORLD!! Aisee kama mlikula hela za Waarabu wenu zirudisheni haraka. Watanganyika wengi hatuutaki huo mkataba wa kimangungo.
Nyani lazima ateme bungo hakuna jinsi nyingine
 
Kwa maana hiyo hata wenye mamlaka Yani viongozi wa serikali wanaweza kukosea sababu na wao ni watu! Kama hiyo ndio logic basi wamekosea na makosa yamekua dhahiri hawana budi kijirekebisha Kwa hili linaloendelea na makosa yao wameoneshwa na hao TEC Miongoni mwa watu wengine ukiacha anahrakati na mahakama ambayo dhahiri iliomesha kushangaa baadhi ya mambo na ikajizuia kuingilia maamuzi ya hovyo ya bunge!
Nimewazungumzia viongozi wa dini ambao wengine wanawatazama kama watakatifu wasiokosea
 
Yaani unafikiria mpaka tupige kura ya maoni! Kisa tu ni huo mkataba wenu na DP WORLD!! Aisee kama mlikula hela za Waarabu wenu zirudisheni haraka. Watanganyika wengi hatuutaki huo mkataba wa kimangungo.
Kura ndio sauti ya wengi, ikiitishwa kura ya maoni tutajua sauti ya wengi ni ya wakina nani? Wanaopinga au wanaokubali?
 
Kuna aina mbili za mitazamo ya watu juu ya viongozi wa dini:

Aina ya kwanza wanawatazama viongozi wa dini kama wanadamu kamili na wenye ukamilifu wote, kunena mpaka kutenda kwao ni kwa ukamilifu. Hawakosei lolote

Aina ya pili wanawatazama viongozi wa dini kama wanadamu wa kawaida, wanatenda makosa kama wengine ila ukubwa wa makosa unatofautiana na wengine.

Mitazamo ya makundi yote mamili ndio imechangia pakubwa kuwaamini viongozi wa dini na sauti zao kutumika kwenye mengi lakini sio mara zote SAUTI ZAO ni ujumbe wa kinabii.

Baada ya utangulizi huo, niseme machache yafuatayo:

Tunawaamini viongozi wa dini katika mengi ila sio katika yote Kwa sababu nao ni wanadamu wa kawaida.

Kama wanadamu wanakosea katika mengi hivyo kuna hati hati wenye mtazamo wa kundi la kwanza juu ya viongozi wa dini wakaingizwa kwenye makosa ya kuwaamini.

Juu ya suala la uwekezaji bandari, mtazamo na maoni ya baraza la Maaskofu unaweza kuwa ni Moja ya makosa maana nao ni binadamu.

Sipingani na viongozi wa dini Kwa Imani zao bali napingana nao Kwa ubinadamu wao. Kabla ya kuwa kiongozi wa dini alikuwa ni binadamu wa kawaida, hawezi kuacha kuwa binadamu wa kawaida baada ya kuwa kiongozi wa dini.

Maswali ninayojiuliza ambayo natamani TEC waje wayajibu:

Je, ikitokea kutokana na tafsiri na uelewa ,wanachopinga kikawa sio kweli watakuja kuupinga waraka wao?

Je, licha ya yote kukiwa na faida katika uwekezaji huo watapinga waraka wao?

Je, ikiitishwa kura ya maoni Leo, kujua wanaopinga na wanaokubali uwekezaji wapi wengi, na ikaonekana wanaokubali ni wengi watapinga waraka wao?

Ndio maana nimesema Baraza la Maaskofu nao ni wanadamu wa kawaida, wanakosea katika mengi hata hili la waraka ni Moja ya makosa.
 
Hebu ziweke hizo hoja za Tec na ufafanuzi wa Serikali ili tufanye uchambuzi

Nimewazungumzia viongozi wa dini ambao wengine wanawatazama kama watakatifu wasiokosea
Ungebalance storry na kuwaweka pia viongozi wa siasa ambao wafuasi wao wapo tayari kuumwa hata watu wengine au kuwafunga magerezani pale wanapotofautiana nao Kwa kuwaona kwamba Kila wanachofanya au kuamua ni sahihi na hawapaswi kukosolewa au kuhojiwa. Usipofanya hivyo unajitanabaisha upande ulioegemea! Juzi walikua wanashangilia Slaa et al anyongwe mashtaka yamebadilika hao hao hawajui washike wapi tena. Hii Ina maana kuwa na wao wanakosea.

Meanwhile naamini kwenye institution ya TEC iliyosheheni wabobezi na wataalamu katika Kila idara hawafanyi jambo Kwa kukurupuka Bali Kwa utafiti wa kujiridhisha.
Mamlaka imeona na huo ndio msimamo na Kwa jinsi Catholic Church ilivyo imara kitaasisi Leo jumamosi swala Hilo limeanzia ngazi ya kifamilia (jumuiya) kesho ni kitaifa (kanisani) lazima usomwe na ieleweke!
 
Kuwa mpole DP World ndio ishakufa hio kama ulihaidiwa ajira pale kalime nyanya
 
Elekeza malalamiko yako panapohusika mambo binafsi hayatuhusu hata wewe ulipigwa na mke wako lkn hilo jambo hatuwezi kusema hapa.
Badala ajibu hoja zilizopo mezani anakimbia kumuatack Kitima as if yeye ndio amekaa PEKEE na kuandaa tamko la TEC. Ujinga wa Hawa watu haupikiki.
 
Back
Top Bottom