Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Tupo kwenye zama mpya na kila zama na style yake.
Kwa hivi sasa wananchi wana matumaini makubwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwamba atakuwa ni rais atakeyekidhi matarajio yao ya maendeleo lakini pia atakuwa rais atakayeondoa mapungufu makubwa yaliyoonekana katika serikali iliyopita ya rais Magufuli yakiwemo, Kutoheshimu katiba, kutotenda haki ipasavyo, uonevu wa dhahiri, kugeuza bunge kuwa kikaragosi cha mtawala, ukopaji mkubwa sana na hivyo kuongezeka kwa deni la Taifa lililokithiri, kujaza Makada wa CCM kwenye nafasi za kitaalamu (rejea uDAS), Viashiria vya udini na Ukabila katika teuzi, kunyima wananchi haki ya kuchagua na kuchaguliwa kwa kupora chaguzi, kauli tata na chafu, kuharibu sekta binafsi, kuharibu maisha ya watu kwa kupora korosho na kuvuruga kilim cha mbaazi na Kahawa, na mambo mengi ya hovyo
Sasa katika mazingira ya aina hii si sahihi hata kidogo kwa raisi mpya kwenda na timu ileile, katika mtindo uleule ambao wananchi walionyesha kutokuwa na matarajio nayo.
Hivyo basi kutokana na sababu zifuatazo, Tunamtarajia Raisi Samia Suluhu Hassan afanye mabadiriko makubwa kwenye timu yake ya Mawaziri na Manaibu waziri ili aweze kupata Imani thabiti ya wananchi kuwa atakidhi matarajio yao.
1. Mosi, hiyo timu ya sasa si ya Rais Samia bali ni ya Rais Magufuli kwa kusaidiana na Kassim Majaliwa (Sijui alishirikishwa kiasi gani).
Katiba haimpi role Makamu wa Raisi kwenye kuunda baraza la mawaziri, bali inampa role hiyo Rais kwa kushirikiana na Waziri Mkuu, Kwa hiyo ni dhahiri hiyo timu siyo ya Rais Samia, bali imeundwa kulingana na vigezo vya kiutawala, haiba na mawazo ya Hayati Magufuli. Ili Samia aweze kuperform kwa kiwango tunachontarajia ni lazima ateue timu yake mwenyewe ambaye yeye anaiamini na sisi wananchi pia kuiamini kuwa kweli hii ni timu itakayoweza kuleta mabadiriko ya msingi lakini pia kubeba ajenda ya maendeleo. Timu ileile ya watu wale ambamo miongoni mwao kuna wababaishaji wengi na watu makini wachache haiwezi kukidhi matarajio yetu wananchi.
2. Baraza hili la sasa ni sura ya "divisiveness" (ukosefu wa mshikamano wa Kitaifa).
Haiwezekani uuende baraza la mawaziri la Tanzania nzima ambalo haliakisi demografia ya kitaifa, baraza ambalo halina Waziri hata mmoja kutoka Zanzibar, Lina waislamu watatu tu kati ya makumi ya mawaziri, lina wanawake wa kuangalizia kwa tochi, baraza ambalo kanda nyingine za nchi hakuna mtu, Hilo siyo baraza la kujenga umoja, mshikamano na Utaifa, hilo ni baraza kama la vikao vya harusi, ambapo hujali nani kaja kikaoni isipokuwa pesa tu zipatikane!. Tunataka baraza lenye sura ya Kitaifa ambalo halina viashiria vya Udini, Ukabila, Ukanda, Utanganyika au Uzanzibari
3. Hili baraza la mawaziri pamoja na manaibu wake liliundwa Strategically kwa sababu za kisiasa za Hayati na siyo kwa dira ya maendeleo ya Taifa
Ukiangalia hili baraza la sasa la mawaziri, limejaa watu waliokuwa vinara wa kujipendekeza kwa hayati, kuna watu humo ndani wameshatoa oda za kukamata wananchi eti kisa wanahoji wapi alipo kiongozi wao Mkuu wa nchi, kuna Manaibu Waziri humo walikimbia vyama vyao vya awali na kuha CCM kwa ahadi ya fedha na vyeo, Watu wa aina hii wa kununuliwanunuliwa siyo aina ya baraza la mawaziri na manaibu waziri tunaowahitaji chini ya Uongozi mpya.
Hapa rais Samia aache huruma kuwaangalia usoni wateule wa hayati kihurumahuruma, hii biashara si yake, hii ni biashara yetu sisi wananchi. Hatutaki viongozi wenye sura za unafiki, wanaonunuliwa nunuliwa na kubadili misimamo yao kwa ajili ya fedha na vyeo. Hawa walionunuliwa ili kuunga mkono juhudi hawa ndiyo aina ya watu ambao wanaweza kuingiza nchi katika mikataba yenye harufu ya ufisadi kwa sababu wana bei.
Kwa hiyo utaona kuwa Hayati aliunda baraza la ma "yesmen", watu atakaoweza kuwaburuza tu na ambao hawana guts za kusimamia misimamo yao tofauti. Sasa sisi hatuhitaji timu ya wanafiki wanaojali matumbo yao badala ya maslahi ya Taifa
4. Kuna mawaziri ambao kutokana na haiba yao na matendo yao ni heri wakawekwa benchi au wabadirishiwe wizara, hawaakisi Taifa la watu wanaojitambua au hawajatimiza wajibu wao ipasavyo
a) Yule waziri Comedian anayelisha viapo wafanyakazi wa ofisi yake, anayeuliza "wanaume mpo, sioni mwanaume hata mmoja hapa)
b) Yule waziri aliyetoa agizo la kukamata wananchi na kuwaweka ndani kisa eti wananchi wanahoji afya ya rais wao na kwamba yuko wapi? —Huyu pia ana rekodi ya kuwa na msimamo alioutoa bungeni kuwa watoto wenye mimba hawafai kuendelea na masomo kwenye shule za serikali
c) Yule Waziri ambaye Ulisema kama Kashindwa kazi basi asaidiwe, haiwezekani wizara yake ina underperform halafu abaki katika wizara hiyohiyo
Hata hivyo, kwenye kubadili mawaziri hakuna haja ya kumbadili Waziri Mkuu, licha ya kauli zake tata za hivi karibuni ambazo zina uongo mwingi ikiwemo, kudanganya umma juu ya hali ya afya ya rais na pia kuandaa maziko ya hayati ambayo aliyaendesha katika mrengo wa KiCCM bila kutambua uwepo wa viongozi wakuu wa chama kikuu cha upinzani nchini, na kuongopea Watanzania kuwa eti watu bilion 3.9 wamefuatilia msiba wa hayati kitu ambacho ni uongo dhahiri na mtu wa calibre yake hapaswi kuongopaongopa, Kiapo chake cha uwaziri mkuu kinamtaka kujiconduct kwa namba ambayo hatadhalilisha heshima ya kiti chake, Sasa uongo unadhalilisha heshima ya nafasi ya waziri mkuu.
Hata hivyo huyu tunaweza kuendelea naye kutokana kwanza, na gharama za kutunza mawaziri wakuu wastaafu na pili ni dhahiri anajitahidi kuchapa kazi. Ila kwa mawaziri na manaibu waziri, Bila mabadiriko katika timu hiyo sioni ni kwa namna wananchi wanaweza kuwa na matarajio na serikali hii ya Rais Samia Suluhu Hassan
Kwa hivi sasa wananchi wana matumaini makubwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwamba atakuwa ni rais atakeyekidhi matarajio yao ya maendeleo lakini pia atakuwa rais atakayeondoa mapungufu makubwa yaliyoonekana katika serikali iliyopita ya rais Magufuli yakiwemo, Kutoheshimu katiba, kutotenda haki ipasavyo, uonevu wa dhahiri, kugeuza bunge kuwa kikaragosi cha mtawala, ukopaji mkubwa sana na hivyo kuongezeka kwa deni la Taifa lililokithiri, kujaza Makada wa CCM kwenye nafasi za kitaalamu (rejea uDAS), Viashiria vya udini na Ukabila katika teuzi, kunyima wananchi haki ya kuchagua na kuchaguliwa kwa kupora chaguzi, kauli tata na chafu, kuharibu sekta binafsi, kuharibu maisha ya watu kwa kupora korosho na kuvuruga kilim cha mbaazi na Kahawa, na mambo mengi ya hovyo
Sasa katika mazingira ya aina hii si sahihi hata kidogo kwa raisi mpya kwenda na timu ileile, katika mtindo uleule ambao wananchi walionyesha kutokuwa na matarajio nayo.
Hivyo basi kutokana na sababu zifuatazo, Tunamtarajia Raisi Samia Suluhu Hassan afanye mabadiriko makubwa kwenye timu yake ya Mawaziri na Manaibu waziri ili aweze kupata Imani thabiti ya wananchi kuwa atakidhi matarajio yao.
1. Mosi, hiyo timu ya sasa si ya Rais Samia bali ni ya Rais Magufuli kwa kusaidiana na Kassim Majaliwa (Sijui alishirikishwa kiasi gani).
Katiba haimpi role Makamu wa Raisi kwenye kuunda baraza la mawaziri, bali inampa role hiyo Rais kwa kushirikiana na Waziri Mkuu, Kwa hiyo ni dhahiri hiyo timu siyo ya Rais Samia, bali imeundwa kulingana na vigezo vya kiutawala, haiba na mawazo ya Hayati Magufuli. Ili Samia aweze kuperform kwa kiwango tunachontarajia ni lazima ateue timu yake mwenyewe ambaye yeye anaiamini na sisi wananchi pia kuiamini kuwa kweli hii ni timu itakayoweza kuleta mabadiriko ya msingi lakini pia kubeba ajenda ya maendeleo. Timu ileile ya watu wale ambamo miongoni mwao kuna wababaishaji wengi na watu makini wachache haiwezi kukidhi matarajio yetu wananchi.
2. Baraza hili la sasa ni sura ya "divisiveness" (ukosefu wa mshikamano wa Kitaifa).
Haiwezekani uuende baraza la mawaziri la Tanzania nzima ambalo haliakisi demografia ya kitaifa, baraza ambalo halina Waziri hata mmoja kutoka Zanzibar, Lina waislamu watatu tu kati ya makumi ya mawaziri, lina wanawake wa kuangalizia kwa tochi, baraza ambalo kanda nyingine za nchi hakuna mtu, Hilo siyo baraza la kujenga umoja, mshikamano na Utaifa, hilo ni baraza kama la vikao vya harusi, ambapo hujali nani kaja kikaoni isipokuwa pesa tu zipatikane!. Tunataka baraza lenye sura ya Kitaifa ambalo halina viashiria vya Udini, Ukabila, Ukanda, Utanganyika au Uzanzibari
3. Hili baraza la mawaziri pamoja na manaibu wake liliundwa Strategically kwa sababu za kisiasa za Hayati na siyo kwa dira ya maendeleo ya Taifa
Ukiangalia hili baraza la sasa la mawaziri, limejaa watu waliokuwa vinara wa kujipendekeza kwa hayati, kuna watu humo ndani wameshatoa oda za kukamata wananchi eti kisa wanahoji wapi alipo kiongozi wao Mkuu wa nchi, kuna Manaibu Waziri humo walikimbia vyama vyao vya awali na kuha CCM kwa ahadi ya fedha na vyeo, Watu wa aina hii wa kununuliwanunuliwa siyo aina ya baraza la mawaziri na manaibu waziri tunaowahitaji chini ya Uongozi mpya.
Hapa rais Samia aache huruma kuwaangalia usoni wateule wa hayati kihurumahuruma, hii biashara si yake, hii ni biashara yetu sisi wananchi. Hatutaki viongozi wenye sura za unafiki, wanaonunuliwa nunuliwa na kubadili misimamo yao kwa ajili ya fedha na vyeo. Hawa walionunuliwa ili kuunga mkono juhudi hawa ndiyo aina ya watu ambao wanaweza kuingiza nchi katika mikataba yenye harufu ya ufisadi kwa sababu wana bei.
Kwa hiyo utaona kuwa Hayati aliunda baraza la ma "yesmen", watu atakaoweza kuwaburuza tu na ambao hawana guts za kusimamia misimamo yao tofauti. Sasa sisi hatuhitaji timu ya wanafiki wanaojali matumbo yao badala ya maslahi ya Taifa
4. Kuna mawaziri ambao kutokana na haiba yao na matendo yao ni heri wakawekwa benchi au wabadirishiwe wizara, hawaakisi Taifa la watu wanaojitambua au hawajatimiza wajibu wao ipasavyo
a) Yule waziri Comedian anayelisha viapo wafanyakazi wa ofisi yake, anayeuliza "wanaume mpo, sioni mwanaume hata mmoja hapa)
b) Yule waziri aliyetoa agizo la kukamata wananchi na kuwaweka ndani kisa eti wananchi wanahoji afya ya rais wao na kwamba yuko wapi? —Huyu pia ana rekodi ya kuwa na msimamo alioutoa bungeni kuwa watoto wenye mimba hawafai kuendelea na masomo kwenye shule za serikali
c) Yule Waziri ambaye Ulisema kama Kashindwa kazi basi asaidiwe, haiwezekani wizara yake ina underperform halafu abaki katika wizara hiyohiyo
Hata hivyo, kwenye kubadili mawaziri hakuna haja ya kumbadili Waziri Mkuu, licha ya kauli zake tata za hivi karibuni ambazo zina uongo mwingi ikiwemo, kudanganya umma juu ya hali ya afya ya rais na pia kuandaa maziko ya hayati ambayo aliyaendesha katika mrengo wa KiCCM bila kutambua uwepo wa viongozi wakuu wa chama kikuu cha upinzani nchini, na kuongopea Watanzania kuwa eti watu bilion 3.9 wamefuatilia msiba wa hayati kitu ambacho ni uongo dhahiri na mtu wa calibre yake hapaswi kuongopaongopa, Kiapo chake cha uwaziri mkuu kinamtaka kujiconduct kwa namba ambayo hatadhalilisha heshima ya kiti chake, Sasa uongo unadhalilisha heshima ya nafasi ya waziri mkuu.
Hata hivyo huyu tunaweza kuendelea naye kutokana kwanza, na gharama za kutunza mawaziri wakuu wastaafu na pili ni dhahiri anajitahidi kuchapa kazi. Ila kwa mawaziri na manaibu waziri, Bila mabadiriko katika timu hiyo sioni ni kwa namna wananchi wanaweza kuwa na matarajio na serikali hii ya Rais Samia Suluhu Hassan