Barua Rasmi kutoka kwa wanaume kwenda kwa wake zao kufuatia kinyang'anyiro Cha kombe la Dunia nchini Qatar

Barua Rasmi kutoka kwa wanaume kwenda kwa wake zao kufuatia kinyang'anyiro Cha kombe la Dunia nchini Qatar

Raymanu KE

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2022
Posts
8,611
Reaction score
16,118
Dear Wives,

Tungependa kuwatia ufahamu kwamba kombe la Dunia linaanza mnano tarehe 20 Mwezi Novemba 2022 nchini Qatar na litachezwa kwa takribani siku 28.

Kutokana na hilo, tunaomba kuwakumbusha nyinyi wake zetu mambo yafuatayo na myatilie maanani:

1. Kwamba muachie( surrender) rimoti za runinga mapema iwezekanavyo ili kuepukana na migogoro ya dakika za mwisho.
Tunaomba muachie( surrender) rimoti kuanzia leo Ijumaa tarehe 19 November 2022.Kinyume na hapo mnaweza mkasababisha remote zikapotea ama zikaharibika kimasihara.

2. Kwamba mtahitajika kusupport timu ambazo waume zenu tutakuwa tunazisupport huko Qatar bila kujali kiwango na uwezo wa timu husika.Kumbeni a United home is a happy home!

3. Kwamba mjitahidi kuepuka kuuliza maswali ya hovyo na yasiyo ya lazima,haswa kipindi ambacho mechi imepamba Moto ama timu ya mume wako inahemeshwa na timu pinzani.Maswali Kama " beby mbona simuoni Haaland?" na " huyu Ni Pogba?" hayatavumiliwa kamwe.
Kaeni mkijua kwamba Haaland na Pogba hawatashiriki michuano ya kombe la Dunia kwa sababu mbali mbali zizizoepukika.

4. Kwamba zipo mechi fulani ambazo zitahudhuriwa na waume zenu katika sehemu zingine tofauti na nyumbani.Sehemu hizo zinaweza kuwa Kama vile kwenye hoteli,vilabu na kadhalika.Kumbukeni kwamba Wayne zenu tutakuwa tunahudhuria hizo mechi tukiwa na marafiki zetu kwa hiyo tunaweza tukachelewa kurudi manyumbani Ana turudi siku za jumatatu baada ya kushinda huko vilabuni tukiangalia mechi za wikendi.
Kwa hiyo tunatanguliza radhi zetu katika Hilo.

5. Kwamba mtatakiwa kupunguza budget kwa kiwango cha nusu ili pesa iliyotengwa itumike kwenye pre- match analysis ama/ au kwenye post- match celebration( s).

6. Tunawaomba wake zetu kwamba msionyeshe hisia Kali kwenye matokea ya mechi, especially timu tunazozipigia upato zipoteze mechi kwa bahati mbaya.Hatutaki makasiriko ya aina yoyote ile.

Kufikia hapo, tunatumai mtayatilia maanani Sheria na masharti tuliyowaelezea happy juu bila usumbufu wowote.
Kama tutakuwa na lolote la ziada Basi tutawaambia baadae.We love you so much.

Ahsanteni.
Mwenyekiti,
Married Men Association (MMA).
 
 
Yani juzi tu hapa naambiwa me nitashangilia Tanzania kombe la dunia,kwani si ishafika Qatar ee! Nilichoka hadi maini. Hawa watu!
 
Yani juzi tu hapa naambiwa me nitashangilia Tanzania kombe la dunia,kwani si ishafika Qatar ee! Nilichoka hadi maini. Hawa watu!
Ni vizuri umejua mapema kwamba Tanzania haipo kwenye hio michuano.
 
Tunawakumbusha kutosahau majukumu yenu ama laah vinginevyo................malizia.
Nawasilisha
 
Back
Top Bottom