Barua ya Rais Mobutu kwenda kwa Rais wa Ufaransa Jacques Chirac

Barua ya Rais Mobutu kwenda kwa Rais wa Ufaransa Jacques Chirac

Basi Nenda

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2017
Posts
20,774
Reaction score
47,866
Kinshasa, May 11 1997
Kwa Mheshimiwa Rais,
Bwana Jacques Chirac
Rais wa Jamhuri ya Ufaransa

Mheshimiwa Rais,

Kwanza kabisa ningependa kutanguliza salamu zangu za dhati kwako na kwa mkeo, vile vile kwa jina la urafiki mrefu sana ambao umetuunganisha kwa zaidi ya miaka kumi.

Leo hali ni ya machungu sana kwangu mbele ya mvuto wa muda mfupi kwanza kwenye kiwango cha madaraka yangu ambapo nimepoteza ufanisi katika watu, pili katika kiwango cha kijeshi ambapo ni vigumu mimi kuzuia maendeleo ya wanamgambo kuja Kinshasa ambapo wanaweza kufika muda wowote.

Na kuhusu Kinshasa siwezi kukuza umwagaji wa damu usiohitajika kwa namna yoyote ile wanamgambo wataifikia Kinshasa ni suala la muda tu. Je, nina budi kukukumbusha ninapambana na vita visivyokuwa na usawa? Leo Marekani na Uingereza kupitia Afrika Kusini, Uganda, Rwanda na Angola wanamtumia kiongozi wa genge la waharifu Laurent Kabila kunichoma kisu mgongoni huku wakitumia mwanya wa maradhi yangu.

Zamani Marekani walikuwa ni washirika wangu; kumbuka visa vya Angola ninabakiza haki ya kuchapisha kumbukumbu zangu katika siku chache zijazo ili dunia nzima ipate kujua ukweli uliofichika

Rafiki yangu unafahamu kama mimi ninavofahamu kwamba Laurent Kabila ni mtu wa kutilia shaka, muuaji na mwenye tabia zisizofaa kuiongoza Zaire, kama kiongozi wa nchi nimejaribu kwa kila namna kuzuia hili lakini mabwana zake wa Magharibi, Wamarekani, wanamuunga mkono.

Kutokana na ukaidi wa Marekani na kuzidi kuzorota kwa Afya yangu ninalazimika kutangaza lengo langu la kumpa madaraka Kabila katika kikao chetu kijacho katika meli ya Utenika mnamo May 14.

MOBUTU SESE SEKO KUKUNGBENDU WA ZABANGA
MARECHAL
RAIS WA JAMHURI

IMG_2885.JPG
IMG_2886.JPG


Sent using Jamii Forums mobile app
 
IMG_2891.JPG
Chirac alimtembelea sana Mobutu inadaiwa pia Mobutu alimfadhili pesa za kampeni Chirac na viongozi wengine wa Ulaya huenda hii ni sababu pesa za Mobutu hazijulikani ziliwekwa Bank gani mpaka leo miaka 20 baada ya kuzitafuta
serikali ya Congo huwa inaambiwa zilikuwepo ila sasa hazipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MOBUTU SESE SEKO KUKU NGBENDU WA ZA BANGA. 🤣🤣🤣

Pia alijipa majina mfano chui mkubwa, the guide, helmsma , rais muanzilishi wa taifa, marechal, papa mobutu,nk

Idd Amin alimuheshimu sana. Kuna wakati Amin alitoa hukumu ya kumuua mwananchi fulani wa Uingereza ilibidi Mobutu aombwe kumshauri lakini ilichukua masaa na baadae Amin alikubali kitu kimoja kusogeza mbele siku za yule jamaa kuishi lakini sio kumuachia🤣


Sent using Jamii Forums mobile app
 
pia alijipa majina mfano chui mkubwa, the guide, helmsman, rais muanzilishi wa taifa, marechal, papa mobutu, nk
idd amin alimuheshimu sana. Kuna wakati amin alitoa hukumu ya kumuua mwananchi fulani wa uingereza ilibidi mobutu aombwe kumshauri lakini ilichukua masaa na baadae amin alikubali kitu kimoja kusogeza mbele siku za yule jamaa kuishi lakini sio kumuachia🤣


Sent using Jamii Forums mobile app
Viongozi wa enzi zile walipata elimu ya mkoloni.
Kwame Nkurumah alikuwa mwanafunzi wa PhD London School of Economics kabla hajaanza harakati za ukombozi

Kamuzu Banda alikuwa MD

Nyerere alikuwa na Masters ya Edinburgh

Patrice Lumumba usipime

Amin na Mobutu walionekana karumekenge kwenye club hivyo walielewana wenyewe.
 
Huyu jamaa alifikiri hatakufa, lile kasri lake alilojenga na mil dollars za wazaire kijijini kwake likaishia kuwa zizi la mbuzi na popo.



Alijenga majumba mengi ndio maana familia yake haihangaiki na hayo ya kijijini wapo ureno,ufaransa na moroco
lakini mkuu wanasiasa wanajuana, familia ya Mobutu ilirudishiwa mali zote zilizokuwa congo ikiwemo majumba makubwa ya Kinshasa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio Mkuu Viongozi wa juu nyuma ya pazia hawana tofauti kubwa km inavyokuwa wakiwa public
alijenga majumba mengi ndio maana familia yake haihangaiki na hayo ya kijijini wapo ureno,ufaransa na moroco
lakini mkuu wanasiasa wanajuana, familia ya Mobutu ilirudishiwa mali zote zilizokuwa congo ikiwemo majumba makubwa ya kinshasa


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu bwana suit zake zilikuwa designer tupu kutoka France na Belgium

Mambo sky? Siku nyingi sana sijakuona mpaka nimekumiss[emoji6]
ndio suit zote alizovaa zilikua designer cloth maalumu kwa ajili yake na alichagua vitambaa vya bei kubwa tu
kampuni iliyozitengeneza inaitwa Arzoni ipo zellic, Belgium fundi aliyekuwa anampima anaitwa Alfons Mertens
ndiye alimtengenezea mpaka military suit ya dhahabu na kofia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mambo sky ? siku nyingi sana sijakuona mpaka nimekumiss[emoji6]
ndio suit zote alizovaa zilikua designer cloth maalumu kwa ajili yake na alichagua vitambaa vya bei kubwa tu
kampuni iliyozitengeneza inaitwa Arzoni ipo zellic, Belgium fundi aliyekuwa anampima anaitwa Alfons Meryens
ndiye alimtengenezea mpaka military suit ya dhahabu na kofia


Sent using Jamii Forums mobile app
Ninadhani nilichelewa kidogo kuzaliwa au Mobutu aliwahi kidogo. We could have made a perfect couple maana Nina test ya vitu quality 😂
 
Viongozi wa enzi zile walipata elimu ya mkoloni.
Kwame Nkurumah alikuwa mwanafunzi wa PhD London School of Economics kabla hajaanza harakati za ukombozi

Kamuzu Banda alikuwa MD

Nyerere alikuwa na Masters ya Edinburgh

Patrice Lumumba usipime

Amin na Mobutu walionekana karumekenge kwenye club hivyo walielewana wenyewe.

kweli kabisa na ilikua ukitaka ukosane na Amin umdharau [emoji23] ila natamani sana angekuwepo sasa ningemtafuta tupige stori
Amin aliamini waafrica tunadharauliwa na Wazungu hivo alifanya makusudi tu ili awakere kwa mfano amewahi kupanga kuivamia Israel ipo video anaelezea mikakati anakwambia ndani ya masaa machache sjui matatu israel yote anaiteka


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kweli kabisa na ilikua ukitaka ukosane na Amin umdharau [emoji23] ila natamani sana angekuwepo sasa ningemtafuta tupige stori
Amin aliamini waafrica tunadharauliwa na Wazungu hivo alifanya makusudi tu ili awakere kwa mfano amewahi kupanga kuivamia Israel ipo video anaelezea mikakati anakwambia ndani ya masaa machache sjui matatu israel yote anaiteka


Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna wakati Amin alikwenda kumpokea mgeni wake kutoka Falme za Kiarabu mmoja wa wanafamilia wa Kifalme. Alifika Entebe Airport akiwa kwenye baiskeli kumbe nia yake ni kumpa ujumbe kuwa wana shida ya mafuta Uganda.

It worked, mgeni alivyorudi kwao alituma meli ya mafuta Uganda.
 
Back
Top Bottom