Barua ya Rais Mobutu kwenda kwa Rais wa Ufaransa Jacques Chirac

Barua ya Rais Mobutu kwenda kwa Rais wa Ufaransa Jacques Chirac

duuu hebu tupia mkuu

IMG_2906.JPG
IMG_2905.JPG
IMG_2903.JPG
IMG_2902.JPG

video pia ipo nimeshindwa kuidownload



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi wa enzi zile walipata elimu ya mkoloni.
Kwame Nkurumah alikuwa mwanafunzi wa PhD London School of Economics kabla hajaanza harakati za ukombozi

Kamuzu Banda alikuwa MD

Nyerere alikuwa na Masters ya Edinburgh

Patrice Lumumba usipime

Amin na Mobutu walionekana karumekenge kwenye club hivyo walielewana wenyewe.

Hata wa enzi hizi mbona, umesahau "aliyekimbia corona" anatuambia alisoma University of Salford, UK?!
 
Ninadhani nilichelewa kidogo kuzaliwa au Mobutu aliwahi kidogo. We could have made a perfect couple maana Nina test ya vitu quality 😂
Mbona kuna mwingine yupo hapa hapa nae ni mvaa suti quality sana na hazeeki alipokuwa baba wa nyumba yetu kila week alikuwa majuu eti alikuwa anaenda kutuombea ugali
 
Kinshasa, May 11 1997
Kwa Mheshimiwa Rais,
Bwana Jacques Chirac
Rais wa Jamhuri ya Ufaransa

Mheshimiwa Rais,

Kwanza kabisa ningependa kutanguliza salamu zangu za dhati kwako na kwa mkeo, vile vile kwa jina la urafiki mrefu sana ambao umetuunganisha kwa zaidi ya miaka kumi.

Leo hali ni ya machungu sana kwangu mbele ya mvuto wa muda mfupi kwanza kwenye kiwango cha madaraka yangu ambapo nimepoteza ufanisi katika watu, pili katika kiwango cha kijeshi ambapo ni vigumu mimi kuzuia maendeleo ya wanamgambo kuja Kinshasa ambapo wanaweza kufika muda wowote.

Na kuhusu Kinshasa siwezi kukuza umwagaji wa damu usiohitajika kwa namna yoyote ile wanamgambo wataifikia Kinshasa ni suala la muda tu. Je, nina budi kukukumbusha ninapambana na vita visivyokuwa na usawa? Leo Marekani na Uingereza kupitia Afrika Kusini, Uganda, Rwanda na Angola wanamtumia kiongozi wa genge la waharifu Laurent Kabila kunichoma kisu mgongoni huku wakitumia mwanya wa maradhi yangu.

Zamani Marekani walikuwa ni washirika wangu; kumbuka visa vya Angola ninabakiza haki ya kuchapisha kumbukumbu zangu katika siku chache zijazo ili dunia nzima ipate kujua ukweli uliofichika

Rafiki yangu unafahamu kama mimi ninavofahamu kwamba Laurent Kabila ni mtu wa kutilia shaka, muuaji na mwenye tabia zisizofaa kuiongoza Zaire, kama kiongozi wa nchi nimejaribu kwa kila namna kuzuia hili lakini mabwana zake wa Magharibi, Wamarekani, wanamuunga mkono.

Kutokana na ukaidi wa Marekani na kuzidi kuzorota kwa Afya yangu ninalazimika kutangaza lengo langu la kumpa madaraka Kabila katika kikao chetu kijacho katika meli ya Utenika mnamo May 14.

MOBUTU SESE SEKO KUKUNGBENDU WA ZABANGA
MARECHAL
RAIS WA JAMHURI



Sent using Jamii Forums mobile app
Barua hii psychologically anaonekana aliiandika kwa machungu makubwa sana moyoni mwake..maandishi huwa yanaongea aiseeeee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mobutu na Chirac walikuwa ni personal friends, katika barua hii Mobutu anamfahamisha Chirac kusudio la kutoa siri za wamarekani Africa hasa Angola na kuachia madaraka ya nchi

Hii ni moja ya barua za mwisho alizoandika Mobutu akiwa rais

Sent using Jamii Forums mobile app
Binafsi sijawahi kuamini kwamba Mzungu anaweza kua na urafiki wa kweli na mtu mweusi, HAKUNA, yaani hakuna kabisa. Mifano ipo mingi, huyu Mabutu aliyesaliriti weusi wenzie wengi tu akiwepo Nyerere na wapigania Uhuru wengine, hope Angola aliunga mkono kuondolewa madarakani huyu bwana kwasababu ya yeye kua upande wa Savimbi Enzi zile Savimbi anapigana na Do santos kwenye ile vita ilogharimu Maisha ya Waangola wengi, lala vibaya kuzimu Mobutu
 
Binafsi sijawahi kuamini kwamba MZungu anaweza kua na urafiki wa kweli na mtu mweusi, HAKUNA, yaani hakuna kabisa. Mifano ipo mingi, huyu Mabutu aliyesaliriti weusi wenzie wengi tu akiwepo Nyerere na wapigania Uhuru wengine, hope Angola aliunga mkono kuondolewa madarakani huyu bwana kwasababu ya yeye kua upande wa Savimbi Enzi zile Savimbi anapigana na Do santos kwenye ile vita ilogharimu Maisha ya Waangola wengi, lala vibaya kuzimu Mobutu
mkuu katika vita ile mobutu alikuwa mpatanishi tu hadi aliitisha mazungumzo ya amani yaliyopelekea kuwa na GBADOLITE DECLARATION lakini walipoanza kupigana tena Mobutu kama kawaida yake alikuwa na tabia moja katika karibu kila jambo analofanya lazima afaidike kwa kupata pesa
alichokifanya alicheza mchezo wa upigaji yani vifaa vya kivita vilitumwa kwa savimbi kupitia uwanja wa ndege wa Mobutu pale gbadolite so alipata mamilioni ya dollar za kimarekani, huyu mzee alikuwa mjanja yeye anahimiza amani lakini akiona fursa za pesa haachi hata wakati anawasaidia wanyarwanda kuzima mauaji ya wenyewe kwa wenyewe alifanya vile sababu ya rafiki yake
kwenye migodi ya almasi ya Zaire wale ma boss waliowekwa kusimamia walikuwa kila wakienda wanampelekea zawadi briefcase nzima imejaa almasi
 
mkuu katika vita ile mobutu alikuwa mpatanishi tu hadi aliitisha mazungumzo ya amani yaliyopelekea kuwa na GBADOLITE DECLARATION lakini walipoanza kupigana tena Mobutu kama kawaida yake alikuwa na tabia moja katika karibu kila jambo analofanya lazima afaidike kwa kupata pesa
alichokifanya alicheza mchezo wa upigaji yani vifaa vya kivita vilitumwa kwa savimbi kupitia uwanja wa ndege wa Mobutu pale gbadolite so alipata mamilioni ya dollar za kimarekani, huyu mzee alikuwa mjanja yeye anahimiza amani lakini akiona fursa za pesa haachi hata wakati anawasaidia wanyarwanda kuzima mauaji ya wenyewe kwa wenyewe alifanya vile sababu ya rafiki yake
kwenye migodi ya almasi ya Zaire wale ma boss waliowekwa kusimamia walikuwa kila wakienda wanampelekea zawadi briefcase nzima imejaa almasi
Ni kweli mkuu, usemalo upo sahihi sana but apart from huo ujanja wake kuhusu upigaji wa pesa but pia alikua anatumiwa sana na wazungu hasa mataifa ya Magharibi yakiongozwa na USA na Ufaransa; mfano wa kuthibitisha hilo ni hiyo barua yake kwa bwana Chirac, kaonesha kabisa jinsi gani Marekani walikua wakimtumia kwa ile vita ya Angola, vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo upande wa waasi uliongozwa na bwan Savimbi ( Rest in hell ) na huyu bwana alikua financed na mataifa ya magharibi kupitia utawala wa Makabaru, baadhi ya askari wa makaburu waliopigana vita ile kwa upande wa Savimbi nimefanya nao kazi, najua humu kuna watu wamefanya kazi mgodi wa Williamson Diamonds Limited miaka ya mwishoni mwa 90 hadi 2010, yupo bwana mmoja alikua anaitwa Kelvin mmiliki wa mgodi ulikua unaitwa CAD, huyu bwana alikua na mguu wa bandia, akivaa suruali huwezi kujua, alipigwa bomu kwenye vita ile, wapo na wengine wengi nimefanya nao kazi but again, kwenye kikao kimoja wapo cha OAU ( sasa AU ) Mobutu alikua akivujisha sana taarifa kwa Ufaransa na USA kuhusu mijadara yao kwao hao jamaa hadi ikamletea ugomvi kati yake na Nyerere. Pia kama kuna mtu aliwahi kusoma moja kati ya vitabu vya bwana Musiba ( sio huyu mwehu wa sasa hivi ) kinaitwa Kikosi cha Kisasi, utakuta baadhi ya story zihusuzo serikali ya Kinshasa na uhusiano wake na Makaburu na mataifa ya magharibi
 
Jamaa alikua na shule kweli mbona saini yake kama wale wasiojua kusoma na kuandika ukimwambia saini yeye anachora alama tu.😁😁
 
Meli kutoka Falme za Kiarabu kwenda Uganda. Sawa.
Kuna wakati Amin alikwenda kumpokea mgeni wake kutoka Falme za Kiarabu mmoja wa wanafamilia wa Kifalme. Alifika Entebe Airport akiwa kwenye baiskeli kumbe nia yake ni kumpa ujumbe kuwa wana shida ya mafuta Uganda.

It worked, mgeni alivyorudi kwao alituma meli ya mafuta Uganda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wakati Amin alikwenda kumpokea mgeni wake kutoka Falme za Kiarabu mmoja wa wanafamilia wa Kifalme. Alifika Entebe Airport akiwa kwenye baiskeli kumbe nia yake ni kumpa ujumbe kuwa wana shida ya mafuta Uganda.

It worked, mgeni alivyorudi kwao alituma meli ya mafuta Uganda.
Meli ya mafuta Uganda ilipitia njia ipi?
 
Uzuri wa JF ni mwalimu tosha.Nimejifunza kitu kikubwa sana,dunia ni ya Mungu,mali,madaraka,na kila aina ya utajiri tulionao ni vitu vya kupita,cha msingi ni kuishi kwa utashi na kumweka mwenyezi mbele.

Nothing last forever, Power will shift, enemies will vanish.
 
Back
Top Bottom