Barua ya Rais Mobutu kwenda kwa Rais wa Ufaransa Jacques Chirac


Hata wa enzi hizi mbona, umesahau "aliyekimbia corona" anatuambia alisoma University of Salford, UK?!
 
Ninadhani nilichelewa kidogo kuzaliwa au Mobutu aliwahi kidogo. We could have made a perfect couple maana Nina test ya vitu quality πŸ˜‚
Mbona kuna mwingine yupo hapa hapa nae ni mvaa suti quality sana na hazeeki alipokuwa baba wa nyumba yetu kila week alikuwa majuu eti alikuwa anaenda kutuombea ugali
 
Barua hii psychologically anaonekana aliiandika kwa machungu makubwa sana moyoni mwake..maandishi huwa yanaongea aiseeeee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sijawahi kuamini kwamba Mzungu anaweza kua na urafiki wa kweli na mtu mweusi, HAKUNA, yaani hakuna kabisa. Mifano ipo mingi, huyu Mabutu aliyesaliriti weusi wenzie wengi tu akiwepo Nyerere na wapigania Uhuru wengine, hope Angola aliunga mkono kuondolewa madarakani huyu bwana kwasababu ya yeye kua upande wa Savimbi Enzi zile Savimbi anapigana na Do santos kwenye ile vita ilogharimu Maisha ya Waangola wengi, lala vibaya kuzimu Mobutu
 
mkuu katika vita ile mobutu alikuwa mpatanishi tu hadi aliitisha mazungumzo ya amani yaliyopelekea kuwa na GBADOLITE DECLARATION lakini walipoanza kupigana tena Mobutu kama kawaida yake alikuwa na tabia moja katika karibu kila jambo analofanya lazima afaidike kwa kupata pesa
alichokifanya alicheza mchezo wa upigaji yani vifaa vya kivita vilitumwa kwa savimbi kupitia uwanja wa ndege wa Mobutu pale gbadolite so alipata mamilioni ya dollar za kimarekani, huyu mzee alikuwa mjanja yeye anahimiza amani lakini akiona fursa za pesa haachi hata wakati anawasaidia wanyarwanda kuzima mauaji ya wenyewe kwa wenyewe alifanya vile sababu ya rafiki yake
kwenye migodi ya almasi ya Zaire wale ma boss waliowekwa kusimamia walikuwa kila wakienda wanampelekea zawadi briefcase nzima imejaa almasi
 
Ni kweli mkuu, usemalo upo sahihi sana but apart from huo ujanja wake kuhusu upigaji wa pesa but pia alikua anatumiwa sana na wazungu hasa mataifa ya Magharibi yakiongozwa na USA na Ufaransa; mfano wa kuthibitisha hilo ni hiyo barua yake kwa bwana Chirac, kaonesha kabisa jinsi gani Marekani walikua wakimtumia kwa ile vita ya Angola, vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo upande wa waasi uliongozwa na bwan Savimbi ( Rest in hell ) na huyu bwana alikua financed na mataifa ya magharibi kupitia utawala wa Makabaru, baadhi ya askari wa makaburu waliopigana vita ile kwa upande wa Savimbi nimefanya nao kazi, najua humu kuna watu wamefanya kazi mgodi wa Williamson Diamonds Limited miaka ya mwishoni mwa 90 hadi 2010, yupo bwana mmoja alikua anaitwa Kelvin mmiliki wa mgodi ulikua unaitwa CAD, huyu bwana alikua na mguu wa bandia, akivaa suruali huwezi kujua, alipigwa bomu kwenye vita ile, wapo na wengine wengi nimefanya nao kazi but again, kwenye kikao kimoja wapo cha OAU ( sasa AU ) Mobutu alikua akivujisha sana taarifa kwa Ufaransa na USA kuhusu mijadara yao kwao hao jamaa hadi ikamletea ugomvi kati yake na Nyerere. Pia kama kuna mtu aliwahi kusoma moja kati ya vitabu vya bwana Musiba ( sio huyu mwehu wa sasa hivi ) kinaitwa Kikosi cha Kisasi, utakuta baadhi ya story zihusuzo serikali ya Kinshasa na uhusiano wake na Makaburu na mataifa ya magharibi
 
Jamaa alikua na shule kweli mbona saini yake kama wale wasiojua kusoma na kuandika ukimwambia saini yeye anachora alama tu.😁😁
 
Meli kutoka Falme za Kiarabu kwenda Uganda. Sawa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meli ya mafuta Uganda ilipitia njia ipi?
 
Uzuri wa JF ni mwalimu tosha.Nimejifunza kitu kikubwa sana,dunia ni ya Mungu,mali,madaraka,na kila aina ya utajiri tulionao ni vitu vya kupita,cha msingi ni kuishi kwa utashi na kumweka mwenyezi mbele.

Nothing last forever, Power will shift, enemies will vanish.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…