Uchaguzi 2020 Barua ya Wazi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu (2020) za Mheshimiwa Tundu Lissu

Baada ya 28/10/2020 utamuonea huruma tu sana sana atakimbilia Ubelgiji na kukuacha wewe unapata kipigo cha mbwa koko!!
Tundu Lissu anakwea pipa anaenda kusikilizia Ubelgiji huku anakunywa wine taratiiibu na mamsapu wake
 
Nadhani inabidi apingwe kwa hoja zenye nguvu. Ikiwa aliyoyasema ni uongo ama la
 
Sema yote lakini uadilifu wa Rais Magufuli sio wa kutiliwa shaka hata kidogo.

Sio muadilifu, bali anashurutisha kuonekana muadilifu. Madictotar wote hutengeneza taswira ya kutaka kuonekana waadilifu. Mtu muadilifu sio adui wa uhuru wa habari. Ogopa sana mtu anayetumia madaraka yake kulazimisha kuonekana mtu mwema. Tuna akili zetu na tunaweza kupima uadilifu wa mtu. Mfano mrahisi sana, toka ameingia madarakani, chaguzi zetu ndio zimegubikwa na ukatili, ukiukwaji mkubwa wa sheria, uhayawani na ukatili wa wazi. Kwa mtu muadilifu, uchaguzi wa SM usingeweza kuwa ulivyokuwa, na yote ni maagizo yake.
 
Acha kuweweseka! Tulienda dawa ya Lissu iwaingie vizuri
 
Point hapo ni " Uchaguzi wa huru a haki". Ikitokea umeona hujatendewa haki basi Kuna njia za kisheria za kufuata na sio kumwaga damu ya wananchi
Acha kuota ndoto za vurugu na umwagaji wa damu usiokuwepo!
Zile propaganda za kizamani za kutuwekea sinema za kivita kwenye tv zenu ili kuutisha umma usiache kuichagua ccm eti ni chama chenye kuilinda amani zimekukaa ubongoni mwako na kuganda!
Hizi fitina zako ziko wazi kwani umewaadress wateule wa ccm na ambao ni mawakala na makada wa ccm ambao Wana maagizo ya kulazimisha na kumtangqza mshindi kutoka ccm hata Kama hajashinda! Hamasa yako hii inahanikiza hizo vurugu na uvunjivu wa amani Kama hukujua ujue hivyo!
Binafsi nakuona mjinga usiyeweza kuwaza sawasawa bila kuwa na upande! Hakuna wa kutishiwa kipuuzi Kama unavyodhani na ikibidi kuidai haki na demokrasia isiyo na konakona tutafanya hivyo bila ushawishi na kikwazo Cha aina yoyote kutoka kwa mwanasiasa! Wananchi wa Sasa wanajitambua hivyo usiwapangie!
 
Mkuu shida ni kuwabtunataka amani na unoja wetu udumu na kuwa hatutamvumiliaa yeyote anauetaka kupoka vitu hivyo
umoja na amni bila haki mkuu hawezekaniki, haki kwanza mengine hufuata, haki..haki...haki...haki..haki, sio maneno yangu bali limehubiliwa enzi na enzi toka zama za mitume na manabihi mkuu, penye haki kila kitu huwa shwari . tafakari na chukua hatua mkuu
 
Hilo la kura za vijijini umelisema wewe, mimi nilikuletea na kuongezea Hilo la kura za bure ukidhani vijijini hawajielewi. So usinilishe maneno. Baki mwenyewe na dhambi yako ya ubaguzi

Ni kweli hawajielewi, na kutokujielewa si kosa, ni matokeo ya elimu duni inayotolewa na chama unachokipigia debe. Kusema mtu hajielewi na neno ulilonipandikizia la ubaguzi si sahihi. Hata hivyo TL anawapenda ndio maana kila siku anawafundisha elimu ya uraia ili watambue wajibu na haki zao. Kama kawaida yenu nimewashauri muwekeze huko kabla TL hajafika ili mjipatie kura za bure. Huku hampati watu na mnalipwa buku 7 za bure tu!
 
Waambie pia juu ya kutenda haki kwenye mchakato wa wagombea na wakati wa uchaguzi ili kuepusha vurugu na ukosefu wa amani kwa wagombea ambao wataona hawajatendewa haki.

Waambie wawarudishe wagombea wote walioenguliwa ili wananchi wapate haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi kwa sanduku la kura na si wengine wateuliwe(wakisemwa wamepita bila kupingwa) kama wale wa viti maalum

Waambie wasimamie maadili kwa kuwaonya wagombea kutumia lugha zao za asili na si lugha ya taifa pasipo wakalimani na pia kutumia nyimbo za lugha zao pasipo kuwa na beti za tafsiri.

Waambie viongozi wenye nafasi za kiserikali waache kutoa ahadi/maelekezo majukwaani ambazo zina mwonekano wa rushwa ili wapigiwe kura.

Waambie wagombea walioko serikalini wasitoe maelekezo kwa watumishi kuhudhuria kwenye mikutano ya kampeni kwa lazima kwani watumishi wanatokana na vyama mbalimbali. Wananchi waudhurie kwa hiari yao kama watapenda.
 
We umeambiwa na nani?
Kwa iyo uwanja wa kimataifa Chagonja haujajengwa??? Kwa iyo Mayanga contractors sio kampuni inayojenga??? Kwa iyo Bunge lilipotisha ujenzi wa uwanja wa ndege chato????

Au unataka kusemaje kilaza wa lumumba wewe????
 
Tangu kampeni zianze sijamuona mgombea yeyote akipiga kampeni kwa kilugha chake au lugha yoyote zaidi ya lugha yetu adhimu, lugha ya taifa kiswahili. Sana sana nimewasikia wagombea wakichomekea kisukuma na kiingereza (Magufuli) na kiingereza (Lissu).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…