Barua ya wazi kwa Tundu Lissu kumuonya dhidi ya kutetea masikini na wapumbavu

Barua ya wazi kwa Tundu Lissu kumuonya dhidi ya kutetea masikini na wapumbavu

Mbona barua hii haimuhusu
Haimhusu kivipi wakati yeye ni rais wa wanyonge hao ambao ni maskini na wapumbavu.

Najua umetumia fasihi kumfikishia ujumbe. Jiandae tunakutafuta ukaeleze upupu mbele ya wazee wa kazi .
 
Niliipitiaga kipindi kabla hata lissu hajarudi bongo nadhan, niliielewa sana na niliiafiki, ktk wakt huu nilikuwa naitafuta sana hii mada bt hatimae imefufuliwa so umeongea ukweli mtupu mkuu, unapigania wa pumbavu na wajinga.
 
Haimhusu kivipi wakati yeye ni rais wa wanyonge hao ambao ni maskini na wapumbavu.

Najua umetumia fasihi kumfikishia ujumbe. Jiandae tunakutafuta ukaeleze upupu mbele ya wazee wa kazi .

Wewe ni panya mdogo tuu,
Jina hilo hapo, namba hizo hapo na location nimekuwekea huna haja ya kunitafuta, piga simu nije. Sitishwagi na panya
 
Unasema, awatetee matajiri na wenye uwezo na akili, SAWA....

Unasema aachane na masikini na wapumbavu kwa sababu hao hao ndiyo wanaoweza kumgeuka na kuanza kumponda mawe, SAWA....

Logic ya hoja hii ni kuwa ajiunge na matajiri, watawala na wanaonyanyasa na kuonea masikini...

Hawa ndiyo kina Magufuli na maCCM wenzake... HII SIYO SAWA. Nitaeleza kwanini;

å Umetoa mifano ya watetezi wa masikini wa kale kina Mussa na Yesu Kristo...

Kwamba, hawa masikini waliwageuka hawa wanaharakati na watetezi wao kwa kuwapiga kwa mawe (Mussa) na kuuwawa kabisa (Yesu Kristo)...

å Ni kweli, ndivyo ilivyokuwa. Na infact hii ndiyo gharama (price) ya kutetea masikini. Na yeyote anayejitosa kutetea masikini na wajinga anapaswa kujua kuwa anatetea watu ambao hata hawaelewi kuwa wako utumwani na hawastahili kuwa hivyo walivyo. Wao wanajua, hayo ndiyo maisha na stahili yao...

å Kwa mwanaharakati yeyote wa haki za binadamu ambaye hajui gharama ya harakati zake, ni vyema asishiriki kabisa kutetea na kuwakomboa masikini, wajinga na wapumbavu...

å Lengo la kuwatetea masikini, wajinga na wapumbavu ni ili huo umasikini wao na ujinga wao na upumbavu wao uwatoke. Ili umtibu kichwa, sometimes utalazimika kula makonde na mateke...

å Ndivyo ilivyokuwa na ndilo lengo la Mungu aliyewatuma Mussa na Yesu Kristo. Hawa mitume, walijua kabisa wanawatetea na kuwaongoza watu wasiojielewa walq kujitambua, wasiojua wajibu na haki zao...

KWA HIYO;

Binafsi, sikubaliani na onyo lako la kumtaka Tundu Lissu kuachana na mission yake, kuachana na harakati zake kuwatetea masikini na wajinga wengi...

Akiacha ni nani atafanya kazi hiyo?

Umesema, masikini hawa watatetewa na kukombolewa na Mungu muumba wao...

Hii ni kweli kabisa, kwamba Mungu muumba ndiye mkombozi wetu...

Lakini Mungu hawezi kushuka yeye physically na kuanza kufanya kazi hii. Mungu huwatumia watu na kuwapa uwezo wake kufanya kazi ya kukomboa na kutetea watu wake...!

Mimi ningependa kuwaona watu wa aina ya Tundu Lissu na wengine wasonge mbele so long as wana wito wa kuwakomboa na kuwatetea ndugu zao masikini na wajinga wanaoonewa na kunyanyasika maana wafanyalo hakika ni mapenzi ya Mungu Yehova....!!
 
Mwandishi hongera kwa uwezo na kipaji cha uandishi. Ila kwa upande wa mantiki andiko lako ni general falacy.

Ulichokiandika kina ukweli katika mazingira flani ila haina ukweli wa jumla.

Ulichokiandika hakina back up ya kimantic na kihistoria ya maumbile bali ni hisia na imagination tu.

Funzo la historia ni kuwa reward iko kwa mtu aliyepigana kuleta au kuongeza thamani kwenye humanity

Unyonyaji, ubinafsi , kutokuwajibika na kujinufaisha kuliwezesha watu kujenga makasri, kumilki nguvu ya kiutawala na kunufaisha wachache. Kwa bahati mbaya mambo kama haya hayajawahi kuthaminiwa wala kukumbukwa na vizazi bali wahusika wanapokufa na historia yao uzimika kama mshumaa.

Najiuliza Nyerere angekua na akili kama hizi taifa letu lingekuaje?

Najiuliza Nelson mandela angekua na akili za kibnafsi kama hizi SA historia yake ingekuaje?

Najiuliza Patrick Limumba angekua na akili kilema kama hizi harakati za pan africanism zingekua wapi ?

Twende sasa kwenye hoja ya msingi.

Imagine Musa, joshua, Samsoni, Daudi, Isaya, Yeremia na wengine kama hao ambao walitoa maisha yao ya kitume kujaribu kuongeza heshima kwenye utu wa mwanadamu, wengi wao walipitia magumu sana ila wito wao uliwafanya wafike mwisho.

Jamii zote zina matabaka . Liko tabaka lenye nguvu na tabaka la malofa na lingine ni tabaka la kati. Kilicho cha ajabu harakati nyingi uhibuka kulitetea kundi la malofa ambalo umeliita la masikini na wapumbafu. Sijui kwa nini hakuna historia inayoonyesha harakati ya jamii ililenga kulifanya tabaka lenye nguvu liimarike na kuzidi kuwa bora zaidi. Nazani kuna uungu na nguvu ya kiasili ambayo mwanadamu ameumbiwa ya kujali na kupenda kukiongezea thamani kilicho kinyonge.

Musa alichokifanya ni kuongeza thamani ya ndugu zake watumwa. Walimpinga toka nchi ya Misri ila kwa msaada wa Bwana kizazi kipya kilifaidi matunda ya kuishi kwenye nchi ya ahaadi ilijaa maziwa na asali.

Kristo pia alifanya the same. Alisalitiwa na rofa aliyemfanya rafiki na mwanafunzi. Aliposhikwa rafiki zake hawakuweza kumtetea, aliposurubiwa baadhi ya akina mama na wanaume wachache wanyonge waliishia kumlilia na kumbea. Thanks to God kumbe sadaka ya kifo chake kimekua msingi wa maisha ya matumaini kwa vizazi vyote duniani. Ni mpambanaji na mwanafalsafa mwenye wafuasi wengi kuliko wote waliowahi kuishi. Injiri yake inanguvu hadi leo. Mafundisho yake yakifanyiwa reference hadi leo wakuu na wenye mamlaka wanapiga magoti hata kama ni kwa unafiki?

Kwa mifano chanya kama hii ambayo inaongeza thamani katika maisha ya binadamu nani atasimama na kuwaziba midomo wana harakati , watetezi wa wanyonge, sauti ya wasio na nguvu kama hawa?

Tundu lisu ni miongoni mwa nafsi zilizojitoa sadaka. Achilia maumivu anayotembea nayo mwilini mwake na moyoni mwake ila amebaki kama mshumaa wa shujaa kwa jamii hii ya kitanzania.

Tulio wengi tutamuombea daima na mungu amtangulie.
 
Mwandishi hongera kwa uwezo na kipaji cha uandishi. Ila kwa upande wa mantiki andiko lako ni general falacy.

Ulichokiandika kina ukweli katika mazingira flani ila haina ukweli wa jumla.

Ulichokiandika hakina back up ya kimantic na kihistoria ya maumbile bali ni hisia na imagination tu.

Funzo la historia ni kuwa reward iko kwa mtu aliyepigana kuleta au kuongeza thamani kwenye humanity

Unyonyaji, ubinafsi , kutokuwajibika na kujinufaisha kuliwezesha watu kujenga makasri, kumilki nguvu ya kiutawala na kunufaisha wachache. Kwa bahati mbaya mambo kama haya hayajawahi kuthaminiwa wala kukumbukwa na vizazi bali wahusika wanapokufa na historia yao uzimika kama mshumaa.

Najiuliza Nyerere angekua na akili kama hizi taifa letu lingekuaje?

Najiuliza Nelson mandela angekua na akili za kibnafsi kama hizi SA historia yake ingekuaje?

Najiuliza Patrick Limumba angekua na akili kilema kama hizi harakati za pan africanism zingekua wapi ?

Twende sasa kwenye hoja ya msingi.

Imagine Musa, joshua, Samsoni, Daudi, Isaya, Yeremia na wengine kama hao ambao walitoa maisha yao ya kitume kujaribu kuongeza heshima kwenye utu wa mwanadamu, wengi wao walipitia magumu sana ila wito wao uliwafanya wafike mwisho.

Jamii zote zina matabaka . Liko tabaka lenye nguvu na tabaka la malofa na lingine ni tabaka la kati. Kilicho cha ajabu harakati nyingi uhibuka kulitetea kundi la malofa ambalo umeliita la masikini na wapumbafu. Sijui kwa nini hakuna historia inayoonyesha harakati ya jamii ililenga kulifanya tabaka lenye nguvu liimarike na kuzidi kuwa bora zaidi. Nazani kuna uungu na nguvu ya kiasili ambayo mwanadamu ameumbiwa ya kujali na kupenda kukiongezea thamani kilicho kinyonge.

Musa alichokifanya ni kuongeza thamani ya ndugu zake watumwa. Walimpinga toka nchi ya Misri ila kwa msaada wa Bwana kizazi kipya kilifaidi matunda ya kuishi kwenye nchi ya ahaadi ilijaa maziwa na asali.

Kristo pia alifanya the same. Alisalitiwa na rofa aliyemfanya rafiki na mwanafunzi. Aliposhikwa rafiki zake hawakuweza kumtetea, aliposurubiwa baadhi ya akina mama na wanaume wachache wanyonge waliishia kumlilia na kumbea. Thanks to God kumbe sadaka ya kifo chake kimekua msingi wa maisha ya matumaini kwa vizazi vyote duniani. Ni mpambanaji na mwanafalsafa mwenye wafuasi wengi kuliko wote waliowahi kuishi. Injiri yake inanguvu hadi leo. Mafundisho yake yakifanyiwa reference hadi leo wakuu na wenye mamlaka wanapiga magoti hata kama ni kwa unafiki?

Kwa mifano chanya kama hii ambayo inaongeza thamani katika maisha ya binadamu nani atasimama na kuwaziba midomo wana harakati , watetezi wa wanyonge, sauti ya wasio na nguvu kama hawa?

Tundu lisu ni miongoni mwa nafsi zilizojitoa sadaka. Achilia maumivu anayotembea nayo mwilini mwake na moyoni mwake ila amebaki kama mshumaa wa shujaa kwa jamii hii ya kitanzania.

Tulio wengi tutamuombea daima na mungu amtangulie.

Here we Goo
 
Unasema, awatetee matajiri na wenye uwezo na akili, SAWA....

Unasema aachane na masikini na wapumbavu kwa sababu hao hao ndiyo wanaoweza kumgeuka na kuanza kumponda mawe, SAWA....

Logic ya hoja hii ni kuwa ajiunge na matajiri, watawala na wanaonyanyasa na kuonea masikini...

Hawa ndiyo kina Magufuli na maCCM wenzake... HII SIYO SAWA. Nitaeleza kwanini;

å Umetoa mifano ya watetezi wa masikini wa kale kina Mussa na Yesu Kristo...

Kwamba, hawa masikini waliwageuka hawa wanaharakati na watetezi wao kwa kuwapiga kwa mawe (Mussa) na kuuwawa kabisa (Yesu Kristo)...

å Ni kweli, ndivyo ilivyokuwa. Na infact hii ndiyo gharama (price) ya kutetea masikini. Na yeyote anayejitosa kutetea masikini na wajinga anapaswa kujua kuwa anatetea watu ambao hata hawaelewi kuwa wako utumwani na hawastahili kuwa hivyo walivyo. Wao wanajua, hayo ndiyo maisha na stahili yao...

å Kwa mwanaharakati yeyote wa haki za binadamu ambaye hajui gharama ya harakati zake, ni vyema asishiriki kabisa kutetea na kuwakomboa masikini, wajinga na wapumbavu...

å Lengo la kuwatetea masikini, wajinga na wapumbavu ni ili huo umasikini wao na ujinga wao na upumbavu wao uwatoke. Ili umtibu kichwa, sometimes utalazimika kula makonde na mateke...

å Ndivyo ilivyokuwa na ndilo lengo la Mungu aliyewatuma Mussa na Yesu Kristo. Hawa mitume, walijua kabisa wanawatetea na kuwaongoza watu wasiojielewa walq kujitambua, wasiojua wajibu na haki zao...

KWA HIYO;

Binafsi, sikubaliani na onyo lako la kumtaka Tundu Lissu kuachana na mission yake, kuachana na harakati zake kuwatetea masikini na wajinga wengi...

Akiacha ni nani atafanya kazi hiyo?

Umesema, masikini hawa watatetewa na kukombolewa na Mungu muumba wao...

Hii ni kweli kabisa, kwamba Mungu muumba ndiye mkombozi wetu...

Lakini Mungu hawezi kushuka yeye physically na kuanza kufanya kazi hii. Mungu huwatumia watu na kuwapa uwezo wake kufanya kazi ya kukomboa na kutetea watu wake...!

Mimi ningependa kuwaona watu wa aina ya Tundu Lissu na wengine wasonge mbele so long as wana wito wa kuwakomboa na kuwatetea ndugu zao masikini na wajinga wanaoonewa na kunyanyasika maana wafanyalo hakika ni mapenzi ya Mungu Yehova....!!


Huwezi ukatetea masikini au wajinga ukafika popote
 
Lissu, watanzania wanakuelewa na ndiyo maana kama mifumo ya kiutawala ingekuwa sawa leo hii wewe ungekuwa Rais wa nchi. Tatizo la nchi yetu mifumo yote inatetea na kulinda utawala uliopo madarakani na ndiyo maana wewe unatuongoza leo tupate KATIBA MPYA ambayo itaweka sawa check & balance ya mihimili yote, na msingi wa utawala wa nchi yetu urudi mikononi mwa wananchi wenyewe.

Usikate tamaa, ukiona mbu wanashambulia miguuni kwa ushirikiano mkubwa basi elewa panakaribia kucha.
 
Lissu, watanzania wanakuelewa na ndiyo maana kama mifumo ya kiutawala ingekuwa sawa leo hii wewe ungekuwa Rais wa nchi. Tatizo la nchi yetu mifumo yote inatetea na kulinda utawala uliopo madarakani na ndiyo maana wewe unatuongoza leo tupate KATIBA MPYA ambayo itaweka sawa check & balance ya mihimili yote, na msingi wa utawala wa nchi yetu urudi mikononi mwa wananchi wenyewe.

Usikate tamaa, ukiona mbu wanashambulia miguuni kwa ushirikiano mkubwa basi elewa panakaribia kucha.


😃😃😃😃😃😃
 
BARUA YA WAZI KWA TUNDU LISU

Na, Robert Heriel
Taikon wa Fasihi,
S.L.P 9977, JIBI,
Kutoka Nyota ya Tibeli.
30, 07. 2020.

YAH: KUKUONYA DHIDI YA KUTETEA MASIKINI NA WAPUMBAVU.

Ndugu Mhe Lisu, Kichwa cha habari hapo juu cha husika.

Ninafuraha kubwa kukuandikia barua hii ya wazi ambapo najua watu wengi wataisoma nawe itakufikia. Utanisamehe ikiwa njia hii niliyoitumia pengine isikufurahishe lakini ni katika hali ya kukupa ujumbe wenye manufaa wewe na wale wote wenye tabia kama zako, mimi nikiwa mmoja wao.

Mhe. Lisu, nimekufuatilia kwa miaka saba sasa, sisemi nakufahamu lakini angalau ninachakusema kidogo kukuhusu. Umejipambanua kama mtu apendaye haki, mtu apendaye utawala wa sheria, mtu apendaye demokrasia. Lisu umekuwa mstari wa mbele kukemea maonevu uyaonayo ndani ya nchi yako, umejigeuza kama msemaji wa wanaoonewa, kutetea wanyonge wanaonyimwa haki zao. Upo sawa, lakini umekosea jambo moja; nalo ni kushindwa kujua unatetea watu wa aina gani. Hilo ndilo kosa lako kuu.

Huwezi tetea haki za masikini ukabaki salama, huwezi tetea haki za wapumbavu ukabaki salama. Huwezi tetea watu wasiojielewa, huwezi tetea watu wasiojua unapigania nini kwao, huko ni kujitafutia matatizo makubwa ambayo hao unaowatetea hawatakusaidia kitu kwa sababu wao ni wapumbavu na masikini.

Kikawaida masikini ni watu wasiojithamini, watu wasio na shukrani, watu wasiojitambua, wengi wao ni wachawi, wanga, watu wasio na fadhila, masikini ukimsaidia huyo huyo ndio atakuja kukusema unajidai, ukimtetea masikini au mpumbavu huyo huyo ndio atakuambia unakihere here. Kamwe nakusihi acha mara moja kuhangaika na masikini.

Masikini unachoweza kuwasaidia ni kuwadhulumu hata kile kidogo walichonacho, kuwabagua, kuwatenga, kuwadharau, hicho ndicho wakipendacho masikini. Lakini ukijifanya unawapenda, unawajali nakuhakikishia unajiingiza mkenge, utaumia, utasagika na hakika utamalizika.

Nikukumbushe Ndugu Mhe. Lisu, hakuna aliyewahi kuwatetea masikini, na kuwapigania masikini akabaki salama. Wote waliojiingiza katika harakati hizo walikufa vifo vibaya, wengine walipewa adhabu kali za kuliwa na mamba, kuliwa na simba, kuchomwa moto, wakapotea na kuangamia.

Katika Dini, wapo Manabii walikuja kutetea haki za wanyonge, haki za masikini lakini wote waliuawa, tena wakazomewa na hao hao masikini. Nakupa mifano ya watu katika dini waliokuwa wanaharakati kama wewe, Musa, ndiye yule Mlawi aliyewatoa waisrael Misri, naye aliwapigania watumwa wale na kutaka kuwa uhuru wao. walichomlipa wote tunajua, walianza kulalamika kuwa bora warudishwe utumwani Misri kuliko kuwa huru Kanaani katika nchi yao. Mungu alitaka kuwaua lakini Kihere here cha Musa akawatetea, siku zilizofuata wakataka kumuua Musa wasijue huyo ndiye aliwatetea wasiuawe na Mungu. Musa alipowashtaki kwa Mungu, Mungu akamuambia, wewe si uliwatetea hao masikini, watumwa, wapumbavu wasiojielewa. Acha wakuue ili uwe na akili. Musa akabaki katumbua macho. Biblia inasema, Mungu aliwafyeka wote njiani, akambakiza Joshua na Kalebu. Huwezi kukomboa masikini, huwezi komboa watumwa, huwezi komboa wapumbavu ukabaki salama. Kuwatetea wapumbavu ni kutaka kutofika kanaani, usishangae kwa nini Musa hakufika Kanaani, aliwaendekeza wapumbavu wale.

Yesu naye walimuua, wakamsulubisha, na kumtemea mate. Na wale aliokuwa anawatetea ndio hao hao waliomtukana, walioimba asulubiwe. Huwezi Mkomboa masikini hata siku moja. Huwezi komboa mtu mpumbavu ukasalimika.

Hata kwenye maisha ya kawaida, wale unaowasaidia ndio hao hao watakaogeuka maadui zako. Hao hao ndio watakao kuteta.

Mhe Lisu, naomba nikuonye, na ikikupendeza fuata ushauri wangu. Acha kutetea haki za wapumbavu, haki za masikini, haki za wanyonge sijui upuuzi gani. Mungu mwenyewe atahangaika na watu wake. Ikiwa yeye kaacha watu waonewe wewe unakuja kuwatetea huoni unatafuta maneno.

Masikini ni kama swala au digidigi mbugani, huwezi mgeuza digidigi akawa simba alafu ukabaki salama. Ili mbuga iwe na amani ni lazima swala aliwe, kumtetea swala ni kuchafua amani ya mbugani.

Nature inataka dunia iende hivyo, wote waliojifanya kutetea tabaka la chini walipotezwa, na uhakika ni kuwa watazidi kupotezwa.

Nakushauri; tetea watu wenye akili, watu matajiri, watu wenye nguvu, hao utapata ulinzi, hao hawana unafiki, hao utapata cheo, na utaishi kwa amani.

Matajiri ukiwatetea wanajua thamani ya kile unachokifanya, hivyo nawe watakutetea siku yakikukuta yako. Lakini masikini ukiwatetea kwanza wao wenyewe hawajui thamani yao iweje wajue thamani ya kile ukifanyacho, zaidi sana watakutelekeza siku yakikupata kisha watakuambia ulikuwa unakihere here.

Watu wenye akili ukiwatetea watakulinda, kwa maana wanajali kile ukifanyacho, watakulipa hisani na fadhila. Lakini wapumbavu ukiwatetea hao hao watakuwa wakwanza kukusnitch na kukuuza kwa bei ya kutupwa, mwisho utauawa na kuangamizwa.

Wenye nguvu ukipendekeza kwao, watakulinda. Wao wanajua na kuthamini mchango wako kwao. Lakini sio kwa watu wanyonge na fukara. Wanyonge wataishia kukusengenya na kukuloga, ukiwa mbele yao wanakushangilia ukitoka wanakusema. Wataachaje kukusema ikiwa hawana kazi, kazi yao ni kusengenya watu vijiweni.

Mhe. Lisu, acha kupoteza muda wako. Hutapata zawadi popote pale iwe huku duniani au kwa yule aliyeiumba hii dunia.

Aliyeumba hii dunia ndiye anataka dunia iwe hivi ilivyo, wapumbavu wahenyeke, wenye hekima wale bata. Masikini wachapike, matajiri wale upepo mwanana.

Namna bora ya kumsaidia masikini ni kumdhulumu na kumuonea. Namna bora ya kumsaidia mpumbavu ni kumfundisha upumbavu,.

Kufikia hapa Mhe, Lisu niseme ni matumaini yangu barua hii utakuwa umeielewa. Na utaifanyia kazi.

Wako katika majukumu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
robertheriel99@gmail.com

Nakala moja kwa

1. Tundu Anthipas Lisu
2. Wanaharakati wote
3. Wanamageuzi

Nakala nyingine nitabaki nayo.
A touch of genius - with a light touch, for sure. Salute!
 
Back
Top Bottom