Uchaguzi 2020 Barua yangu na wito wangu kwa IGP, Tume ya Uchaguzi na wenyeviti wa Vyama vya Siasa Taifa

Uchaguzi 2020 Barua yangu na wito wangu kwa IGP, Tume ya Uchaguzi na wenyeviti wa Vyama vya Siasa Taifa

Brightg

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2013
Posts
372
Reaction score
662
1. Tusimamie haki, tutende haki na tuhamasishe watu wetu kutotumia nguvu inayo dhuru mtu, ua watu , kupoteza watu na kuharibu uchaguzi. Toka tulipoanza na tulipofikia kuna matukio mengi tayari (kwa mujibu wa picha na malalamiko). Tunakokwenda na baada ya uchaguzi matukio hayo yasiwepo kamwe.

2. Kuna maisha baada ya uchaguzi, maisha haya yanaweza yakawa ya kuhangaika na mahakama hapa nchini au nje ya nchi popote pale huwezi jua, kwa tetesi ni kwamba kuna ushahidi unakusanywa mwingi kwenye ngazi zote kutoka kwa waliodhurika, waliokuwepo eneo la tukio na wanaoishi maeneo ya tukio, ushahidi ni wa picha, makovu na sauti, hii ni mbaya sana kwetu sisi watanzania kufikia hatua hii au watu wengine wa nje kupewa ripoti kama hizi (kuna ripoti imeandikwa na mwanasheria flan ina ukurasa zaidi ya 27) hatujafurahia kuisoma sio nzuri kwetu mtu wa nje kupokea na kuandika.

3. Dunia imebadilika na watanzania wamesoma sana, sio kama ile ya miaka yote. Tukumbuke kilicho mtokea Rais wa Kenya, Makamu wake na mwandishi wa Habari hakikuwa kizuri, walihangaika sana na mahakama hawakuwa na amani mioyoni mwao, ni Umoja wa Africa tu ndio uliwasaidia kuwaombea wasishtakiwe kwa majukumu waliyo nayo ila walijuta na walisikitika sana kwa kilichotokea ndio maana sasa hivi maisha yao ya uongozi hawataki kamwe kujihusisha na lolote lile ovu maana wanaelewa, tunaweza tukajifunza kutoka kwao.

4. Madaraka yasitulevye, kuna maisha baada ya vyeo tulivyo navyo, tuandalie vizazi vyetu maisha mema ya badae, tusiache kumbukumbu ya vitu ambavyo havitaleta Baraka na havitaacha alama ya kazi nzuri kwa nchi yetu. Kisheria hamna mwenye hati miliki ya nchi ya Tanzania, kwanza Tanzania ipo kisheria kuanzia ngazi ya umoja wa mataifa hadi huku chini hakuna mwenye uwezo wakuongeza mipaka ya ramani yake nje ya nchi ndivyo ilivyo hakuna mwenye mamlaka wa kujimilikisha kuwa ni yakwake binafsi. Tutakufa tutaiacha na itaendelea kuwepo tu.

5. Ushahidi anao ukusanya huyu Robert Amsterdam kutoka kwa Mwananchi mmoja mmoja au makundi kama alivyoandika kwenye twitter yake; nimeambatanisha hapa, ipo siku tutashangaa aliupataje, sio mzuri tuhakikishe ushahidi huo haupatikani ni pamoja na kuwasisitiza watu tunao waongoza waache tamaa na wasimtendee yeyote yule chochote kile.

robert.png

MUNGU ATUSAIDIE NA MUNGU AIBARIKI TANZANIA YETU
 
1. Tusimamie haki, tutende haki na tuhamasishe watu wetu kutotumia nguvu inayo dhuru mtu, ua watu , kupoteza watu na kuharibu uchaguzi. Toka tulipoanza na tulipofikia kuna matukio mengi tayari (kwa mujibu wa picha na malalamiko). Tunakokwenda na baada ya uchaguzi matukio hayo yasiwepo kamwe...
Mkuu umeandika mambo mazito sana,sijui kama watakuelewa,masikio yao yameziba, macho yao hayaoni.

Tusubiri muda ndio utaongea.
 
Umeandika mambo ya msingi sana mkuu.

Hakika kumbe JF bado kuna ma greathinker

Ila wengi uliowataja hapo ni vibaraka wanatetea matumbo yao wapo tayari Kuiba, kuchinja na kuharibu ili wapate wanacho kitaka.

Namnukuu lissu.
"Uchaguzi huu ni uchaguzi muhimu sana kwa watanzania.
Pia amekuwa akisisitiza kuwa hayupo tayari kuibiwa kura hata moja.
Yeye sio kama wale wanosema tumuachie Mungu.

Na bahati mbaya zaidi CCM wamezoea Wizi je itakuwaje??????

Watanzania wanataka Haki na amani.
 
Nliwambia mapema hamkusikia Pambaneni na hali zenu mi nipo Hapa Denmark nakula maisha kwanza
Taarifa za huko home sio nzur huku wajamen
 
Umeandika mambo ya msingi sana mkuu.

Hakika kumbe JF bado kuna ma greathinker

Ila wengi uliowataja hapo ni vibaraka wanatetea matumbo yao wapo tayari Kuiba, kuchinja na kuharibu ili wapate wanacho kitaka.

Namnukuu lissu.
"Uchaguzi huu ni uchaguzi muhimu sana kwa watanzania.
Pia amekuwa akisisitiza kuwa hayupo tayari kuibiwa kura hata moja.
Yeye sio kama wale wanosema tumuachie Mungu.

Na bahati mbaya zaidi CCM wamezoea Wizi je itakuwaje??????

Watanzania wanataka Haki na amani.

Mkuu , mleta mada ameelezea vizuri sana na wewe umenukuu kauli ya mmoja wa wagombea. Nukuu hiyo isichukuliwe kimazoea au mzaha wowote ule, inamaanisha. Aidha madai ya mazoea ya wizi wa kura katika chaguzi zilizopita nayo yasibezwe kwa vigezo vilevile vya mazoea. Zama zimebadilika sana, Tanzania ya amani inaweza ikatoweka kimzaha mzaha tu kwa kukosekana haki hasa katika uchaguzi huu kulingana na mwenendo na matukio yanayojitokeza wakati huu wa kampeni.

Tunaomba sana Tume za Uchaguzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vitimize wajibu wao bila kuegemea upande wowote na watende haki ili amani iwepo.
 
Natamani waelewe ulichoandika............................ Natamani wajue jinsi watanzania mioyo yetu inavuja damu. lakini ndio hivyo tena... Nimesoma nimelewa natamani tusifike huko lakini ndio hivyo viziwi na upofu wao umeamua kutupeleka huko. Naona hata jinsi aliyepita hataki kuwa mmoja wa watakaopelewa huko ICC na kwa kuonyesha hilo hayuko kwenye any convo............... najiuliza sipati jibu
 
1. Tusimamie haki, tutende haki na tuhamasishe watu wetu kutotumia nguvu inayo dhuru mtu, ua watu , kupoteza watu na kuharibu uchaguzi. Toka tulipoanza na tulipofikia kuna matukio mengi tayari (kwa mujibu wa picha na malalamiko). Tunakokwenda na baada ya uchaguzi matukio hayo yasiwepo kamwe.

2. Kuna maisha baada ya uchaguzi, maisha haya yanaweza yakawa ya kuhangaika na mahakama hapa nchini au nje ya nchi popote pale huwezi jua, kwa tetesi ni kwamba kuna ushahidi unakusanywa mwingi kwenye ngazi zote kutoka kwa waliodhurika, waliokuwepo eneo la tukio na wanaoishi maeneo ya tukio, ushahidi ni wa picha, makovu na sauti, hii ni mbaya sana kwetu sisi watanzania kufikia hatua hii au watu wengine wa nje kupewa ripoti kama hizi (kuna ripoti imeandikwa na mwanasheria flan ina ukurasa zaidi ya 27) hatujafurahia kuisoma sio nzuri kwetu mtu wa nje kupokea na kuandika.

3. Dunia imebadilika na watanzania wamesoma sana, sio kama ile ya miaka yote. Tukumbuke kilicho mtokea Rais wa Kenya, Makamu wake na mwandishi wa Habari hakikuwa kizuri, walihangaika sana na mahakama hawakuwa na amani mioyoni mwao, ni Umoja wa Africa tu ndio uliwasaidia kuwaombea wasishtakiwe kwa majukumu waliyo nayo ila walijuta na walisikitika sana kwa kilichotokea ndio maana sasa hivi maisha yao ya uongozi hawataki kamwe kujihusisha na lolote lile ovu maana wanaelewa, tunaweza tukajifunza kutoka kwao.

4. Madaraka yasitulevye, kuna maisha baada ya vyeo tulivyo navyo, tuandalie vizazi vyetu maisha mema ya badae, tusiache kumbukumbu ya vitu ambavyo havitaleta Baraka na havitaacha alama ya kazi nzuri kwa nchi yetu. Kisheria hamna mwenye hati miliki ya nchi ya Tanzania, kwanza Tanzania ipo kisheria kuanzia ngazi ya umoja wa mataifa hadi huku chini hakuna mwenye uwezo wakuongeza mipaka ya ramani yake nje ya nchi ndivyo ilivyo hakuna mwenye mamlaka wa kujimilikisha kuwa ni yakwake binafsi. Tutakufa tutaiacha na itaendelea kuwepo tu.

5. Ushahidi anao ukusanya huyu Robert Amsterdam kutoka kwa Mwananchi mmoja mmoja au makundi kama alivyoandika kwenye twitter yake; nimeambatanisha hapa, ipo siku tutashangaa aliupataje, sio mzuri tuhakikishe ushahidi huo haupatikani ni pamoja na kuwasisitiza watu tunao waongoza waache tamaa na wasimtendee yeyote yule chochote kile.


MUNGU ATUSAIDIE NA MUNGU AIBARIKI TANZANIA YETU
Mleta mada ameandika vizuri Sana kwa sababu mpaka muda huu kampeni zinaendelea vizuri kwa kuwa TUME imetenda haki ya kwa vyama vyote vya siasa kuwa na wagombea na kupiga kampeni zao lakini pamoja na hayo tusitishwe na huyu anaejiita Robert Amsterdam tukamshabikia hadi uchaguzi wetu uingie doa Tanzania ni nchi huru TUME imetenda haki kwa kweli mbona hawazungumzii mfano wagombea wote waliorudishwa kwenye kinyang'anyiro? Pia yeye ameegemea upande mmoja? Mbona haongelei wagombea wanaokiuka maadili ya uchaguzi waliyopitisha wao na kusaini wao? Ukijiuliza hayo maswali utagundua huyu anakua bias Sana kwa hiyo huyu sio wa ku-intertain mambo yake
 
Natamani waelewe ulichoandika............................ Natamani wajue jinsi watanzania mioyo yetu inavuja damu. lakini ndio hivyo tena... Nimesoma nimelewa natamani tusifike huko lakini ndio hivyo viziwi na upofu wao umeamua kutupeleka huko. Naona hata jinsi aliyepita hataki kuwa mmoja wa watakaopelewa huko ICC na kwa kuonyesha hilo hayuko kwenye any convo............... najiuliza sipati jibu
Wenye uelewa mzuri wa hali halisi ilivyo na uzoefu walionao, wamejiengua mapema sana.
 
Siukio la Kufa Halisikiiga Dawa "CCM" Ushindi 85% watuambie ni Kivipi wataupata wakati watanzania Wamenuna. Chichiem Wamelelax, ni Mwendo wa singelii tu za Wanii . Timer will tell let them relax..God has HIS own Plan for Tanzania "0". Taifa Stars "CCM' = Burundi "Intamba Murugamba "CHADEMA" "1" ni asbh tu....
 
Mleta mada ameandika vizuri Sana kwa sababu mpaka muda huu kampeni zinaendelea vizuri kwa kuwa TUME imetenda haki ya kwa vyama vyote vya siasa kuwa na wagombea na kupiga kampeni zao lakini pamoja na hayo tusitishwe na huyu anaejiita Robert Amsterdam tukamshabikia hadi uchaguzi wetu uingie doa Tanzania ni nchi huru TUME imetenda haki kwa kweli mbona hawazungumzii mfano wagombea wote waliorudishwa kwenye kinyang'anyiro? Pia yeye ameegemea upande mmoja? Mbona haongelei wagombea wanaokiuka maadili ya uchaguzi waliyopitisha wao na kusaini wao? Ukijiuliza hayo maswali utagundua huyu anakua bias Sana kwa hiyo huyu sio wa ku-intertain mambo yake
Haki inatendeka kwa kiasi kidogo ,Tena baada ya mbinyo kutoka pande tofauti,tofauti na bado hola za kutokutenda haki zipo nyingi.
 
1. Tusimamie haki, tutende haki na tuhamasishe watu wetu kutotumia nguvu inayo dhuru mtu, ua watu , kupoteza watu na kuharibu uchaguzi. Toka tulipoanza na tulipofikia kuna matukio mengi tayari (kwa mujibu wa picha na malalamiko). Tunakokwenda na baada ya uchaguzi matukio hayo yasiwepo kamwe.

2. Kuna maisha baada ya uchaguzi, maisha haya yanaweza yakawa ya kuhangaika na mahakama hapa nchini au nje ya nchi popote pale huwezi jua, kwa tetesi ni kwamba kuna ushahidi unakusanywa mwingi kwenye ngazi zote kutoka kwa waliodhurika, waliokuwepo eneo la tukio na wanaoishi maeneo ya tukio, ushahidi ni wa picha, makovu na sauti, hii ni mbaya sana kwetu sisi watanzania kufikia hatua hii au watu wengine wa nje kupewa ripoti kama hizi (kuna ripoti imeandikwa na mwanasheria flan ina ukurasa zaidi ya 27) hatujafurahia kuisoma sio nzuri kwetu mtu wa nje kupokea na kuandika.

3. Dunia imebadilika na watanzania wamesoma sana, sio kama ile ya miaka yote. Tukumbuke kilicho mtokea Rais wa Kenya, Makamu wake na mwandishi wa Habari hakikuwa kizuri, walihangaika sana na mahakama hawakuwa na amani mioyoni mwao, ni Umoja wa Africa tu ndio uliwasaidia kuwaombea wasishtakiwe kwa majukumu waliyo nayo ila walijuta na walisikitika sana kwa kilichotokea ndio maana sasa hivi maisha yao ya uongozi hawataki kamwe kujihusisha na lolote lile ovu maana wanaelewa, tunaweza tukajifunza kutoka kwao.

4. Madaraka yasitulevye, kuna maisha baada ya vyeo tulivyo navyo, tuandalie vizazi vyetu maisha mema ya badae, tusiache kumbukumbu ya vitu ambavyo havitaleta Baraka na havitaacha alama ya kazi nzuri kwa nchi yetu. Kisheria hamna mwenye hati miliki ya nchi ya Tanzania, kwanza Tanzania ipo kisheria kuanzia ngazi ya umoja wa mataifa hadi huku chini hakuna mwenye uwezo wakuongeza mipaka ya ramani yake nje ya nchi ndivyo ilivyo hakuna mwenye mamlaka wa kujimilikisha kuwa ni yakwake binafsi. Tutakufa tutaiacha na itaendelea kuwepo tu.

5. Ushahidi anao ukusanya huyu Robert Amsterdam kutoka kwa Mwananchi mmoja mmoja au makundi kama alivyoandika kwenye twitter yake; nimeambatanisha hapa, ipo siku tutashangaa aliupataje, sio mzuri tuhakikishe ushahidi huo haupatikani ni pamoja na kuwasisitiza watu tunao waongoza waache tamaa na wasimtendee yeyote yule chochote kile.


MUNGU ATUSAIDIE NA MUNGU AIBARIKI TANZANIA YETU
Tatizo ni tume kutokuwa huru. Inapendelea CCM waziwazi. Lawama zote kwa haya mabaya yote yanayojiri zielekezwe tume ya uchaguzi.
 
Mkuu , mleta mada ameelezea vizuri sana na wewe umenukuu kauli ya mmoja wa wagombea. Nukuu hiyo isichukuliwe kimazoea au mzaha wowote ule, inamaanisha. Aidha madai ya mazoea ya wizi wa kura katika chaguzi zilizopita nayo yasibezwe kwa vigezo vilevile vya mazoea. Zama zimebadilika sana, Tanzania ya amani inaweza ikatoweka kimzaha mzaha tu kwa kukosekana haki hasa katika uchaguzi huu kulingana na mwenendo na matukio yanayojitokeza wakati huu wa kampeni.

Tunaomba sana Tume za Uchaguzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vitimize wajibu wao bila kuegemea upande wowote na watende haki ili amani iwepo.
Tayari msingi wa amani ambao ni "Haki" umeshavunjwa na NEC kwa kuwaengua wagombea wa upinzani. Tusubiri "repercussion" tu.
 
Mleta mada ameandika vizuri Sana kwa sababu mpaka muda huu kampeni zinaendelea vizuri kwa kuwa TUME imetenda haki ya kwa vyama vyote vya siasa kuwa na wagombea na kupiga kampeni zao lakini pamoja na hayo tusitishwe na huyu anaejiita Robert Amsterdam tukamshabikia hadi uchaguzi wetu uingie doa Tanzania ni nchi huru TUME imetenda haki kwa kweli mbona hawazungumzii mfano wagombea wote waliorudishwa kwenye kinyang'anyiro? Pia yeye ameegemea upande mmoja? Mbona haongelei wagombea wanaokiuka maadili ya uchaguzi waliyopitisha wao na kusaini wao? Ukijiuliza hayo maswali utagundua huyu anakua bias Sana kwa hiyo huyu sio wa ku-intertain mambo yake
Wewe mdanganye tu mwenzio,siku akipelekwa ubeberuni wewe utakuwa unaomba kibarua kwa hao hao unaowananga hivi leo.
 
Back
Top Bottom