Pre GE2025 Bashungwa: Jeshi la Polisi litaendelea kusimamia usalama shughuli za Vyama vya Siasa bila kujali itikadi

Pre GE2025 Bashungwa: Jeshi la Polisi litaendelea kusimamia usalama shughuli za Vyama vya Siasa bila kujali itikadi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
WhatsApp Image 2025-01-22 at 17.23.22_f3100594.jpg

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kutekeleza jukumu lake la kikatiba kwa kusimamia usalama katika mikutano na shughuli za Vyama vya Siasa bila kujali itikadi ya Chama cha Siasa chochote.

Amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kusimamia ulinzi na usalama kwa Vyama vyote vya Siasa kwa weledi katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mpinduzi uliofanyika Dodoma pamoja na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es salaam.

Bashungwa ameyasema hayo leo tarehe 22 Januari 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma ambapo amesisitiza Vyama vya Siasa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti ili kuepuka kulazimishwa kutii sheria.
WhatsApp Image 2025-01-22 at 17.22.54_e79cc167.jpg

WhatsApp Image 2025-01-22 at 17.23.22_f3100594.jpg

WhatsApp Image 2025-01-22 at 17.24.41_0d79e330.jpg

WhatsApp Image 2025-01-22 at 17.24.42_6d3ea4a0.jpg
“Matarajio yangu kama Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ni kwamba haki hii mnayoitenda Jeshi la Polisi kwa kutoangalia itikadi, pia Vyama vya Siasa vya Upinzani na Vyama vya siasa kwa ujumla, haki hii ije na wajibu kwa wao kutii sheria bila shuruti, hakuna haki bila wajibu” amesisitiza Bashungwa

Aidha, Bashungwa ameliagiza Jeshi la Polisi kuendelea kujipanga kusimamia kikamilifu usalama kwa raia na mali zao wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Waheshimiwa Madiwani, Wabunge na Rais utakaofanyika Mwaka huu 2025 ili kuendelea kudumisha usalama, amani na utulivu wa nchi yetu.

Awali, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP. Camillus Wambura ameeleza kuwa Jeshi la Polisi limejiimarisha vyema kwa kuweka mikakati dhabiti ya kuimarisha usalama kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu.

Chanzo: MoHA
 
Ninyi mnajua ukweli kwamba nchi hii inabidi kurudi mikononi mwa Tanganyika, lissu atagombea Urais na atashinda.

Mmefanya watu kuwa waoga na watumwa, lakini mioyoni wanajua, wasanii wanaogopa hata Kumpongeza lissu, asasi, wafanya biashara kisa wanaogopa nyie. Hata kujiteua kuchukua kugombea wa Urais kibabe bila kushirikisha wajumbe, mwisho wenu waja.
 
Back
Top Bottom