JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kusimamia ulinzi na usalama kwa Vyama vyote vya Siasa kwa weledi katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mpinduzi uliofanyika Dodoma pamoja na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es salaam.
Bashungwa ameyasema hayo leo tarehe 22 Januari 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma ambapo amesisitiza Vyama vya Siasa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti ili kuepuka kulazimishwa kutii sheria.
Aidha, Bashungwa ameliagiza Jeshi la Polisi kuendelea kujipanga kusimamia kikamilifu usalama kwa raia na mali zao wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Waheshimiwa Madiwani, Wabunge na Rais utakaofanyika Mwaka huu 2025 ili kuendelea kudumisha usalama, amani na utulivu wa nchi yetu.
Awali, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP. Camillus Wambura ameeleza kuwa Jeshi la Polisi limejiimarisha vyema kwa kuweka mikakati dhabiti ya kuimarisha usalama kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu.
Chanzo: MoHA