Bastola iliyoua wawili Sinza ni dili kishirikina, lakini pengine pia imebeba mikosi na laana

Bastola iliyoua wawili Sinza ni dili kishirikina, lakini pengine pia imebeba mikosi na laana

Hawa ndiyo wanatufanya sasa hata kama ulitaka uongeze silaha ya pili nyumbani kwa ulinzi wa mali zako serikali inakupa masharti kibao.kama ulikasirika au umevamiwa kuna ile tukio la kwanza kama tahadhari huyo adui wako akuelewe unaimiliki piga juu.ya pili pia kama ameona kuna ile kama kujilinda kama tahadhari unapiga kwenye miguu tu.tatu kama alikuwa unaona na wewe maisha yako huyo mwengine ana silaha ndiyo kujiokoa ushamtahadharisha umepiga juu bado anakutafuta na silaha yake unamuwahi yeye kabla hajakuwahi ya moyo.ila huyu kaitumia silaha vibaya kwa hali zoote kwanza hao hawakuwa na silaha kama yake,ipo haja serikali ipitie upya sheria za umiliki wa silaha ili tusirudi kama mauaji ya marekani na south africa.Mambo haya tulishawahi kujadili toka zama za mkapa hapo silaha zitakapoanza kuuzwa dukani kama pipi.kwanza kuna kipengele chake unapoachiwa uimiliki huruhusiwi kwenda nayo club kama za pombe inatgemea uliiomba kama wewe ndiye mmiliki halali wa club.Huyu katuharibia ambao tunataka tumiliki silaha tena sana.Na hili litaongeaa kutubana upyaaaa.
 
Silaha tajwa tayari imeshaondoka na roho mbili na tayari iko mikononi mwa jeshi la polisi.. Haijajulikana kama mmiliki alinunua 'used' au brand new!
Kama kanunua mtumba ni kwamba hapo kabla ilishawahi kutumika mostly ilishauwa.. Wangapi? Haijulikani..labda mpaka kupata historia yake..! Kama kanunua mpya na yeye ndio mtumiaji wa kwanza basi kama sio silaha yenyewe basi pesa iliyotumika haikuwa na baraka.. Ilikuwa na mazonge..Na tayari silaha husika imeshaingia kwenye ulimwengu hasi
Kimsingi hakuna kesi tena ...! Muuaji naye kajimaliza.. Jalada litafunguliwa kisha baada ya muda litafungwa! Hakuna mshtakiwa...kidhibiti kinaweza kuwa huru na kuingizwa kwenye mirathi ama vinginevyo
Kama kitaingizwa kwenye mirathi kitakuja kuuzwa kama mali za marehemu .. Silaha hairithishwi.. Mnunuzi anaweza kutafutwa na ndugu na itauzwa kupitia jeshi la polisi na kitakachopatikana atakabidhiwa msimamizi wa mirathi

Silaha iliyoondoa uhai wa mtu hasa at close range ni dili sana kwa majambazi na wezi wanaotumia silaha kupora ama wauaji wa kukodishwa! Hiyo tayari ina damu kubwa hivyo kafara lake ni rahisi.. Silaha iliyouwa maranyingi zaidi kishirikina ina thamani kubwa zaidi kuliko ile ambayo haijawahi kuondoka na roho hata moja! Hivyo hii silaha ya Sinza inaweza kuwindwa na watu wabaya...!

Kwa upande mwingine ile silaha inawezekana kabida ina nuksi, laana ama imebeba maagano mabaya hasa kama ilikuwa mtumba...! Kuna vitu ni mali ya kuzimu na kazi yake ni kuharibu na kuumiza tuu..Ndio maana kuna watu hawapendi kabisa kununua vitu mtumba..vingi vimebeba nuksi laana na maagano kama nilivyosema hapo juu..!

Tukio limeshatokea na kuzua mijadala mingi mitandaoni.. Pengine kuna watu watawajibishwa hasa kama utaratibu wa kummilikisha mhusika silaha haukufuatwa inavyotakikana
Niandikapo haya kuna familia mbili ziko kwenye msiba mzito.. Wa kuondokewa na baba, kaka mume nknk.. Tayari kuna maisha mapya wanaenda kuyaanza bila mhimili wa familia.. Ni hali ngumu sana..
Haya yote yatasahaulika baada ya muda.. Na itafika mahali kama silaha husika haitateketezwa na jeshi la polisi basi itaingizwa kwenye mirathi na kuuzwa kwa mwingine...

Kuna maroho na mapepo ya kuzimu yapo duniani kuharibu na kutesa na hujipenyeza kwenye vitu na watu... Haya mavitu ya mtumba tunayotumia hatujui huko nyuma yalipitia mikono gani na yalinenewa nini.. Kuna baadhi vimebeba mapepo mapepo na maroho mabaya
Kuna baadhi vimelaaniwa na wamiliki wa kwanza au wa pili nk
Kuna baadhi vimenenewa vibaya
Kuna baadhi vimetumika kwenye madhabahu za kishirikina
Jitahidi unapopata kitu cha mtumba kitakase kwa imani yako

Nimeandika mada hii kwa mtazamo wa kiroho.. Wanaoona ni tukio la kawaida wasione ni kituko kuwaza tofauti na wao..!
View attachment 1858067
Mshana kwa hiyo haya magari used ya Beforward na SBT ambayo sisi tukinunua tunaita gari mpya tuachane nayo?
 
Mshana kwa hiyo haya magari used ya Beforward na SBT ambayo sisi tukinunua tunaita gari mpya tuachane nayo?
Hapana sijasema hivyo mimi mwenyewe natumia hayo hayo ila ziogope zile zilizopata ajali nje zinarekebishwa na kuja kuuzwa huku
. kuna gari baada tu ya kununuliwa zikaondoka na mmiliki au familia
. Zingine hazikufanikiwa kupata hata namba
.Zingine kila siku zinakula hela.. Ni matatizo mwanzo mwisho
. Zingine zimefanyika baraka zina miaka hazijawahi kuchunwa hata bumper
 
Mkuu silaha ni silaha tu, imepitia mikononi mwa mtu safi ama mtu katili ishaitwa silaha. Kwa namna yoyote (ukatili/ ulinzi) kama sio kuondoa uhai wa mtu basi itamwaga damu ya mtu.
Zipo silaha zimemwaga damu lakini hazijaondoka na roho na zimeokoa wasio na hatia na kama ni kuua zimeua wabaya wanaostahili kufa
 
Hapana sijasema hivyo mimi mwenyewe natumia hayo hayo ila ziogope zile zilizopata ajali nje zinarekebishwa na kuja kuuzwa huku
. kuna gari baada tu ya kununuliwa zikaondoka na mmiliki au familia
. Zingine hazikufanikiwa kupata hata namba
.Zingine kila siku zinakula hela.. Ni matatizo mwanzo mwisho
. Zingine zimefanyika baraka zina miaka hazijawahi kuchunwa hata bumper
Sasa mimi ntajuaje hili gari lina laana na hili halina?
 
Mpe masikini kileo asahau shida zake kwa muda ila tajiri na wafalme uamuzi wao hauta kuwa wa hekima. Pombe mbaya.
Napingana nawe kwenye ubaya wa pombe...pombe sio mbaya kama mtumiaji anajitambua.. Kuna watu wamenenewa vibaya na pombe hao haiwafai. Kuna malimbukeni kuna waigaji kuna wataka sifa ... Wote hao haiwafai
 
Vipi kuhusu nguo za mitumba? % 68 tz ndio viwalo vyetu, ufafanuzi ndugu Jr.
Inategemea huko ilikotoka ilikuwa na historia gani.. Nyingi hazina shida ila kama iligusa damu ya mfu shida ipo
 
Napingana nawe kwenye ubaya wa pombe...pombe sio mbaya kama mtumiaji anajitambua.. Kuna watu wamenenewa vibaya na pombe hao haiwafai. Kuna malimbukeni kuna waigaji kuna wataka sifa ... Wote hao haiwafai
Nipe maandiko yanayo sifia pombe hasa yanayo toka katika vitabu takatifu.
 
Ndio maana nikasema tunaponunua vitu lazima tuvifanyie ibada ya kuvitakasa kwa imani zetu.. Hata kukitolea sadaka ya shukrani pia inasaidia
Imani zingine ni potofu hazina nguvu. Tuswalie hivyo hivyo hata kama hazileti impact?
 
Back
Top Bottom