BAWACHA watangaza kuchoma vitenge walivyopewa kama zawadi na Rais Samia mwaka jana

BAWACHA watangaza kuchoma vitenge walivyopewa kama zawadi na Rais Samia mwaka jana

Baraza La Wanawake CHADEMA maarufu kama BAWACHA imetoa tamko rasmi kufuatia matendo ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini.

BAWACHA wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari siku ya leo wametangaza kuwa kutokana na kitendo cha Rais Samia kutokuwawajibisha wote waliohusika na mauaji ya Mzee Ali Kibao na wanachama wengine wa CHADEMA waliotekwa, wameamua kuchoma moto vitenge walivyopewa na Rais Samia kwenye tukio la kuadhimisha siku ya mwanamkd duniani mwaka jana.

"Leo tumewaita hapa ili kuonesha hasira zetu dhidi ya Rais Samia kwa kutokuchukua hatua dhidi ya watekaji na wauaji, BAWACHA kanda ya Pwani leo tutaenda kuchoma vile vitenge alivyotupa Samia kama zawadi siku ya wanawake duniani mwaka jana"

Source: Jambo TV
Ni vyao

Wachome…. Walishaookea
 
Tuliza makasiriko. na Mipasho.

😭



Ndio, sio tu naona, lakini ni uhalisia.

CHADEMA wanatengeneza mazingira magumu sana ya kisiasa. Yaani sio kwa CCM tu, bali nchini.
Call spade a spade juha namuita juha , siyo mipasho, upuuzi wote unaofanywa na serikali ya CCM awamu hii na awamu zilizopita unaona sawa? Hii ni case ya Mirembe.

Wanaoteka wanaoua wako sawa? Na Kabendera kachafukwa huko, utasema alitekwa na CHADEMA. Pathetic
 
Back
Top Bottom