Uchaguzi 2020 BBC: Ilani ya uchaguzi ya CHADEMA haielezei nafasi za wanawake katika uongozi, CCM na ACT wameweka 50 - 50!

Ukiona hilo genge limeweka 50/50, ujue hao wanawake waliowekwa ni chakula ya faru John. Ni chama cha demokrasia na maendeleo ya tumboni tu.
 
Hili jamaa likishakunywa mataputapu hapo lumumba linaleta thread za kitoto...huon CDM wameweka wagombea wengi wa majimbo ambao ni wanawake?Yaan maccm ni utapeli mtupu kana kwamba watz wote manyumbu,ndio maana hizi campaign zinawatoa ushuzi kwa sbb plans zenu nyingi ni za kale
 
Uhalisia wa hili umeonekana kwenye teuzi za wagombea.
 
Toka Chadema imeanza haijawahi kuwa na mgombea Urais Mwanamke wala mgombea mwenza mwanamke,

Kwa uchache ni kuwa Chadema hakina imani na wanawake kabisa.
Hicho ulichoandika sio kweli.
Mwaka 2005 ndio mara kwanza kwa CHADEMA kuwa na mgombea urais, na hapo aligombea Mbowe na mgombea mwenza alikuwa Rajabu Jumbe ambaye alifariki kabla ya tarehe ya kupiga kura, hivyo uchaguzi ukasogezwa mbele, na CHADEMA wakapitisha mgombea mwenza mwingine ambaye alikuwa ni mwanamke.
 
Best wenu DKt. Mahera hamjamsikia? Kasema kila chama wajikite kwenye ilani zao. Ilani ya CDM uijue wewe kuliko wao wanao wanayoinadi?!
 
BBC wamewabebabeba chadema naona mbeleko imeanza kukatika rasmi baada ya wazungu kuona kumbe hawa watu ni hopeless maandazi kabisa.
Mjinga kama ww ni miongoni mwa wajinga wengi huku Africa wanaolishwa ugoro na watawala wapuuzi naww kwakuwa unamiliki kichwa kama sanduku la kubebea meno huna uwezo wakufikiri ujinga huo wakuambiwa wazungu wabaya alifanya Mugabe na wapuuzi wadzaini walipiga mbinja kwamba huyo ndio mkombozi wakanyang'anya mpaka mashamba .... umesikia Sasa hivi kinachoendelea huko labda nikusaidie kinachoendelea ni kwamba sio tu Mnangagwa kawarudishia mashaamba pia ametunga sheria wasibugudhiwe jiulize walijinga wadzaini wanajisikiaje

Zimbabwe! acheni ujinga hamna chakufanya bila mzungu... kama alikuja kuwatawala wazee wetu miaka iliyopita manake walikuwa na aakili before sisi usidanganywe na watawala hawana wanaloweza bila mzungu tafakari
 
CHADEMA ndiyo inayoongoza kuwa na viongozi wengi wanawake kuliko vyama vyote.
 
Mkuu hii chai ya Kusini Unguja
 
50 kwa 50 ni sera ya mabeberu! Inakuwaje kwa chadema wametupa kapuni na kuishikilia ile ya faragha tu?
 
Toka Chadema imeanza haijawahi kuwa na mgombea Urais Mwanamke wala mgombea mwenza mwanamke,

Kwa uchache ni kuwa Chadema hakina imani na wanawake kabisa.
Umeandika ujinga Mbowe alihombea na nani
 
Sasa kama chadema nzima mko busy na kingereza cha Magufuli unategemea nini?..

Nyie ni wakuchapwa tu mpaka mibichwa hiyo ipate moto akili zirudi.

Kila siku tunawaambia watu wako hyku field kusaka ushindi, nyie mko busy kumsindikiza Lissu akanunue nyanya kariakoo,
.
Hakuna uchaguzi mtapigwa kama huu.
 
Nitajie wagombea wanawake kwenye nafasi za uongozi mwaka huu kwa CHADEMA ni wangapi na kwa CCM ni wangapi??

Tuanzie na wabunge tu
 
Mleta mada ngoja nikujibu hapa hapa.

CHADEMA wanasema hiyo ahadi ya 50/50 ni ahadi ya hadaa za kisiasa, tangu imeanza kuimbwa na CCM toka 1995 mpaka leo hii haijawahi kutekelezwa kivitendo hata nusu, wao CHADEMA hawawezi kuiga vitu hewa bali wanajifunza vitu vya msingi vyenye uhalisia. Mantiki ya 50/50 kwenye nafasi ya uongozi kisayansi haipo. Uongozi utazamwe kiuwezo na kamwe usitazamwe kijinsia, kiumri, kidini au kikabila.

Nafasi ya ushiriki wa mwanamke na mwanaume kisiasa ndani ya sera ya CHADEMA ipo sawa, hawawezi kumbeba mwanamke kwa gharama ya kumshusha mwanaume na Vice versa. Wanawake wote waliopitishwa na CHADEMA kugombea nafasi mbali mbali za kisiasa mwaka huu, walishindana na wanaume ndani ya CHADEMA na wakashinda. Hakuna wakubebwa. Ndio maana huwezi kuwasikia CHADEMA wakijisifu kuwa wameteua wagombea wengi wanawake kuliko vyama vingine. Why? Uanamke sio kigezo cha kuchaguliwa au kutokuchaguliwa.

Wanawake wa CHADEMA wanaweza na sio wanawake wa kuwezeshwa.
 
Hii 50% kwa 50% ni uwendawazimu. Sijui ni kitu hawa wanaokitaka wanajifunza kutoka ulimwengu upi!
 
Bwashee ilani inazungumzia mgawanyo wa madaraka kijinsia kwenye level zote siyo ubunge pekee ndio maana Dr Victoria aliwashangaa sana Chadema!
 
Nimekuelewa bwashee!
 
Umesikia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…