Issue sio kushabikia bali kusimamia ukweli na kuupinga uongo na upotoshaji bila kujali kausema nani!!Never... Soma posts zangu humu
Sibabaikii wazungu Wala jiwe
Nasimama penye maana
Tangu issue ya COVID-19 ianze nimepinga na kukejeli kauli za Trump, Magufuli, za Iran, za Italy na nyingine bila kujali nani anaongea!!
Na kama kweli unasimamia penye maana, simamia basi kwa kutaja hiyo propaganda iliyopo kwenye hiyo habari ya BBC... mbona swali ni rahisi tu?!
Kwamba eti Western Media zinafanya propaganda ni hoja isiyo na maana yoyote... Na ni hoja inayotumika na watetezi wa mfumo!!
Na kama sio watetezi wa mfumo basi ni wale waliokuwa brainwashed na mifumo ya kijamaa ambao walizoea state media kudaganya raia wake, huku zikipiga propagandaz za kutukuza watawala ili waonekane kama miungu watu!!
Matokeo yake, zikitokea "free media from West" zikaandika mathalani "Serikali ya Julius Nyerere inashindwa hata kutoa huduma za msingi kwa wananchi wake", kinachofuata hapo ni mfululizo wa makala na mazungumzo baada ya habari kutoka RTD na vyombo vyake vikihangaika kuaminisha umma kwamba mabeberu yanatuonea kijicho, yanaonea wivu maendeleo na umoja wetu; na porojo zingine kibao!!
Wananchi wakaaminishwa kwamba Media za Magharibi ni waongo wanaotuonea husuda!!
All in all, mbona hizo hizo Western Media zinalomfyatua Trump hamsemi kwamba ni wapiga propaganda?!