BBT waanza mafunzo, hii ni safari ya kuelekea katika kilimo cha biashara

BBT waanza mafunzo, hii ni safari ya kuelekea katika kilimo cha biashara

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Baadhi ya Vijana wa BBT wakiwa katika kituo atamizi cha Bihawana jijini Dodoma, wakiendelea na mafunzo ya uandaaji na uzalishaji wa miche! Gharama yote ya mafunzo ikiwa ni pamoja na chakula na malazi itagharamiwa na serikali na baada ya Miezi 4 washiriki watapewa mashamba na ruzuku kwaajili ya kufanya biashara ya kilimo.


337164429_225736296678266_1754098517784375624_n.jpg
337282244_165036006033536_5580571728512423958_n.jpg
 
Baadhi ya Vijana wa BBT wakiwa katika kituo atamizi cha Bihawana jijini Dodoma, wakiendelea na mafunzo ya uandaaji na uzalishaji wa miche! Gharama yote ya mafunzo ikiwa ni pamoja na chakula na malazi itagharamiwa na serikali na baada ya Miezi 4 washiriki watapewa mashamba na ruzuku kwaajili ya kufanya biashara ya kilimo.


View attachment 2563993View attachment 2563994
Posho hawapewi za kuhudumia Familiya zao?
 
Hao vijana wamepatikana kwa utaratibu upi?

Wale wanaojitolea jeshini pia wangepitia mafunzo haya na muda uwe mchache ili kuwafikia vijana wengi zaidi.

Unapewa maarifa na mtaji juu ila waendelee kuwa chini ya ufuatiliaji baada ya mafunzo kuna hadi wanyoa viduku hapo ruzuku watazibetia.
 
Kilimo cha photoshoot na Instagram.

Bashe ktk hili amechemka na hatoboi.

Njia sahihi ambayo Bashe alipaswa kuifuata ni kutafuta masoko ya mazao.
Nakubaliana na ww asilimia 100%,tatizo tulilo nalo zaidi tanzania ni la SOKO na siyo mafunzo,elimu wanayoitoa leo Dodoma ingefaa kutolewa zaidi mashuleni kilimo kikipewa kipaumbele kama sehemu ya mafunzo ya lazima kwa vijana,tunachakula kingi lakini hatujui njia bora za KUHIFADHI,NAMNA BORA YA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YETU,URASIMU WA TAARIFA SAHIHI NA UUZAJI WA MZAO YETU.
 
Saa ingine waliojitokeza ni wale watapewa nini na sio wale wenye bidii zao hata wasipopewa

Vijana soft soft namna hiyo kweli?
 
Nakubaliana na ww asilimia 100%,tatizo tulilo nalo zaidi tanzania ni la SOKO na siyo mafunzo,elimu wanayoitoa leo Dodoma ingefaa kutolewa zaidi mashuleni kilimo kikipewa kipaumbele kama sehemu ya mafunzo ya lazima kwa vijana,tunachakula kingi lakini hatujui njia bora za KUHIFADHI,NAMNA BORA YA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YETU,URASIMU WA TAARIFA SAHIHI NA UUZAJI WA MZAO YETU.
Mafunzo yangetafutwa na wakulima wenyewe mkuu kama soko lingekuwa Zuri.

Nani aliendesha mafunzo ya ufugaji wa kuku wa kisasa?
Nani aliendesha mafunzo ya umachinga na umama ntilie?
Nani aliendesha mafunzo ya bodaboda, taxi na daladala?

Waliomaliza SUA miaka yote tangu kuwnzishwa kwa chuo hicho wako wapi?

Shughuli ya kiuchumi ikiwa inalipa huwa inavuta watu yenyewe na watu huanza kujielimisha wenyewe.
 
Kilimo cha photoshoot na Instagram.

Bashe ktk hili amechemka na hatoboi.

Njia sahihi ambayo Bashe alipaswa kuifuata ni kutafuta masoko ya mazao.
Hayo yote yameshafanywa mkuu basi wewe utakua sio mfuatiliaji maana Rais Samia Suluhu ametafuta masoko ya mazao nje ya nchi

Chini ya Rais Samia Suluhu, Tanzania imefanikiwa kupata masoko yafuatayo
🔵Korosho nchini Marekani
🔵Tumbaku nchini Japan
🔵Nyama Saudi Arabia
🔵Maparachichi nchini China
🔵Mchele nchini Ubelgiji
🔵Mabondo ya samaki China

Haya ni baadhi tu lakini upande wa mazo Tanzania tupo vizuri ndio maana ukiona mipaka imefungwa nchi nyingi zinazotegemea Tanzania kwa chakula zinapata shida sana
 
Mafunzo yangetafutwa na wakulima wenyewe mkuu kama soko lingekuwa Zuri.

Nani aliendesha mafunzo ya ufugaji wa kuku wa kisasa?
Nani aliendesha mafunzo ya umachinga na umama ntilie?
Nani aliendesha mafunzo ya bodaboda, taxi na daladala?

Waliomaliza SUA miaka yote tangu kuwnzishwa kwa chuo hicho wako wapi?

Shughuli ya kiuchumi ikiwa inalipa huwa inavuta watu yenyewe na watu huanza kujielimisha wenyewe.
Point kubwa hii
 
Mafunzo yangetafutwa na wakulima wenyewe mkuu kama soko lingekuwa Zuri.

Nani aliendesha mafunzo ya ufugaji wa kuku wa kisasa?
Nani aliendesha mafunzo ya umachinga na umama ntilie?
Nani aliendesha mafunzo ya bodaboda, taxi na daladala?

Waliomaliza SUA miaka yote tangu kuwnzishwa kwa chuo hicho wako wapi?

Shughuli ya kiuchumi ikiwa inalipa huwa inavuta watu yenyewe na watu huanza kujielimisha wenyewe.
Lengo la BBT ni kuwaleta vijana wengi katika kilimo ili waweze kujikwamua kiuchumi maana sasa kilimo ni biashara Mama alisema atahakikisha anamaliza tatizo la ajira Tanzania na hii ni moja wapo ya njia kuondoa tatizo hilo
 
Hao vijana wamepatikana kwa utaratibu upi?

Wale wanaojitolea jeshini pia wangepitia mafunzo haya na muda uwe mchache ili kuwafikia vijana wengi zaidi.

Unapewa maarifa na mtaji juu ila waendelee kuwa chini ya ufuatiliaji baada ya mafunzo kuna hadi wanyoa viduku hapo ruzuku watazibetia.
CCM ni wanafiki sana mkuu.! hii pia ni siasa!!! wilaya yangu wamechukuliwa UVccm tu,

Sent from my SHV45 using JamiiForums mobile app
 
Nafikiri tatizo la ajira nchini ni la kisera zaidi kama tuna vijana wanatoka vyuoni (vya kati na juu) halaf wanashindwa kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wenzao kuna haja kubwa ya kutazama mitaala ya Elimu yetu ili iweze kwa namna moja kuendana na nyakati hizi maana serikali haina uwezo wa kuajiri vijana wote wanaomaliza elimu vyuoni. Sekta binafsi haina budi kupatiwa kipaumbele na serikali iweze kukua na kustawi ili vijana wengi zaidi waweze kuajiriwa na wengine kuvutika na kufungua ofisi/taasisi/viwanda vidogo/kati/makampuni nk. Hiyo ya BBT sina hakika kamą ndio suluhisho kwa vijana kupata ajira yasijekuwa ndo mambo yaliyotokea kwenye kilimo kwanza maana malalamiko yashaanza siasa zinapenyezwa kila kona.
 
Baadhi ya Vijana wa BBT wakiwa katika kituo atamizi cha Bihawana jijini Dodoma, wakiendelea na mafunzo ya uandaaji na uzalishaji wa miche! Gharama yote ya mafunzo ikiwa ni pamoja na chakula na malazi itagharamiwa na serikali na baada ya Miezi 4 washiriki watapewa mashamba na ruzuku kwaajili ya kufanya biashara ya kilimo.


View attachment 2563993View attachment 2563994
Hawanyanduani huko kweli? Posho za kujikimu wamepewa kiasi gani?
 
Serikali iache siasa, tatizo la wakulima nchini ni MITAJI NA MASOKO. Ijikite kutatua hilo
 
Lengo la BBT ni kuwaleta vijana wengi katika kilimo ili waweze kujikwamua kiuchumi maana sasa kilimo ni biashara Mama alisema atahakikisha anamaliza tatizo la ajira Tanzania na hii ni moja wapo ya njia kuondoa tatizo hilo
Hatofaulu. Labda kama ameamua kugawa hizo hela vijana wanunue bandle waangalie connection halafu hivo. Lkn kilimo kama kilimo hatofaulu.

Kilimo kina kina hatua 3 ambazo lazima ziende sambamba. Nazo ni INPUT,,,,,,PROCESS,,,,,,OUTPUT.

Ikiyumbaa mojawapo mnyororo wote unakatika. Mama anahangaika na PROCESS wakati input (mashamba, mbolea, viwatilifu na huduma za ugani bado hazijawekewa mifumo mizuri. Na OUTPUT (mifumo ya masoko na taratibu za uuzaji mazao ndani na nje ya nchi bado haiko sawa).

Anachokifanya rais Samia hakina tofauti na alichokifanya rais Kikwete cha kugawa bilioni kumi kila mkoa. Hela zilidakwa na kupigwa na wajanja mpk leo.

Nakuhakikishia SAMIA HATOFAULU

Kilimo is a self driving process
 
Nafikiri tatizo la ajira nchini ni la kisera zaidi kama tuna vijana wanatoka vyuoni (vya kati na juu) halaf wanashindwa kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wenzao kuna haja kubwa ya kutazama mitaala ya Elimu yetu ili iweze kwa namna moja kuendana na nyakati hizi maana serikali haina uwezo wa kuajiri vijana wote wanaomaliza elimu vyuoni. Sekta binafsi haina budi kupatiwa kipaumbele na serikali iweze kukua na kustawi ili vijana wengi zaidi waweze kuajiriwa na wengine kuvutika na kufungua ofisi/taasisi/viwanda vidogo/kati/makampuni nk. Hiyo ya BBT sina hakika kamą ndio suluhisho kwa vijana kupata ajira yasijekuwa ndo mambo yaliyotokea kwenye kilimo kwanza maana malalamiko yashaanza siasa zinapenyezwa kila kona.
Kwenye uongozi wa Rais Samia Suluhu hakuna kitakachoshindikana hili limeanza na lazima liwanufaishe vijana wengi zaidi kama ilivyokusudiwa

lakini pia umeongelea Elimu ni kweli elimu ya Tanzania haimuandai mwanafunzi kujiajiri na Rais Samia Suluhu ameliona hilo na ndio maana unaona anamkakati wa kubadili sera ya elimu ili ifundishwe kwa kuwawezesha wahitimu kuajiajiri

Kilimo pekee haiwezi kuwa suluhisho la ajira na ndio maana vinajengwa vyuo vya veta katika wilaya zote nchini lengo ni kuhakikisha vijana wanapata uwezo wa kujiajiri na kuajiri Mama hajaishia hapo tu anaboresha na ufugaji pia kwa kugawa madume ya ng'ombe kwa wafugaji ili waweze kufuga kisasa na kuboresha biashara ya nyama na mifugo
 
Hatofaulu. Labda kama ameamua kugawa hizo hela vijana wanunue bandle waangalie connection halafu hivo. Lkn kilimo kama kilimo hatofaulu.

Kilimo kina kina hatua 3 ambazo lazima ziende sambamba. Nazo ni INPUT,,,,,,PROCESS,,,,,,OUTPUT.

Ikiyumbaa mojawapo mnyororo wote unakatika. Mama anahangaika na PROCESS wakati input (mashamba, mbolea, viwatilifu na huduma za ugani bado hazijawekewa mifumo mizuri. Na OUTPUT (mifumo ya masoko na taratibu za uuzaji mazao ndani na nje ya nchi bado haiko sawa).

Anachokifanya rais Samia hakina tofauti na alichokifanya rais Kikwete cha kugawa bilioni kumi kila mkoa. Hela zilidakwa na kupigwa na wajanja mpk leo.

Nakuhakikishia SAMIA HATOFAULU

Kilimo is a self driving process
Mimi nakuhakikishia lazima afaulu kwasababu vitu ulivyovisema vyote vipo na ameweka bajeti ya kutosha katika kilimo kwaiyo tukae hapa tusubiri jinsi vijana wengi watakavyonufaika na kilimo
 
Back
Top Bottom