Be Forward wamekuwa wajanja na waongo, magari yanaletwa mabovu

Be Forward wamekuwa wajanja na waongo, magari yanaletwa mabovu

Aaha kumbe ukienda kununua Kuna doc unapewa za utangulizi kujua condition ya gari??? Lakini nadhani kampuni ingekuwa inawapa doc wateja bila kuulizwaa..
hapa sasa kwenye hali kama hii inabaki serikali yetu kupitia mamlaka zake kuhakikisha raia wake hawaingizwi kingi kwa kufanya vitu kama hivi viwe vya lazima, mimi naamini nchi za wenzetu kudhulumu watu hata kama mtu hana uelewa ni ngumu kwa sababu kabla kujamuingiza mtu kingi unakua umekutana na mamlaka zao
 
Wakuu natumai mu wazima!

Kuna wimbi la Be Forward kuleta magari mabovu ambayo yanasabibisha usumbufu mkubwa kwetu sisi wateja.

Nimenunua Alphard- nikaambiwa imefanyiwa mpaka na Inspection, na tena Be Forward Tanzania ndio walifanya clearance. Sasa cha ajabu gari imefika inavuja oil, pia imepigwa rangi nyeusi kumbe Original color ilikuwa ni Nyeupe, ikabidi tena ifanyiwe service hapa Tanzania kwenye yard ya Be Forward ndio TBS wakaipitisha.

Lakini gari bado ina matatizo mengi sana ya check engine, rejeta, masega na Engine box. Nimejaribu kufuatilia Be forward Tanzania wananijibu sababu niliagiza moja kwa moja Japan na Singapore hiyo haiwahusu. Nimefuatilia ilipotoka wananizungusha bila majibu ya kueleweka. Sasa nimeishia kupaki gari sababu haina nguvu na injini inachemsha.

Naomba mnisaidie kama kuna mwenye ushauri wa nini cha kufanya.

Asanteni wakuu.
kwani yard za magari yale ni mapambo wameweka? tabu yote ya nini kuagiza gari toka nje. ulimbukeni na ushamba tu. watu weusi bado ni warugaruga ila mnatofautiana viwango vya urugaruga. umejitakia.
 
Be Forward kwa bongo ndio kampuni ambayo inaaminika sana kama wameanza business za kubahatisha basi wengi wanaenda kuumia ila ushauri unaponunua kitu chochote cha gharama yakupaswa uwekeze muda mwingi kwenye kukichunguza maana gari ikishaingia bongo kulikataa ni gharama na kuna take time
Huyo ujuaji umemponza ofc za beforwad Tanzania zipo posta kwanini yeye awasiliana na ma agent wa sehemu nyingine alafu jumba bovu uwape watu wa nchi yako..
 
kwani yard za magari yale ni mapambo wameweka? tabu yote ya nini kuagiza gari toka nje. ulimbukeni na ushamba tu. watu weusi bado ni warugaruga ila mnatofautiana viwango vya urugaruga. umejitakia.

Hata wewe inaonekana ni mshamba pia ingawa unajiona mjanja. Gari za yard hapa bongo asilimia 80 wameshachezea mileage na bei ziko juu.
Na nia yangu ni kukuambia kabla hujamcheka mwenzio au kumuona boya kuwa mnyenyekevu na msaidie. Usifikiri tunaoagiza nje hatuzioni yard au tunaleta ujuaji. Binafsi nishaagiza gari kama 5 Japan(2 hazikuwa zangu) na zote sijajuta. Muhimu kujua unachofanya.
Tusaidiane badala ya kuchekana.
 
Hata wewe inaonekana ni mshamba pia ingawa unajiona mjanja. Gari za yard hapa bongo asilimia 80 wameshachezea mileage na bei ziko juu.
Na nia yangu ni kukuambia kabla hujamcheka mwenzio au kumuona boya kuwa mnyenyekevu na msaidie. Usifikiri tunaoagiza nje hatuzioni yard au tunaleta ujuaji. Binafsi nishaagiza gari kama 5 Japan(2 hazikuwa zangu) na zote sijajuta. Muhimu kujua unachofanya.
Tusaidiane badala ya kuchekana.
ningekua sirikali ningepiga marufuku kuagiza magari mnatujazia matakataka. ukiagiza uagize gari mpya. mnunue za yard ziishe. huo utafiti wako wa 80% umetoa wapi? tafuta fundi makini nenda naye afanye kazi yake ya ukaguzi uchomoe chombo.
 
Kuagiza ni Bora zaidi SEMA kama hujui uliza maana Kuna website ukiingiza you chasis numba unapata full history ya gari hasa kwa zilizopo Japan
Gari imesajiliwa lini
Imeshamilikiwa na watu wangapi
Accident history
Km ilizoingia nazo kwenye auction
Grade iliyopewa
Service history
Aina ya matumizi iliyokuwa inafanya(town trip or high way)
Hiyo gari ninauhakika hiyo engine huwenda ilibadilishwa maana engine za 2az za chino ya 2005 zilikuwa na shida ya nati kati ya Brock na cylinder head kufunga Kwa mizunguko michache hivyo kuleta tatizo la kuachia kutokana na compression ya engine hata ukaze vipi
Hiyo gari imeharibiwa na mafundi uchwara gear box haikuwa na shida
Hapo ilibidi kupeleka block engineering lakini sio reliable au ununue block ila hakikisha imetengenezwa zaidi ya 2005/6
Pia badili oxygen air sensor pia inachangia gari kukosa nguvu
Mkuu kama hutojali hiyo website iweke hapa jukwaani
 
Back
Top Bottom