Bei ya mafuta ya petroli, dizeli toka Urusi sasa ni $30 kwa pipa. China na India wachangamkia fursa. Kwanini Tanzania isifanye hivyo pia?

Mwamba wa Dunia USA wakisikia tutapigwa ban IMF, WORLD BANK, na kuzuiwa kuuza chochote duniani
Waulize ma Ayattollah wa Iran nchi yao inavyoteseka
Unauhakika na kuteseka huko!? Brics inakuja.
 
Mwamba wa Dunia USA wakisikia tutapigwa ban IMF, WORLD BANK, na kuzuiwa kuuza chochote duniani
Waulize ma Ayattollah wa Iran nchi yao inavyoteseka
... ni rahisi zana kwao; they will just disconnect us from SWIFT; that simple. Hakuna kununua wala kuuza.
 
Nakumbuka Mzalendo #1 aliwahi kusema tutumie fulsa ya kuuza chakula kwenye nchi zilizokuwa na njaa watu wakamjia juu na kusema huwezi kuombea mwenzio apate njaa ili wewe unufaike.
Yap, mara zote ni vigumu kukubali ukweli na hata ukiukubali bado utaufanya kwa njia nyingine kuepuka kuonekana unafanya kutoka kwa aliyesema ukweli.

Na issue ya ununuzi wa mafuta yasiyo safishwa ndg waziri akiona fulsa hiyo lazima atengeneze issue ya 10% kufufua zile mashine za tipper ili tuyanunue, vinginevyo hayana kazi yakifika.
 
Ukisikiliza viongozi wetu wanavyoongea kwenye vyombo vya habari, utajua kabisa kwamba hapa hatuna viongozi.. kuwaambia wachangamkie fursa ya mafuta ya Russia ni kuwatwika zigo wasiloweza
 
Hapo unazungumzia crude Oil. Sasa sisi tukinunua hiyo crude oil tutaiweka wapi. Hatuna refinery wala nini. Sisi tupambane na petroli zetu tu
Siku zote ukisikia bei ya mafuta kwenye soko la dunia hua wana maana ya crude oil na sio petrol, diesel nk. Well, OPEC kwa ujumla wake leo wanauza dola 130 hiyo hiyo crude oil
 
Mleta mada unaongelea Crude oil "Mafuta ambayo hayajasafishwa" Hao India na China wanazo Refinery za kusafisha hiyo Crude oil,
Sasa Bongo wakinunua hizo Crude oil watasafishia wapi? ni lazima uwe na Refinery.
Kusimika mitambo ya kuchuja inagharama kiasi gani? Au kutafuta mwekezaji alete mzigo wa refinery na ifanyike hapa nchini
 
Tunaweza kununua kupitia Marafiki zetu China na India, hakuna vikwazo

Wao wanayo refinery, na watatupa unafuu

Makamba afufue TIPER , refinery yetu
Makamba hana akili ya kufufua refinery, bali ana akili ya kuiba tu kura.
 

Usikute hata sasa wananunua huko ila tunapigwa
 
... ni rahisi zana kwao; they will just disconnect us from SWIFT; that simple. Hakuna kununua wala kuuza.
Bado kidogo tu Putin anaenda kuwa LORD OF THE WORLD !! by VANGA BWANGA !!
 
Wabongo mna maneno mepesi sana. Hivi mnajua gharama za kujenga refinery au hata kuifufua hiyo ya zamani? Ni zaidi ya 10 billion USD. Huyo mwekezaji yuko wapi? Na mpaka hiyo refinery ikamilike bado Urusi watakuwa kwenye vikwazo tuu na kulazimika kuuza mafuta yao kwa bei ya chini?
 
Hivi ilikuwaje Nyerere kwa miaka ile aliweza kuwa na uchumi wa viwanda hadi kuwa na refinery pale TIPER ambapo tulikuwa na uwezo wa kuagiza crude oil na kusafisha wenyewe, hivi kuna watu ambao mnahisi kama mimi kwamba kuna kitu hakiko sawa kwenye namna ambayo nchi yetu inatafsiri hatua za kimaendeleo (development realization)......
 
Hata enzi za Nyerere na TIPER refinery bado tulikuwa tunaagiza mafuta na bado kulikuwa na uhaba wa mafuta. TIPER ilikuwa ni refinery ndogo.
 
Ukisikiliza viongozi wetu wanavyoongea kwenye vyombo vya habari, utajua kabisa kwamba hapa hatuna viongozi.. kuwaambia wachangamkie fursa ya mafuta ya Russia ni kuwatwika zigo wasiloweza
Hata hivyo wananunua Rusia lakini wanauza bei mara 10 ya manunuzi
 
Beberu ni mtu mbaya sana. Usishangae ndiye anayenunua mafuta ya Russia kwa mgongo wa India na wenzake.
Hata hivyo ushauri wako kwa nchi yetu ni muhimu sana. Sijui balozi wetu Moscow anafanya kazi gani.
 
Hata enzi za Nyerere na TIPER refinery bado tulikuwa tunaagiza mafuta na bado kulikuwa na uhaba wa mafuta. TIPER ilikuwa ni refinery ndogo.
Ndo maana nikasema kama tulikuwa na refinery ndogo enzi za mwalimu, kwenye kutathmini hatua za kimaendeleo leo hii tulitakiwa tuwe na refinery kubwa ambayo ingeweza kusafisha hadi mafuta ya nchi jirani......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…