Bei ya maharage Kenya ni 2861 Tsh/Kg huku Tz ni 4,200Tsh/Kg lakini wakenya wapo Barabarani huku watanzania tukipongezana miaka 2

Kwa kahama acha uongo ni 3500
 
Nadhani umeona nguvu ya kiongozi na nn maana ya kusimama mstari wa mbele kama alichokifanya odinga,ukizungumzia na kuwaambia wapinzani wa Tanzania akina CHADEMA,CUF ,ACT kwa uchache watakwambia watanzania ni wajinga ilhali wao kazi yao kubwa ni kupiga deals za siasa.Watanzania wana Uwezo mkubwa sana wa kuandamana zaidi hata ya wakenya tatizo kubwa lililopo ni nani wa kuorganise?hayupo kinachoendelea kwa wanasiasa wa Tanzania ni mavibe ya kishamba na kijingajinga na kuwahadaa wananchi na cha ajabu watanzania hawajajua kuwa wanasiasa wetu wanacheza political game wao wanafuata tu na kujaza mikutano na wakitoka kwenye mikutano wanatoka na mihemuko ya kipumbavu ambayo haina maana yoyote kwenye maendeleo yao,watu wanapiga kelele na wanashiriki uchaguzi kama kawaida na mwisho wanaibiwa ushindi na kusaini fedha mezani lkn watanzania wanawafuata tu,kweli Umaskini wa akili ni mbaya sana.ndio maana hata upindani ngangari haupo.CCM wanaoharibu nchi hii ni walewale tofauti ni rangi na jinsia tu hakuna cha maana chochote kinachopaswa kupongezwa.CCM inajisifu na kumsifia Mama Samia,upinzani nao wanamsifia kama wanavyofanya CCM Eti hivyo ni vyama vya siasa vinavyopaswa kusimamia maendeleo ya watu.Kazi tunayo watanzania.
 
Huwezi kulinganisha Wakenya na sisi Watz....Wakenya wanajitambua sana....

Watanzania ni tatizo na wanasiasa wetu ni bure kabisa
 
"Sasa wangekuwa wao ndio wako madarakani katika hali kama hii wangekuwa na majawabu Gani? Au ndio bei ingeshuka? Mafuta yamepanda hata Uingereza'- Jakaya Kikwete
 
Mmechagua kubet badala ya kulima ardhi kibao tunayo lakini watu tunabanana mjn wenzetu Kenya ardhi 85% Ni semi desert....hyo bei ujue ina ruzuku serikali imeweka.
 
Yeye ametumia Maharage kama mfano, lakini hoja yake ni kupanda kwa gharama ya maisha kutokana na kupanda kwa bidhaa mbalimbali ikiwemo vyakula na anashangaa kwa nini Watanzania hawaandamani kama Kenya na badala yake wanasifu.
 
Kweli yapo mambo mengine yanahitaji ufuatiliaji wa karibu yanyooke katika governance system lakini hili la mfumko wa bei unalizuwiaje. Tuelewe pia kwamba kuna faida zake, saiv wengi wanafikiria au tayari wamewekeza kwenye kilimo kufuatia bei nzuri.
Kama waTz hawajaandamana kama wakenya tunamshukuru Mungu kwa sababu hayo hayana mashiko na yana hasara zaidi kuliko faida! Biashara zinasimama, watalii wamekimbia n.k. Ni siasa mbovu za visasi vinavyotokana uchaguzi uliopita kwa kisingizio cha ugumu wa maisha! Hatuzihitaji hizo!
 
UJINGA, MARADHI NA UMASKINI ndivyo vinavyoisumbua Tanzania..
 
Ya Kenya iko katika Tshs au Kshs?
 
Nendani na familia yako barbrn mnatosha kbsa.
 
Umezingatis ubora na aina ya hayo maharage maana hayawezi yote kuwa Bei moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo watu wote twende Kibondo mashambanikununua maharage? Mimi nimrpita juzi Uvinza, kilo ni zaidi ya 3500. Kinachoongelewa hapa ni bei kztika masoko ambapo watumiaji ndipo wanapată huduma
 
Brother naomba nije inbox unisaidie mawazo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…