Bei za Mafuta zapanda kuanzia Septemba 1, 2021

watanzania wapole sana wewe pandisha bei kila kitu wao wapo sawa tu . ila ukipandisha bei ya kiingilio ya uwanjani kuona mechi ndio utasikia kelele kila kona au azam na dstv wapandishe bando la kuona mechi watanzania hawalali watalalamika sana

🤣🤣🤣

Ushuru wa magari uko juu mno na makodi mengine + foods kupanda bei lakiniii uwezi ckia wakiilalamikia sana serikali,,, ngoja sasa bundle za kuongea/internet weeeee kama unakumbuka nini kilitokea babaa.
 
Ila hawa jamaa wanaudhi kinoma. Bado nini? Pandisheni na bei za daladala, M/Kasi, Kivuko, Kodi ya Kichwa, Bei za Bia, Maji, Matibabu.. Kila sehemu kabeni tufe tu mfurahi.
 
Ngoja tusubiri na mwezi October, ila naona tumepiga u turn ya hatari, very soon tutakua kama Zimbabwe
 
Sasahv ni aibu hata kumuita mama. Hastahili heshima
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei za mafuta kuongezeka kutokana na kubadilika kwa bei katika Soko la Dunia na gharama za uagizaji.

Mabadiliko ya bei hizo yanaanza kutumika kuanzia leo Jumanne Septemba Mosi, 2021
 
Eti kwenye soko la dunia!..

Fungeni mikanda watz! Mambo bado!

Magufuli pamoja na kutukanwa kote kwamba ni dikiteta lakini hakukuwa na ujinga wa namna hii!

Sikumbuki kama kuna kipindi mafuta yaliwahi kufika 2500 katika utawala wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…