Beki wa zamani wa Simba SC, Israel Mwenda atua Yanga kwa Mkopo akitokea Singida Big Stars

Beki wa zamani wa Simba SC, Israel Mwenda atua Yanga kwa Mkopo akitokea Singida Big Stars

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mchezaji wa zamani wa Simba SC, Israel Patrick Mwenda, amekamilisha uhamisho wake wa mkopo wa miezi sita kutoka Singida Big Stars kwenda Young Africans (Yanga).
IMG_1472.jpeg
Pia, Soma: Singida Black Stars yasema imemlipa Mwenda Tsh. 140m yamtaka aripoti mazoezini

Beki huyo anauwezo wa kucheza kama beki namba 2 na 3 amekuwa na msimu mfupi na Singida BS, sasa anajiunga na mabingwa mara 30 wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara katika hatua ya kuimarisha kikosi chao kuelekea michuano ya ndani na ya kimataifa.
IMG_1471.jpeg
Beki huyo anatarajiwa kuongeza ushindani kwa Kouassi Attohoula Yao ambaye ndio amekuwa chaguo la kwanza kwa beki wa kulia wa timu hiyo pamoja na Kibwana Shomari ambaye amekuwa akianzia benchi.

Huu ni usajili wa kwanza kwenye dirisha hili la usajili ambalo linatarajiwa kufunguliwa Desemba 15.
1733900764295.png
 
Yanga wangese kweli kwa nini wasimchukue yule fullback wa kulia ande koffi bonge la mchezaji
 
Akaribie team ya wananchi
Aje acheze beki wa kulia pale Ukoloni Kapombe alimroga sana
Kila siku mnahoji mchezaji gani wa Simba akija uto anapata namba ila wakishasaini tu huko utopoloni mnaanza kuwapamba. Israel anachukua namba vizuri tu mbele ya Yao na vile viandunje vingine.

Baada ya msimu mmoja zaidi, first 11 yenu yote watakuwa ex wa Simba.
 
Back
Top Bottom