Hii ndiyo inaitwa unaweza ukasoma alafu elimu isikusaidie kwa sababu ya sifa za kijinga.
Awe ametishiwa kweli au hajatishiwa, awe ametishiwa na serikali au CHADEMA wenyewe au mpuuzi yoyote wa mtaani, kwa kuandika taarifa hii hapa namuona Saa Nane Ben anakitafuta kifo kwa nguvu zote huku mwenyewe akizani anapata Kiki za kisiasa.
Kinachoweza kutokea hapa ni kwamba CHADEMA wenyewe wanaweza wakamua na wakasimama kidete wakisema Serikali ndiyo imemua, ili wapate agenda ya kisiasa. Hapo atakuwa ametolewa kafara kwa manufaa ya CHADEMA.
Au Serikali inaweza ikamuua na kusema wamemua CHADEMA wenyewe ili kupata Kiki za kisiasa, kwa hoja kwamba Serikali ikitaka kukuua haiwezi kukutumia sms ya kipumbavu kama hii kabla ya kukuua.
Au anaweza kukuua mtu yoyote ambae una ugomvi nae huko kitaa au kwenye siasa zenu za maji taka, akiwa na uhakika kabisa kifo chako kitakuwa cha utata na yeye hatapatikana.
Mwisho kabisa umekuja kuvuruga uchunguzi wa polisi kwa kuandika taarifa hii hapa na kuweka namba ya mtuhumiwa, kama ni kweli basi hiyo line ya simu na simu aliyotumia atakuwa imeshaiingiza chooni.
Jamani hizi elimu zetu ziwe zinatusaidia katika maisha ya kila siku, alafu tusitafute Kiki za kisiasa hata kwa gharama za uhai wetu.