Benaco Ngara: Madereva wa Malori wa Tanzania, wamejichukulia sheria mkononi kuzuia Malori yote kutokea Rwanda kuingia nchini

Unampataje sasa huyo mnyarwanda wa kumuamini kumuachia gari? Bado tatizo lipo palepale
Kama huwaamini madereva wa kinyarwanda unaruhusiwa kufaulisha mzigo mpakani palepale. Kuna warehouses maalumu kwa kazi hio na makampuni makubwa ya clearing kama Balloré na Dubai port world wako pale eneo la mpakani.

Magari ya mafuta na mizigo inayohitaji storages maalumu ndio lazima wabadilishe dereva. Magari ya transit hawabadilishi dereva bali tu wanapewa escort ya police.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na hii ni bado, tutatengwa na dunia nzima kutokana na uzembe wetu kupambana na Korona na uongo wetu eti ni wachache wenye nayo nchini.
 
Kiukweli hakuna sababu ya msingi ya kuyakuuza mambo haya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Superiority ideology wanayotaka kuimanifest subconsiously juu yetu hatuwezi kuikubali, waishie mpakani then dereva wa Tz apokee gari kama wao wanavyotufanyia, hata sisi hatutaki kuletewa Corona toka Rwanda.
 
Hivi hawa madereva wanatoa wapi hii corona??
Ni dhahiri huu ugonjwa ushasambaa sana na sisi tumeshindwa na tumeridhika na hali yetu.
Ona sasa aibu...nchi jirani zinatuvua nguo dah
Total tests 652
infections 480
deaths 16
recovered 167
unaweza kuona ukubwa wa tatizo kama katika tests 652 kuna idadi hiyo ya wagonjwa katika tests million moja tungepata wangapi ?
 
Mizigo ishushiwe mpakani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko Mombasa ndo salama sasa?
 
Hilo sitoshangaa kabisaa, lakini hivi tujiulize kama madereva wa Tz Wana Corona na hawaruhusiwi kuingia nchini Rwanda kwanini hawa madereva wa Rwanda waje huku kwetu, hawajui kwamba wanakuja kuichukua hiyo corona kuipeleka kwao.
Akili zao fupi. Wamepewa limebeneke kiduchu wanalialia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
picha kubwa (sijui kama utaelewa though)..... katika ushindani wa kibiashara miongoni mwa nchi zenye bandari, ni Tanzania ndiyo inayozihitaji land-locked countries zaidi kuliko kinyume chake.
Mkuu soma tena ulichokiandika kama ndicho ulitaka kuandika.
 
kama serikali ya Rwanda hawataki madrive wetu kuingia tanzania wanaona madrive wewe wana corona basi hata madrive wa Rwanda wasije Tanzania wasije kurudi na corona Rwanda kila mtu akae kwao au tupeane mizigo boda na kila moja arudi kwao


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…