Benazir Bhutto Assassinated!!


JIBU LAKO LIKO HAPA:


Charges of corruption

 
masanja,
hata mimi simo na sitakuwemo mpaka na mimi niwe na haki ya kuchaguliwa bila kupitia chama chochote cha siasa.
Turudi kwenye mada huyu mama hana tofauti na mafisadi wa bongo wako tayari kupandisha gharama za maisha ya watanzania ilikulipia ufisadi wao baada ya kutuingiza ktk mikataba yao bila idhini yetu.sasa na yeye amevuna alichokipanda
 
duh aisee ndio maana waambiwa usijue mengi maana......
her dad alinyongwa,braza mmoja alinywesha sumu, mwingine aliuwawa naye kauwawa!vya kaka zake yasemwa semwa kuwa huenda ni yeye mwenyewe alihusika!sasa hii ndio itakua balaa kumjua mhusika ila mpaka sasa wagombea wakubwawa post hiyo ya uhusika ni Taleban na Al Qaeda wakiwa mstari wa mbele...wakifuatiwa na mheshimiwa sana Musharaf
 
ama kweli nacho kifo kikikuita walaa huwezi kimbia hata kwa kujikwaa tuu utaanguka na kufa!
haiwezekani pamoja na mikwala yoote unayopigwa na majamaa usirudi nyumbani else tutakuu,alafu wewe urudi,okay fine mara ya kwanza wakajilipua within a week uliyofika wakakukosa kosa na kuua mamia...ila bado nawe upo tuuu eti waendelea ku fight kwa ajili ya nchi yako...okay fine alikua anataka kuleta maendeleo na vitu kama hivyo hata basi na hela zoote walizokuwa wameiba mwanzoni alishindwa nunua hata gari moja bullet proof?sembuse gari hata ya kwake mwenyewe??as imedhibitishwa alipigwa risasi ya shingoni na kifuani so it means hakuwa na hata hiyo vest ya kuzuia risasi!
haya sasa now she is dead..atakumbukwa kwa siku tatu hizo za maombolezo then after some time what will be next??nothing uchaguzi utafanyika,musharaf atashinda then life will endelea kama kawa watu wengi wakiwa wameuawa!!
AMA KWELI SIASA NI MCHEZO MCHAFUUUUUUUU

Hata Remmy alishaimba...kifoo kifooo kifoo hakina huruma!!
 
anyways naona hizi channel za western huko hazionyeshi situation ya pakistan hivi sasa sijui wanaficha nini au lada wanashow pindi ninapo channel kwenye tv yangu...ila huko pakistan now ni choma choma kitu chochote possible kuchomwa moto chachomwa tuu kuanzia majumba,taa za barabarani,maduka na kila kitu wafuasi wa PPP wana hasira mbaya!
which is something mbaya will follow kuanzia now kutakua na hali hiyo ya ugomvi amabako sijui ni lini katamalizwa as PPP pipo waliamini mno with huyu mama angalau they can defeat Musharaf..sidhani kama amani itarejea soon huko pakistan
 
Ni nani aweza ongeza hata sekunde moja kwa kuishi na hofu?

Hofu haitusaidii kuongeza muda wa kuishi Duniani kwa sababu usipo kufa kwa bomu chakula kitaukuua.

Kama unapinga vitendo vya unyanyasaji na ukandamizaji wewe endelea kupinga.

Sisi wa TZ hatuwezi kaa na kufumbia macho Ufisadi eti kwa sababu tunaogopa kuuana.

Ufisadi tu ni hoja tosha ya kuleta mfakarakano wa kumwaga damu.
 
hii ndio dawa ya mafisadi, mama huyu aliondoka madarakani kwa kura, hakutosheka sasa amegharimu maisha ya binadamu wasiokuwa na hatia. waheshimiwa wasingetishia kumkata mtu kichwa hijja ya mwaka huu wangeisikia kwenye bomba, nauli ilikuwa imeshaliwa.
 
Game nimeona ni maneno gani umechagua kuyatilia mkazo. Na nimeona ni mchango wa wikipedia ambayo umeipa authority ya kuaamua ukweli. Kama huyu mtu alikuwa na utajiri wote huo wa kumfanya "kula na kusaza" alikuwa ni mwandawazimu wa hali ya juu kurudi Pakistani na kulipuliwa! Unless uniambie why she risked her life for corruption? Why would she do that? leo tuna mabilionea lukuki hivi unafikiri Mkapa na wenzake wataandamana katika yetu kupinga ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi? HIvi kweli tuwatarajie kina Andy Chande na wenzao kusimama na kuwa tayari kulipuliwa?

NImesoma yote uliyoyakopi hapo but the question still lingers.. "why would she risk her life to bring back corruption and a corrupt regime?". Help me out.
 

Eeeer, and the same question to game here:..

 
Inasikitisha sana. Mungu amlaze mahali pema peponi, Amin. Tena kumbe bado alikuwa mbichi sana tu, amezaliwa 1953! Too sad.
 


MWANAKIJJI

First things first: Umequestion validity yangu kuhusu hito corruption dhidi ya Bennazir.

WIKIPEDIA uzuri wake ni kuwa ni sehemu ambako watu wanafanya independent corrections etc...lakini kama unaona bado una doubts nzyo then nimejaribu kukufanyia wepesi kwa kukupa hizi links na kama utahitaji zingine nipe tuu taarifa

Swiss prosecutor gets case against Bhutto, 29
October 2007, Monday, by The Associated Press

http://www.iht.com/articles/ap/2007/10/29/europe/EU-GEN-Switzerland-Pakistan-Corruption.php

£4m Surrey mansion in Bhutto ‘corruption’ row
http://www.timesonline.co.uk/tol/news/uk/article393637.ece

THE BHUTTO MILLIONS; A Background Check Far From Ordinary
http://query.nytimes.com/gst/fullpage.html?res=9C00E2D61E30F93AA35752C0A96E958260

Pakistan: Bhutto Sentenced In Switzerland
http://query.nytimes.com/gst/fullpa...F935A3575BC0A9659C8B63&partner=rssnyt&emc=rss

NAB says Swiss order names Benazir: Ursus tractor case

http://www.dawn.com/2004/07/23/top8.htm

Swiss Want Bhutto Indicted in Pakistan for Money Laundering

http://query.nytimes.com/gst/fullpage.html?res=940DE7DA123DF933A1575BC0A96E958260

Asif Zardari lays claim to 4-mn-pound UK estate

http://timesofindia.indiatimes.com/articleshow/823259.cms

Kisha ukaendelea kusema kuwa:

NImesoma yote uliyoyakopi hapo but the question still lingers.. "why would she risk her life to bring back corruption and a corrupt regime?". Help me out.


Ohh well MKJJ here are the answers to your second Question

1)Her return was the result of a power-sharing agreement with President Pervez Musharraf wherein she was granted an amnesty from those charges AND she promised to promote democracy in Pakistan.

2)She promised to rein in terrorism and militant violence in the country and help stabilize its neighbor, Afghanistan.


3)She believed that it was imperative for her to be in touch with her followers: that she couldn’t be a leader of a democratic, secular party and hide from view all the time.


4) She knew her own family’s tragic history; her father [former Pakistani president, Zulfikar Ali Bhutto] being executed by a previous military dictatorship 7 her brother [Murtaza Bhutto] dying in politically motivated violence in 1996.

5) She knew the risks, but she felt that being a political figure and standing for democracy meant that you had to be out there among the people and you couldn’t be hiding.
 
Game, hilo suala la madai ya ufisadi dhidi ya Benazir Bhutto linaeleweka kwa kini kwani madai hayo hayakuanza leo. Kama vile sisi tunavyohangaika na Mkapa ndivyo wa Pakistani wamehangaika na familkia ya Bhutto. Sizungumzii hilo.

Hoja yangu iko katika majibu yako kuanzia mbili hadi mwisho. Yawezekana kuwa alikuwa na masuala mbalimbali na tuhuma mbalimbali dhidi yake; lakini kitendo cha yeye kukubali mizimu yake na kurudi kwao ni kitendo cha kijasiri hasa ukiangalia jibu lako la nne kuwa:
4) She knew her own family's tragic history; her father [former Pakistani president, Zulfikar Ali Bhutto] being executed by a previous military dictatorship 7 her brother [Murtaza Bhutto] dying in politically motivated violence in 1996.

Kwanini alikuwa na wafuasi wengi na wengine walihatarisha maisha yao kumlinda? Je wote walinufaika na corruption zake? Bila ya shaka kuna kitu zaidi ya ufisadi kilichowavutia watu. Na ninadhani wewe mwenyewe unakipata vizuri kitu hicho kwenye jibu lako la mwisho kuwa:


She knew the risks, but she felt that being a political figure and standing for democracy meant that you had to be out there among the people and you couldn't be hiding.

Sasa kama maneno yako ni kweli (I don't have any reason to believe otherwise) basi pamoja na makosa ya kwake na ya familia yake kuuawa kwa Bhutto hakuwezi kuwa ni jambo la kufurahia au kuona "amekiona alichostahili". Kuuawa kwake ni pigo kwa wale wote ambao wanataka kutengeneza walipoharibu na kuwapa watu matumaini.

Leo hii Lowassa na Karamagi wakaamua kubadilika na kuanza kuwa watetezi wa nchi yetu na mali zake, wengi wetu tunaweza kusahau tuliyoyasema dhidi yao. Na kama itokee katika harakati zao hizo walipuliwe kwa vile wako tayari kusimama upande wa haki (ambao hawakuusimamia huko nyuma).

Mfano mzuri ni filamu ya "War Bus" kama mnaikumbuka ambapo askari mmoja alijifanya yeye mjanja na kuwaacha wenzake na kumfuata mwanamke wa kivietcong ambapo hadi akawaweka askari wenzake kwenye lile basi hatarini. Alikuwa ni yule jamaa mlevi mlevi hivi. Hata hivyo siku ambapo lilirushwa bomu wakati wanakimbia toka kambini ili kulilipua lile basi ni yeye aliyetoka alikokuwa na kujirusha juu ya bomu lile la mkono ambalo lilimlipua na kunusuru lile basi. Wale maafisa wenzake pamoja na chuki na hasira ya mwenzao kuwasiliti lile tendo moja la kutoa gharama ya maisha yake kwa ajili ya wenzake lilikuwa ni tendo la kishujaa!

Benazir Bhutto alikuwa na makosa? absolutely! Alikuwa na madai mazito dhiti yake? No question Did she died a hero today (a martry of sort)? You betcha!
 
Sisi sote tutakufa. Wengine watakufa kitandani, wengine kwenye ajali, wengine kwenye uwanja wa mapambano. Kabla yake waliuawa kina Gandhi, Luther, Malcom, Walter Rodney n.k .....

Mwanakijiji nakupa tano. kwani kinyume na wengi umeeleza jinsi binaadam tunavyopenda kuuana au kifo kilivyokuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku.
Wengi hapa wamekimbilia waislamu wenye siasa kali au al qaeda nk. Mimi sikubaliani na hayo kwa sababu moja kubwa, hata kama Pakistan wangekuwa ni wa hindu, wakristo, au Sikh watupu bado huyu mama angeuwawa- kama Mwanakijiji alivyoonesha hapo juu. Binadamu tuna hiyo tabia ya kuuana, nadhani kwa kiasi kikubwa inaonesha ile sehemu ya binaadamu kama mnyama mwingine yeyote hapa duniani- na hii ndo mana unasikia watu wanasema misemo kama hii"...amemfanyia unyama..."au "...jamaa yule mnyama sana...."
tafsiri ya misemo hiyo ni kuwa jamaa huyo ubinadamu wake umepitwa na ile tabia ya kinyama zaidi, na hivyo hata kufikiria amefikiria kama mnyama na ndiyo maana amefanya maovu aliyofanya.

Tukirudi kwa huyu marehemu ni kuwa kule India akina Gandhi nao ilikuwa vivyo hivyo, Gandhi mtoto naye aliuwawa na mwanamke aliyejilipua (alikuwa amejifunga mabomu), wala hakuwa Muislam au Al-Qaeda!!! Ila hao wasiowapenda akina Gandhi walioamua mradi tu wawaue...... Ukienda Marekani wapo ambao hawataki kusika jila la hiyo familia ya Kennedy, na kwa sababu hizo hizo za unyama wa binadamu walimua JFK aliposhinda na kutakiwa awe raisi wao- wale siyo Al Qaeda au nani.....ni watu wenye chuki na hicho kizazi nk.

Mengi yameandikwa, ila mimi nadhani Bado huyu mama alikuwa na wengi ambao wanamchukia sana, wawe al qaeda ul siyo al qaeda...Yeye uwezekano wa kuuliwa ulikuwa kama 80%, na hata huyo Musharraf mwenyewe alishasema hivyo watu wa west wakaanza kusrema ati anaogopa atamshinda uchaguzi.

Pia wengi bado wanakumbuka UKAPA uliotokea Pakistan baada ya huyu mama kuwa waziri mkuu na jinsi ambavyo nchi likuwa imejaa rushwa!!!

Game Theory ameeleza na kuandika mengi, wengi wanamkandia au hawaafikiani naye, ingawa mengi aliyoandika ni ya kweli au yana ukweli mkubwa sana. Na kutona na hivyo stapenda nianze kutoa mifano ya hizo rushwa nk.

Wachache wamesema ati afadhali Tanzania yetu tukae na amani na labda tuiache CCM ili tusije fikia kuuana!!!-- Jibu langu ni hivi sasa watanzania tunauwawa na kuuana kila siku, tofauti ni kuwa CNN, BBC, au security Council hawafanyi vikao kutujali au kuwa na spesho programu......Yaani ukipeleka mgonjwa hospitali na ukashindwa kutoa rushwa na ndugu, mtoto, mzee nk wako akafariki huyo anakuwa ameuawa na CCM na serikali yake. Mabasi yanayopinduka na kuua watu wengi tu hao ni serikali imewau, Jambazi akipiga mtu risasi na kufa hiyo ni serikali imemuua!!
 
Admin, naomba umerge hii thread na hii

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=6924&highlight=PAKISTAN


MWANAKIJIJI

what i object ni watu kutaka RE-WRITE history kwa sababu mtu kafa

mfano: Nyerere alikuwa akituambia kuwa lazima tuwe wazalendo lakini alipoumwa huo uzalendo ulimshinda na akafi ST THOMAS HOSPITAL LONDON badala ya Muhimbili

Benazir alikuwa ni corrupt na kama unaielewa historia ya Pakistan then utakubali kuwa alikuwa PM wa nchi ile mara mbili and what did she do?

Of course kaiba pesa na kuiacha Pakistan in a very sorry state..na narudia maneno ya TARIK ALI hivi punde on channel 4 news...its sad that she lost her life lakini maybe it might be a good think for Pakistan to get away from dynasty politicians
 
MWANAKIJIJI

what i object ni watu kutaka RE-WRITE history kwa sababu mtu kafa


Unfortunately au fortunately historia ya mtu haiishi akiwa bado hai hadi anapokufa. Na watu hawahukumiwi kwa matendo waliyoyafanya mwanzoni mwa maisha yao bali katika context ya maisha yao yote. Hivyo, maisha ya Bi. Bhutto yamehitimishwa leo na hapa historia ndiyo inaweza kuandikwa na zaidi ya yote haitaandikwa kwa usahihi kwa sababu ya proximity ya maisha ya mtu na historia hiyo. Ndio maana ni vizuri kutunza kumbukumbu za historia lakini ni vizazi vya baadaye vitakavyoweza kuelezea vizuri.


mfano: Nyerere alikuwa akituambia kuwa lazima tuwe wazalendo lakini alipoumwa huo uzalendo ulimshinda na akafi ST THOMAS HOSPITAL LONDON badala ya Muhimbili

Mfano huu ni miongoni mwa mifano mibovu kabisa iliyowahi kutolewa katika historia ya mifano!



yawezekana kalipia makosa yake kwa kifo chake, can anybody top that?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…