Bendera ya Israel ndani ya magari ya Dar ni siasa tu au kuna la zaidi?


Mkuu hilo jina Phillipo Bukililo ni lako?
 
Bendera zao labda zinapatikana kirahisi Na wengine wanaozitundika wanaiga tu
 
Naaam, mkuu.
Ni kawaida kwa watu kufunga bendera fulani (kwenye gari au popote) kwa sababu ya imani waliyonayo, itikadi na mapenzi. Ukienda uarabuni waweza ona vijana wa kiarabu wamefunga bendera za kimarekani. Lakini sehemu nyingine wanafunga bendera za ISIS. Wako wanaofunga bendera za team kama Arsenal, ManU n.k. Na wako wanaofunga bendera ya Israel. Wengine wanafunga za CCM na wengine CHADEMA. Ni kitu cha kawaida sana. Ndio maana twavaa hata jezi au sare za kitu tukipendacho, hata team za mataifa ya nje. Wote tunafanya kitu kimoja.
 
Nalipenda mno neno "Israel" kuliko neno "Tanzania" maana neno Israel limeasisiwa na Mungu Mkuu
muumba wa mbingu na nchi; Mungu wa Ibrahimu; Mungu wa Isaka; Mungu wa Yakobo na baadae huyu ndiyo Israel; Maana ya jina lenyewe ni mshindi: Lakini neno Tanzania limeasisiwa na binadamu kwahiyo ni la kawaida tu. Hakuna nchi ya kusimama kupigana na Israel na ikashinda si Urusi,Marekani, Ujerumani wala China.

Fimbo ya enzi haitaondoka mikononi wa Yuda mpaka atakapokuja yeye mwenye kumiliki: Wafilisiti na Waarabu wote wanaifahamu vyema hii fimbo tokea enzi za Musa, Joshua na Daudi mwana wa Yese pia Mfalme wa Israel. Hii historia ilikuja kujirudia ule wa miaka ya 1962-1968-9 pale nchi takribani 9 za kiarabu ziliposalimu amri kwa taifa lenye watu wasiozidi milioni moja.
 
Kuweka bendera ya Israel ama stika ya T. B. Joshua, au ya mzee ya upako, au ya Nabii Mwingira, au shehe Yahaya ni mahaba tuu ya mwekaji sioni kingine.
 
Waafrika ni watoto nakuomba usiulize maswali mengi utoto wako unakufanya ushindwe kudadavua mambo. Donald Trump anasema there is no shortcut to maturity mwombee ashinde aje atusaidie kukua.
Point yako imesimamia wapi....kwamba ni halali kwa hao watu weusi kujivunia bendera ya Israel ili hali hao wenyewe hawana mapenzi na wao...??
 
Bado hujaijua Israel mpaka sasa, hilo ni taifa pekee duniani lenye uwezo wa kujitegemea kwa kila kitu na limezungukwa na majirani maadui, bendera ni ishara ya upendo

Israel haijetegemi hata kidogo. Ni taifa tegemezi tena kwa kiwango cha juu. Ulinzi na usalama wa israeli unategemea fedha kutoka mataifa ya magharibi. Marekani, Uingereza, Ufaransa na Ujermani kwa mfano hujachangia fedha nyingi kwenye jeshi la israeli (Here's How Much America REALLY Spends On Israel's Defense).

Hapa kuna suala la imani kutoka kitabu cha kijulikanacho kama biblia takatifu. Waamini katika kitabu hicho wanaamini kuwa israeli ni taifa teule, na endapo mtu atalisema vibaya mungu wa israeli atamuadhibu kwa mapigo ya laana yeye na familia yake wakiwa hapa duniani na huko ahera. Hadithi inachangia waamini sana watu kuunga mkono israeli. Upeperushaji bendera ni njia moja ya kuikubali hadithi ya uteule wa israeli. Makanisa kama ya Gwajima, Lusekelo (kuyataja kwa uchache), yanaweka bendera za israel mbele kama mapambo.

Kwa uapande mwingine inaweza kuwa kuonesha 'power'. Watu wengi hasa vijana hupenda kuonesha nguvu yao aidha ya fedha au ushawishi kwa kupeperusha bendera za mataifa yenge nguvu kama marekani, israel nk. Pia kuna kasumba ya kujiita aka za matajiri mfano mwanamuziki Nasibu alamraarufu kama diamond kujiita Chibu Dangote. Makundi mengine ya kisiasa minjini na vijijini kujiita NATO, COSOVO, Talebani, Kunduz nk. Mambo hayo ni yakisaikolojia zaidi, peingine ni hofu ya kutambuliwa na kuonesha nguvu. Ingawa madhara yake ni pamoja na kupoteza 'identity' (utambulisho) binafsi.
 
Ni ujinga na upumbavu tu! Wengi husema ni taifa teule la Mungu. Kiuhalisia Israel ya leo siyo ile ikiyotajwa kwenye Biblia. Hawa Waisrael wa leo ni mazayuni washenzi tu hawana hata punje ya uteule.
Kwaiyo muarabu wa leo ndo muarabu wa enzi zile jihad moja ya kitu muhimu kwa iman ya muarabu na wafuasi wake wao wako sawa ubaguzi ata wabongo ni wabaguzi sema amjijui tu acheni ujinga nina jamaa huu mwaka wa 4 yuko israel anaish saf kabs bila shida swala la kubagua ni kitu cha kibinadam roho inavyomruhusu kufanya ndo mana aliyeanzisha utumwa ndio aliyekomesha utumwa uyo muarabu mnaemuina mtu ndo aliyekua anaendelea na kufanya utumwa kwa mtu mweusi mpk alipokua anakamatwa bahani na mzungu je umemchukia muarabu kama bendera basi marekan bendera hayo kwa mataifa mengi yamevaa sna mbona amuoni ilo bali israel tu lil wryne amevaa bendera ya uingereza bora ata kusikia ameitwa limbukeni akuna kwa taarifa yako zunguka ulaya utakutana na wazungu wamevaa bendera ya tanzania kama uwezi tafuta watengeneza kacha watakwambia kwann wamepunguza tengeneza kwa design ya mataifa mengine na kuweka za tanzania ujue kua nao wanamapenz ya kwel kwa watu weusi pia ingawa sio wote ila ni kawaida na ndo mana mipaka walikua wanabisha kufunga au kutofunga ili kupokea wakimbiz je mataifa mangapi africa wanauana wenye kwa wenyewe je huo nn kama sio ubaguzi ni kawaida binadam kupenda cha mwenzie acha roho ya kishetani sisi wote ni wamoja bana fanya yote ila usimkwaze mwenzio bona we unambagua mtanzania mwenzio kisa mkristo we muislamu acha ushamba bana
 
Sidhani kama wazungu wanaonunua kacha za kibongo zenye rangi ya bendera ya tanzania wamepoteza identity yao pia nimewai ona wazungu ulaya wengi tu tena uingereza na marekan wamevaa flana ya bendera ya tanzania sijui wamepoteza identity yao au kisa we unachuki zako binafsi nimewai fanya kaz ya kutafuta flana za kacha ya ramani ya tanzania kwaajili ya wazungu wanataka je walitaka kwaajili ya nn mbona apo umevaa flana ndani ina rebo ya italy umeona mbona ujavua uvae ya fundi wa kibongo ahahahahahahaha acha ushamba bana
 
Mkuu una pumzi ya hali ya juu, yaani unaongea weeee na kuandika weeee bila hata nukta!!
 
Mungu anabagua viumbe vyake?Wengine watakatifu,wengine si watakatifu,ubaguzi wa rangi wa wazi.
 

Samahani mkuu, KACHA ni nini?
 

Samahani mkuu, KACHA ni nini?
Ni vitu vya kitamaduni uvaliwa mikononi au shingoni siku hizi wana design ki modern zaid na kuvaliwa sna zikiwa na muonekano wa bendera ya tanzania kwa muonekano tofauti hasa watu jamii ya rasta ndo wanatengenezaga sna na kuuza hata ukienda bagamoyo utawaona rasta wakifanya biashara ya kacha mbali mbali
 
Rejea kwenye maandiko matakatifu ya BIBLIA,hapo utafahamu kwa nini watu wanapepeza bendera ya Israel.
 

embu soma zaidi kuhusu Israel sio unakariri tu unadhani Israel inapewa economic aid kama Tanzania?nyway wengi wa matajiri wakubwa ndani ya marekani ni wahayuni ,mind u any jew is a citizen of Israel
 



Mkuuu ni kweli unayoyasema
Lakiin Taifa gani waafrica wanakabiribishwa unalolijua wewe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…