Bendera ya Israel ndani ya magari ya Dar ni siasa tu au kuna la zaidi?

Bendera ya Israel ndani ya magari ya Dar ni siasa tu au kuna la zaidi?

Ukiataka kujua mgogoro kati ya Palestina na Israel urejee kwenye historia. Wanaolalia kwenye Historia ndio wanaoiunga mkono Israel, na wanaosimamia mikataba na makubaliano ya Umoja wa Mataifa, wanailaani Israel.

Ukirudi kwenye historia ya kale, hilo Eneo lote la Palestina lilikuwa sehemu ya Israel. Baada ya waisrael kutawanyika Duniani kote, Wapalestina waliweza kuyachukua maeneo yote, hata yale ambayo kabla ya Waisrael kutawanyika, yalikuwa yanakaliwa na Waisrael.

Kama ingekuwa ni rahisi, hao wote Waisrael na Wapalestina, wote walistahili kuwa kwenye Taifa moja. Kihistoria kulikuwa na matukio mengi ya Waisrael kushambuliwa na kuuawa na Waarabu kuliko Waarabu kuuawa na Waisrael. Siku zote binadamu akidhulumiwa sana, atatumia muda wake mwingi kujenga ulinzi imara ili uonevu utoweke, na ndiyo walichofanya Waisrael.

linajitegemea kwa kitu gani? hebu fafanua tuelewe. Israel ni nchi inayoongoza kupokea misaada ya kijeshi na kiuchumi kutoka marekani. Kwa afrika Egypt ndiyo inayoongoza. sasa sijui unamaanisha nini unaposema Israel inajitegemea kwa kila kitu?

bendera ya Israel ni ishara ya upendo? hebu weka sawa maelezo yako. maana naona bendera yao ina hexagram/ two inverted triangles iliyopo katikati mistari miwili ya rangi ya blue (two strips of blue colour) na background nyeupe. sasa sijui hiyo ndiyo ishara ya upendo.

Pia nashangaa kuona watu wengi wanaipenda hii bendera sasa sijui ndiyo wanafuata hiyo ishara ya upendo? pia sijui huo upendo unatolewa kwa ishara unamaanisha nini wakati nchi yenywewe inaikalia Palestine kwa mabavu na kuipora ardhi yake mchana kweupe huku ikiweka blockage ya kuingia Gaza hata misaada ya kibinadamu kama madawa na chakula.

Israel ni nchi inayopigana vita ya mara kwa mara, ingawa naweza sema sio vita bali ni kwenda kutuliza mamlaka ya Palestine (maana hadi sasa sio nchi ila inaitwa Palestinian authority) isiyo na jeshi bali ni wanachama wa chama cha siasa cha Hamas ambacho kinatabuliwa kama kikundi cha kigaidi na mataifa ya magharibi.
 
embu soma zaidi kuhusu Israel sio unakariri tu unadhani Israel inapewa economic aid kama Tanzania?nyway wengi wa matajiri wakubwa ndani ya marekani ni wahayuni ,mind u any jew is a citizen of Israel
Israel inaogoza kwa kupokea misaada mikubwa ya kiuchumi na kijeshi kutoka marekani na misaada isiyo na masharti. waafrika tumedanganywa kuwa tunapewa misaada walati Israeli government inanufaika na misaada ya kweli sisi tunaambulia misaada midogo tena yenye masharti magumu. ikitokea siku ambayo Marekani atasitisha misaada na uhusiano na Israel huo ndio utakuwa mwisho wa Israel.

Amini usiamini Israel inapokea misaada kuliko nchi yoyote ile Afrika, Tanzania tunapokea misaad a kidogo kuliko Israel inavyopokea misaada kutoka Marekani
 
Nalipenda mno neno "Israel" kuliko neno "Tanzania" maana neno Israel limeasisiwa na Mungu Mkuu
muumba wa mbingu na nchi; Mungu wa Ibrahimu; Mungu wa Isaka; Mungu wa Yakobo na baadae huyu ndiyo Israel; Maana ya jina lenyewe ni mshindi: Lakini neno Tanzania limeasisiwa na binadamu kwahiyo ni la kawaida tu. Hakuna nchi ya kusimama kupigana na Israel na ikashinda si Urusi,Marekani, Ujerumani wala China.

Fimbo ya enzi haitaondoka mikononi wa Yuda mpaka atakapokuja yeye mwenye kumiliki: Wafilisiti na Waarabu wote wanaifahamu vyema hii fimbo tokea enzi za Musa, Joshua na Daudi mwana wa Yese pia Mfalme wa Israel. Hii historia ilikuja kujirudia ule wa miaka ya 1962-1968-9 pale nchi takribani 9 za kiarabu ziliposalimu amri kwa taifa lenye watu wasiozidi milioni moja.
mbona inasemekana hitler aliwapiga sana au miaka hiyo walikuwa hawajajipanga
 
Jiulize kwanini hawatundiki bendera ya nchi nyingine zaidi za Israel zimezidi,people know what they are doing
 
jamani!jamani!jamani! yanini kulumban kwa kitu kisicho na mashiko?unalumban kisa bendera kutundika ndani ya gari?nina akili tatu nataka nishare na wewe kitu,moja kuna hili la kuifananisha israeli ya sasa na habari iliyopo katika biblia ,hapa napata wasiwasi kwa sababu kuna baadhi ya vitabu katika bibilia vinajikanganya na aya hiyo.(mimi sio mlumbi sana wa biblia) nakumbuka nilishawai kuelezwa na mtumishi mmoja juu ya hili akanifunulia kuwa israel unayopaswa kuirehemu na kuibariki ni ile tunayoisoma na kujaribu kuiishi katika biblia(akagusia kuwa ya sasa si mbaya ukaiombea kwa maana ni binadamu wanaoishi kule na wanafanya maasi makubwa kama tufanyavyo wengine) akaendelea kusema kuwa israel ya kweli ni wewe ambaye umeokoa na kumkiri yesu kuwa bwana na mwokozi wa maisha yako na kuamini katika yeye,pia akagusia kuwa katika injili yesu alisema yeye ndiye mwanzo na mwisho hakuna awaye kama yeye na njia ya uzima wa milele inakuja kupitia kwake(hakutaja israel hapo,soma hata biblia)

akili ya pili,inaungana na akili ya mchangia mada mmoja kuwa kama unaamua kufanya hayo yote basi utakuwa na mashabiki yako binafsi juu ya taifa hilo kama ambavyo tunaona mashabiki wa yanga.simba na timu mbalimbali wakining'iniza bendera na viambata vya vitu wanavyopenda katika malango yao(magari na n.k)

Akili ya tatu,inaload itakuja na jibu soon.........!!!!......!!!
kwanini ulimsikiliza Mtumishi mjinga na muongo.... hana akili pia.... hajui kuwa vizazi vya waisrael ndio hivyo hivyo hadi leo hii.... Most of christian followers hawajui Mungu wao anaitwa jina gani na anataka aabudiweje.... Roman empire ilifanikiwa kuwapumbaza ili kuenda tofauti na Mungu wa Waisrael so watumishi wake hubabaika na majibu ya kijinga kama hilo alilokupa.... Waisrael ndio Wenye Mungu huyo ambaye Yesu Myahudi alikuwa akimuabudu tena Siku ya Saba ya Juma... siku hiyo kazi unasema basi yaani ni kuget rest. ndio imeandikwa hivyo... Roman akaipindisha watu waende maboya hao hao Watumishi Wakiulizwa hujibu kijinga ati siku zote ni za Mungu sio ya Saba pekee....Wao ndio waliotoa maagizo ya uungu? STUKA.. kwa akili ndogo Watumishi ni wapotofu... na ukiwafuata ndio njia potofu.... Ukitizama Mafundisho ya Wayahudi ni tofauti na huu uitwao Ukristo yaani ni total different yaani hapo unabakia kutowaelewa wakristo hizi njia za kuabudu wanafuata Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo? maana wanaofuata ni Waisrael wao wana Mungu wao? Mkuu kama Dini watu wengi wanapotoshwa sana sometimes huwa Natamani Nilie maana ni Sawa na mtu unasafari ya kwenda Arusha kibao cha kuelekea Mtwara ndio kimeandikwa ARUSHA ukishika njia hiyo Arusha hufiki hakika.... STUKA ndugu
 
Jiulize kwanini hawatundiki bendera ya nchi nyingine zaidi za Israel zimezidi,people know what they are doing
Za saudi Arabia tunatundika mbona Sana..... ila Nadhani za Israel zina market zaidi....
 
Kwa wale ambao sio Wakristo,si rahisi sana kuelewa tendo hili.Katika Biblia hata hivyo yapo maandiko yanayo-onyesha kwamba ukiibariki Israel kama taifa by whatever means na wewe utabarikiwa.Sina hakika kama ukiweka bendera ya serikali ya Israel kwenye gari lako umeibariki Israel,nadhani umeonyesha solidarity with the government of Israel.Andiko ambalo watu wengi wanali-quote ni Mwanzo 12:3.Hata hivyo hili linamzungumzia Ibrahim zaidi as a person.Ambalo liko straight forward zaidi ni Zaburi 122:6.

Kwa upande mwingine kuna jambo ambalo watu wengi hawalifahamu.Israel inayo ongelewa kwenye biblia ni Israel as a nation,not the Israel government.The foundations of the Israel government are Satanic.Ndio maana mfadhili mkuu wa taifa la Israel ni familia ya Rostchild ambaye ni kati ya zile familia 13 za Illuminati.Hii inathibitishwa na nembo ya Freemason ambayo ipo kwenye lango kuu la Mahakama kuu ya Israel(The israel Supreme Court). Ile alama ya nyota iliyopo kwenye bendera ya Israel ukiifuatilia utagundua kwamba ni satanic (uki-google satanic symbols utaliona hili).It follows therefore that it represents the government of Israel and not the nation of Israel.Kwa mtu anayejua maana ya bendera ya Serikali ya Israel kwa hiyo hawezi kuitumia huku akidhani kwamba he is in solidarity with the nation of Israel.
Waungwana kuna mambo maishani huwa yanapotazamwa humuachia mtazamaji kila aina ya tafakuri kichwani mwake. Ndani ya miaka kadhaa ya hivi karibuni, kumezuka tabia ya watu kuitundika bendera ya Israel kwenye sehemu ya chini ya kioo cha ndani ya gari, kile ambacho dereva hukitumia kutazama magari yanayokuja kutokea nyuma ya gari.

Mwanzoni nilidhani ni mahaba binafsi ya mtu mmoja, lakini kadri siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo mashabiki wa bendera hiyo maarufu duniani, walivyozidisha tabia hiyo.

Huwa najiuliza kama Waisrael na wao wanayo tabia ya kuitundika bendera ya Tanzania, katika sehemu ile ile ambayo sisi tunaitundika bendera yao ndani ya magari yetu. Huwa najaribu kujiuliza iwapo Mtanzania anayekatiza katika mitaa ya Jerusalem au Tel Aviv anaweze kukutana na gari ambalo ndani yake kuna bendera ya Tanzania imetundikwa, na muisrael akiendesha gari huku akiufurahia uwepo wa bendera yetu.


Haya ni mawazo yangu, kwani tabia hii imenifanya nijiulize iwapo upendo unaotoka mioyoni mwetu kuelekea kwa Waisrael, unaweza na wenyewe kuwa unathaminiwa na Waisrael bila ya sisi Watanzania kujua ni jinsi gani tunavyothaminiwa.
 
Na hapo ni ndipo ninaposhindwa kumshangaa mungu wenu anayewapanga watu kwa magroup.. Kwamba huyu in first class mja na huyu ni second class mja.. Tena huwapanga hivyo wala so kwa uchamungu wao ! Bali ni kutokana na kuzaliwa by chance katika taifa hilo tu ! What a miracle ![emoji57]
halafu wanamwita eti ni mwenye haki!!
 
Kwanza kimtazamo wangu wengi hufikiria kuwa Israel ni taifa la kikristo wakati si kweli israel ni taifa la wayahudi na ndani yake kuna waarabu ambao ndio wakristo na waislamu
 
Mbona hao waisraeli hawabebi bendera za Tanzania. Na haya mambo yanafanyka kwenye nchi za kiafrika maana Marekani PAMOJA NA ushosti wote na Israeli huwezi ona raia wake wakitembea na hizo bendera never ni sisi tu wafuata mkumbo bila kuelewa.
Halafu kuna kitu nakishangaa kwa hawa wakristo wanaobeba hizi bendera maana sio wote. Wanasena wanamuamini YESU Kristo but wanapeperusha bendera za watu wasiomuamini YESU kristo
na ukiwauliza wanatokwa na povu na kutukana mbaya
 
Bendera ya Israel inaitwa 'the star of David.' Wanaoitundika popote pale ni wakristo na wanaihusisha na imani yao ya kikristo. Wengi wetu tunafahamu uhusiano kati ya mfalme na nabii Daudi na masihi Yesu Kristo. Hakuna siasa katika hili.
Wengi hawajui hili
 
Wanaweka ktk kuonesha love &support kwa Israel, ambapo wakristo wengi wanaamini ktk baraka za mzaliwa wa kwanza, na wanaamini kuwa Israel ni mzaliwa wa kwanza kati ya mataifa kwa Yehevoh

Nembo hiyo naitwa STAR of David au King david shield inaaminika ilikuwa ni ngao ya Mfalme Daud, na Muhuri wa Mfalme Suleiman.

Daudi ni moja ya wababu katika uzao wa Yesu kristo wanaoheshimika sana na wakristo pamoja na wayahudi

Lazima ukumbuke kuwa japo wahayudi si wakristo, lakin ukristo umetokana au umeundwa kwa misingi ya historia ya uyahudi.

Inafahamika kuwa founders wa taifa jipya la Israel, walikuwa ni wajenzi huru na hata uchaguz wa bendera hyo ulikuwa na utata sababu kuna ambao waliamin kuwa kuna symbols nyingine ambazo zina maana kubwa zaid ktk uyahud na hata ukristo mfano Taa ya vinara 7 .lakin inasemekana ma fore fathers hao walifanikiwa kuifanya nembo hyo ya kuwa bendera japo ina mahusiano sana na alama za wajenzi huru.
 
Hakuna utumwa mbaya kama utumwa wa akili,baada ya miaka mingi ya kufanywa watumwa,iwe slavery au colonialism au religion waafrika tumekuwa nothing but zombies,hatujitambui matokeo yake ndio hayo ya kuweka bendera za nchi za watu ambao hawana huruma na wewe hata chembe....NOTHING CAN FREE OUR MINDS BUT OURSELVES..BLACK PEOPLE WAKE UP !!
 
Hawa wana wa Ibrahim yakobo(Israel) na ishmail(mwarabu) wasiopendana wanaisumbua dunia kwakweli. Sisi wala ugomvi wao hautuhusu lakini tunatumika km marungu yao . Kila mmoja wao anataka dunia itambue dini yao, wanaiburuza dunia huku kule km tambara bovu, ni mkorogano kila wanakopita
 
Tofautisheni kati ya kabila la waisrael na Taifa la KIZIONIST , wayahudi wengi hawana imani na siasa za kiisrael. Taifa la Israel ni la watu wenye itikadi za kidini za Judaism, Christianity, Islam na Druz, unfortunately wale wenye ability ya kiArabu ndio hao wa madhehebu mengine matatu.

Lakini mbona sisi waafrika tunakuwa wapumbavu sana, kwa nini tunaumizana roho kwa sababu ya ugomvi wa mwarabu na myahudi?

Sisi ndio Ndugu, majirani tanaosaidiana pakitokea Tatizo, tunazikana. Sasa tuudhiane kisa bendera ya Israel?????
 
Back
Top Bottom