Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mama Samia wanamchezea sana. Kila siku kubadilisha sababu sababu huku uchumi ukiharibika. Nakuona huruma RAIS wangu. Dhamira yake Kwa Taifa ila Hawa aliowapa dhamana akili za Kwenye makaratasi wengi sio wabunifu na wafanya maamuzi(𝐈𝐦𝐞𝐚𝐧𝐝𝐢𝐤𝐰𝐚 𝐍𝐚 𝐒𝐚𝐥𝐨𝐦𝐞 𝐊𝐢𝐭𝐨𝐦𝐚𝐫𝐢)
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imesema nchi haina uhaba wa dola, bali baadhi ya watu wamezihifadhi wakitarajia bei itapanda, ikisisitiza hakutakuwa na ongezeko hilo kutokana na hatua za ndani na nje zinazochukuliwa katika kuimarisha upatikanaji wake.
Imezitaja hatua hizo zinajumuisha uamuzi wa Marekani kulegeza masharti ya riba kwenye masoko yake ya fedha, kupungua kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia na ya nchini na kuendelea kutoa bei elekezi na kufuatilia kwa karibu sekta ya fedha nchini.
Meneja Msaidizi Utafiti wa BoT, Dk. Lusajo Mwankemwa, amebainisha hayo alipotoa mada kuhusu majukumu ya taasisi hiyo benki hiyo wakati wa semina kwa waandishi wa habari, ambao walitaka kujua hatua zinazochukuliwa kuimarisha upatikanaji dola nchini.
"BoT tunajua na tunaona dola zipo ila ni ngumu kukufuata kutaka tuchukue dola nyumbani kwako, mimi (BoT) nitasema dola moja ni kiasi hiki (bei elekezi).
NIPASHE
Na zote zinatumika dola!!!?
Mtanikumbuka 😂🔥Kama ndo hivyo basi magufuli alikuwa sahihi kuban huu ujinga wa bureau de change.
Huwezi kuwa na ofisi au taasisi ambazo huwezi kudhibiti uendeshaji wao hasa wanapoenda kinyume na taratibu..
Nirushie tu mimi kwa Mpesa😀😀🙂Mimi nina dola 2 zipo tu kwenye pochi nifanyeje? Nisije kupata kesi ya uhujumu uchumi bure kwa kauli hizi.
Umesoma kweli unaelewa? BoT hawajasema kuna mtu kaficha, wamesema watu wamehifadhi wakitegemea zitaongezeka bei.
Ni kama sh ngapianaetaka 17 bucks jameni nsije nikapewa Uhujumu uchumi
Hizo ndio faida za uchumi wa fremu, frameconomics. Kila kitu kinaagizwa, hakuna kitu kinachozalishwa. Hakuna uzalishaji wa bidhaa au huduma.
Kama nchi haiuzi bidhaa na huduma, je dollar zitatoka wapi?
Frameconomics