Benki Kuu (BoT) yadai kuna watu wameficha dola

Benki Kuu (BoT) yadai kuna watu wameficha dola

Hata wakati wa kikwete hali ilikuwa hivihivi,,lakininwakati wa mawanza dolla zilikuwa nyingi
 
(𝐈𝐦𝐞𝐚𝐧𝐝𝐢𝐤𝐰𝐚 𝐍𝐚 𝐒𝐚𝐥𝐨𝐦𝐞 𝐊𝐢𝐭𝐨𝐦𝐚𝐫𝐢)

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imesema nchi haina uhaba wa dola, bali baadhi ya watu wamezihifadhi wakitarajia bei itapanda, ikisisitiza hakutakuwa na ongezeko hilo kutokana na hatua za ndani na nje zinazochukuliwa katika kuimarisha upatikanaji wake.

Imezitaja hatua hizo zinajumuisha uamuzi wa Marekani kulegeza masharti ya riba kwenye masoko yake ya fedha, kupungua kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia na ya nchini na kuendelea kutoa bei elekezi na kufuatilia kwa karibu sekta ya fedha nchini.

Meneja Msaidizi Utafiti wa BoT, Dk. Lusajo Mwankemwa, amebainisha hayo alipotoa mada kuhusu majukumu ya taasisi hiyo benki hiyo wakati wa semina kwa waandishi wa habari, ambao walitaka kujua hatua zinazochukuliwa kuimarisha upatikanaji dola nchini.

"BoT tunajua na tunaona dola zipo ila ni ngumu kukufuata kutaka tuchukue dola nyumbani kwako, mimi (BoT) nitasema dola moja ni kiasi hiki (bei elekezi).

NIPASHE
Mama Samia wanamchezea sana. Kila siku kubadilisha sababu sababu huku uchumi ukiharibika. Nakuona huruma RAIS wangu. Dhamira yake Kwa Taifa ila Hawa aliowapa dhamana akili za Kwenye makaratasi wengi sio wabunifu na wafanya maamuzi
 
Defensive mechanism kwenye management huwa ni upumbavu tu, kiongozi unapaswa kuwa na suluhu na sio kulialia.
 
Sasa kama zimefichwa sisi tufanyeje wakati wao ndio serikali nawanamiliki tools zooote.
Wana mabunduki, vifaru, meli za kivita, majet fighter na majeshi yoote, watoke wakazitafute zilikofichwa.
 
Sisi tunapaswa kuona dola mitaani, sukari, umeme, maji nk na sio excuse na blah blah.

Mama toa kauli Moja kama Amir Jeshi Mkuu.
 
Kama ndo hivyo basi magufuli alikuwa sahihi kuban huu ujinga wa bureau de change.

Huwezi kuwa na ofisi au taasisi ambazo huwezi kudhibiti uendeshaji wao hasa wanapoenda kinyume na taratibu..
Mtanikumbuka 😂🔥
 
Tatizo ni sera.
Wekeni soko huria,kusiwe na masharti kwa muuzaji na mnunuzi.(Kuweka dola benk sio shida,mtu akitaka kutoa dola benki inakuwa na masharti).
Serikali idhibìti mfumuko wa bei,na bei za bidhaa zisipande kiholela.(ili kuwa na imani na kuondoa hofu ya mabadiliko ya thamani ya fedha na bidhaa miongoni mwa wafanyabiashara).
 
Kama unanunua na kuagiza Kila kitu hiyo dola utaiona wapi?

Sukari ambayo tungeweza kuzalisha na kuuza nje na kuingiza hizo dola nayo leo tunaagiza nan kulipa dola kwa wenye akili na uwezo wa kuzitumia.

Umeme ambao tulikuwa na uwezo wa kuuza nje na kuingiza dola nao hatuna.

Yaani tumeshindwa hata kuzalisha cemet ikatosheleza soko la ndani na excess tukapelekaa visiwani huko Comoro, Madagascar, usherisheri nk.

Tumeshindwa hata kuuza mawe na mchanga huko visiwani na uarabuni tukapiga dolali.

Haya madini yetu, dhahabu, tanzanite, almasi nk yanatusaidia nini Sasa.

KIPI TUNAWEZA SASA.?
 
Hizo ndio faida za uchumi wa fremu, frameconomics. Kila kitu kinaagizwa, hakuna kitu kinachozalishwa. Hakuna uzalishaji wa bidhaa au huduma.
Kama nchi haiuzi bidhaa na huduma, je dollar zitatoka wapi?

Frameconomics
 
Back
Top Bottom