Benki yapiga mnada nyumba ya mwandishi wa habari wa Gazeti la RAIA MWEMA kisa deni la Tsh. Milioni 5.2

Benki yapiga mnada nyumba ya mwandishi wa habari wa Gazeti la RAIA MWEMA kisa deni la Tsh. Milioni 5.2

1. Mama Mwandishi anasema deni analifahamu

2. Anasema ana kesi mahakamani na mumewe kwa kuwa alibadili nyaraka na kusema nyumba ni yake pekee na sio ya familia.
Kwa hiyo benki hawakuhitaji saini ya mke kwa kuwa jina lilikuwa linasoma la mume kama mmiliki pekee.

3. Mama mwandishi anakiri kuwa taratibu zote za mahakama na mnada zimefuatwa - sijui ataweka zuio kwa jambo lipi na ili iweje

4. Mahakama ya Rufaa ilikwishaamua kuwa kama mtu unaona una maslahi kwenye kiwanja - sajili, hakikisha jina lako linakaa kwenye makaratasi bila ya hivyo hutahesabika kama una mali.
 
Sasa fanya kuwa wakili wa mdaiwa kwa muda ukamtetee dhidi ya bank
Mimi sio wakili wala bush lawyer ungeuliza professional yangu kwanza naelezea uhalisia wa jambo kwani na mm ni mkopaji mzuri tu wa bank na terms and conditions za mikopo yao naisoma vzr kabisa
 
Siamini kuna wanaume wanashindana na sidiria
Watu wanafikia hadi kuuwana wwe unasema Nini! Kuna Ndoa Wana Ndoa wanapigana sana matukio! Ukipata wa kusomana nae somo moja wwe shukuru Mungu wako!!!
 
Mikopo ilivyokuwa ya kishenzi hata kama umebakiza laki wanauza nyumba yako na pesa wanakula kwa ufupi wanakutapeli
Sio Kweli, wakiuza wanachukua kinachowahusu tu,kingine wanakuachia kwenye account yako. Kwa hiyo kama ikiuzwa mil 30 na deni ni mil 5 maanake chenji yako mil 25 watakuwekea kwenye account yako. Usifananishe bank na matapeli wa mtaani
 
Sio Kweli, wakiuza wanachukua kinachowahusu tu,kingine wanakuachia kwenye account yako. Kwa hiyo kama ikiuzwa mil 30 na deni ni mil 5 maanake chenji yako mil 25 watakuwekea kwenye account yako. Usifananishe bank na matapeli wa mtaani

ni uongo kabisa na watu wamefilisika mpaka kuwa omba omba kabisa .kama ingekuwa hivo tusingesikia hayo
 
ni uongo kabisa na watu wamefilisika mpaka kuwa omba omba kabisa .kama ingekuwa hivo tusingesikia hayo

ni uongo kabisa na watu wamefilisika mpaka kuwa omba omba kabisa .kama ingekuwa hivo tusingesikia hayo
Huo ndio utaratibu mkuu, kufikia hatua ya kufilisika ni ambapo deni ni kubwa zaidi,mfano kama mkopo ni mil 40 halafu nyumba imepigwa mnada milioni 30 maana yake watauza vitu vingine zaidi hadi itimie. Ila mkopo ukiwa mdogo kuliko thamani ya nyumba wanakupa chenji yako bila shida kabisa hata kama hutaki maana wao wanachukua chao tu
 
Wewe mzazi wako wa kike angetelekezwa na madeni na weww uko nae hamna msaada ungejiskiaje?
Hamna MWANAUME.mpumbavu atajenga nyumba yake kwa mamilioni kibao afu aje kuitelekeza nyumba na familia nzima eti kwa kukosa pesa mil 5 tu.

Jaribu kufikiria kwa kutumia akili na sio hisia mkuu
 
Atafute msaada wa kisheria kwanza. Hizi nyumba za familia kuwekwa dhamana zina utaratibu wake.
 
si kwa ubaya au dhamira hasi ikitokea umeiaga dunia itakuwaje baba j?
Nikifariki
Wanangu na ndugu zangu wanajua kila kitu, kwanza tukianza kua na kuviziana kwenye Mali ndo Yale MKE anakutanguliza ili arithi Mali.

Huo Ujinga kwangu haipo
 
Hamna MWANAUME.mpumbavu atajenga nyumba yake kwa mamilioni kibao afu aje kuitelekeza nyumba na familia nzima eti kwa kukosa pesa mil 5 tu.

Jaribu kufikiria kwa kutumia akili na sio hisia mkuu
Unaniambia nifikirie au nikupe experience iliyopo kwa watu niliokutana nao? Mwanaume anajenga nyumba peke yake ataiacha?? Wengi wanajenga na wake zao wanakuja kukopa hela bank kwa kufoji spousal consent ili wapewe hela.

End of the day anaondoka na hela anamwachia deni mwanamke na watoto wanateseka. Wewe utatetea because you are a man ila kwa yaliyowakuta watakupa
Experience.
 
Ninaamini mashauri haya yanakwenda kubatilishwa ( bank na dalali wake kuna kosa la kisheria hapo)
 
View attachment 2436797
Nyumba hii ambayo ni mali ya Mary Victor Mahundi, mwandishi wa habari wa Gazeti la Raia Mwema la Dar es Salaam imepigwa mnada kwa Tsh. Milioni 30 ili kufidia deni la benki la Tsh. Milioni 5.2 ambalo alikuwa akidaiwa mume wa mwanahabari huyo.

Inaelezwa kuwa nyumba hiyo iliyopo Tabata, Kata ya Kinyerezi, Mtaa wa Kichangani ilipigwa mnada siku chache zilizopita na tayari mwandishi huyo na familia yake wametakiwa kutoka ndani ya nyumba ndani ya siku 14, leo Desemba 5, 2022 ikiwa ni siku ya 9 kati ya siku alizopewa kuhama.

Mary amesema taarifa hiyo ni ya ukweli na kudai kuwa alikuwa akifahamu juu ya deni hilo la mumewe lakini hakuwa anajua kilichokuwa kikiendelea hadi kufikia hatua ya nyumba hiyo kupigwa mnada.

“Nilikuwa Dodoma katika shughuli zangu za uandishi wa habari, nikapokea simu kutoka Serikali ya Mtaa kunijulisha kuwa nyumba yangu inapigwa mnada.

“Niliporejea nikapata nakala ya barua ya taratibu za nyumba kupigwa mnada moja ikiwa imetumwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya na benki wamefuata taratibu nyingine zote inavyotakiwa, lakini hilo deni ni la mume wangu ambaye kwa sasa hatupo naye pamoja.

View attachment 2436799
“Nimewasiliana na Mkuu wa Wilaya kumueleza hali ninayopitia kwa kuwa hii nyumba si ya mume wangu peke yake ni mali ya familia, yeye (mume) kwa sasa hayupo nasi anaishi sehemu nyingine, inamaanisha kuwa tutatakiwa kuondoka ndani ya siku hizo 14, na kuwa watatuletea mabaunsa na kututoa kwa nguvu. Mkuu wa Wilaya ameniambia anashughulikia suala langu.

“Wakati huohuo, napambana kutafuta msaada wa kisheria ili kuweka zuio kabla ya hakimu na Majaji kwenda likizo ya kufunga mwaka, kwa kuwa sikushirikishwa katika huo mchakato wao wa mnada,” anasema Mary.

Nyaraka za benki zinaonesha kuwa deni lililosalia ni Tsh. 4,759,368 (Milioni 4.7), asilimia 10 ya deni ni Tsh. 475,936, hivyo jumla deni ni Tsh. 5,235,304.

Mary ameongeza kuwa: "Naomba kama kuna yeyote ambaye anaweza kunipa msaada wa kisheria anisaidie katika hilo kwa kuwa hapa nawazi nitaishi vipi na wanangu, kwanu hata huyo mume bado nina kesi naye kwa kuwa alibadili nyaraka na kuofanya nyumba ionekane ya kwake peke yake wakati hii nyumba ni ya familia, nina watoto, nitaenda wapi mimi na watoto wangu!
View attachment 2436800

View attachment 2436801
Huu ni ugomvi wa mapenzi unaochochewa na visasi kutoka pande zote mbili ...mwanamke ana hasira na uchungu na kaona njia rahisi kwake ni kuamua kutafuta huruma ya watanzania kwenye social media .. kumbuka hapo mwanamke hatafuti msaada wa kisheria kama alivyoanisha bali ameutangazia umma hilo tatizo lake ili ampate mtu atakayeweza kumlipia hilo deni lililobakia ili nyumba ibaki kuwa yake.. hii vita haitaishia hapo huko mbele kuna mtu atarogwa au kuuwawa katika mazingira yasiyoeleweka, Mungu awasaidie.
 
Back
Top Bottom