Benki za Biashara Tanzania zinaogelea kwenye faida. Je, nini kimefanyika awamu ya sita?

Mnapambana sana kuonesha mama hawezi ila mmeshindwa hata kabla ya kuanza,
Nani kapambana mbona Nimesema atamwaga trillion 5 kufufua uchumi??

Nachosema ni timeline, yaani mafanikio ya sera zake yataonekana latest 2023 ila sio miezi 6!! Mama hta BOT ndio kwanza recruitment na reshuffle zinaendelea kuweka timu yake vizuri alafu ghafla ndio mafanikio ya kibenki ni sababu ya miezi 6 yake??

Hoja yangu ni kwamba hatua zilishaanza chukuliwa toka mwaka jana ikiwemo Mkopo wa Trillion moja kwa mabenki, sasa unapodai ni mafanikio ya mama je hyo trillion moja aliitoa yeye??

Embu tupende kuwa watu wa facts sio ushabiki
 
Si nasikia BoT wamepunguza riba kutoka 7% - 5%, na kutoa 1 T stimulus package kwa mabenki; ili hali benki zimebaki na riba zilezile za 17% - 20%
 
Ukiona benki inapata faida sana ujue kuna watu wameumia sana, benki ni taasisi za dhuluma, wanakupa fedha makaratasi afu wanakukopesha kwa bond ya kitu halisi kama mjengo, ardhi yako nk.
 
Lakini hyo difference ya 7% na 16% ndio inaleta multiplier effect kuchochea uchumi. Coz benki zitaajiri zaidi, zitakopesha zaidi, wafanyabiashara kuongeza mitaji n.k

Hela hizo ni kodi zetu sio mali ya serikali maana haina shamba!! So kuigawa kwa private sector ni jambo jema kiuchumi
 
Ni kweli inaomgeza zaidi kwa watu wenye hisa kwenye mabenki! Pia ujue kabisa deni la taifa linaongezeka sana maana riba inakuwa kubwa!
Sasa mwenye hisa hizo pesa hatumii?? Hatoajiri watu kwenye uwekezaji mwingine atakaofanya? Hatolipa kodi akiuza hisa ama dividend anayopata haikatwi kodi??

Multiplier effect ndio muhimu kuangalia na hata ukifuatilia duniani kote ukwasi unaanzia juu ndio uje kwa makapuku hakuna uchumi wa bottom-up!! Ni uongo wa Ruto huo.
 
upo sahihi sana... utawala wa mama umerejesha confidence kwenye uchumi. Matokeo yake investors wa ndani wana ari ya kufanya kazi.

Kwahiyo fursa za kiuchumi zinafunguka kwa kasi sana, na mabenki kupata faida maana yake ni kwamba wakopaji wake ambao ni sekta binafsi nao pia kwa sasa wapo vizuri.

Na hichi ni kiashiria kikubwa kwamba uchumi unaanza kupaa.. kuna viashiria vingi sana kwa sasa
 
Hizi taarifa zote zinazohusu mabenki kupata faida kubwa sana siyo za kweli kwa vile mabenki siyo maduka ya kuuza na kupata faida papo kwa papo, bali faida za mabenki hutokana mikopo ambayo hulipwa baada ya muda mrefu kwa faida (riba). Benki haiwezi kukopesha miezi sita tu na kupata faida kubwa sana, hizi taarifa ni za propaganda tu.
 
Na bado waongeze bidii , hizo faida sio kubwa kulinganisha na nchi nyingine zenye mabenki makubwa na imara Afrika.
Wafanye kazi kwa kiu , kwa ustadi na ubunifu.

Walegeze masharti ya kutoa mikopo.
 
Na bado waongeze bidii , hizo faida sio kubwa kulinganisha na nchi nyingine zenye mabenki makubwa na imara Afrika.
Wafanye kazi kwa kiu , kwa ustadi na ubunifu.

Walegeze masharti ya kutoa mikopo.
Nikweli kabisa naungana na wewe kwenye hili
 
Wachumi mtusaidie hili, Hivi mabenki yetu ya biashara kupata faida ya TZS 471B kwa miezi tisa tu,Wakati huko nyuma yalipata TZS 286B kwa mwaka ina maana gani kwa Uchumi wa nchi yetu...
safi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…