Benki za Marekani kufeli ni ishara ya nini?

Shikamoo Putin na wenzako mlio form BRICS - the beginning of the end ya mfumo wa wenzetu kifedha/ kiuchumi ndio unaanza kujongea taratibu kwenye meat grinder ya kigeuziwa kibao - hawata amini macho yao.
Putin hausiki kwa lolote.

Mnamkuza bure tu huyo jamaa.

Benki zimeanguka kwa management mbovu tu.
 
Kwenye benki mikopo ndo chanzo kikubwa cha kipato. Then other investments zinafuatia.
 
Dollar ikianguka kila pesa inaanguka maana currencies zote ziko denominated Kwa us dollar , currencies zote ni scams
Dollar ipo inverse na other currencies hasa Euro.

Majuzi USD was strong while Euro was weak.
 
Dollar ipo inverse na other currencies hasa Euro.

Majuzi USD was strong while Euro was weak.
Hujaelewa ! Unajua ni currency ipi ambayo central banks dunia yote wanihold kama reserve ? , na Central Banks ndio wanaotake risk in case ya bank failures kama iliyotokea hapo USA , so kila currencies iko pegged Kwa us dollar na benki kuu dunia nzima wanahold US dollar kama reserve currency Yao na risk mitigator ukiachana na assets nyingine kama gold na silver ambapo mabenki na serikali nyingi duniani reseerve yao ya silver na gold ni ndogo sana so currencies zao ni simply worthless pieces of paper , sababu pesa/ currencies zilizopo kwenye mzunguko kama store of value inatakiwa kuwe na kitu chenye value kuiback up incase watu wameloose confidence na hiyo pesa na thamani yake imeshuka sana au kucollpase kabisa , so dollar ikicollapse ,na hayo makaratasi yanaporomoka na kuteketea , nenda kasome brettonwoods uone kwa nini central banks zote duniani kupeg currencies zake
 
Central banks pekee dunia hii ambazo atleast wanareserve kubwa ya gold na silver ukitoa United States federal reseve kama risk mitigator ni China na Russia hao atleast hizo reseve zao zinaweza saidia kidogo kustahilize currencies zao kwa kiasi fulani japo nazo zitacollapse pia ,wengine ni zero tu , na wataalamu na manalysts wa mambo ya finance & economics kama akina Jim Rickards na Peter Schiff wanasema US dollar ikicollapse hizo currencies nyingine zote zinaenda na maji na central banks wataintroduce digital currencies mfano wa bitcoin au Blockchain currencies Ila ambazo zitakuwa chini. Ya central banks duniani kote
 
Uchumi wa Marekani ukitetereka na uchumi wa dunia unazubaa vilevile. Great economic depression ilitokea miaka ya 1920, mdororo wa uchumi 2008 ulianzia kule. Ingetokea COVID-19 ikaanzia Marekani uchumi wa dunia ungeyumba zaidi.
Yeah ! Sure no vile watu hawajui tu globalisation iliyosababisha interconnectivity katika mifumo ya finance na uchumi kiasi kwamba nchi zote ziko vulnerable na mtikisiko katika nchi moja unaweza sababisha maafa katika nchi nyingine nyingi kuanzia flow of capital ,biashara , misaada , mikopo , madeni ,thamani ya pesa na mambo chungu mzima
 
Na pia kiasili bonds za serikali ni uwekezaji salama zaidi wa kifedha. Ni kama risk free. Wengi wanawekeza huko, tungeona mabenki na taasisi nyingi zikianguka. Sidhani kama benki inaweza pata shida sababu ya kununua bonds.
Iko hivi central banks zinapopandisha riba / interest rates ni kwamba juu inasabanisha mikopo na madeni kuwa ghali ,mfano leo hii BOT wakiamua kupandisha riba kwa kudictate kutoka asilimia 10-Lets say wakafanya asilimia 25 wewe utajiuliza mara mbili mbili kwenda kukopa kwenye hizo commercial banks na hautaweza kwenda kukopa maana utapiga mahesabu utaona riba ni kubwa na hailipiki then common sense ya risk analysis itakwambia Hamna , na lengo ni kupambana na mfumuko wa bei kwa kupunguza mzunguko wa fedha katika nchi ,so benki kuu ikifanya kitu kama hicho thamani ya treasury bonds inashuka sana na mabenki binafsi na ya kibiashara wanascramble kuziuza ndio kilichotokea kwa hao SvB Marekani hapo watu na makampuni ya kiteknolojia / tech startups ambao ndio walikuwa wateja wakubwa wa hiyo benki wakaanza kuscramble kwenda kuwithdraw pesa toka katika hiyo benki baada ya kukosa confidence na kama mnavyojua benki ni pyramid scheme , hawawezi watu wote kwenda kuwithdraw pesa zao zote kwa wakati mmoja na ikaendelea kusurvive
 
Wiki iliyopita Benki ya Marekani Silicon Valley Bank ilipatwa na bank run(watu wengi kutaka kutoa pesa benki kwa pamoja) na kupelekea kufilisika. Tena benki ya pili, Silvergate, imepatwa na kitu kama hicho.

Haya mambo yanaashiria nini? Tujipangaje?
Shida ushabiki mwingi. Mbona hii ya China ilikufa?
 
Hiv ndio tok jaana nimekua nachek.hii imekaaje kitaalam hiz benk kufilisika?benk zetu zina mkakat upi? Naskia wat wana rush kuwa na reserves ya yuan.wataalam wa uchumi vip
Nunua dhahabu au silver achana na paper money
 
Ndio maana waliunda FDIC Kule Marekani wao ndio insuarer wa hiyo kitu benki ikifaik wana take over kuhakikisha wateja wanalipwa pesa zao na kuendesha hiyo benki au kuuza assets za hiyo benki mpaka sintofahamu itakapoisha ,wamefanya hivyo jana kwa Signature bank , ingawa kwa giants kama city banks ,Morgan Stanley Dousche bank , JP Morgan NK wao ni too big to fail ,wao huwa wanapewa" bailout " au fidia na serikali ili kufidia hiyo pesa ya hao wateja , ndio maana kuna mjadala Marekani wa kwanini zinapofail hizo bank ndogo wao wanafilisiwa lakini banks kubwa wao wanapewa " bailout " ambazo ni pesa za walipa kodi ,
 
Kwa kipindi hiki hasa kuanzia 2021-huu mwaka federal reserve walikuwa wanaongeza interest rates ili kupambana na inflation au mfumuko wa bei .
 
Banksters aka mafioso na wanakucharge pesa ya kufanya kila miamala + pesa ya kuhifadhi pesa na bado pesa yako wanajichotea bila ruhusa na wanaikopesha huko yet ukitaka kuitoa yote kwa wakati mmoja wanakuzingua na hiyo interest rate wanaochukua baada ya kukopesha pesa yako hawakupi ,ni almost nothing in comparison to the amount that Wana make tokana na pesa ulioweka hapo , banksters are biggest institutionalised thieves through fractional reserve banking
 
Huyo hajui hata anachokisema mkuu,
Tangu lini bonds zikateteresha bank
Acha undezi , interest rate ni inversely proportional na bonds value ,interest rate ikiwa juu thamani ya bond inashuka na ikishuka banks wanapigania kuziuza na hiyo ina lead fear Kwa depositor na wao wanapambana kuwithdraw then kinachofuata total collapse ya benki husika maana hakuna depositor kila mtu anatoa chake kukimbia
 
Gram moja ya gold inacheza kwenye laki moja na sabini huko. Kununua gold inataka uwe na moyo sana. Gold tamu ni ile ya bure au ya wizi maana itakulipa vizuri sana.
Gold au silver ni unanunua kama hedge dhidi ya inflation au kidhibiti cha kuhifadhi thamani ya pesa yako dhidi ya mfumuko wa bei na kuporomoka kwa thamani ya pesa kitu kinachozikumba currencies nyingi karibia zote duniani kwa sasa
 
Na hizi concepts walufanya makusudi kuzificha si unajua tena kula na kipofu. Watu wamesoma finance ,uchumi ,business administration , accountancy na banking ila ukija kwenye hizi Concept za muhimu watwange maswali kama haya ,heheeee wanapoteana
 
Hii Siri watu wengi Huwa hawajui , I've never understood why people rarely question pesa Huwa created vp?
The level of greed the banking system inafanya ni ya kushtua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…