Benki zina kinga gani dhidi ya uchawi?

Benki zina kinga gani dhidi ya uchawi?

Ukishajua kwanini Nabii akitaka kununua gari anachangiwa na waumini wake ila muumini akitaka gari anamwombea na kumpa mafuta ya upako basi utakuwa ushajibu hili swali lako
Hii pointi ya msingi sana, watu wanapigwa sana kwenye majumba ya ibada huko; unajua zile za... "Mbeeengoooo foongooookaaaaaa! Poookeeeaaaa gariiiiiii!"
 
Mchawi halisi hahitaji pesa! Pesa ni mzigo mzito wenye kuhitaji michakato mingi.. Akili ya kibinadamu ni kumiliki pesa ili anunue atachacho..
Mchawi hahitaji kwenda bank akaibe pesa kwakuwa kwanza wizi ni kosa kwa mchawi .. Anaweza kuwasaidia wengine sio afanye yeye
Mbili mchawi hahitaji pesa kwakuwa anapata kila atakacho bila pesa na hata akizihitaji ataziita zitamfuata hapo alipo na sio kujisumbua kwenda mpaka bank
Tatu kuna mazingaombwe na ushirikina wa kuchukua pesa bank lakini hujichukulii tu marundo kuna kiasi .. Ni kama chuma ulete hawezi kuchukua pesa ya kufanya maendeleo ni ya kumtosha kwa siku moja tuu tena mahitaji muhimu kama chakula

Nne hata kama atatokea mtu akapiga ndefu bank .. Unadhani Bank itatangaza? Au unadhani mwizi atajitangaza kwamba kapiga ndefu bank?

Mchawi ana miliki pesa za aina tatu
1. Za kuvuta toka popote atakapo kulingana na uwezo wake
2. Za kutengeneza kimazingara/mazingaombwe
3. Za kuletewa na wateja
Shukrani kwa ufafanuzi mkuu, nimekupata!
 
Mimi Njemba ni mchawi na kanuni za uchawi ni kusumbua tu watu na siyo kupata pesa.
Kwamba raha yake akuhamishe usiku kutoka kutandani akakulaze juu ya mti! For no reason hahaha
 
Mkuu,Mchawi hawezi kuiba JINI (Jini Pesa). Yani ni sawa na MCHAWI kuiba UCHAWI. Sijui umenielewa?

Pesa si karatasi kama wengi wadhaniavyo.
Naendelea kuichakata hii niielewe.... inamaana zile sadaka tunazotoa kwenye majumba ya ibada... au basi.
 
Naendelea kuichakata hii niielewe.... inamaana zile sadaka tunazotoa kwenye majumba ya ibada... au basi.
Usisite Kaka,funguka.

Ila nikupe kitu hapa utafakari;
Je unazijua au kuzisikaa pesa za ndagu?
Kama uliwahi kuzisikia labda,acha tujiulize pamoja swali hili; "Inakua vipi,mfano mimi nina pesa ya manyoka (hela ya kishetani) ambayo ukikiuka masharti inapotea/kufirusika au kugeuka takataka kwa maana ya nyasi au karatasi (hili nina ushahidi nalo kabisa). Ile pesa (kwa mfano ile ya kutega Jaba konani chumbani) nikiichukua nikampa mtu mwingine kwake inakua halali kwasababu hana mambo hayo,ila yeye akinipa yake ambayo hata kama kaitoa Bank muda huo huo na ukampa huyo mtu wa pesa za kukinga konani na akazingua kwake zinaweza kuwa si pesa,kwamba akajikuta kashika karatasi au nyasi."
 
Nilisoma mahali fulani wanasema uchawi sio halisi, ni viinimacho tu - manaake uchawi hauna madhara/matokeo kwa ambae haamini au haogopi uchawi. Kwa lugha rahisi uchawi ni mchezo wa kisaikolojia tu, hauna uhalisia kwa hiyo hauna madhara kwa vitu vinavyoonekana/ kushikika, isipokuwa panapo imani na hofu; Ukiamini basi kitatokea ulichokiamini, na ukiogopa lazima madhara yatokee kwasababu ya hofu yako (Kumbuka: Sio kwasababu ya uchawi!)
Gamboshi wapo kama unabisha nenda tu kaulizie huko
 
Mshana Jr na wajuzi wengine hapa inabidi mtupe shule sana kwenye haya mambo



Je inawezekana, Jini akakutunuku tuu hela na zikawa salama?

mfano kama zile unaambiwa nenda sehemu fulani then utakuta hiki na hiki apo utakuta pesa iko sehemu kadhaa, ichukue
 
Mshana Jr na wajuzi wengine hapa inabidi mtupe shule sana kwenye haya mambo



Je inawezekana, Jini akakutunuku tuu hela na zikawa salama?

mfano kama zile unaambiwa nenda sehemu fulani then utakuta hiki na hiki apo utakuta pesa iko sehemu kadhaa, ichukue
Jini ni kiumbe mwenye wivu uliopitiliza.. Akikutunuku chochote kitaendana na masharti ambayo mwanzoni utayaweza lakini mwishoni utachemsha
 
Hakuna uchawi zaidi ya story za kusadikika ila kuna imani za kishirikina. Imani hii inaaminiwa na watu wapumb.avu na wavivu wa kufikiri. Watu kama nyumbu wanaamini tu bila reasoning yeyote ukiwaambia wathibitishe au wamewahi kushuhudia wenyewe watakupa story zisizo na kichwa wala miguu. Afrika bado tuna safari ndefu sana.
 
Usisite Kaka,funguka.

Ila nikupe kitu hapa utafakari;
Je unazijua au kuzisikaa pesa za ndagu?
Kama uliwahi kuzisikia labda,acha tujiulize pamoja swali hili; "Inakua vipi,mfano mimi nina pesa ya manyoka (hela ya kishetani) ambayo ukikiuka masharti inapotea/kufirusika au kugeuka takataka kwa maana ya nyasi au karatasi (hili nina ushahidi nalo kabisa). Ile pesa (kwa mfano ile ya kutega Jaba konani chumbani) nikiichukua nikampa mtu mwingine kwake inakua halali kwasababu hana mambo hayo,ila yeye akinipa yake ambayo hata kama kaitoa Bank muda huo huo na ukampa huyo mtu wa pesa za kukinga konani na akazingua kwake zinaweza kuwa si pesa,kwamba akajikuta kashika karatasi au nyasi."
Inafikirisha sana... Binafsi sina nia ya kuingia huko, tayari nilisha-experience kidogo nikagundua sio njia ninayotaka kupita. Ni udadisi tu ndo umenisukuma kutafuta taarifa zaidi.
 
Uchawi ungekuwa wa kweli biashara ya Bank ingekufa, hakuna uchawi ni michezo tuu kama mazingaombwe, na wachawi 99% ni mafukara wa kutupa hata ugali maharage kwao ni issue
 
Mchawi hawezi kuiba benki kwakuwa masanduku yote yanayohifadhi na kubebea pesa ni ya chuma na hufungwa kwa kufuri.

Ipo hivi: mchawi anaweza kuiba pesa zilizotunzwa kwenye sanduku au box la mbao sababu dawa zake nyingi zinatokana na mimea na box au sanduku pia linatengenezwa kwa mmea. Hivyo inampa urahisi sana mchawi kukuibia au kuiba popote.

Kwa mazingira ya bank ni ngumu sana japo kuwa huwa wanaweza kuiba kwa chuma ulete ikiwa cashier kajisahau kuhifadhi pesa vizuri hasa wakati anapokuwa busy.
 
Bank haziwezi kuwa na kinga dhidi ya wachawi kwakuwa zile pesa sio zake bali ni za wateja na kila pesa inayopokewa bank inaingia na nguvu yake kiroho
Nyingine ni za wizi
Nyingine ni za dili
Zingine ni za mauaji zinanuka damu
Nyingine ni za dili chafu kama madawa nk
Zingine ni za makafara nknk
@Mshana Jr hivi kwanini huanzishi chuo chako rasmi cha uganga na ulozi tuje kisomwa na kupata vyeti kabisa?

Nahofia siku ukitutoka, utaenda na hazina kubwa ya elimu ambayo wengi tutakuwa hatuijui wala kupata nafasi ya kunufaika nayo.
 
Back
Top Bottom