Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii pointi ya msingi sana, watu wanapigwa sana kwenye majumba ya ibada huko; unajua zile za... "Mbeeengoooo foongooookaaaaaa! Poookeeeaaaa gariiiiiii!"Ukishajua kwanini Nabii akitaka kununua gari anachangiwa na waumini wake ila muumini akitaka gari anamwombea na kumpa mafuta ya upako basi utakuwa ushajibu hili swali lako
Shukrani kwa ufafanuzi mkuu, nimekupata!Mchawi halisi hahitaji pesa! Pesa ni mzigo mzito wenye kuhitaji michakato mingi.. Akili ya kibinadamu ni kumiliki pesa ili anunue atachacho..
Mchawi hahitaji kwenda bank akaibe pesa kwakuwa kwanza wizi ni kosa kwa mchawi .. Anaweza kuwasaidia wengine sio afanye yeye
Mbili mchawi hahitaji pesa kwakuwa anapata kila atakacho bila pesa na hata akizihitaji ataziita zitamfuata hapo alipo na sio kujisumbua kwenda mpaka bank
Tatu kuna mazingaombwe na ushirikina wa kuchukua pesa bank lakini hujichukulii tu marundo kuna kiasi .. Ni kama chuma ulete hawezi kuchukua pesa ya kufanya maendeleo ni ya kumtosha kwa siku moja tuu tena mahitaji muhimu kama chakula
Nne hata kama atatokea mtu akapiga ndefu bank .. Unadhani Bank itatangaza? Au unadhani mwizi atajitangaza kwamba kapiga ndefu bank?
Mchawi ana miliki pesa za aina tatu
1. Za kuvuta toka popote atakapo kulingana na uwezo wake
2. Za kutengeneza kimazingara/mazingaombwe
3. Za kuletewa na wateja
Naendelea kuichakata hii niielewe.... inamaana zile sadaka tunazotoa kwenye majumba ya ibada... au basi.Mkuu,Mchawi hawezi kuiba JINI (Jini Pesa). Yani ni sawa na MCHAWI kuiba UCHAWI. Sijui umenielewa?
Pesa si karatasi kama wengi wadhaniavyo.
Usisite Kaka,funguka.Naendelea kuichakata hii niielewe.... inamaana zile sadaka tunazotoa kwenye majumba ya ibada... au basi.
Kwamba raha yake akuhamishe usiku kutoka kutandani akakulaze juu ya mti! For no reason hahaha
Nimeona tayar ankalTayari Ankal
Gamboshi wapo kama unabisha nenda tu kaulizie hukoNilisoma mahali fulani wanasema uchawi sio halisi, ni viinimacho tu - manaake uchawi hauna madhara/matokeo kwa ambae haamini au haogopi uchawi. Kwa lugha rahisi uchawi ni mchezo wa kisaikolojia tu, hauna uhalisia kwa hiyo hauna madhara kwa vitu vinavyoonekana/ kushikika, isipokuwa panapo imani na hofu; Ukiamini basi kitatokea ulichokiamini, na ukiogopa lazima madhara yatokee kwasababu ya hofu yako (Kumbuka: Sio kwasababu ya uchawi!)
Jini ni kiumbe mwenye wivu uliopitiliza.. Akikutunuku chochote kitaendana na masharti ambayo mwanzoni utayaweza lakini mwishoni utachemshaMshana Jr na wajuzi wengine hapa inabidi mtupe shule sana kwenye haya mambo
Je inawezekana, Jini akakutunuku tuu hela na zikawa salama?
mfano kama zile unaambiwa nenda sehemu fulani then utakuta hiki na hiki apo utakuta pesa iko sehemu kadhaa, ichukue
Inafikirisha sana... Binafsi sina nia ya kuingia huko, tayari nilisha-experience kidogo nikagundua sio njia ninayotaka kupita. Ni udadisi tu ndo umenisukuma kutafuta taarifa zaidi.Usisite Kaka,funguka.
Ila nikupe kitu hapa utafakari;
Je unazijua au kuzisikaa pesa za ndagu?
Kama uliwahi kuzisikia labda,acha tujiulize pamoja swali hili; "Inakua vipi,mfano mimi nina pesa ya manyoka (hela ya kishetani) ambayo ukikiuka masharti inapotea/kufirusika au kugeuka takataka kwa maana ya nyasi au karatasi (hili nina ushahidi nalo kabisa). Ile pesa (kwa mfano ile ya kutega Jaba konani chumbani) nikiichukua nikampa mtu mwingine kwake inakua halali kwasababu hana mambo hayo,ila yeye akinipa yake ambayo hata kama kaitoa Bank muda huo huo na ukampa huyo mtu wa pesa za kukinga konani na akazingua kwake zinaweza kuwa si pesa,kwamba akajikuta kashika karatasi au nyasi."
Utakuwa tajiri sana wewe! Sio swali hili...Bibi yangu alikua ana iba bank ki uchawi...
Sitaki maswaliii
@Mshana Jr hivi kwanini huanzishi chuo chako rasmi cha uganga na ulozi tuje kisomwa na kupata vyeti kabisa?Bank haziwezi kuwa na kinga dhidi ya wachawi kwakuwa zile pesa sio zake bali ni za wateja na kila pesa inayopokewa bank inaingia na nguvu yake kiroho
Nyingine ni za wizi
Nyingine ni za dili
Zingine ni za mauaji zinanuka damu
Nyingine ni za dili chafu kama madawa nk
Zingine ni za makafara nknk