Uchaguzi 2020 Bernard Kamilius Membe: Nitagombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo

Uchaguzi 2020 Bernard Kamilius Membe: Nitagombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo

Membe umefeli. Bila hao kuungana basi unatwanga maji kwenye kinu tu. Ila ninachojua baadae utarudi CCM na utachukua form ya urais kupitia CCM 2025.

Yaliyotokea kwa Lowassa 2015 ni somo tosha kwa wapinzani wa kweli. Sio kila siku ni Ijumaa. Sisi tunataka tume huru ya uchaguzi, mbwembwe za mazee ya ccm zimetuchosha. Tuna kampeni nzito ya kuhakikisha wapiga kura wanakuwa wachache kupita maelezo iwapo hakuna tume huru ya uchaguzi. Na kampeni hii vizuri na itatoa majibu chanya.
 
"Huu ni wakati muafaka kwangu wa kushiriki katika mazungumzo na vyama vingine kama CHADEMA ili tusimamishe "KISIKI CHA MPINGO" kimoja!"

Yeye ni mgeni tu then anaanza kuja na terms&conditions alizotumwa kutoka huko CCM,yeye aendelee na ACT yake mambo ya mgombea mmoja(ambapo anataka yeye ndiye awe Mgombea huyo) hayapo.

Ahaaaa ahaaaa nimecheka ile mbaya, halafu huyo mzee anakuja na swagga za Lowassa zile alizoleta 2015. Nikisikia hayo maneno ya kitapeli ya huyo mzee nakumbuka ya yule tapeli mwingine Lowassa. Huyo Membe ajue shida ni wakati wa kwenda, wakurudi anajua pabaya na pazuri. Aendelee na hiyo ACT kwa cdm hapana.
 
Membe hana msaada wowote ule,Membe ni Lowassa part 2.FULL STOP

Atagawa kura za upinzani,atashindwa kwny uchaguzi kama kawa na akimaliza kazi yake atarudi zake kwao Ccm kama kawa.

Membe ni Lowassa wa Lindi. Wapiga kura wengi wa upinzani tunajitambua, hata Mbowe alibahatika sana kumleta Lowassa na watu wakamkubali. Ila baada ya wanaccm waliokuja na mafuriko ya Lowassa kuanza kurudi ccm, sasa tutaonyesha kuwa tunajitambua vizuri sana.

Haturudii kosa, acha ACT arudie kosa maana wao ndio wanategemea siasa za kunyanyuka kwa umaarufu. Cdm walishavuka hatua hiyo kwa somo kali. Ni vyema tukajikita kwenye kudai tume huru ya uchaguzi, na sio kuendelea kushiriki hizi chaguzi za kihuni.
 
Na kuondoa hiyo hofu yako, kama umemfatilia , amewahi kukiri yupo tayar kumuunga mgombea yoyote watakayekubaliana.

Anaweza kusimama, akasimama Lissu, lkn mwisho akaamua kumuunga Lissu... nani anajua???? .


Hapa nilazima wapinzani wakae vzuri wajadiliane.


Kama wasipoungana, CCM haitatikiswa hata kidogo.

Ni vyema zaidi kuungana kushinikiza kupata tume huru ya uchaguzi, kuliko kuungana ili kushiriki uchaguzi kwa kuwatumia makada wa ccm. Tukishusha idadi ya wapiga kura nchini, itakuwa na impact kubwa sana, kuliko kushiriki uchaguzi ambao tayari Magufuli ana matokeo yake mfukoni.
 
Membe kila alicho nacho kwny maisha yake kuanzia kazi yake'ukipepeo',mali zake,kazi nzuri za watoto wake/ndg zake vyote amevipatia CCM na hawezi kwenda kinyume nao hata dakika 1 maana anaelewa 'consequences' zake.

Na Membe ataleta zile Kampeni za kina za kikondoo za kina Lowassa kuogopa kupiga mawe huko alikotoka na tutaishia tu kusema jamaa ana kampeni za kistaarabu.

Mkuu hivi kipindi Zitto anaanzisha ACT akawa anapokea pesa kutoka kwa kina Zoka mpk na a/c Zao na amount zikawa hadharani hukuwahi kufahamau?

Unajua Zoka&Membe hao ni wa kutoka 'ofisi' 1?

Mkuu kunywa utakacho nakuja kulipa. Hiyo ACT iliasisiwa na kina JK, Membe, Mwigulu nk. Na lengo ilikuwa ni kukabiliana na cdm kwa faida ya ccm. Huyo Membe ndio mmiliki halisi wa ACT, hivyo mmliki rasmi wa ACT ndio katua kwenye mali yake. Kwa sasa tumestuka. Cdm haina tatizo na wapiga kura, na wapiga kura wake wengi wanajitambua, na wanajua hizi siasa za kishamba za Magufuli zitaisha, na chama kweli cha upinzani kitaendelea kuwepo kwa kasi kubwa zaidi.
 
Yaliyotokea kwa Lowassa 2015 ni somo tosha kwa wapinzani wa kweli. Sio kila siku ni Ijumaa. Sisi tunataka tume huru ya uchaguzi, mbwembwe za mazee ya ccm zimetuchosha. Tuna kampeni nzito ya kuhakikisha wapiga kura wanakuwa wachache kupita maelezo iwapo hakuna tume huru ya uchaguzi. Na kampeni hii vizuri na itatoa majibu chanya.
Sasa wapinzani watashinda vipi kama watu hawatojitokeza kupiga kura ?Pigeni kura lindeni kura hakuna wa kuwaibia. Ondoeni negativity. Mkicheza Bunge halitakuwa na mbunge hata mmoja wa upinzani. Kama ni kosa mtafanya basi ni kuwaambia watu wasiende kupiga kura.
 
Safi sana lazima nimpigie kura MTU huyu mwerevu,muungwana anayejali UTU... Sasa Lissu,nyalandu etc wamuunge mkono hats tusiposhinda tumpe tumbojoto pengine atabadilika na kutuskiliza pale tunapomwambia jambo fulani hatulitaki...
 
Nia ye Membe iko wazi , kwa bahat mbaya ukakasi anaoupata ni kukubalika sababu hamna aujuaye moyo.


Ila ukweli nikua, Membe ni hazina kubwa kwa Upinzani.

Hivi kama CCM lengo ni kuua upinzani ,wangehangaika na haya wanayoendelea nayo et mpaka wamtumie Membe??.


E.Lowassa?? Lowassa alirudi CCM kwa sababu ya Serikali kumuwinda ktk shuguli zake za kiuchumi, kuwindwa kwa waty wake wa karibu.

Nin angefanya??????? ...... kama lengo ilikua nikuua upinzani.. ..haya Lowassa alileta wabunge wangapi??? Kwann asingejitoa kwa kinyang'anyiro siku chache kabla ya uchaguzi???.
Mzee E.Lowassa aliamua kukubali yaishe sababu kwake aliguswa panapouma.



Upinzani usipoungana et kisa Membe... ni kosa kubwa watakalokua wamefanya .

Zanzibar Chadema haipo.. Seif yuko ACT... na wazinzibar siasa zao ni MVUTO WA MTU SIO CHAMA.

Chadema inanguvu Huku Bara.... aya , wasipoungana wanataka nn?????


Mchezo ulikua Lissu wa chadem, Seif wa ACT..

Sasa Kuja kwa Membe kusifanye upinzani utoke nje ya Reli... Nafasi bado ni kubwaa ya kukaaa, Hata Membe mwenyewe anajua .

Kitu ambacho hufahamu ni kuwa cdm ina wapiga kura wa kweli wa upinzani. Kilichotokea uchaguzi wa 2015 kisha Lowassa kuamua kurudi ccm na wale waliokuja naye hakijawaacha wasaka mabadiliko wa kweli na furaha. Leo hii anapotokea mtu wa aina hiyo hiyo, na maneno yale yale, na mtindo ule ule, tena kutoka kule kule, ni wajinga tu wanaweza kukubali hilo.

Kama Lowassa alibanwa akaamua kujisalimisha, huyu yeye ana ushujaa gani? Kama kweli ni shujaa kwanini hakuonyesha huo ushujaa akiwa huko huko ccm? Cdm haihitaji kura hata moja ya Zanzibar, ili kupata ushindi, au uwakilishi mkubwa bungeni. Hatuna muda wa kuokoteza tena mgombea, wakati tuna wagombea wetu. ACT ndio inahitaji mgombea wa aina hiyo lakini sio cdm. Sisi wapiga kura wengi wa cdm tunajua fika tatizo ni tume isiyo huru ya uchaguzi, na sio mgombea wa kuokoteza. Ni vyema kuungana kupigania tume huru ya uchaguzi, na sio kuungana kumpa tapeli nafasi ya kuongoza wapinzani.
 
Sasa wapinzani watashinda vipi kama watu hawatojitokeza kupiga kura ?Pigeni kura lindeni kura hakuna wa kuwaibia. Ondoeni negativity. Mkicheza Bunge halitakuwa na mbunge hata mmoja wa upinzani. Kama ni kosa mtafanya basi ni kuwaambia watu wasiende kupiga kura.

Yaani suala la kuwa hatutaenda kupiga kura wengi tumeshafanya maamuzi, na impact yake utaiona kwenye huo ushenzi uitwao uchaguzi. Mtu pekee anayeweza kutufanya tujitokeze kwa shingo upande kupiga kura kwa tume hii ya kihuni, ni Tundu Lissu tu.

Wapinzani hatuna muda wa kuendelea kuumizwa, kufanyiwa ukatili, unyama na uhayawani wa wazi ili ccm watangazwe washindi, au mpinzani akipita kwa watu kuumizwa hivyo, bado anunuliwe kwenda kuunga mkono juhudi. Kwa hilo hatuko tayari. Huo unyama, ukatili na uhayawani wa wazi tumeuona kwa macho yetu, tena umekuwa ukiratibiwa na jeshi la polisi na tume ya uchaguzi, kwa maagizo ya jiwe.

Yaani sio wapinzani kukosa hata mbunge mmoja wa upinzani, hata wabunge wa ccm wakiamua kwenda na wake/waume zao ni sawa tu, kwani hata hilo bunge halina chochote cha maana, zaidi ya kupitisha kila atakacho Magufuli. Hilo bunge tunalidharau kuliko uchafu mwingine wowote. Tutatafuta namna nyingine ya kupata viongozi nje ya box la kura lisiloheshimiwa.
 
Jana niliombwa na leo nimekubali rasmi kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama cha ACT Wazalendo. Huu ni wakati muafaka kwangu wa kushiriki katika mazungumzo na vyama vingine kama CHADEMA ili tusimamishe "KISIKI CHA MPINGO" kimoja!.

=======


Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe. Kwa kabila, Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe.

Elimu:
1962 – 1968:
Elimu ya msingi katika shule ya msingi ya Chiponda, Lindi.
1969 – 1972: Elimu ya Sekondari, (O-level) Namupa Seminary, Lindi
1973 – 1974: Kidato cha tano na sita (A-level) Itaga Seminary, Tabora
1975 – 1980: Aliajiriwa serikalini, ofisi ya rais
1981 – 1984: Alipata Shahada ya kwanza katika tasnia ya Sayansi katika maswala ya Siasa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor Political Science and International Relations with Hons, First class, University of Dar es salaam)
1985 – 1989: Aliendelea na ajira yake serikalini katika katika ofisi ya rais
1990 – 1992: Alipata Stashada ya Uchumi, Mahusiano ya Kimataifa na Sheria za Kimataifa (Masters- Economics, International Relations and International Law, John Hopkins University Marekani)
1993 – 1994: Alirudi serikalini kuendelea na kazi kama mchambuzi za mambo ya ulinzi na usalama

Mafunzo:
Kati ya mwaka 1975 na 1976 Ndugu Bernard Membe alijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Oljoro, Arusha. Hii ni kwa mujibu wa Sheria ambapo vijana wote waliohitimu kidato cha Sita walitakiwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi kwa muda wa mwaka mmoja. Baada ya kuhitimu mafunzo hayo ya Jeshi, Ndugu Membe aliajiriwa katika Ofisi ya Rais, Utawala bora.

Mwaka 1978, Ndugu Membe alipata Mafunzo ya sheria za Jinai na usalama wa nchi, nchini Uingereza. Aidha, mwaka 1980, Ndugu Membe alipata mafunzo ya siasa, katika Chuo cha Chama cha Mapinduzi (CCM), Kivukoni, Dar es Salaam.

Familia:
Mwaka 1986, Ndugu Bernard Membe alifunga ndoa Takatifu na Dorcas Richard Masanche, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam. Ndugu Membe na mama Dorcas wamejaliwa kupata watoto watatu, Cecilia, Richard na Denis.

Siasa:
Ndugu Membe ametumikia nafasi mbalimbali ikiwemo Kamanda wa Vijana wa Mkoa wa Lindi, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, na Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Mwaka 2000, aliingia Bungeni baada ya kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Mtama, kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Licha ya uchanga wake bungeni, akiwa kama mbunge wa kawaida (back bencher), Bernard Membe alikuwa mchangiaji mkubwa wa mijadala inayohusu Amani, Ulinzi na Usalama pamoja na Utawala Bora.

Mwaka 2005, Bernard Membe alichaguliwa tena na wananchi wa Jimbo la Mtama kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tofauti na kipindi cha nyuma, Bernard Membe alianza muhula wa pili wa Ubunge, Januari 2006, kama ‘front bencher’ baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Kufuatia mabadiliko ya baraza la Mawaziri mnamo mwezi Oktoba, 2006, Bernard Membe alihamishwa Wizara na kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Nishati na Madini – moja ya wizara ngumu na nyeti kwa Taifa.

Hata hivyo miezi michache baadae, yaani January 2007, rais Jakaya Mrisho Kikwete alimteua Bernard Membe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa baada ya aliyakuwa anashikilia wadhifa huo - Dr Asha Rose Migiro - kuteuliwa na Katibu Mkuu Baraza la Umoja wa Kimataifa na kuwa Naibu Katibu mkuu wa baraza hilo. Bernard Membe amehudu katika nafasi hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu 2007 hadi 2015, akiwa ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo kwa miaka mingi mfululizo, akitanguliwa na Rais Kikwete ambaye alidumu katika Wizara hiyo kwa miaka 10 mfululizo.

Mafanikio:
Bernard Membe ameongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kipindi ambacho Tanzania na dunia, kwa ujumla, ilikabiliwa na changamoto kubwa katika mambo mbalimbali yanahusiana na ulinzi na usalama, uchumi na ajira (hasa kwa vijana). Changamoto hizo zimepelekea hali ya amani kwa ujumla kutetereka katika maeneo mengi ya dunia.

Hata hivyo, chini ya uongozi wa Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatafa, Tanzania imeendelea kuwa mtetezi na mshirika mkubwa wa ulinzi na usalama ndani ya Ukanda wa Afrika na duniani. Tanzania imeshiriki kuleta amani katika nchi za Maziwa makuu yaani, DRC, Burundi na Malawi, lakini pia Tanzania imeshiriki katika utatuzi wa migogoro ya kisiasa katika nchi za Comoro, Madagasca, na Sudan ya Kusini. Aidha, Tanzania imekuwa mshiriki mzuri katika kuchangia vikosi vya kulinda amani katika mataifa ambayo yalipata machafuko kisiasa.

Uchumi: Bernard Membe amesimamia vema utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya uchumi ili kuwezesha Tanzania kufanya mageuzi ya kiuchumi na kijamii na kuininua hali za wananchi wake. Ni katika kipindi chake, nchi imeshuhudia uwekezaji mkubwa katika eneo la viwanda, gesi, makaa ya mawe, kilimo na utalii. Chini ya uongozi wa Ndugu Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilipata tuzo ya utendaji bora iliyotolewa na sekta binafsi kwa kutambua mchango mkubwa wa Wizara katika kukuza sekta binafsi Tanzania.

Kudumisha mahusiano kimataifa: Katika kipindi chake, Tanzania imefanikiwa kuipaisha Diplomasia yake katika Jumuiya ya Kimataifa kwa kutembelewa na viongozi mbalimbali mashuhuri kama, Marais George W. Bush na Baraka Obama wote wa Marekani, Xi Jinping wa Uchina, Joachim Gauck wa Ujerumani, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Mwai Kibaki na Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda, Piere Nkuruzinza wa Burundi, Joseph Kabila wa DRC, Philipe Nyusi wa Msumbiji, Mwana wa Mfalme wa Malkia wa Uiengereza, na Mwana wa Mfalme wa Japan.

Pia chini ya uongozi Ndugu Bernard Membe Tanzania imefanikiwa kupanua wigo wa mahusiano yake Kaimataifa kwa kufunguwa Balozi mpya katika nchi za Malaysia, Brazil, Comoro, Oman, Umoja wa Falme za Kiarabu na Kuwait. Aidha, Wizara imefanikiwa kufungua upya Ubalozi wa Tanzania the Hague, Uholanzi uliofungwa mwaka 1994. Kadhalika Balozi Mpya za Brazil, Oman, Uturuki, Kuwait, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Namibia zilifunguliwa hapa nchini.

Kutambuliwa:
Kwa kutambua mchango wake katika kurejesha hali ya amani na utulivu katika Visiwa vya Comoro, mwaka 2008, Bernard Membe alikuwa miongoni mwa watanzania waliotunukiwa Nishani ya Operesheni Demokrasia Comoro na rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Uozefu:
2006 – hadi 2015:
Mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2008 – Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Africa, Addis Ababa, Ethiopia.
Mkuu wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe kutoka muungano wa nchi za ukanda wa Afrika Kusini, SADC
2006 – 2011: Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, CCM
2006 – 2011: Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa.
2006 – 2015: Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Taifa
2013 – 2015: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Madola Commonwealth
2014 – 2015: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amekuwa mjumbe wa kamati za usuluhishi katika migogoro kwenye nchi za Sudan ya Kusini, Madagascan na katika mzozo wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi.

Pia Tanzania imefanikiwa kushiriki katika zoezi la Uangalizi wa chaguzi kwa niaba ya SADCC katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Madagasca, Kenya, Comoro na Afrika ya Kusini.

Zaidi, soma:

Uchaguzi 2020 - Bernard Membe achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo
Anafaa
 
Habari mbaya kwa Tundu Lisu plan B yakev akibwagwa na Chadema imeshazibwa na Membe hatalala Leo Lisu

Pole Lisu hizo ndio siasa.Tulikwambia humu jamii Forums don't overate yourself

Ni hivi, Tundu Lissu ndio chaguo letu wapiga kura wa ukweli wa upinzani. Yaani hata wajichanganye Mbowe, Nyalandu, Membe, Msigwa nk, bado wote kwa pamoja hawana mvuto kwetu wapiga kura wa kweli wa upinzani kama alivyo Lissu. Hivyo Lisu hana lolote la kuogopa maana ana watu wa ukweli nyuma yake. Sana sana Lisu asipopitishwa, ni ahueni kwa Magufuli maana yeye ndio hawezi siasa za ushindani.
 
Ngoja kwanza, something or some details are missing somewhere kwenye nii CV ya Membe! Hili hatalisema yeye, Membe wala viongozi wa ACT - Wananchi (siyo Wazalendo, it is too big a name, what fits them is Wananchi and not Wazalendo) ni suala la ufisadi, wizi na ubadhirifu mkubwa wa fedha za Watanzania zilizorudi kama chenji ya RADAR (Si mnakumbuka ule ufisadi katika ununuzi wa ile RADAR kutoka Uingereza), ambazo ilikubaliwa zielekezwe kwenye sekta ya elimu na yeye, Membe, kwa kusaidiwa na viongozi mafisadiwenzake, akalichukua hilo jukumu. Na mwisho wa hizo pesa, kila mtu anaulizia ZILIPOKWENDA. Anao wajibu kulielezea hili kwa Watanzania wote. Hili halina ushabiki wa upenzi wa vyama vya siasa ni suala la maslahi yetu Watanzania. Suala jingine ni hili la pesa za uwekezaji zilizo tolewa na Serikali na Wawekezaji kutoka Libya. Peas zilifika na kabla mambo hayajawa sawasawa ukatokea mzozo huko Libya. Kwa uzoefu wake, Bernad Membe alijua hilo limetoka na hakuna atakaye kumbuka hizo peas kutoka Libya.Akaamua KUZIPIGA JUU KWA JUU. Hivyo hili pia anao wajibu wa kutueleza Watanzania, kwani inaweza kutokea neema huko Libya siku moja mambo yakawa shwari, watakuja kudai pesa zao kwani haki ya mtu haipotei. TUSUBIRI MAJIBU.

Simtetei Membe kwa lolote, hebu tuambie Magufuli alijibia wapi zilipo zile 250b za wizara ya ujenzi mpaka akawa rais? Au hizi 1.5t ni wapi alizitolea majibu?
 
Simtetei Membe kwa lolote, hebu tuambie Magufuli alijibia wapi zilipo zile 250b za wizara ya ujenzi mpaka akawa rais? Au hizi 1.5t ni wapi alizitolea majibu?
Kwa kweli mimi nimeandika kitu mabacho kinajulikana na matokeo yake yako wazi- nenda Lindi ukatafute kiwanda cha sementi kilichokusudiwa na hiyo pesa ya Libya. Ukikiona tueleze. Mahoteli ya Membe huko Lindi na Mtwara ni mazao hiyo pesa za Libya na ile CHENJI YA RADAR ambayo ililengwa kunufaisha shule zetu. Tuonyeshe hayo madaftari na madawati yaliyokusudiwa na hizo pesa za CHENJI YA RADAR1 Hizo za unazozungumzia za Rais Magufuli hebu zitolee maelezo zaidi ili tujue details zake na tuone namna ya kuchangia.
 
Kwa kweli mimi nimeandika kitu mabacho kinajulikana na matokeo yake yako wazi- nenda Lindi ukatafute kiwanda cha sementi kilichokusudiwa na hiyo pesa ya Libya. Ukikiona tueleze. Mahoteli ya Membe huko Lindi na Mtwara ni mazao hiyo pesa za Libya na ile CHENJI YA RADAR ambayo ililengwa kunufaisha shule zetu. Tuonyeshe hayo madaftari na madawati yaliyokusudiwa na hizo pesa za CHENJI YA RADAR1 Hizo za unazozungumzia za Rais Magufuli hebu zitolee maelezo zaidi ili tujue details zake na tuone namna ya kuchangia.

Hayo macho uliyoonea wizi wa Membe, ungeyatumia hayo hayo kuona wizi wa Magufuli.
 
Hayo macho uliyoonea wizi wa Membe, ungeyatumia hayo hayo kuona wizi wa Magufuli.
Wewe uliyeuona TUELEZE. Wizi wa Membe una hizo data na facts au mapenzi yana pofusha? Halafu huo uoga wa Rais Magufuli uko wapi?Ni nani, ni Rais gani, ukimwacha Baba wa Taifa, J.K. Nyerere, aliyewakabiri wakoloni na wanyonyaji wa mali na uchumi wetu ANA KWA NA NA MACHO KWA MACHO na kuwaeleza ukweli wa mambo yalivyo.
 
nimependa kuona Membe alipata first class , Mlimani si pa kispoti spoti japo nasi tunazo honours zetu za pale ila first class kiboko!!big up Membe! salute!!

Membe Chukua sera ya ajira , njaa kali na hali ngumu , mikopo bila riba na udhamini, uhuru wa kujieleza na maandamano ukajiuze kwenye kampeni, zako
 
Jana niliombwa na leo nimekubali rasmi kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama cha ACT Wazalendo. Huu ni wakati muafaka kwangu wa kushiriki katika mazungumzo na vyama vingine kama CHADEMA ili tusimamishe "KISIKI CHA MPINGO" kimoja!.

=======


Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe. Kwa kabila, Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe.

Elimu:
1962 – 1968:
Elimu ya msingi katika shule ya msingi ya Chiponda, Lindi.
1969 – 1972: Elimu ya Sekondari, (O-level) Namupa Seminary, Lindi
1973 – 1974: Kidato cha tano na sita (A-level) Itaga Seminary, Tabora
1975 – 1980: Aliajiriwa serikalini, ofisi ya rais
1981 – 1984: Alipata Shahada ya kwanza katika tasnia ya Sayansi katika maswala ya Siasa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor Political Science and International Relations with Hons, First class, University of Dar es salaam)
1985 – 1989: Aliendelea na ajira yake serikalini katika katika ofisi ya rais
1990 – 1992: Alipata Stashada ya Uchumi, Mahusiano ya Kimataifa na Sheria za Kimataifa (Masters- Economics, International Relations and International Law, John Hopkins University Marekani)
1993 – 1994: Alirudi serikalini kuendelea na kazi kama mchambuzi za mambo ya ulinzi na usalama

Mafunzo:
Kati ya mwaka 1975 na 1976 Ndugu Bernard Membe alijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Oljoro, Arusha. Hii ni kwa mujibu wa Sheria ambapo vijana wote waliohitimu kidato cha Sita walitakiwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi kwa muda wa mwaka mmoja. Baada ya kuhitimu mafunzo hayo ya Jeshi, Ndugu Membe aliajiriwa katika Ofisi ya Rais, Utawala bora.

Mwaka 1978, Ndugu Membe alipata Mafunzo ya sheria za Jinai na usalama wa nchi, nchini Uingereza. Aidha, mwaka 1980, Ndugu Membe alipata mafunzo ya siasa, katika Chuo cha Chama cha Mapinduzi (CCM), Kivukoni, Dar es Salaam.

Familia:
Mwaka 1986, Ndugu Bernard Membe alifunga ndoa Takatifu na Dorcas Richard Masanche, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam. Ndugu Membe na mama Dorcas wamejaliwa kupata watoto watatu, Cecilia, Richard na Denis.

Siasa:
Ndugu Membe ametumikia nafasi mbalimbali ikiwemo Kamanda wa Vijana wa Mkoa wa Lindi, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, na Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Mwaka 2000, aliingia Bungeni baada ya kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Mtama, kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Licha ya uchanga wake bungeni, akiwa kama mbunge wa kawaida (back bencher), Bernard Membe alikuwa mchangiaji mkubwa wa mijadala inayohusu Amani, Ulinzi na Usalama pamoja na Utawala Bora.

Mwaka 2005, Bernard Membe alichaguliwa tena na wananchi wa Jimbo la Mtama kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tofauti na kipindi cha nyuma, Bernard Membe alianza muhula wa pili wa Ubunge, Januari 2006, kama ‘front bencher’ baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Kufuatia mabadiliko ya baraza la Mawaziri mnamo mwezi Oktoba, 2006, Bernard Membe alihamishwa Wizara na kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Nishati na Madini – moja ya wizara ngumu na nyeti kwa Taifa.

Hata hivyo miezi michache baadae, yaani January 2007, rais Jakaya Mrisho Kikwete alimteua Bernard Membe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa baada ya aliyakuwa anashikilia wadhifa huo - Dr Asha Rose Migiro - kuteuliwa na Katibu Mkuu Baraza la Umoja wa Kimataifa na kuwa Naibu Katibu mkuu wa baraza hilo. Bernard Membe amehudu katika nafasi hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu 2007 hadi 2015, akiwa ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo kwa miaka mingi mfululizo, akitanguliwa na Rais Kikwete ambaye alidumu katika Wizara hiyo kwa miaka 10 mfululizo.

Mafanikio:
Bernard Membe ameongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kipindi ambacho Tanzania na dunia, kwa ujumla, ilikabiliwa na changamoto kubwa katika mambo mbalimbali yanahusiana na ulinzi na usalama, uchumi na ajira (hasa kwa vijana). Changamoto hizo zimepelekea hali ya amani kwa ujumla kutetereka katika maeneo mengi ya dunia.

Hata hivyo, chini ya uongozi wa Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatafa, Tanzania imeendelea kuwa mtetezi na mshirika mkubwa wa ulinzi na usalama ndani ya Ukanda wa Afrika na duniani. Tanzania imeshiriki kuleta amani katika nchi za Maziwa makuu yaani, DRC, Burundi na Malawi, lakini pia Tanzania imeshiriki katika utatuzi wa migogoro ya kisiasa katika nchi za Comoro, Madagasca, na Sudan ya Kusini. Aidha, Tanzania imekuwa mshiriki mzuri katika kuchangia vikosi vya kulinda amani katika mataifa ambayo yalipata machafuko kisiasa.

Uchumi: Bernard Membe amesimamia vema utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya uchumi ili kuwezesha Tanzania kufanya mageuzi ya kiuchumi na kijamii na kuininua hali za wananchi wake. Ni katika kipindi chake, nchi imeshuhudia uwekezaji mkubwa katika eneo la viwanda, gesi, makaa ya mawe, kilimo na utalii. Chini ya uongozi wa Ndugu Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilipata tuzo ya utendaji bora iliyotolewa na sekta binafsi kwa kutambua mchango mkubwa wa Wizara katika kukuza sekta binafsi Tanzania.

Kudumisha mahusiano kimataifa: Katika kipindi chake, Tanzania imefanikiwa kuipaisha Diplomasia yake katika Jumuiya ya Kimataifa kwa kutembelewa na viongozi mbalimbali mashuhuri kama, Marais George W. Bush na Baraka Obama wote wa Marekani, Xi Jinping wa Uchina, Joachim Gauck wa Ujerumani, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Mwai Kibaki na Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda, Piere Nkuruzinza wa Burundi, Joseph Kabila wa DRC, Philipe Nyusi wa Msumbiji, Mwana wa Mfalme wa Malkia wa Uiengereza, na Mwana wa Mfalme wa Japan.

Pia chini ya uongozi Ndugu Bernard Membe Tanzania imefanikiwa kupanua wigo wa mahusiano yake Kaimataifa kwa kufunguwa Balozi mpya katika nchi za Malaysia, Brazil, Comoro, Oman, Umoja wa Falme za Kiarabu na Kuwait. Aidha, Wizara imefanikiwa kufungua upya Ubalozi wa Tanzania the Hague, Uholanzi uliofungwa mwaka 1994. Kadhalika Balozi Mpya za Brazil, Oman, Uturuki, Kuwait, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Namibia zilifunguliwa hapa nchini.

Kutambuliwa:
Kwa kutambua mchango wake katika kurejesha hali ya amani na utulivu katika Visiwa vya Comoro, mwaka 2008, Bernard Membe alikuwa miongoni mwa watanzania waliotunukiwa Nishani ya Operesheni Demokrasia Comoro na rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Uozefu:
2006 – hadi 2015:
Mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2008 – Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Africa, Addis Ababa, Ethiopia.
Mkuu wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe kutoka muungano wa nchi za ukanda wa Afrika Kusini, SADC
2006 – 2011: Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, CCM
2006 – 2011: Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa.
2006 – 2015: Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Taifa
2013 – 2015: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Madola Commonwealth
2014 – 2015: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amekuwa mjumbe wa kamati za usuluhishi katika migogoro kwenye nchi za Sudan ya Kusini, Madagascan na katika mzozo wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi.

Pia Tanzania imefanikiwa kushiriki katika zoezi la Uangalizi wa chaguzi kwa niaba ya SADCC katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Madagasca, Kenya, Comoro na Afrika ya Kusini.

Zaidi, soma:

Uchaguzi 2020 - Bernard Membe achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo
Akapumzike,ACT inafutwa.
 
Back
Top Bottom