Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 122,494
- 96,074
Akikujibu naomba unijulishezimeshanunuliwa tani ngapi mpaka sasa, na ni wakulima wangapi wameshalipwa pesa yao taslimu?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Akikujibu naomba unijulishezimeshanunuliwa tani ngapi mpaka sasa, na ni wakulima wangapi wameshalipwa pesa yao taslimu?
Eti zimemwinua Magufuli, subiri uone jinsi zinavyomshusha baada ya kufelisha wakulima na wafanyabiashara.
Membe kaamua kushusha mvua kabisa ili kuwaharibia.
Umenena vyema. Ni mkakati mzuri. Wawangalie vizuri huenda wanapata ushawishi wa fedha na mambo mengine kutoka kwa mabeberu wa nje. Ikithibitika watoswe mapema.
Ruksa aende chadema. Huku tumemchoka mtu wa visasiMembe kawashika mayai ya downtown... 2020 twende na Membe
Mwisho wa siku watatupangia hata chakula cha kwenye familia zetu, kwamba kama wewe si mkulima wa mahindi usiewe nayo ndani maana hata hutakiwi kuwa na unga maana wewe si mkulima wa mahindi! Karanga, mbaazi, ufuta na mengine mengi tuu, mwisho wa siku watatuambia kila mtu ale anachozalisha! Si tutakulana wenyewe sasa?? Maana wengine wanazalisha watoto tuu na kubeba mzigo ferry ndo wanapata hela ya kununua chakula!pole sana kiongozi, ila wanatuaminisha kwamba tupo kwenye RAITI TRAKI Mungu baba awalaani wote
Mwisho wa siku watatupangia hata chakula cha kwenye familia zetu, kwamba kama wewe si mkulima wa mahindi usiewe nayo ndani maana hata hutakiwi kuwa na unga maana wewe si mkulima wa mahindi! Karanga, mbaazi, ufuta na mengine mengi tuu, mwisho wa siku watatuambia kila mtu ale anachozalisha! Si tutakulana wenyewe sasa?? Maana wengine wanazalisha watoto tuu na kubeba mzigo ferry ndo wanapata hela ya kununua chakula!
Kwenye hii kampeni yao wanaleta unyonyaji wa dhahiri kabisa!
Kwani ni lazima wainunue korosho yangu?? Kama mi si mkulima waniache na mazao yangu nitakaanga nitazila mwenyewe kuliko kunifunga na kuninyang'anya na kuwalipa hela tena ya kutoka mahabusu!
Ccm wote ni wapuuzi na wasio na utu, kwa kifupi ni mashetani ndo maana wanataka na wengine tuishi kama wao!
Ujinga sasa wao ni mashetani ya kishua ila sisi wanataka tuwe mashetani malofa!
Hahahahaaaa
Mtaongea yote aisee....
Mtaongea kama kasuku.....sikujua kama Membe ni jitu linawaogopesha namna hii aisee!
CCM bana...mahoka matupu!
DuhEti zimemwinua Magufuli, subiri uone jinsi zinavyomshusha baada ya kufelisha wakulima na wafanyabiashara.
Membe kaamua kushusha mvua kabisa ili kuwaharibia.
Well said Genta, ukiwa na kiongozi ambaye anaamini yeye hakosei na anajitahidi kuaminisha watu kuwa matatizo yote yaliyopo yamesababishwa na wengine na kama ingekuwa yeye yasingekuwepo jua una janga. Haijaloshi huyo kiongozi ni wa ngazi ya familia, mtaa, kata, wilaya au Taifa, lakini bado itakupa shida. Kwenye ngazi ya familia kila mnapoomba viatu vya shule baba anawajibu, kama isingekuwa mama yenu kupenda kukaangiza kila siku wote mngekuwa na viatu pea mbili mbili, huyo ni baba mkwepa lawama. Anakwepa kuwajibika kwa yanayomhusu na kuwasukumia yasiyowahusu. Tabia hii sasa imeambukizwa kwa wapambe ambao ubovu wa serikali unatafutiwa wa kumtwisha. Sasa hivi unawaona wako kimya kuhusu pensheni ya 25%, lakini usidhani wamelala, hawalali wanatafuta wa kumtwisha zigo hilo. Serikali ya Wasafi Classic, hawataki uchafu na wako tayari kupaka rangi uchafu ili waonekane wasafi muda wote.Japo nina ' Upinzani ' wangu na Mheshimiwa Benard Membe hasa katika suala lake zima la Yeye kutaka kuwa Rais wa Tanzania na pia kuhusu ' Strategies ' zake kwasababu zangu ambazo nazijua mwenyewe ( na sihitaji niziweke hapa ) ila naomba nami leo niseme kwamba nadhani sasa huyu Benard Membe ' anaonewa ' tu na kuna Watu sasa wanataka ' Kuhalalisha ' maovu yao na unafiki wao kupitia mgongo wa Membe ili tu waaminike ama waaminiwe na mambo yao yaende sawa.
Benard Membe kama Mwanadamu, Mwanasiasa na Mwana CCM ( tena Kada kabisa ) ana mapungufu yake fulani fulani kama ambavyo Mimi GENTAMYCINE, Wewe na Yule tunayo lakini naanza kuona kama vile kuna Watu sasa ' nchi imewashinda ' hivyo wanataka kuanza ' Kuhalalisha ' huko ' Kushindwa ' Kwao kwa ' Kumsingizia ' Membe wakati ukweli ni kwamba waliaminiwa, wakapewa dhamana na kuna mahala ' wamekengeuka / wamekosea ' sasa yanawashinda wanakimbilia ' Kumsakama ' Mzee wa Watu Membe.
Jengeni nchi kama mlivyowaaminisha Watanzania na acheni Kumsumbua na Kumnyanyasa Mzee wa Watu Benard Membe. Sasa imetosha na hatutaki kusikia haya ' Malumbano ' ya ' Kipopoma / Kipumbavu ' ambayo sioni ' Tija ' yake kwa nchi na Taifa huku tukijua ya kwamba bado kuna matatizo mengi sana tena ya ' Kimaendeleo ' yanaisibu Tanzania yetu na Watanzania mmoja mmoja.
Binafsi ' nimechoka ' na huu Upuuzi / Upupu.
Wewe subiri tu mwaka 2019 kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na wa ule wa 2020, hakuna cha kampeni mzee kila kitu kishaisha. Mlimu-beep Magufuli akawapigia, sasa mnalialia, why?Imemuinua kwenye nini, wakati wakulima had I sasa hivi wanalia na haijulikani kama watoto wataenda shule January?
Malipo ya mwaka huu yanazidi Yale ya mwaka Jana na juzi ambapo bei ilifika elfu tatu na mia nane?
Nyie mpo Dar huko mnaongelea watu wanaolima korosho? Mliwatengeneza wanakijiji wa Mtonya-Tunduru wawasifie sasa hivi wanalia njaa.
View attachment 955390
Siasa za korosho zimemuinua zaidi Rais Magufuli na kumdhohofisha zaidi Bernard Membe katika ngome yake.
Kumekuwepo na tetesi kuwa, Bernard Membe, pamoja na mtandao wa watu wake wakiwemo, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia na wengine wanaotokea Mikoa ya Ukanda wa Pwani; hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli wa kununua korosho kwa wakulima tena kwa bei ya juu kuliko iliyokuwa imepangwa hapo awali.
Maneno aliyoongea Nape Nnauye bungeni yanaonyesha wazi kuwa bado hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali kununua korosho kwani Nape badala ya kufafanua uamuzi wa Serikali kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu, yeye:
- Aliwasifia wakulima kwa kuwa wavumilivu na watulivu.
- Kukosoa Serikali kuwa, haikutumia busara kushughulikia sakata la korosho.
- Kuitaka Serikali inunue haraka korosho ili wakulima wasipate hasara zaidi.
- Halmashauri kuingia hasara kutokana na kutegemea korosho.
Aidha, akiwa ziarani mkoani Arusha, Rais Dk. John Pombe Magufuli aliwatuhumu baadhi ya wanasiasa kwa kutaka kuihujumu Serikali katika uuzaji wa zao la korosho. Alisema kuwa, baadhi yao walinunua korosho changa kwa wakulima katika mfumo wa kangemba na sasa wanataka kuiuza wakati hawana mashamba. Rais alisema korosho itakayonunuliwa ni ile ya wale watakaoonyesha mashamba yao na watakaoshindwa kuonyesha mashamba yao, korosho yao itataifishwa.
Hivyo, ni wazi kuwa, wanasiasa wa Mikoa ya Kusini anakotokea Membe na Nape, walijisikia vibaya sana kuona Serikali ikiamua kununua korosho tena kwa bei ya Tsh. 3,300.
So alichofanya Dk. Bashiru ni mwendelezo wa hatua za kisiri siri za kundi la Membe kuihujumu Serikali ya Awamu ya Tano, tena kwa kusaidiwa na baadhi ya Makada wa Chama, ambao wengi wao ndio waliokuwa Viongozi kwenye utawala uliopita na ambao wameachwa ama kutumbuliwa katika Awamu ya Tano.
Hata kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia ni kutokana kushindwa kwake kuishauri Serikali kwa kuwa, alikuwa katika kundi linalohujumu Serikali.
Kwa ujumla, kitendo cha Rais Dk. John Pombe Magufuli kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu ya Tsh. 3,300 kimewaacha Wapinzani wake ndani ya CCM midomo wazi kwani hawakutegemea kabisa kuwa, Serikali ingekuwa tayari kwenda that extra mile. Walijidai kumu-beep Magufuli, naye akawapigia - sasa wanaugulia mioyoni mwao.
Na ghafula Kanda ya Ziwa, Kanda Kati, Kanda ya Kusini na Kanda ya Magharibi zimeenda kwa Magufuli huku Nyanda za Juu yote (isipokuwa Mbeya) ikiwa pia kwa Omuzilankende. Kanda ipi imebaki? Huko Kaskazini baada ya CHADEMA kumkorofisha na kumdharau Lowassa, ni wazi 2020, itakuwa nusu kwa nusu.
Ngoja tuone!!
View attachment 955390
Siasa za korosho zimemuinua zaidi Rais Magufuli na kumdhohofisha zaidi Bernard Membe katika ngome yake.
Kumekuwepo na tetesi kuwa, Bernard Membe, pamoja na mtandao wa watu wake wakiwemo, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia na wengine wanaotokea Mikoa ya Ukanda wa Pwani; hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli wa kununua korosho kwa wakulima tena kwa bei ya juu kuliko iliyokuwa imepangwa hapo awali.
Maneno aliyoongea Nape Nnauye bungeni yanaonyesha wazi kuwa bado hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali kununua korosho kwani Nape badala ya kufafanua uamuzi wa Serikali kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu, yeye:
- Aliwasifia wakulima kwa kuwa wavumilivu na watulivu.
- Kukosoa Serikali kuwa, haikutumia busara kushughulikia sakata la korosho.
- Kuitaka Serikali inunue haraka korosho ili wakulima wasipate hasara zaidi.
- Halmashauri kuingia hasara kutokana na kutegemea korosho.
Aidha, akiwa ziarani mkoani Arusha, Rais Dk. John Pombe Magufuli aliwatuhumu baadhi ya wanasiasa kwa kutaka kuihujumu Serikali katika uuzaji wa zao la korosho. Alisema kuwa, baadhi yao walinunua korosho changa kwa wakulima katika mfumo wa kangemba na sasa wanataka kuiuza wakati hawana mashamba. Rais alisema korosho itakayonunuliwa ni ile ya wale watakaoonyesha mashamba yao na watakaoshindwa kuonyesha mashamba yao, korosho yao itataifishwa.
Hivyo, ni wazi kuwa, wanasiasa wa Mikoa ya Kusini anakotokea Membe na Nape, walijisikia vibaya sana kuona Serikali ikiamua kununua korosho tena kwa bei ya Tsh. 3,300.
So alichofanya Dk. Bashiru ni mwendelezo wa hatua za kisiri siri za kundi la Membe kuihujumu Serikali ya Awamu ya Tano, tena kwa kusaidiwa na baadhi ya Makada wa Chama, ambao wengi wao ndio waliokuwa Viongozi kwenye utawala uliopita na ambao wameachwa ama kutumbuliwa katika Awamu ya Tano.
Hata kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia ni kutokana kushindwa kwake kuishauri Serikali kwa kuwa, alikuwa katika kundi linalohujumu Serikali.
Kwa ujumla, kitendo cha Rais Dk. John Pombe Magufuli kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu ya Tsh. 3,300 kimewaacha Wapinzani wake ndani ya CCM midomo wazi kwani hawakutegemea kabisa kuwa, Serikali ingekuwa tayari kwenda that extra mile. Walijidai kumu-beep Magufuli, naye akawapigia - sasa wanaugulia mioyoni mwao.
Na ghafula Kanda ya Ziwa, Kanda Kati, Kanda ya Kusini na Kanda ya Magharibi zimeenda kwa Magufuli huku Nyanda za Juu yote (isipokuwa Mbeya) ikiwa pia kwa Omuzilankende. Kanda ipi imebaki? Huko Kaskazini baada ya CHADEMA kumkorofisha na kumdharau Lowassa, ni wazi 2020, itakuwa nusu kwa nusu.
Ngoja tuone!!