Bernard Membe rasmi ACT Wazalendo, kutambulishwa kesho

Bernard Membe rasmi ACT Wazalendo, kutambulishwa kesho

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe katika ukurasa wake wa Twitter amepakia picha akiwa anatabasamu huku akiwa ameshika Katiba ya chama cha ACT Wazalendo . Je, inaashiria kwamba amehamia katika chama hiki? Ikumbukwe Membe amefukuzwa kwenye chama cha Mapinduzi siku za hivi karibuni.

Amenukuliwa mara kwa mara akitaka kugombea Urais wa JMT.

Membe1.JPG



=====================================​
Kiongozi mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameweka wazi kuwa kesho Julai 16, 2020 watamtambulisha rasmi aliyekuwa waziri wa mambo ya nje Bernard Membe kuwa mwanachama rasmi wa chama hicho baada ya kufukuzwa na chama chake cha zamani (CCM).

Zitto ameweka wazi hayo kwenye ujumbe alituma kwenye ukurasa wake wa twitter akiwa ameweka picha ya Membe huku akiwa ameshikilia kitabu cha ACT-Wazalendo.

Kwa muda mrefu sasa Bernard Membe amekuwa akihusishwa na kuhamia kwenye chama cha ACT wazalendo baada ya kufukuzwa CCM baada ya kukiuka baadhi ya taratibu za chama hicho.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa mwanahalisi Membe atatambulishwa kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mlimani City mbele ya wanachama wa chama hicho.
 
Kiongozi mkuu wa ACT wazalendo Zitto Kabwe ameweka kwenye akaunti yake ya twitter picha ya Bernad Membe na kuandika:

Kesho.....

Je kesho kuna nini?
Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
 
Kesho Julai 16 Benard Membe ataingia rasmi ACT kisha atakabidhiwa form ya kugombea urais JMT kupitia chama hicho.
 
Ndugu wana jamvi,

Kuna hiki kinachoendelea ndani ya bongo politics. Tuliyashuhudia ya EL sasa ni zamu ya MB.

Swali la msingi la kujiuliza je kuondoka kwao ccm ni kunafanana kwa maana membe ameondoka km lowasa na atarud km lowasa au kuna tofauti kati yao?
 
Ndugu wana jamvi
Kuna hiki kinachoendelea ndani ya bongo politics
Tuliyashuhudia ya EL sasa ni zamu ya MB.
Swali la msingi la kujiuliza je kuondoka kwao ccm ni kunafanana kwa maana membe ameondoka km lowasa na atarud km lowasa au kuna tofauti kati yao?????
Membe kafukuzwa lowasa hakufukuzwa...
 
Ndugu wana jamvi
Kuna hiki kinachoendelea ndani ya bongo politics
Tuliyashuhudia ya EL sasa ni zamu ya MB.
Swali la msingi la kujiuliza je kuondoka kwao ccm ni kunafanana kwa maana membe ameondoka km lowasa na atarud km lowasa au kuna tofauti kati yao?????
IMG_20200715_122616.jpg
 
Wanaondoka kwa kukosa maslahi then wanageuzwa mitaji ktk chama chao kwa udhaifu wa upinzani
 
Back
Top Bottom