Bernard Membe: Tanzania diplomasia imeshuka awamu hii. Tutatengwa na majirani wakiona hatufuati vigezo vya WHO kupambana na COVID19

Bernard Membe: Tanzania diplomasia imeshuka awamu hii. Tutatengwa na majirani wakiona hatufuati vigezo vya WHO kupambana na COVID19

Bernard Membe ameongea kwa unyenyekevu tu. Siyo kwamba Diplomasia imeshuka bali Diplomasia imekufa. Tuna pimbi tu pale Ikulu ndiyo tumemkabidhi nchi
Watu wasipokuwa na hoja hukimbilia matusi!! Rais wetu ametusimamia vizuri na imara sana katika kipindi hiki ambacho vinginevyo kingekuwa kigumu sana! Walitegemea atateleza lakini hakuteleza! Wala hakuyumba!! Kwa hiyo maadui wa nchi yetu na mawakala wao wamekasirika sana baada ya kukosa kabisa mpenyo wa kuitikisa nchi yetu!! Hivi haujishangai kwa nini una hasira Kali kiasi hicho?
 
Msumbiji wamefanya upanuzi mkubwa wa bandari yao. kuna kampuni ya uholanzi imefanya hiyo kazi. Last week Maersk kashusha chombo kikubwa sana hapo port kwao. Na wanajitahidi kuimarisha ulinzi na usalama eneo lao kutengeneza njia salama kwa Zambia kutumia bandari yao. Ni kitu wameshashinda hadi sasa.

Hapa kwetu kuna siasa na uchaguzi, kuna mtu anahujumiwa live live. Kuna namna mtu anatafutiwa ili jamii isimkubali. Halafu najiuliza wale watanzania waliohamishia mitaji na biashara zao Zambia kuwakwepa kina Zakayo wa hapa, kwa sasa hali yao ikoje? Biashara zao wataziendeleza vipi kwa kufungwa mpaka?

Nyumbani ni nyumbani tuu,
Panueni tu magoli,Tanzania is the best place ,ngoja huko mizigo yao ikutane na waasi ili wapate akili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alitishia eti "niguse ninuke" Alivyoguswa badala ya kunuka akanukia!! Hana chochote Huyo!
Mkuu Membe anajua kuzungumza na mabeberu ,akiongezewa Oxygen na kaka mkubwa huoni kama anaweza akajimambafy?
Yeye anatumia leadership vacuum kuomba mechi ya marudio.
 
Nchi ya Viawanda inakosa hat akilo moja ya sukari hahahahaa tunadili na Wapinzani. Sasa tunatengwa na na majirani zetu. Hakuna mjadala serious kuhusu mambo yanayotokea nchini kila mtu anatetea uhai wake, njaa yake, familia yake. Nani atasimama ahesabiwe kwa kalamu ya moto na damu tuikoe Tanzania? Karibuni kwa kejeli na matusi


Verified Member.
 
Nimesikilza
Kwa makini mahojiano hayo,yalipangwa na DW na ni bias kabisa
Nasema hivyo kwa sababu eti ni Watanzania tu pekee ndio tutaathirika wakati hata Zambia wataathirika tena pakubwa kuliko sisi watanzania kwa sababu asilimia 70 %ya mizigo ya Zambia inatoka Tanzania
Hivi Zambia wanashindwa kutumia Beira

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akihojiwa na DW, waziri wa zamani wa mambo ya nje mheshimiwa Bernard Camilius Membe amesema katika awamu hii ya utawala wa Magufuli, diplomasia imeshuka mno.

Membe anaonya kwamba, tanzania awamu hii inajiendeshea mambo kivyakevyake nje ya utaratibu wa jumuia ya kimataifa.

Akoingelea suala la korona, Membe amedai kuwa Tanzania haiheshimu na imejitenga na miiko ya shirika la afya WHO.

Chanzo: DW

KUna mtu anataka kufungua utalii, sasa sijuhi utalii na nchi gani huku covid inasambaa kw akwenda mbele ?
 
Nimesikilza
Kwa makini mahojiano hayo,yalipangwa na DW na ni bias kabisa
Nasema hivyo kwa sababu eti ni Watanzania tu pekee ndio tutaathirika wakati hata Zambia wataathirika tena pakubwa kuliko sisi watanzania kwa sababu asilimia 70 %ya mizigo ya Zambia inatoka Tanzania

Mkuu aliyekuambi 70% i8natoka huku nani?
wacha upotoshaji
 
Watu wasipokuwa na hoja hukimbilia matusi!! Rais wetu ametusimamia vizuri na imara sana katika kipindi hiki ambacho vinginevyo kingekuwa kigumu sana! Walitegemea atateleza lakini hakuteleza! Wala hakuyumba!! Kwa hiyo maadui wa nchi yetu na mawakala wao wamekasirika sana baada ya kukosa kabisa mpenyo wa kuitikisa nchi yetu!! Hivi haujishangai kwa nini una hasira Kali kiasi hicho?
Haya watu wa kusifia na kuabudu mumevamia uzi. Hivi unajua kufika leo tu jumla ya vifo ni 1,200 kwa Tanzania bara na maambukizi ni zaidi ya 10,000.

Halafu jitu linalipwa Buk 7 na Bashite linakuja kumsifia huyu pimbi aliyejificha Chato wakati Watanzania wanakufa kisa UKAIDI wake.
 
MEMBE: KUTENGWA NI ANGUKO LA TANZANIA
"Kukosoa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) na kukataa kushirikiana na washirika wa kimataifa na kikanda katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona itagharimu Tanzania kiunajimu, Waziri wa zamani wa Mambo ya nje wa Tanzania", Bernard Membe alisema.

"Tutanyimwa fedha, utalii utashuka, ndege hazitakuja, wawekezaji wataambiwa wasije Tanzania na tunaweza hata kuwekewa vikwazo," Membe aliambia chapisho hili.
Kila mtu, alionya, hafurahii kwa jinsi Tanzania inavyopambana na janga hili ikiwa ni pamoja na WHO, Viongozi wa Afrika Mashariki, Viongozi wa SADC, Jumuiya ya Afrika (AU), benki ya IMF / Dunia, nchi za Ulaya, Merika na Uchina.

"Ni jambo rahisi tu kuelewa kuwa janga la kidunia kama hili inahitaji suluhisho la ulimwengu. Suluhisho za ulimwengu na kikanda zinahitaji mshikamano na mbinu na mikakati ya pamoja. Tunaonekana tukijitenga, tunalaumu na kutuhumu hata marafiki wetu bora duniani. Tunahitaji kufanya kazi pamoja na ulimwengu kupunguza na kutatua janga hili. Ninamsihi Rais na Serikali kufanya hivyo, lazima tubadilike na kwenda sambamba na ulimwengu! " alisema Membe.
Alitoa wito kwa nchi kufuata kikamilifu mahitaji yaliyowekwa na WHO na kufuata ushauri wa wataalam
Image may contain: 1 person, eyeglasses and closeup
 
Mtu mweusi kweli hajiamini ! Usa kila siku analitukana shirika la afya kuwa linatumika na China
Magufuli kuwa challenges Ndio iwe kosa?

Huyu Baba sijui Kwanini hampendi Rais wetu
Mkuu

Naona Uko na speed kureply Kila uzi humu jf Kwa sasa

Natumai wamekulipa buku 7 zako za mwezi huu..

Ngoja waanze kukukopa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom