best maandazi recipe

best maandazi recipe

Kuumua hamira kabla pia inafanya maandazi yako yasinuke hamira na kutofanya vidoto vyeusi ikiwa umezidisha hamira...


Kama ivo poa coz sipendi harufu ya hamira mara nyingi natumia baking powder
 
Best umesahau kuweka hatua ya kuchanganya hamira. mdogo wangu Eiyer atapika bila kutia hamira hapo lol. na utukumbushe kuweka samli ya moto kabla hatujaweka hamira kusudi isife nguvu.

asante mamito, hadi likizo iishe mmh! maandazi na mie huwa nashibia jikoni, lol

kumbe kula jikoni ndo kunakufanya unisubirishe chamber?
 
Mwenzio sipendi harufu ya hamira kabisaaaaaa.

Tena napenda maandazi ya kimombasa ambayo hayajajaa unga ndani. Yaani kunakuwa empty halafu hayana harufu ya hamira.

Wanakula asubuhi na mbaazi.

Hapo umetulia zako unasubiri Tahmeed ujirudie Bongo Daslaam.

Kudaadeki.
 
Hayo yawe motoo ooo sinia linaishia jikoni. ...mi hupendelea na katles za samaki/kuku....nitashibaje?
 
Mwenzio sipendi harufu ya hamira kabisaaaaaa.

Tena napenda maandazi ya kimombasa ambayo hayajajaa unga ndani. Yaani kunakuwa empty halafu hayana harufu ya hamira.

Wanakula asubuhi na mbaazi.

Hapo umetulia zako unasubiri Tahmeed ujirudie Bongo Daslaam.

Kudaadeki.

Mm linone kabisaa nyama ndani ilimradi liive. Hapo nitahisi nakula andazi!! Na mate yalee yanatrremka kooni..lol
 
Mwenzio sipendi harufu ya hamira kabisaaaaaa.

Tena napenda maandazi ya kimombasa ambayo hayajajaa unga ndani. Yaani kunakuwa empty halafu hayana harufu ya hamira.

Wanakula asubuhi na mbaazi.

Hapo umetulia zako unasubiri Tahmeed ujirudie Bongo Daslaam.

Kudaadeki.

Andazi kwa maharage linapendeza pia.
 
Hayo ya kubake tunaitaga ya kipemba/kupambia...
Upembani yanaokwa na mkaa huzidi utamu naona!!

Yeah yanakua matamu basi mie nafkiri yale yanayosukwa ndo yanaitwa ya kupambia...unajua hata mishkaki ya kuchomwa na mkaa na ya kuchomwa na grill ni tofauti utamu ya mkaa inakua mitamu zaidi....
 
Pia mazuri ukiya bake unaweka ufuta juu

Farkhina nieleweshe vizuri nikamsapraizi mama watoto, nini tofauti ya samli na siagi. Nipe kipimo cha maji na tui la nazi maana haya mambo ya jikoni yamenipita kushoto kidogo.
 
Heee usinikumbushe hiyo ya kupika maandazi bila hamira....nliwahi pigwa kofi la haja nlipika maandazi wakati wa kusubiri kuumuka hayaumuki kumbe nlisahau hamira weee ilikua kesi si ndogo maskini mama angu lile kofi alonipiga hadi leo sisahau kutia andazi hamira....

Ha ha haaaaaaaa. Wazee wetu hao. Ndo mpk leo yanakusaidia maskin
 
Ahsanta habibty. Vp haya yanafaa kuweka ile bizari tam? Mana mi napenda kuweka bizari tam yanakua yana ladha nzuri.
 
Farkhina nieleweshe vizuri nikamsapraizi mama watoto, nini tofauti ya samli na siagi. Nipe kipimo cha maji na tui la nazi maana haya mambo ya jikoni yamenipita kushoto kidogo.

Namsaidia. Siagi ni margarine/butter ile tunapaka kwenye mikate ya slices. Samli ghee ni ile tunatumia kupikia hata kwenye vitu vya kukarangiza pia tunatumia kama. Mfano wa samli ni aseel, cowboy, tanband kismayuu n.k.

Kuh tui la nazi au maji, ni makisii tu coz unakanda na dough yako iwe kiasi kama inavokua ya chapati. Kwa kuongezea atakuja mwenyewe chief cook farkhina
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom