Mkuu anawanyimaje elimu wananchi aliowaletea contena zima la vitabu toka UK, kitendo ambacho siku ya kuanzwa usambazaji wake rasmi, kilifunguliwa na Lowassa mwenyewe akiwa Waziri Mkuu, na kuonyehswa na media zote nchini?
Mkuu Idd Simba, alikubaliana na serikali wananchi wahamishwe maeneo yanayofurika, sio kitendo kilichokubaliwa na wananchi ndio maana ya kuwa na kiongozi moja ya kazi zake ni kufikiria in advance what is the best kwa wananchi at large, mama hakuzaliwa Uzambara huo ni uongo, familia ya mama inaitwa Kione Kilango, inatokea Kihurio mkuu, mbunge wa West alijaribu kutumia maneno kama yako ya uchonganishi ikabidi rais mwenyewe aje huko Same, na kuamua soko lijengwe East kama mama alivyoshauri, mama anafanya mambo mazito san kwa jimbo, sasa hivi kuna wafadhili wanakuja kutoka Idaho, ambao wanaletwa na kijana mmoja wa ki-Tanzania ambaye ni mwenyekiti wa Obama's Campaign huko, aliye-co ordinate kuja kwao kuleta maji safi na shule zaidi, mkuu acha majungu maana unaona vijana wenzio wa kipare wanavyochacharika na mama kuleta maendeleo huko badala ya matusi hapa JF!
Haya maneno ni yako wewe na yule kiongozi wenu mwenye chama ambacho kipo Same East tu lakini hakipo Tanzania nzima, hakuna mbunge mwenye akili timamu anaweza kusema hayo maneno, na ni maneno mnayozusha kila siku huko kama wakati wa kampeni, mkasema huyu mama amefukuzwa na mme wake ndio haji kwenye kampeni, akaja na kampeni mpaka mwisho yakawashinda, ni kawaida yenu mnaomchukia kuzusha maneno yasiyokuwa na mwisho na huu hapo juu ni uzuzshi na uzandiki!
Yona alipooona kuwa mume wa mama ana dalili za kupata urais, alimuomba kwamba hatagombea ubunge tena kule na kumuachia mama, alipooona mzee amekosa urais, akaamua kugombea, ndipo mama akamuambia kuwa "...Yona nitakutoa ubunge afadhali uache...." akaishia kumtoa kweli, maadui zake mkajaribu kumsaidia mama Kaboyoka yakawashinda maana mama ni jembe ulaya, akipita anasomba kila mtu, mama alimshinda Yona hands down, na aliposhindwa Yona akajaribu sana kumsaidia mama Kaboyoka, akaitwa cc na kuonywa kuwa aache ama sivyo atafukuzwa ccm, kwa hiyo mkuu acha uongo hapa huuu uwanja ni mkubwa sana mkuu!
Jina lake mkuu ni DR. John Samweli Malecela, vipi ukijifunza adabu na kuheshimu viongozi wako waliolifikisha taifa lako lilipo sasa, pamoja na matatizo yetu yote kitaifa mkuu kuna waliotufikisha hapa tulipo as a nation, kwa hiyo kuwa na heshima kidogo, Msuya ni mungu wenu huko mkuu si ndiye aliyeamua kiongozi wa kumrithi huko, na nyinyi siku zote mlikuwa mnampigia magoti mpaka mtu akigombea naye unbunge mnamfukuza kwenye society akipanda basi wote mnashuka, mkuu nyamaza tu maana ni aibu tupu jinsi Musya alivyokuwa akiwatesa huko, wewe labda niye hujui siasa z huko mkuu ninaweza kukusaidia mkuu!
Mama Kilango, hajawahi kufukuzwa kazi mahali popote, alianza kiwa Mwalimu wa Sekondari Kisutu, Accountant Air-Tanzania, Accountant Gulf Air, Mfanya biashara, Mwenyekiti UWT Kinondoni, Mbunge wa Rais, na sasa Mbunge wa Same East, nirudie tena kuwa hajawahi kufukuzwa kazi mahali popote kwa wizi, ni uongo mkuu wa mchana, cc huwa hampitishi mgombea yoyote aliyewahi kutuhumiwa na wizi, ni opportunist wa siasa kama walivyo wote wanasiasa, na kiboko wa ufisadi sasa hivi tunajribu kumuomba ahamie kwenye waliojiuzulu kupelekwa mahakamni, mkuu Bangusile acha uzandiki mkuu uweli ni kwamba huna convincing argument against mama, ila una maneno mengi ya chuki na ya kijiweni huko Same, otherwise nipo mkuu kukusaidia kuhusu jimbo la Same East na mbunge wake mkuu, maana hulijui.
Mkuu Nzoka,
Nafikiri haya mael;ezo yamekutosha maana na wewe siioni point yako iko wapi, halafu tumia majina yako tu ya kawaida huna sababu ya kujificha nyuma ya hili jina la Nzoka, hivi umegundua kuwa huwa unatumia majina ya Kaskazini tu,
Ahsante Mkuu!