Betting ni mchezo unaoweza kukuletea umasikini hata kukuua!

Betting ni mchezo unaoweza kukuletea umasikini hata kukuua!

Sasa ndipo ucheze kama dozi ya dawa (mara 3 kwa siku)?
point yangu ni moja tu, "betting ni kupoteza pesa na muda" baada ya kujua kiasi unachopoteza ndipo utaanza kujiona wa hovyo. Ndo maana nimekwambia wewe bado mchanga kwenye betting huna experience kuweza kumshawishi mtu
 
point yangu ni moja tu, "betting ni kupoteza pesa na muda" baada ya kujua kiasi unachopoteza ndipo utaanza kujiona wa hovyo. Ndo maana nimekwambia wewe bado mchanga kwenye betting huna experience kuweza kumshawishi mtu
Mimi betting haijawahi kunitia hasara. I bet responsibly. Hasara kwenye betiing inakuwaje mkuu?
 
Sidhani kama kuna mtu anabeti/alibeti kunishinda mimi!

Betting ina addiction ile mbaya, ikikukumba siyo rahisi kucomoka!

Hongera nyingi kwa aliegundua hii michezo, alitumia akili kwelikweli! Nimetumia kila mbinu, kila hesabu ninazozijua lakini kipigo kiko palepale!

Pia niwape pole wale mnaoamini kwamba ipo siku watatusua kwenye Betting, mnajidanganya, mtaambulia hasara kiuchumi na kiafya!


Namuona mtu mmoja anataka kusema ati "beti kwa starehe tu" "bet what you can afford to lose" pole sana.


Kadri unavyopoteza ndivyo unavyozidi kupambana ili uokoe ulichopoteza, aidha kwa kuongeza dau au odds. Wazee wa hizo kazi wananielewa


Kwasasa accounts zangu zote za kubetia nimeshazifunga japo kuna wakati nashawishika sana kufungua account mpya (addiction hiyo)najizuia.


Baadhi ya vitu vilivyofanya niamue kuachana na betting;


-Nilikuwa napoteza muda mwingi (hata wa kazi) kutengeneza mkeka (uchambuzi)

-Maumivu makali ya kihisia baada ya timu moja kunichania mkeka niliotumia muda mwingi kuutengeneza, (na hiyo timu iliyochana italaaniwa sana sana😮‍💨)


-Niliona kabisa hapa nikiendelea hivi, presha na kisukari vile palee!

Hakuna wakati mgumu kama pale timu uliyoipa ushindi inafikia dakika ya 70',80' ubao unasoma 0-0, mapigo ya moyo yanaenda mbio, umekaa tu cha ajabu unatokwa jasho kama vile unapanda mlima!!



-Ilifika hatua nikawa napumzika kwa muda mchache sana, muda wa kulala mimi niko live, siyo kwamba nachati wala nini, ni nabetika!

Hata ukinitumia ujumbe WhatsApp usitegemee kujibiwa, ukipiga simu kama sio mtu ambae namheshimu sana jibu ni moja tu "nitakupigia badae kidogo, nipe dakika tano" mpaka pale tukio ninalofuatilia litakapokamilika (tabia mbovu sana hii)

Leo nimemsikia mtu anasema anatafuta mtaji aanze kubeti😆😆
Kama hujawahi kubeti, wala usitake kujifunza.

Kweli betting ni haramu ni heri uraibu mwingine wowote ila sio betting/kamari, betting ni mufilisi janjaruka mapema.
Umeliwa sh ngapi hadi Sasa mkuu?
 
Umeliwa sh ngapi hadi Sasa mkuu?
juzi kati hapa nimedownload mpesa statement nikafuatilia miamala yangu ya miezi sita iliyopita, nikagundua betpawa peke yake wamekula nusu ya mshahara wangu Wa miezi hiyo sita!
 
Uzuri wa kamari.
Leo unashinda milioni 1 baada ya siku 3 umerudisha😂😂😂.
unabaki kapuku hoe hae
 
juzi kati hapa nimedownload mpesa statement nikafuatilia miamala yangu ya miezi sita iliyopita, nikagundua betpawa peke yake wamekula nusu ya mshahara wangu Wa miezi hiyo sita!
Mkuu Kamali ni mbaya Sana Ila ukiacha usiache Kwa kutangaza.

Nilileta uzi humu WA kuacha kunywa pombe lakini huwezi Amini bado nastua mdogo mdogo Yani nimepunguza Tu.

Najua Taratibu nitaacha lakini najiuliza nikiacha mazima kunywa pombe nitatumia starehe gani jibu sijalipata bado.
 
Uzuri wa kamari.
Leo unashinda milioni 1 baada ya siku 3 umerudisha
unabaki kapuku hoe hae
ni hivyo mkuu, wewe umesema ukweli, wanaojifanya wajuaji hapa haiwaijui betting vzuri hawa
 
unapobeti huwa unakosa ama hukosi?
Nakosa lakini nikishinda mara moja naingiza pesa nyingi sana. Kwa mfano naweza kupoteza hadi Tsh 50,000 lakini nikishinda nabutua hadi Tsh 900,000. Kwa hali hii nafilisikaje, kwa mfano?

Tatizo unabet kwa papara ndio maana unaliwa ovyo kisha unakimbilia hapa kulakamika. Bet kwa utulivu uonje faida ya kamari mkuu.
 
Mkuu Kamali ni mbaya Sana Ila ukiacha usiache Kwa kutangaza.

Nilileta uzi humu WA kuacha kunywa pombe lakini huwezi Amini bado nastua mdogo mdogo Yani nimepunguza Tu.

Najua Taratibu nitaacha lakini najiuliza nikiacha mazima kunywa pombe nitatumia starehe gani jibu sijalipata bado.
kama unastua mdogo mdogo una dalili za kuacha. Mara nyingi unapoacha kwa muda, ukirudi unazidisha mara mbili ya mwanzo ila ukiona perfomance iko chini kuliko awali ni dalili nzuri amini utaacha tu.
 
kama unastua mdogo mdogo una dalili za kuacha. Mara nyingi unapoacha kwa muda, ukirudi unazidisha mara mbili ya mwanzo ila ukiona perfomance iko chini kuliko awali ni dalili nzuri amini utaacha tu.
Pamoja Sana mkuu.
 
Nakosa lakini nikishinda mara moja naingiza pesa nyingi sana. Kwa mfano naweza kupoteza hadi Tsh 50,000 lakini nikishinda nabutua hadi Tsh 900,000. Kwa hali hii nafilisikaje, kwa mfano?

Tatizo unabet kwa papara ndio maana unaliwa ovyo kisha unakimbilia hapa kulakamika. Bet kwa utulivu uonje faida ya kamari mkuu.
elfu hamsini?! maana yake ukibeti kwa elfu kumi unatafta odds kuanzia 90!
alafu uniambie unatusua? famasihara nin
 
Hela za freemason ukizipata nunua hata shati,iwe kumbukumbu.ila ukitaka zizidi mawee.zinarudi zote
mkuu, umeongea point, betting utashinda kweli lakini hela unayoipata huko ni kama mkopo wenye riba ya asilimia elfu ya ulichochukua na lazima utailipa tu!
Ndio maana kwenye comments za mwanzo mwanzo kuna watu wanatamba sana kwa historia zao za ushindi lakini 'bado wanabeti'

Hii inaleta maana ya kwamba huwezi kuacha kubeti baada ya ushindi, utaendelea kubeti huku ukilipa mdogo mdogo!
 
inaonyesha wewe kwenye betting ni mchanga sana ipo siku utaelewa, nimekuquote pale juu ili nione uwezo wako
Betting Haina mchanga Wala mzoefu ni akili Yako tu na pesa Yako acha habari zako mtu anaweza akabeti Leo na akapata hela ambayo wewe hujawahi kuipata
 
Back
Top Bottom