Biashara gani ya kunipa faida ya laki mbili kwa siku

Biashara gani ya kunipa faida ya laki mbili kwa siku

Kwa mtaji wa pikipiki 20 akiletewa 200,000 kwa siku bado sio faida aitakayo maana humo kwenye laki mbili ya siku kuna hela iliyo tumika kununulia pikipiki...

Sent using Jamii Forums mobile app

Usimsikilize huyo anayekudanganya kuhusu pikipiki hiyo ni biashara ya kupuuzi mnoo achana nayo kabisa. Kwanza piki piki mpya zinaibiwa sana na hap hajakuwekea hesabu ya service na vingine. Biashara ya kichwani ni tofauti na ya mtaani haiendi ivyo...
 
Upo siriasi kweli unataka kuwekeza m100 upate laki 2 kwa siku? Mbona iyo return ndogo?

Sio ndogo mkuu Ni faida nzuri. Miezi 17 Mungu akiweka mkono wake atakuwa kasharudisha fedha yake.

Kutengeneza mil 6 kwa mwezi awamu kiuhalisia Sio rahisi kama.unavyofikiri.

Na ukikurupuka kufanya biasha biashara ya kupata mil 10+ kwa tamaa mtaji unaweza kata ukiwa unajiona. Laki mbili baada ya miez kazaa lazima iongezeke
 
Mimi ni graduate toka Mlimani Nina biashara ya play station kwa mtaji wa 2M..kila baada ya siku 10 napata 100k na hiyo ni kwa outset 1..kama nikiwekeza 20×2M=40M,,10k×20=200,000/= for 40M..na hiyo yote ni almost profit maana pesa inayoingia yote ni deposited matumiz mengine ni nje ya hiyo per day..
Pia napanga kufungua Car Wash kwa 2M nauhakika wa kupata 50k per day kwa office moja nikiosha gar 10tu ....kila la kheri
 
Wana JF habari za majukumu?

Kati mada ilivyo hapo juu hivi. Naweza kujishughulisha na nini hasa ili faida ya biashara yangu iwe inanilipa laki mbili kwa siku?

Mchango wako ni muhimu kwangu.
Biashara ya kukupa faidi laki 2 kwa siku Moja wapo ni Biashara ya Jumla especially Vinywaji sema sio mwanzo usitegemee ukaanza na iyo faida u need to work hard
 
Biashara yenye faida kubwa ni biashara yenye mtaji mkubwa. Faida unayoizungumzia wewe unatakiwa utoe hapo Kodi, Mshahara wa wafanyakazi wako, Matumizi madogo madogo kama umeme, nauli na chakula nk. Ushahuri wangu kama mfanya biashara, duniani hakuna shortcut, wewe kama unadhania faida inatengenezwa kirahisi utajikuta watu wanakushauri na hawana background na biashara, hawana elimu ya biashara na ulivyouliza ni jambo la busara ila inaonyesha huna elimu ya kutosha ndio maana umeomba ushauri...

Ushauri wa zaida, fanya biashara unayoiweza na uliyo na ujuzi nao, biashara za kuambiwa utapata hasara kubwa mno kama huna uzoefu nazo. Anza biashara hata kama ni ndogo kwa kuwa una ujuzi nayo utafika mbali sana. Na una nafasi ya kukuza biashara yako kuwa kubwa zaidi. Bakhresa katoka kaitoa bishara ya kuuza maandani kutoka mtaa kwa mtaa mpaka imekuwa ni bishara kubwa na anauza nchi nzima wakati wengi wanalenga mtaa mmoja. Ila kwa ndoto zake na udogo wake kaufanya kwa makubwa...

Mie nilianza na shilling elfu 2 ila jimehangaika kwa miaka minne, ila nimenunua viwanja nimeweza kujikimu kimaisha na vitu vingi vyenye thamani ya mamilion ambayo sikutegemea kushika back then...

Ila kwa kwa million 100 afu hujui unataka ufanye nayo nini, manake labda hela ya urithi ila kama ungekuwa mtafutaji mda mrefu ungeweza kujua unachotaka kufanya. Kuwe serious na ukibabaika itakugharimu...
Mkui , tafadhali share nasi hio biashara ulianza n buku 2 mpk mamilion
 
Mimi ni graduate toka Mlimani Nina biashara ya play station kwa mtaji wa 2M..kila baada ya siku 10 napata 100k na hiyo ni kwa outset 1..kama nikiwekeza 20×2M=40M,,10k×20=200,000/= for 40M..na hiyo yote ni almost profit maana pesa inayoingia yote ni deposited matumiz mengine ni nje ya hiyo per day..
Pia napanga kufungua Car Wash kwa 2M nauhakika wa kupata 50k per day kwa office moja nikiosha gar 10tu ....kila la kheri
Hebu changanua mkuu hyo biashara ya play station unavyo ifanya
 
Back
Top Bottom