Biashara inataka watu wenye roho ngumu, fikiria nimewekeza 300M+ napata 5M kama faida Kwa mwezi

hii inawezekana kutegemea na aina ya biashara!

mfano anatefuga kuroiler akawalisha inavyotakiwa na akauza rejareja kila mwezi anaweza fikisha hata 4M

hata anayeweka layers mayai yanalipa kama atachanganya chakula yeye mwenyewe!
Sawa mkuu,ngoja wafugaji waje hapa watatupa uzoefu wao.
 
Mkuu kuna kitu inaitwa Novatechfx.
Unaweka hela yako wanaizungusha.
Wanalipa kila week.
Hiyo 300m kwa week wanakupa sio chini ya 7m.
Nipe elimu kidogo ni bank gani hufanya hivyo?
 
Hiyo return ni ya juu sana sielewi kwa nini unalalamika. Ume invest 300M returns kwa mwaka ni 60M ambayo ni karibia 20%. hamna biashara nyingine yenye such high returns. Hata treasury bills/bonds annual returns ni around 10%.
Return yake ni ndogo mkuu. With 20m investment napata net profit 800k-1.2m kwa mwezi
 
Sawa mkuu,ngoja wafugaji waje hapa watatupa uzoefu wao.
mie pia nafanya ufugaji huu! ingawa si kwa kiwango hiki ila nina muda mrefu! na nimeshafanya research kubwa tu! nikipata mtaji wa kufka 10M nitatoboa! maana mabanda ni yangu na chakula nachanganya mwenyewe! magonjwa ya kuku napambania mwenyewe,
kikubwa usicheze na mtaji kwenye biashara kama hii
 
Vip ukiwa na 114 mende alfu ukaweka tella pili imeekaaje

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 

Check biashara hizi chache kwa mfano
1.Real estate.kununua na kuuza viwanja.mfano unanunua heka 10 kwa m300 then KILA hekta unatoa viwanja 6,kila kiwanja unauza milioni 20
o kwa heka uliyonunua m30 unapata revenue ya m120 so eka kumi unapata total revenue 1.2 bilioni. Toa gharama zote mfano tax, operation cost, nk haizidi milioni 300 per year.

2.Kuwa na plant ya kuponda kokoto total investment ni m250.
Lori moja la kokoto 30 tonn wanauza milioni 1.2 hapa profit ni speed yako ya market unacheza na watu wenye plant za concrete mixers,wakandarasi unawapa percentage yao wakupe tenda.
3.Kusuply madini ya matani mfano chokaa,quartz,nk
4.Kuwekeza kwenye recycling taka za plastic, karatasi,
 
kuna Saccos ukipeleka hiyo wanakulipa 2% kila mwez kama faida
 
Hata zaidi ya bilioni 10 kwa mwaka unapata kwenye madini,unapiga fully yaani madini ya matani na ya gram pia.Inayokata pesa ni madini ya gram.Matani uhakika pesa inarudi.
Ajirisk tu huko kuliko kungojea vimillion 5 kwa mwezi kwa million 300
 
Kiuharisia biashara inahitaji roho ngumu aina. Ila kwa hiyo hela yako hupaswi kupata faida hiyo kwa mwezi. Kama ni hivyo ikusanye hiyo M.300 yote wekeza kwenye hisa za mabank. Kwa pesa hiyo utakuwa unapata return ya si chini ya Milioni 25 kila mwezi. Na hapo hakuna wa kumlipa,wala hakuna pressure hata kidogo. Unakula hiyo ukiwa umetulia tu nyumbani.

Naitamani sana hii biashara,siku nikipata tu mkwanja mrefu lazima nijitupie huko
 
Angalau nimepitia Comments zote na kwa hakika kuna waliotoa maoni mazuri mno.

Tatizo nilioliona kwa Mhusika ni kwamba, aliset expectations kubwa. Au huenda alijiingiza kwenye biashara baada ya kuona returns za mwenzake.

Huenda anailinganisha gross profit yake na gross ya biashara iliyo-mature tayari.

Nikuhakikishie, kama ndo kwanza biashara ina mwezi mmoja maana yake ina faida kubwa sana. Kazia kupiga kazi huku ukisuburi. I'm sure, onto the next month utapata gross ya 8m.

Hao wanashauri juu ya UTT na BOT bonds wameshachelewa. Maana hata ukisema uikimbie biashara yako ya sasa, hutopata tena ile 300m. Lazima ipungue.

Ungesema ni aina gani ya biashara ili ufahamishwe kama ime-under perform.
 
Safi Sana mkuu,all the best.
 
Duh pole sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…