Biashara inayoweza kukutoa ni ile inayokupa faida ya Tsh. 50,000 na kuendelea kwa siku

Biashara inayoweza kukutoa ni ile inayokupa faida ya Tsh. 50,000 na kuendelea kwa siku

Gulio Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
3,325
Reaction score
7,807
Mpaka sasa nipo katika biashara kwa kipindi cha miaka mitano sasa nina uzoefu kiasi chake ila nilichojifunza cha kwanza elimu inahitaji Sana katika ufanyaji wa biashara. Kuna umuhimu mkubwa hata Serikali kuanzisha mitaala ili watu wapate elimu juu somo hili.

Biashara nyingi bado nazoziona hasa hizi ndogo ndio vijana wengi wanaotoka chuo nimeona wanazifanya lakini nyingi hazikui.

Mitaji ya kuanzia laki 8 mpaka million 2.

Wengi nimegundua wanacheza na biashara zenye kuingiza faida ya Tsh. 20,000 akijitahidi sana ni 30,000. Sasa kama unaingiza elfu 20 kwa siku kwa mwezi utaingiza laki sita pesa ambayo haiwezi kukuza mtaji wako.

Mfanyabiashara ambaye anaingiza faida ya elfu 30 kwa mwezi atakuwa na uhakika wa kuingiza laki 9 kwa mtaji alionao itaonekana bado ni pesa kubwa lakini tuangalie matumizi yake kwa mwezi ni laki 6 atasevu laki 3 kwa mwaka ataingiza faida ya mil 3.6 bado ni faida ndogo Sana kuweza kukutoa kimaisha.

Nilichojifunza wafanyabiashara wengi wenye mitaji midogo wanakosa ni elimu bado wengi wana ile hali ya kujibana kwenye matumizi yao binafsi lakini hawafikiri kuzalisha zaidi faida. Mfanyabiashara ukifikiria kujibana ndio kukuza mtaji unakosea utashindwa kuruhusu akili nyingine ya kuzalisha zaidi faida kwenye biashara unayofanya ama chanzo kingine cha kipato.

Angalia sasa kama utaweza kuingiza faida ya elfu 50 kwa siku kwa mwezi utaingiza mil 1.5 matumizi yako binafsi laki 7 utaweza sevu kila mwezi laki 8 kwa mwaka mmoja tu utakuwa umepata faida ya mil 9.6
 
Mkuu Mimi nipo kijjin na mauzo yangu kwa siku Ni laki moja na 50 mpk laki2 ...hapa sijajumlisha miamala....lkn sioni mambo naona magumu
Wakala na biashara gani hiyo nyingine? Labda kwa vile kijijini kuna running costs nyingi ndio maana hauoni faida
 
Ipoje hii mwanakwetu?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app

Bonus Account​

On top of a basic interest, this account has an additional attractive and competitive quarterly paid bonus interest.

Benefits of Bonus Account

  • Offers interest of up to 13% per annum*
  • Interest accrued daily and paid on quarterly basis
  • Enjoy Bonus Interest over and above Basic Interest
  • Saving can be used as a lien to acquire a personal loan
  • Gives access to over 215 branches countrywide
  • Customer money are safe and secured
  • Eligible for free NMB Identity card
  • No monthly maintenance fee
  • One withdraw per quarter without losing Bonus Interest
  • Free cash and on us cheque deposit
 
Mpaka sasa nipo katika biashara kwa kipindi cha miaka mitano sasa nina uzoefu kiasi chake ila nilichojifunza cha kwanza elimu inahitaji Sana katika ufanyaji wa biashara. Kuna umuhimu mkubwa ata serikali kuanzisha mitaala ili watu wapate elimu juu somo hili

Biashara nyingi bado nazoziona hasa hizi ndogo ndio vijana wengi wanaotoka chuo nimeona wanazifanya lakini nyingi hazikui

Mitaji ya kuanzia laki 8 mpaka million 2

Wengi nimegundua wanacheza na biashara zenye kuingiza faida ya Tsh 20000 akijitahidi Sana ni 30000. Sasa kama unaingiza elfu 20 kwa siku kwa mwezi utaingiza laki sita pesa ambayo haiwezi kukuza mtaji wako

Mfanyabiashara ambaye anaingiza faida ya elfu 30 kwa mwezi atakuwa na uhakika wa kuingiza laki 9 kwa mtaji alionao itaonekana bado ni pesa kubwa lakini tuangalie matumizi yake kwa mwezi ni laki 6 atasevu laki 3 kwa mwaka ataingiza faida ya mil 3.6 bado ni faida ndogo Sana kuweza kukutoa kimaisha

Nilichojifunza wafanyabiashara wengi wenye mitaji midogo wanakosa ni elimu bado wengi wana ile hali ya kujibana kwenye matumizi yao binafsi lakini hawafikiri kuzalisha zaidi faida. Mfanyabiashara ukifikiria kujibana ndio kukuza mtaji unakosea utashindwa kuruhusu akili nyingine ya kuzalisha zaidi faida kwenye biashara unayofanya ama chanzo kingine cha kipato

Angalia sasa kama utaweza kuingiza faida ya elfu 50 kwa siku kwa mwezi utaingiza mil 1.5 matumizi yako binafsi laki 7 utaweza sevu kila mwezi laki 8 kwa mwaka mmoja tu utakuwa umepata faida ya mil 9.6
Hiyo biashara ingekuwepo si kila mtu angeifanya?
 
Wakala na biashara gani hiyo nyingine? Labda kwa vile kijijini kuna running costs nyingi ndio maana hauoni faida
Mahitaji ya nyumbani....faida ipo Ila namna ya kuikuza biashara ..

Hebu fikiria haya..

Tra laki1 kwa mwaka.

Kodi ya jengo laki 6

Muuzaji 70k kwa mwezi

Ushuru wa Kijiji 36k kwa mwaka

Leseni ya biashara 20k

Tozo ya umeme ya Kila mwezi.

Gharama nyingine za services.

Notoboaje mkuu?
 

Bonus Account​

On top of a basic interest, this account has an additional attractive and competitive quarterly paid bonus interest.

Benefits of Bonus Account

  • Offers interest of up to 13% per annum*
  • Interest accrued daily and paid on quarterly basis
  • Enjoy Bonus Interest over and above Basic Interest
  • Saving can be used as a lien to acquire a personal loan
  • Gives access to over 215 branches countrywide
  • Customer money are safe and secured
  • Eligible for free NMB Identity card
  • No monthly maintenance fee
  • One withdraw per quarter without losing Bonus Interest
  • Free cash and on us cheque deposit
Hii
Ipoje hii mwanakwetu?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
NMBBonus Account, akaunti maalumu ya kuweka akiba kwa ajili ya malengo yako ya muda mrefu. Akaunti hii inakupa mpaka asilimia 13* ya faida kila robo ya mwaka.
Katika hii account unaruhusiwa kutoa fedha mara moja tu katika miezi mitatu au ukasubiri na kupata gawio lako Kila baada ya miezi mitatu. Sema hii bonus account ni nzuri Kama unaweka mzigo mkubwa Kama million 500 , billion 1 au zaidi
 
Hiyo kodi ya Jengo ni ya mwaka?
Hapana, ipo hivi ukipanga jengo la biashara mfano laki 5 TRA wanachukua 10% ya ulichomlipa mwenye jengo... kwahiyo mwenye jengo utampa laki 4.5 halafu 50k unawalipa TRA Ndio Kodi ya jengo.. kama laki 6 TRA Tozo jengo utawalipa 60k na mwenye jengo atachukua 540k.
 
Hii

NMBBonus Account, akaunti maalumu ya kuweka akiba kwa ajili ya malengo yako ya muda mrefu. Akaunti hii inakupa mpaka asilimia 13* ya faida kila robo ya mwaka.
Katika hii account unaruhusiwa kutoa fedha mara moja tu katika miezi mitatu au ukasubiri na kupata gawio lako Kila baada ya miezi mitatu. Sema hii bonus account ni nzuri Kama unaweka mzigo mkubwa Kama million 500 , billion 1 au zaidi
13% kila robo ya mwaka au ni kwa mwaka mzima?
 
Hiyo kodi ya Jengo ni ya mwaka?
Lakini pia hata Kama TRA utawapa tozo ya jengo Bado lazma uwape Tax ambayo wanakukokotolea kulingana na mtaji wako.....ndio maana tunalalamika tozo umiza ..
 
Back
Top Bottom